Zimbabwe Election: Progress & Results

Zimbabwe Election: Progress & Results

Dhamira ya Mugabe ilikuwa nzuri sana tokea zamani kwa mustakabali wa raia wa Zimbabwe. Tatizo lililotokea Zimbabwe halina tofauti kabisa na hali ya kwetu. Kuwa hiyo nia njema aitakayo mtu haipaswi kufikiriwa njia za kuifuata kwa mawazo ya mtu mmoja bali kwa kufuata sheria na kanuni mnazojiwekea huku ikishirikisha watu na vyombo mbalimbali kama sera ya nchi.
Mugabe alikuwa anafanya maamuzi jinsi anavyojisikia au anavyo shauriwa na mkewe tena bila woga. Hivyo nia yake njema ikawa ni ubabe na mipango duni mbele ya jamii na mwisho akaitia umasikini mkubwa Zimbabwe huku yeye na familia yake wakiwa matajiri sana. Walianza kuficha utajiri wao (kama hapa kwetu) lakini utajiri ukikomaa moyoni ni vigumu tena kuuficha.
Tujifunze hata sisi kutoka Zimbabwe, haya mambo ya mimi siambiwi la kufanya kama vile Taifa ni mali yako, kuto kaa meza moja na wenye mawazo tofauti nawe, kukomesha wenye nacho nk hayatatufikisha pazuri zaidi ya nchi kiuchumi kuangukia pua na mwisho haya yanayotokea sasa
 
Naomba Mods muulete huu uzi hapa SIASA

Kichwa chaweza kubadilishwa to: Zimbabwe & Mugabe: End of an error

Thread yenyewe hii hapa:


Zimbabwe Election: Progress & Results

2008 Kitila Mkumbo alikuwa anapewa darasa kuhusu Zimbabwe mpaka katulia kama maji ya mtungi

Enzi hizo ni JAMBO FORUMS

blast from the past

Thread nzuri ila umeanzisha kishabiki mno, haujiamini, una inferiority complex, sasa kutaja Kitila eti anapewa somo wakati ni mjadala/forums/debate inatokea wapi?

Edit hizo statement ambazo haujaziweka vizuri kulinda heshima mtu

umeona bila kumtaja thread haitasomwa...aisee
 
Nilikuwa nikipita mara kwa mara wakati huo nchini Zimbabwe, niliona hali ilivyokuwa kabla na baada ya hiyo inayoitwa land reform. Kwa kweli baadhi yetu tulijua kwa hakika mzee anaenda kuiharibu nchi, ilikuwa ukiongea na wazimbabwe wa kawaida walikuwa wakisema jambo hilo la sio jambo la majority ila ni la veterans ambao kiukweli ni watu wachache tu.
 
Mimi suala la Mugabe kuwanyang'anya wazungu walowezi ardhi ili kuwapa RAIA naliunga mkono kwa asilimia zote. Hivi kweli piga picha hata hapa kwetu kama wazungu wangechukua ardhi yote yenye rutuba (mikoa ya morogoro, iringa,mbeya, Kilimanjaro, tanga, katavi, nk) halafu sisi tubaki na kanda ya kati watu si tungekuwa watumwa ndani ya nchi yetu? Hili naona alifanya sawa kabisa
 
Kamuulizeni Kitila maoni yake juu ya Mugabe kwa sasa! Atakuwa anajutia kuji.verify kwa kipindi kile
 
..2008 mimi nilikuwa miongoni mwa wana JF waliokuwa wakimtetea Robert Mugabe.

..niliunga mkono msimamo wa Mugabe kuhusu kugawa ardhi kwa Waafrika wa Zimbabwe na kuisaidia kijeshi Jamhuri ya Congo.

..Lakini jinsi muda ulivyosonga mbele Mzee Mugabe akageuka kuwa dikteta mbaya sana na kuendelea kwake kukaa madarakani kulisababisha uchumi wa Zimbabwe kuporomoka kutokana na vikwazo vya uchumi.

..Ilifika mahali nikaona Mzee Mugabe alipaswa kung'atuka ili kuinusuru Zimbabwe na kutunza heshima yake.

..Nawakumbuka Kichuguu, na Dua kama wana JF ambao waliona mbali kuliko mimi kuhusu suala la Zimbabwe.
Hao ndo wanasiasa,usiwaaamiiini
 
Zimbabwe could be added to UN Security Council's Africa summit
Monsters and Critics


Apr 15, 2008, 18:35 GMT



Mugabe is waiting to take the next move.........
what u mean
 
Back
Top Bottom