Zimbabwe Election: Progress & Results

Hivi nani anaweza kuelezea kuanguka kiuchumi kwa Zimbabwe-kutoka ilivyokuwa chini ya wakoloni hadi walipopata uhuru na miaka michache baada ya uhuru na ilipo sasa bila ya kurudi kule kule kwa Waafrika Ndivyo Tulivyo? Yaani hawa Waafrika walipochukua madaraka wameichukua Zimbabwe kutoka moja ya nchi zenye uchumi mzuri Afrika na kuipeleka kuwa moja ya nchi vichekesho na sasa wameifikisha kuwa moja ya nchi zinazotia huruma duniani. Jamani nani anaweza kunieleza nikaelewa hii safari ya kinyume nyume?

Kuna watu watakwambia hiyo yote ni kwa ajili ya UK na USA!!
 
Nyani Ngabu,
Zimbabwe was OK yaani walikuwa vizuri kiuchumi hadi mwaka 2000 pale Mugabe alipochukua ardhi za wazungu... Hilo ndio kosa kubwa la Mugabe kulingana na mtazamo wa nchi za magharibi yaani Mugabe ni racist kinamna bila kujali kwamba hao wazungu walishika asilimia 70 ya ardhi yenye rutba.
Tatizo jingine ambalo nimekuja ligundua ni kwamba siku zote mazao yote ya chakula Zimbabwe yalikuwa yakitokana na modified seeds toka South ambazo tayari zilikwisha badilisha rutuba ya udongo kiasi kwamba huwezi kupanda mbegu nyingine yoyote ile ikaweza kuota vizuri...Hivyo wamekwama hata kwa chakula.
Waswahili akina ndivyo tulivyo hawana access ya mbegu hizo isipokuwa kupitia kwa Kaburu ambaye ndiye kachukuliwa ardhi na kibaya zaidi ni vikwazo walivyopewa Zimbabwe kiuchumi kiasi kwamba mimi binafsi nilitaka kununua kitu toka Zimbabwe nilikataliwa na benki ya hapa kuwa hakuna business transaction yoyote inayoruhusiwa na Zimbabwe.
Kwa hiyo mkuu unaweza pima hawa jamaa zetu walipo simama na tatizo kubwa naloshindwa kuelewa ni kwamba hata huyo Simba akichukua je atarudisha ardhi kwa wazungu?...na akikataa hivyo vikwazo vitakwisha kwa sababu Mugabe hayupo madarakani!
Nikikumbukia Cuba Marekani walisema akiondoka Castrol wataweza kurudisha uhusiano wao na Cuba lakini kilichotokea ni kwamba sababu mpya zimevutwa kuhusu mdogo wake kuwa hawa ni ndugu..Kwa hiyo kazi sii ndogo hata kidogo...
Nikirudi ktk swala la Wazimbabwe mkuu hakuna haja ya kuwaonea huruma kwa sababu FMES kesha sema viongozi wetu ni reflection yetu sisi, hivyo kuna kina Mugabe kibao wamejaa Zimbabwe, hawakubaliani na matakwa ya nchi za magharibi...PIGA, UA.
Na ndio sababu kubwa inayompa kura.. hawa jamaa zetu ni maskini jeuri kama Mugabe mwenyewe!
 
Mimi bado naamini kuwa Mugabe atashindwa hapo kesho.... Kinyume cha hapo inabidi Kikwete ajiandae.....

I beg your Pardon!!!
Mw.WK,Could you please Re-phase that Statement:-"Mimi Bado naamini kuwa Mugabe atashinda hapo kesho...na inabidi Kikwete ajiandae kwenda kwenye Sherehe za kuapishwa kwake"

**That's African Rulers for You!!
 
I beg your Pardon!!!
Mw.WK,Could you please Re-phase that Statement:-"Mimi Bado naamini kuwa Mugabe atashinda hapo kesho...na inabidi Kikwete ajiandae kwenda kwenye Sherehe za kuapishwa kwake"

**That's African Rulers for You!!

Mimi naweza kukubaliana na MwK maana jeshi liko tayari kuua watu wakishinda na kuwaua pia wakiingia mtaani kama Kenya .
 
Nimejaribu kusoma hapa na pale kuhusu uchaguzi wa kesho Zimbabwe. Inafurahisha kwamba angalau watu wengi sasa hatimaye wameweza kuona ubaya wa Mugabe na inaonekana kesho wameamua liwe na lisiwe hawatampigia kura Mugabe. Katika somasoma yangu pia nimegundua kuwa bado kuna watu wa kutosha, japokuwa si kwa kiwango cha kumpa ushindi Mugabe, ambao bado wanampenda Mugabe. Sasa mimi najiuliza hivi hawa watu wanataka Mugabe awafanyeje ndio wamchukie maana ameshawatenda kila aina ya ubaya unaoweza kufikiria? Ninaamini kwa haya aliyokwisha kuyafanya Mugabe ingekuwa ni kwa wenzetu wazungu, hata kura za watoto na mke wake asingezipata. Sasa mimi ndio najiuliza sisi waafrika tuna matatizo gani inapokujwa kwenye kuchagua viongozi?

Ok, kwa Tanzania watu wanaoendelea kuipigia kura CCM wanatoa visingizio kwamba wapinzani wapo wachache wenye uwezo na hawana sera. Haya, na huko Zimbabwe? Mbona upinzani wameshusha kila aina ya sera na kila mwanasiasa hodari yupo kwenye upinzani, iweje basi watu waendelee kumpigia kura Mugabe na CCM ( or sorry I mean, ZANU-PF) yake?

Kibaya zaidi ni kwamba jeshi eti limesema halitatambua mshindi mwingine zaidi ya Mugabe! Sasa najiuliza tena hawa wanajeshi wa nchi zetu mafunzo yao yakoje kiasi kwamba wanashindwa kuelewa wajibu wao kwa kiwango hiki? Halafu lijamaa (Mugabe) limesema eti ikibidi litatumia style ya Kibaki huko Kenya, na limewaonya MDC ole wao wafuata mtindo aliotumia Odinga, watakiona cha mtema kuni-hii hapa soma: http://www.guardian.co.uk/commentisfree/2008/mar/28/zimbabwe

Sasa mimi ndio najiuliza, sisi wabongo (Waafrika) tuna matatizo gani hasa kwenye mambo haya ya kuchaguana?

Je, tunahitaji nadharia (theories) maalumu kwa ajili ya kuelewa siasa za Afrika?

Kitila usisahau wizi wa kura pia ambao sasa hivi unashamiri katika nchi nyingi duniani hata za Magharibi. CCM wameshaiba chaguzi. Kenya uchaguzi wao wa December, 2007 pia kulikuwa na wizi wa kura ambao ulisababisha maafa makubwa katika nchi hiyo, Kichaka mwaka 2000 na 2004 aliiba kura pia katika uchaguzi wa Marekani. Hivyo tusishangae pia kuona Mugabe anaiba kura ili aendelee kuwa madarakani.
 
Habari za uhakika kutoka kwa observours wamekuta majina ya wapiga kura 8000 kwenye kituo kimoja ambayo ni ya uongo.


Hivi nani anaweza kuelezea kuanguka kiuchumi kwa Zimbabwe-kutoka ilivyokuwa chini ya wakoloni hadi walipopata uhuru na miaka michache baada ya uhuru na ilipo sasa bila ya kurudi kule kule kwa Waafrika Ndivyo Tulivyo? Yaani hawa Waafrika walipochukua madaraka wameichukua Zimbabwe kutoka moja ya nchi zenye uchumi mzuri Afrika na kuipeleka kuwa moja ya nchi vichekesho na sasa wameifikisha kuwa moja ya nchi zinazotia huruma duniani. Jamani nani anaweza kunieleza nikaelewa hii safari ya kinyume nyume?

Ukitaka kujua jinsi Mugabe alivyoiharibu Zimbabwe ni lazima uelewe jinsi alivyoingia madarakani, jinsi alivyoua wale ambao walionekana ndio wangechukua ukanda na baada ya kupata, jinsi alivyoendelea kuua hususan Matebeleland. Atakaa kwenye madaraka kwa njia yoyote ile hadi afe. Hawezi kuachia Madaraka hata akishindwa kura. MARK MY WORD.
 
KWA KWELI MAONI MENGI YAMETOLEWA KUHUSU ZIMB.....YANGU NI HAYA......!
ZIMB NI NCHI HURU NA INAFANYA UCHAGUZI WA KIDEMOKRASIA......!
DEMOKRASIA KTK UCHAGUZI NI KUKUBALI MATOKEO NA SIO PALE TU UPANDE MMOJA UNAPOSHINDA...UPANDE HUO UKUSHINDWA UTASIKIA UTASIKIA UCHAGUZI HAUKUWA HURU NA HAKI.......!
WAZUNGU HUTAKA KUONGOZA KWA REMOTE(puppet leaders/regimes),IKITOKEA UKAWA AGAINST NAO WEWE UTAKUWA HUFAI,ADUI,DIKTETA(they will call you names)........!
HIVI HATUSHANGAI KWA NINI WAZIMB WENYEWE BADO WAPO NA ZANU-PF?SHUTUMA NYINGI ZINATOKA NJE YA ZIMB NA SIO NDANI TOFAUTI NA NCHI NYINGI......!(ukikuta shutuma za ndani ya zimb ni zile za vibaraka wachache)......!
AFRIKA INATAKA WATU KAMA MUGABE.....(sio viongozi yes boss)....WENYE KUJUA KUWA UINGIREZA IAMUE MAMBO YAKE,NA ZIMB NAYO IAMUE MAMBO YAKE......! SIO SYSYTEM YA CHAKO CHANGU CHANGU CHANGU......!
I HATE MUGABE....BUT I LOVE HIS POLICIES......!SIPENDI MUGABE AONGOZE ZIMB LAKINI KWA CANDIDATES WALIOPO MUGABE ASHINDE.....BTN THE TWO EVILS...CHOOSE THE LESSER....."

Asante kwa ukweli ulioandika. Waafrica wengi tunasahau asili yetu haraka sana na hasa baada ya kuishi nje ya nchi aka ulaya na marekani kwa muda mrefu.

Ukoloni mambo leo bado upo duniani hivyo ni muhimu sana kuwa makini na hawa watu wa mataifa ya magharibi ambao kila kukicha wanatafuta mbinu mpya ya kutuibia na kuhamisha mali na utajiri wetu.
 
Mimi nimechoka kuona Wazimbabwe wakihangaika kimaisha! Kuna mtu kabandika picha hapa ya mama na mwanae wakivuka mpaka wenye barbed wire kwenda Afrika Kusini...Jamani huyu Mugabe mwenye miaka 84 bado anataka kuwa raisi kwa nini? Na kwa nini watu wamchague....aaaghhh yaani hawa Wazimbabwe wangekuwa wanafikiria kama mimi maisha yao yangekuwa na nafuu kushinda yalivyo sasa chini ya Mugabe

Watanzania wangapi wanazamia Africa kusini kila siku? Watanzania wangapi wanakosa hata mlo mmoja kwa siku?.Kwa kuwa wewe upo hapo unabofya ki-board unafikiri watanzania wenzako pia wana maisha mazuri? maana angalau wewe kama umeweza kubofya kiboard lazima uhakika wa mlo mmoja unao.

Leo hii Tanzania ni tegemezi kwa zaidi ya 40% katika bajeti tu mbali na misaada mingine kupitia taasisi zisizo za kiserikali je hao jamaa leo wakikata misaada unafikiri hii Tanzania itakuwaje? jibu unalo itakuwa mbaya kuliko Zimbabwe ingawa hapa Mugabe hayupo.

Matatizo ya Zimbabwe hayawezi kuondoka hata kama Mugabe akiondoka mpaka hao makaburu wapate wanachotaka maana yake ni kwamba hao wazimbabwe waendelee na utumwa kwenye mashamba ya wazungu ndiko wanakostahili na sio wao kumiliki ardhi.

Kuna mtu anasema Mugabe ni racist,si kweli suala la ardhi ni makubaliano ya siku nyingi kati ya Uingereza na Zimbabwe,serikali ya Uingereza ilitakiwa kutoa fedha za fidia kuwafidia raia wake walioko Zimbabwe ili ardhi igawiwe kwa Wazimbabwe wasio na ardhi lakini Waingereza wamekuwa wanapiga chenga tangu mwaka 1980 hadi mwaka 2000 Mugabe alipoamua kufanya kweli.

Matumaini waliyonayo Waingereza ni kuwa wakifanikiwa kumtoa Mugabe wakaweka mtu wao tatizo la ardhi litaisha,hawatalipa fidia na ardhi wataendelea kuimiliki.

Nawaombea wazimbawe maana wanapita wakati mgumu lakini heri yao maana mwishowe watapata suluhu ya matatizo yao wakati sisi tutaendelea kuwalamba miguu wazungu wakishirikiana na viongozi wetu kutufisadi
 
Kuna watu watakwambia hiyo yote ni kwa ajili ya UK na USA!!

Uchumi mzuri ni neno tata.Hapa JF kuna nchi iliongelewa nafikiri ni Equetorial guinea kuwa na GDP ya dola 30,000 lakini watu wake wanaishi katika umaskini wa kutupa.Juzijuzi tulikuwa tukisikia pongezi kwa Tanzania kuwa uchumi unakua kwa 7% lakini ukienda kwa Wananchi unakuta umaskini umeongezeka.
Sasa unapozungumzia Zimbabwe kuwa na uchumi mzuri wakati 70-80% ya watu wake hawana ardhi wote hao ni peasants kama walivyo watanzania wengi ni lazima uwe mwangalifu.
 
Taizo la issue ya Zimbabwe mara nyingi watu huwa hawataki kudususs form both sides of the issue.

Zimbabwe haiongozi Africa kwa HUman rights violations lakini cha ajabu husikii nchi kama Egypt au Eitrea zikilalamikiwa

let alone DRC ambako zaidi ya watu milioni 4 washauwawa

this is where you see the British hypocrisy at its best

One minute Mugabe mbaya next minute wataongeza close relationship na China. Next minute Mugabe ni mbaya jioni wanamkaribisha King Abdulla ambaye Britain and Saudi Arabia wanashared values


Kula tano za chapchap...
Kuanguka kwa Mugabe itakuwa ni ushindi wa hypocrisy za UK na Marekani.Watu wengi hawaangalii issue ya Zimbabwe from both sides.
Mugabe kabla hajagusa interests za UK( kwa kuwanyang'anya mashamba wazungu)aliitwa kiongozi safi na mtu ambaye anajua kuleta maendeleo nchini mwake.Ila tu alipothubutu kuchukua mashamba yale ndipo alipoanzwa kupachikwa kila aina ya majina na isitoshe UK na Marekani zikaanza kupeleka mabilion ya pesa kwa wapinzani ili kuungusha utawala wa Mugabe.Na Mugabe alipoamua kupambana ndipo UK na mshirika wake Marekani wakatangaza vikwazo vya kiuchumi na pia kuwashurutisha EU kufuata mkondo.
Ni lazima tutambue kuwa vikwazo vya kiuchumi siyo lelemama! ndiyo hasa vinavyosababisha uchumi kudorora siku hadi siku! na ndiyo maana Marekani na washirika wake wanataka pia Irani iwekewe vikwazo vya kiuchumi ili kulidhibiti taifa hilo la kiislamu.
Sasa basi tujiulize nini kwanini Zimbabwe na siyo DRC? maana kila kukicha watu wanauliwa DRC na hatusikii lolote toka kwa Marekani na mshirika wake UK..au ni mimi tu ndiye ninayeona kuwa demokrasia pia inahitajika DRC na tena muda huu!! Hii inatoa jibu kuwa demokrasia inayopigiwa mbiu na UK na Wamarekani huwa tu pale interests za wazungu zinapoguswa na si vingenevyo!.
Leo hii kama unabisha jaribu kupeleka mabilion ya pesa kwa watu weusi walioko UK na Marekani ili kuwamobilize kuziondoa serikali hizo madarakani uone jinsi nchi hizo zitakavyo react kwa nguvu zote za dola!! na tena pengine kufungua guantanamo nyingine!
Kumbe basi tunapata jibu kuwa Mugabe yuko vitani...anapambana na hizi sera potofu za UK na Marekani za kuwakandamiza watu weusi kwa kuwanyima haki zao za kumiliki ardhi na mali kama wazungu au watu wengine.

-Wembe
 
Zimbabwe in cross-road

The rule of law, democracy and good governance are indeed values that we cherish because we fought for them against the very same people who today seek to preach them to us - Robert Mugabe

Having pointed that out, I do believe it is time for change in Zimbabwe... Both within, and from the outside. A Shah, London,


The poverty in Africa is a direct result of Western Imperialism and neo colonialism. In the case of Zimbabwe, Mugabe is just a convenient scapegoat (and a bit of a thorn in the flesh as well to imperialist alliance who expect every African leader to be their stooge)

They are all drooling at the prospect of another puppet so they can once again sink their claws into Zimbabwe's wealth thus perpetuating the imbalance.

ZIMBABWE SHALL NEVER BE A COLONY AGAIN, ALUTA CONTINUA! Dambudzo Marechera, Kumaraini, Zimbabwe


Put all ideological conceptions aside. Robert Mugabe is a metaphor for Zimbabwe et al. Bill, Alabama, USA


Robert Mugabe and President George Bush of America should get together in how they both ruined their nations economies. Down with Mugabe. May the people of Zimabawe vote for someone other then the Black Hitler called Mugabe. John, Cumberland, United States/Maryland


Jin Burks, they may not have had political power under the white spremacist regime, but now - after almost three decades of black majority rule, the people of can't afford the basics of life, even though they have been empowered to make political choices via the ballot box. So how does an accelerating decline over three decades become the fault of the western world that oposed Ian Smith's UDI and supported black majority rule?

The simple truth is that Mugabe has taken away from the people of Zimbabwe any realistic possibility of making a true choice at the ballor box, and has mismanaged the country. Let's hope that he is voted out, and that he goes peacefully. Somwhow, I think he'll try to hang on to power at all costs whatever the result of the election. Richard, Manchester,


I do hope so! The next people to gain power will look to Great Britain holding out the begging bowl for funds and facillities. I hope that this nu labor Government does not throw good money after bad. Look up the history of this once great land. The African did not want the European there and with the help of the UK, America they installed a fool into the highest postion, this fool has cost the life of thousands and ruined want was once Gods own Country. Let the Africans sort their own problems out, but send back any Zimbabwean immigrants that are living in the UK. Brian , Ellesmere, Shropshire


If you are white and you began loving Black Zimbabweans and the Black race since the sacking of white farmers by Mugabe in 2000, you are naturally a white supremacist! Ezhi Opfu, Johannesburg, South Africa


I was in Harare, the Capital City of Zimbabwe just last week. I am a Zimbabwean citizen of mixed race origin , and whilst people may criticise and demonise Mugabe he is on trial by Western Governments primarily for the following reasons:-
( for the moment put aside the gross human rights abuses)

1) For taking from the White man, land which has been given to the black populace, to correct a grave historical injustice

2) For standing up for his people against the exploitation of Zimbabwe's massive mineral resources which include :- uranium , platinum and gold , diamonds , timber and wildlife resources

3) For demanding equality from an avaricious Capitalist West which abhors any sign of an Independent stance from a 3rd world country

4) For exposing the hypocrisy of the British Labour government who wanted lucrative Trade between Zim & the UK to continue on very favourable terms for the UK

5) For handing over the economy to its rightful owners: The PEOPLE of ZIMBABWE. Bertram T bertram tabbett, Milton Keynes, UK


The western politicians did indeed sell out Ian Smith's government, where most of the citizens of the old Rhodesia were so happy that terrorist such as Mugabe's mob had to kill and maim the many villagers to force them to join him with promises of riches and "freedom" (to starve and to die). I was living in that area and most readers will not know the facts.·

Ian Smith forecast what would happen and it has. The real racists are those who would not listen and instead judged by the skin colour, falling for the false propaganda, not the ability of the people concerned. By now under the original system, black politicians would be in a democratic, fair, mixed race government in a very prosperous country.

South Africa is next as we can see. Are you willing to continue to give massive aid to a continent that has self-inflicted woes? Only fools are because they must be forced to do the right thing to overcome the problems and aid only pushes this obvious solution further away. B J Deller, Marbella, Spain


Jim Burks, Memphis - I am SO fed up with people trying to pin the crisis in Zimbabwe on the west, this is Mugabe's fault. He ordered the invasion of the farms, he sent inflation through the roof, he ordered the beating and torturing of opposition politicians..

This has nothing to do with the West and everything to do with African politicians failing to live up to their responsibilities. Work it out. Owen, London, UK


Mugabe was put into power 28 years ago, Jim from Memphis, longer than many readers' lifetimes. You cannot keep blaming western politicians for everything and absolving Mugabe of the consequences of every corrupt, greedy, short-sighted and disastrous decision he has made since. Or are you saying that Africans are so disadvantaged and helpless that they have no power to change their own destinies whatsoever? I would call such an assumption racist in the extreme. Emma, Cambridge,


Do not blame Mugabe for the chaos that Zimbabwe has become.

Blame instead the UK and US politicians, like President Carter who put him in power.

The first two paragraphs of the article say it all. Go back and reread them. This is what you have reduced a once-prosperous country to. Jim Burks, Memhpis, US / TN



The really difficult fact to face about the situation in Africa generally is that it is almost impossible to become
enthusiastic about the end of any particular tyrant, such as Mugabe, as the next one up will almost certainly be the same, if not worse. The poverty of Africa remains leadership. roy, Ankara, Turkey
 
Ningekuwa Mzimbabwe ningempa kura yangu Mugabe kwa mbwembwe zote bila kusita.
Ukiangalia kwa undani sana utaona matatizo ndani ya Zimbabwe yameanza pale tu mgogoro wa Ardhi ulivyoanza. Lakini kabla ya mgogoro huo Zimbabwe ilikuwa shwari na ilikuwa kipenzi kikubwa cha nchi za Magharibi.
Hapa inaonesha wazi kwamba nchi za magharibi zinaangalia masilahi yao zaidi kuliko masilahi ya wananchi wa nchi husika. Nasisi Waafrica kama hatutaamka na kufungua macho katika hilo basi tujue wazi kwamba bado hatuko huru kama tunavyodhani. Tulipigania uhuru hapo awali ili tuweze kuwa na mamalaka ya kuendesha nchi zetu bila ya kuingiliwa na nchi nyingine, ila tutashirikiana na nchi nyingine tutakazo taka kushirikiana nazo bila ya kushurutishwa na mtu ama hali fulani.

Tuwe makini sana na vyombo vya habari vya nchi za magharibi kwani vinapenda sana kupotosha na kupaka matope yale yaliyo mazuri katika Africa ili yaonekane mabaya na tuanze kuichukia Africa yetu. Na hapo ndipo hawa watu wa magharibi wanapopata mwanya wa kutugombanisha sisi wenyewe kwa wenyewe, huku wakituuzia silaha zao.
Nimefika Zimbabwe miezi mitatu iliyopita, hakuna njaa kama vyombo vya habari vya nchi za magharibi vinavyotangaza. Chakula kipo ila kama kawaida ni pesa yako ndiyo inayoweza kukuchagulia nini ule na kwa wakati gani kama sehemu yoyote ile Duniani. Kila nchi duniani kuna watu masikini na pia kuna sehemu ambazo zinakaliwa na watu wenye kipato cha chini. Vyombo vya habari vya nchi za magharibi mara nyingi sana vinapenda kuonesha ama kutangaza sehemu hizo mbaya na masikini, havipendi kuonesha sehemu nzuri na safi. Hayo ndiyo yanayotendeka huko Zimbabwe.
Zimbabwe inaweza kuwa na uhaba wa chakula kuliko Somalia na Sudani?, hamwoni kama hii yote ni propaganda ya hawa watu wa magharibi?
Mnafikiri kwanini nchi nyingi duniani na wala si Africa tu zina muunga mkono na kumtambua Mugabe?. Kwanini Nelson Mandela amekaa kimya kuhusu suala hili?, kwani lingekuwa baya linalohusisha ubaguzi mzee huyu asingeona haya hata kidogo kumwambia ukweli Mugabe.

Hii yote ni kampeni ya nchi za magharibi zikiongozwa na UK+USA kuichafua Zimbabwe na kumchafua Mugabe, huku zikijaribu kuwataka na wengine pia kufuata mkondo huo.

Kumbukeni tulitawaliwa kiasi cha kutosha, tulinyanyaswa kiasi cha kutosha na sasa ni wakati muafaka wa kukataa mambo hayo.


Mimi nasapoti kabisa kitendo cha Mugabe kugawa ardhi kwa kwa waafrika.Asilimia 80 ya ardhi katika nchi yoyote ile haiwezi kuwa chini ya minority 2 % ya population.Kwa wale ambao wanabisha angalia southafrika, land reform yao inaenda polepole sana,na mkisikia kunawaka moto msishangae.

Hata hivyo nafikiri Mugabe sasa inabidi apumzike.He has done the dirty work,and land reform is irreversible, lakini ni bora sasa hivi awaachiwe vijana kama simba makoni waendeleze pale alipoacha, hasa uchumi.
 
Hivi nani anaweza kuelezea kuanguka kiuchumi kwa Zimbabwe-kutoka ilivyokuwa chini ya wakoloni hadi walipopata uhuru na miaka michache baada ya uhuru na ilipo sasa bila ya kurudi kule kule kwa Waafrika Ndivyo Tulivyo? Yaani hawa Waafrika walipochukua madaraka wameichukua Zimbabwe kutoka moja ya nchi zenye uchumi mzuri Afrika na kuipeleka kuwa moja ya nchi vichekesho na sasa wameifikisha kuwa moja ya nchi zinazotia huruma duniani. Jamani nani anaweza kunieleza nikaelewa hii safari ya kinyume nyume?

Nyani:

Swali lako ni la msingi sana. Laiti kama tungepata jibu la swali hilo, tungeweza kuelewa ni kwa nini Zimbabwe ilivyo hivyo leo.

Mimi sina jibu, lakini ngoja nijaribu kutoa changamoto fupi, labda itatuelekeza kwenye wenye majibu.

Kwanza, chukua mfano wa Tanzania kabla ya Azimio la Arusha. Tunafahamishwa kuwa uchumi ulikuwa ni mzuri tokea 1961 na miaka iliyofuata. Tulikuwa na ushirikiano mzuri tu na mataifa yote ya kibepari - hususani watawala wetu Uingereza, Marekani na wengineo. Kutaifisha mali za mabepari, nia ikiwa ni kuwanufaisha raia walio wengi maskini hakukumpa Nyerere sifa; na tokea hapo inaelezwa kuwa uchumi wetu ulianza kuporomoka hadi leo hii.

Pili, angalia mfano wa Kenya. Wao hawakuwabughudhi mabepari - hasa hasa walowezi waliokuwa na mashamba makubwa ya Chai, wenye viwanda, makampuni ya utalii, mabenki, n.k; wengi wa hawa wakiwa ni raia wa Uingereza. Wananchi wachache, hasa waliokuwa kwenye siasa wakajichukulia ardhi nyingi iliyokuwa imerudishwa kwa kulipiwa na serikali ya Uingereza, (hii ni tofauti na yaliyotokea Zimbabwe). Kwa hiyo hapa hapakuwepo na matatizo tunayoyaona Zimbabwe leo. Kwa vile viongozi wa Kenya waliamua kufuata amri za wakubwa hukusikia na hutasikia kelele hizo kutoka Uingereza au Marekani. Hata hivyo, kuwaridhisha wakubwa bila ya kuwanufaisha wenye nchi, matokeo yake ni hayo tuliyoyaona juzi baada ya uchaguzi.

Tatu, Zimbabwe kabla ya mashamba ya wazungu kuchukuliwa, hapakuwa na matatizo makubwa kiuchumi, na wala Mugabe alikuwa haonekani kuwa shetani mkubwa, pamoja na kwamba hali ya wananchi wa kawaida ilikuwa siyo ya maendeleo makubwa. Ahadi zilitolewa kabla ya uhuru, kwamba Uingereza ingetoa pesa kulipia mashamba ambayo yangekuwa yananunuliwa toka kwa wazungu ili wananchi nao wapate ardhi. Uingereza hawakutimiza ahadi hii; na Mugabe akaamua kuanza kuwashughulikia. Hii ilikuwa ni ahadi ya wapiganaji wa ukombozi kwa wananchi wao, kwa hiyo ililazimu waitimize.
Mugabe alipofanya haya, akawa shetani.

Hitimisho:Naomba niazime msemo wako - 'Ndivyo Tulivyo.'
Naomba unielewe kwa nini nasema hivi, pamoja na kwamba sikubaliani na msemo huo:

1. Nyerere alipotaifisha viwanda na kujenga vingine vingi na vizuri tu: Mwatex, Mutex, Moshi Machine tool; Ubungo farm implements; Morogoro Canvas; Mang'ula Machine tool; Mbeya Paper; Urafiki Textiles; Twiga Cement; Tanga Fertilizer; Kioo; Tanga Cement, n.k.
Tazara ikajengwa, Kilimanjaro International Airport,n.k. Mmmmh niendelee mpaka wapi?
Ndivyo Tulivyo- nikiwa na maana ya kwamba baada ya Mugabe naye kuchukua mashamba ya wazungu, waliogawiwa mashamba hayo hawakuwa na uwezo wa kuyatumia kama hao walionyang'anywa, kwa sababu mbalimbali, baadhi yake zikiwa za 'Ndivyo Tulivyo," na baadhi ya sababu zikiwa nje ya uwezo wa Zimbabwe- kwa mfano kuhujumiwa na wakubwa ikiwa pamoja na kuwekewa vikwazo.

Nikirudi Kenya - kwa vile walioshikiria uchumi waliendelea kuwa wale wale, hapajatokea msukosuko kama Tanzania na Zimbabwe walivyo.

Ndivyo Tulivyo?- unataka kufanya majaribio Nyani? Mwambie Mbeki au Zuma awavuruge wazungu pale kwao leo hii, halafu tukutane miaka miwili ijayo tuelezane matokeo.

Matokeo tunayoyaona Zimbabwe na Tanzania, lakini sio Kenya wala Afrika Kusini - Yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na sisi wenyewe wananchi kwa (Uhujumu wetu? au kutokuwa na uwezo kuendesha mambo yetu, kama uchumi vizuri. Matatizo yanazidi kuwa makubwa tunapoanza kutumiwa kama mifano na hao wakubwa, huku wakitumia kila hila tuonekane kuwa hatuwezi.

Kenya wakianza kugusa maslahi ya wakubwa, tutakuwa nao pamoja.
 
Kalamu umeniacha hoi kichizi ndugu yangu...
Ndio bana nataka nifanye majaribio kama kweli ni Ndivyo Tulivyo au la...?

Hivi uchumi wa Afrika Kusini sasa hivi ukoje ukilinganisha na enzi za kabla ya utawala wa walio wengi?

Kinadharia tu...tuseme leo hii Mbeki anawatimua wazungu na kuwarudisha kwa Uholanzi au popote walipotokea...je Afrika Kusini itaendelea kuwa economic powerhouse?

Kati ya Afrika Kusini na Nigeria ni ipi yenye maliasili nyingi na ipi imeendelea kuliko nyenzake?

Na kuna mtu humu ndani anayeamini kuwa Afrika Kusini bila kuwepo na wazungu ingeendelea kama ilivyoendelea hivi sasa?
 
Mugabe385_309332a.jpg


masks_309794a.jpg

mm185x_309864a.jpg


Do you wanna fight?



Will Zimbabwe be free of Robert Mugabe? Stricken nation reaches polling day
 
SIGNIFICANT INROADS

He said Tsvangirai had made significant inroads in Mugabe's rural strongholds by leading in the southern province of Masvingo and Mashonaland Central Province, north of Harare, where the MDC has not won a parliamentary seat since 2000.

Tsvangirai's winning trend had also extended to Mugabe's home province of Mashonaland West, where the MDC had taken a rural parliamentary seat, said Biti. He said that in Zimbabwe's second city of Bulawayo, another opposition power base, Tsvangirai had a slight edge over former Finance Minister and ruling ZANU-PF official Simba Makoni -- also standing against Mugabe.

But Makoni, whose decision to run was seen by many analysts as a sign of increasing unease in ZANU-PF ranks, was leading in Zimbabwe's southwestern Matabeleland South Province.

The Zimbabwe Electoral Commission said it would start to announce official results later on Sunday. Final results are not expected for several days from the presidential, parliamentary and local polls. Observers from the Pan-African parliament said in a letter to the commission they had found more than 8,000 non-existent voters registered on empty land in a Harare onstituency.

Most international observers were banned and a team from the regional grouping, the Southern African Development Community (SADC), did not comment on Saturday. Critics say the SADC, which has tried to mediate over Zimbabwe, is too soft on Mugabe.

The powerful heads of the security forces have backed Mugabe, and voters said they had seen patrolling police and army units with armoured vehicles and water cannon. Some security chiefs say they will not accept a Tsvangirai victory but the opposition leader told reporters: "I am not seeking the security chiefs
mandate but the people's mandate."

If no candidate wins more than 51 percent of the vote, the election will go into a second round.

By the end of the day some results will come out.
 
Wana-JF,
Hatima ya Zimbabwe ipo mikononi mwa wananchi wa Zimbabwe wenyewe, wana haki ya kumchagua yeyote yule ambaye wanamtaka, hata kama ni Robert Gabriel Mugabe. Yanayotokea Zimbabwe chanzo chake wote tunakijua ni ubeberu wa nchi za Magharibi dhidi ya rasilimali za nchi ya Zimbabwe. Mugabe alikuwa amefikia mahali ambapo mikuki miwili imeelekezwa kwake. Mkuki wa kwanza alitakiwa akubaliane na matakwa ya nchi za magharibi au akatae na kutekeleza matakwa ya wananchi wake. Alichokifanya Mugabe ni kuwakatalia 'wakubwa' na kujali maslahi ya wananchi wake kwa kugawa ardhi iliyokuwa inamilikiwa na weupe wachache.

Namalizia kwa kusema kuwa 'kitanda usichokilalia huwezi kujua ubaya wa kunguni wake'.

Wazimbabwe kama Mugabe anawafaa, tafadhalini mrejesheni madarakani na nitawapongeza kwa hilo kwani haki yenu ya kidemokrasia kumchagua yeyote mnayemtaka bila ya kulazimishwa na nchi yeyote.
 
Kula tano za chapchap...
Kuanguka kwa Mugabe itakuwa ni ushindi wa hypocrisy za UK na Marekani.Watu wengi hawaangalii issue ya Zimbabwe from both sides.
Mugabe kabla hajagusa interests za UK( kwa kuwanyang'anya mashamba wazungu)aliitwa kiongozi safi na mtu ambaye anajua kuleta maendeleo nchini mwake.Ila tu alipothubutu kuchukua mashamba yale ndipo alipoanzwa kupachikwa kila aina ya majina na isitoshe UK na Marekani zikaanza kupeleka mabilion ya pesa kwa wapinzani ili kuungusha utawala wa Mugabe.


Kaka, ubaya wa Mugabe sasa hivi huko Zimbabwe hauhitaji kuhubiriwa na US au UK. Kila mzimbabwe anaujua isipokuwa aliye waziri wa serikali ya Mugabe na familia na ndugu zake wa karibu sana. Hebu jaribuni kuongea basi na hata wa Zimbabwe; piga simu kwa mtu yeyote ZImbabwe. Uzuri kupiga simu Zimbabwe ni very cheap.

Jamani, tutaacha lini kuwalaumu wazungu kwa matatizo yetu? Halafu hawa wazungu kwa nini wanakuwa wabaya tu pale wanapotukosoa lakini hatuachi kutega mikono yetu kwao? Haya mashamba aliyoyachukua Mugabe aliyapeleka wapi? Kwa nini uzalishaji ulishuka? Kwani hawa US na UK walienda huko wakawataza wananchi wasilime? Hawa US na UK ndio wamepeleka njaa Zimbabwe? Hivi, ni hawa US na UK wanaomwambia Mugabe awape waduasi wake tu mahindi na awanyime wale ambao wanampinga? Hivi ni US na UK waliowaambia wananchi wamchukie Mugabe? And, kwa nini ni Mugabe, ina maana hakuna mtu mwingine anayekubaliana na sera za chama chake na anayeweza kuzisimia zaidi yake? Kwa nini mtu mmoja aruhusiwe kuiharibu nchi nzima kwa kiasi kile kisa aliwanyang'anya wazungu mashamba? I mean, kwa nini hata sisi ambao tunafikiri ni kizazi kipya katika bara letu tunashindwa kukubali kuwajibika kwa kushindwa kwetu kutekeleza wajibu wetu?
 
Back
Top Bottom