Zamani watoto walitafuta wazazi wao waliowatelekeza, zama hizi wazazi ndiyo wanatafuta watoto wao

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
Kwema Wakuu!

Sikuwepo zamani sana. Lakini miaka ya tisini mpaka elfu mbili hivi ilikuwa kawaida Baba kumtelekeza mtoto au watoto huku akiacha maneno ya shombo, jeuri na kiburi. Kuwa akikua atanitafuta mwenyewe.

Na kweli zamani hizo niliona watoto wengi wakifanya hivyo, wakitafuta wazazi wao hasa kina baba waliowatelekeza.

Sababu zilikuwa nyingi lakini kubwa zaidi ni Mambo ya mali (urithi) na michango ya maisha pamoja na Baraka(Radhi) kwani iliaminika zamani hizo kuwa huwezi kufanikiwa bila baraka za wazazi (jambo ambalo ni uongo wa wazi).

Sasa kuanzia miaka ya 2010 mpaka hapa ninapoandika mambo yamegeuka sio kidogo.

Siku hizi Wazazi hasa Baba ndio wanaotafuta Watoto wao(waliowatelekeza) na watoto hawana habari kabisa na kuwatafuta wazazi wao.

Ile kasumba ya Wababa waliyokuwa nayo kuwa Mtoto akikua atamtafuta kwa sasa ni useless, yaani ukijichanganya umekwisha.

Watoto hawategemei tena urithi, watoto hawategemei tena michongo kutoka kwa wazazi wao. Watoto siku hizi hawategemei ule uongo wa kizamani kuwa ili ufanikiwe itakupasa upewe sijui baraka sijui radhi za wazazi.

Wapo watoto maelfu kwa maelfu duniani kote ambao hawana mahusiano mazuri na Baba na wazazi wao na wanamaisha mazuri kuliko wale wenye mahusiano mazuri. Hii inatoa picha kuwa kauli zile zilikuwa uongo.

Nami kama Mtibeli nasema, ukitelekeza utatekelezwa tuu. Ukifanya wajibu wako na watoto watafanya wajibu wao. Watoto wa kizazi hiki wamevurugwa sio Pouwa.

Tufanye wajibu wetu.
 
Usidanganyike!! Baba mzazi amebeba baraka kwa ajili ya wanawe!! Ukijiona umefanikiwa japo huna mahusiano mazuri na wazazi au umewatelekeza kwa makusudi ni kwamba arobaini zako ziko njiani zinakuja!! Kuna watu wana pesa lakini wanaishi maisha chini ya laana.

Magonjwa yasiyoponyeka!! hasara za mara kwa mara kwenye biashara! kudhulumiwa makazini au kwenye biashara, kuibiwa, watoto kukuasi pia, mahusiano mabaya kwenye ndoa na mambo mengine ya hovyo kukuandama.

Wanaokutazama wanaweza kudhani una raha na maisha mazuri lakini wewe mwenyewe unajua huna raha wala amani yoyote katika maisha yako!! Usicheze na wazazi!! Ukifanya hivyo usitafute mchawi!! wewe ndo mchawi wa maisha yako mwenyewe.
 
Zamani unatekelezwa alafu unaambiwa utanitafuta kwani utamfanya nini na ni mzazi wako?
Ni kweli miaka ya 90 kurudi nyuma, kule kwetu Moshi mali za urithi zilikuwa muhimu sana kwa watoto.

Na hata wazazi wengine walizaa watoto kulingana na uwepo wa eneo la kuwagawia.

Hata kwenye kuoa na kuolewa, msingi ni shamba la migomba kwamba binti asiende kuteseka njaa.

Watoto walikuwa wanawatafuta wazazi wao ili wapate urithi utakaowawezesha kuwa na msingi wa maisha.

Siku hizi, mahari anatafuta kijana wakati zamani wazazi ndiyo waliwajibika kutafutia vijana wenza, kutoa mahari na kusimamia show nzima ya ndoa.

Kijana wa sasa anawajibika kutafuta mali, mke wa kuoa, ajenge, na pia asaidie wazee.

Mambo yamebadilika!
 
Usidanganyike!! Baba mzazi amebeba baraka kwa ajili ya wanawe!! Ukijiona umefanikiwa japo huna mahusiano mazuri na wazazi au umewatelekeza kwa makusudi ni kwamba arobaini zako ziko njiani zinakuja!! Kuna watu wana pesa lakini wanaishi maisha chini ya laana!! magonjwa yasiyoponyeka!! hasara za mara kwa mara kwenye biashara! kudhulumiwa makazini au kwenye biashara, kuibiwa, watoto kukuasi pia, mahusiano mabaya kwenye ndoa na mambo mengine ya hovyo kukuandama!! Wanaokutazama wanaweza kudhani una raha na maisha mazuri lakini wewe mwenyewe unajua huna raha wala amani yoyote katika maisha yako!! Usicheze na wazazi!! Ukifanya hivyo usitafute mchawi!! wewe ndo mchawi wa maisha yako mwenyewe!!
Umenena vyema mkuu
 
Kwema Wakuu!

Sikuwepo zamani sana. Lakini miaka ya tisini mpaka elfu mbili hivi ilikuwa kawaida Baba kumtelekeza mtoto au watoto
Kizazi cha miaka ya 2000 ni kizazi ambacho hakina maadili.

Ni kizazi cha singel mothers 60%..

Hawajuwi umuhimu wa baba ktk family..

Dawa ni baba kutafuta pesa kwa bidii ili mtoto ajute yeye na mama yake single mother..
 
Usidanganyike!! Baba mzazi amebeba baraka kwa ajili ya wanawe!! Ukijiona umefanikiwa japo huna mahusiano mazuri na wazazi au umewatelekeza kwa makusudi ni kwamba arobaini zako ziko njiani zinakuja!! Kuna watu wana pesa lakini wanaishi maisha chini ya laana!! magonjwa yasiyoponyeka!! hasara za mara kwa mara kwenye biashara! kudhulumiwa makazini au kwenye biashara, kuibiwa, watoto kukuasi pia, mahusiano mabaya kwenye ndoa na mambo mengine ya hovyo kukuandama!! Wanaokutazama wanaweza kudhani una raha na maisha mazuri lakini wewe mwenyewe unajua huna raha wala amani yoyote katika maisha yako!! Usicheze na wazazi!! Ukifanya hivyo usitafute mchawi!! wewe ndo mchawi wa maisha yako mwenyewe!!
Acha vitisho weweee
 
Mimi ni wa zamani pia, mzee aliingia mitini tangu nikiwa kichanga, lakini hata siku moja sikuwahi kumuulizia licha ya mama kutaka kufanya juhudi nionane nae lakini moyo wangu haukuwa tayari, niliwahi kupewa simu siku moja nimsalimie ila sikufanikiwa kumaliza hata sekunde 30 kuzungumza nae.

Sijawahi kulishwa sumu juu yake ila ni vile tu nahisi nilishamtoa kwenye maisha yangu. Kwenye nyaraka zangu zote muhimu zinazohitaji taarifa za wazazi upande wa baba huwa naandika amefariki.

Hata nikisema nikutane nae katika umri huu huwa naona ni suala la kinafiki tu nitazungumza nae kitu gani??. Hakuna bond.
 
Mimi ni wa zamani pia, mzee aliingia mitini tangu nikiwa kichanga, lakini hata siku moja sikuwahi kumuulizia licha ya mama kutaka kufanya juhudi nionane nae lakini moyo wangu haukuwa tayari, niliwahi kupewa simu siku moja nimsalimie ila sikufanikiwa kumaliza hata sekunde 30 kuzungumza nae. Sijawahi kulishwa sumu juu yake ila ni vile tu nahisi nilishamtoa kwenye maisha yangu. Kwenye nyaraka zangu zote muhimu zinazohitaji taarifa za wazazi upande wa baba huwa naandika amefariki. Hata nikisema nikutane nae katika umri huu huwa naona ni suala la kinafiki tu nitazungumza nae kitu gani??. Hakuna bond.
Kweli ni baba ila shida ni bond..akija unaweza salimiana ukitoka nje ukirudi unahisi nipita njiaa tu kwasababu ule ukaribu since mdogo haupo..
 
Kizazi cha miaka ya 2000 ni kizazi ambacho hakina maadili.

Ni kizazi cha singel mothers 60%..

Hawajuwi umuhimu wa baba ktk family..

Dawa ni baba kutafuta pesa kwa bidii ili mtoto ajute yeye na mama yake single mother..

Kati ya Baba na Mtoto ni nani anapaswa kujua umuhimu wa mwenzake?

Ikiwa Baba katelekeza familia na hajui umuhimu wa familia na watoto iweje useme watoto hawajui umuhimu wa Baba?
Mtoto hajui kitu, vile unavyomlea ndivyo anavyokua.
 
Mimi ni wa zamani pia, mzee aliingia mitini tangu nikiwa kichanga, lakini hata siku moja sikuwahi kumuulizia licha ya mama kutaka kufanya juhudi nionane nae lakini moyo wangu haukuwa tayari, niliwahi kupewa simu siku moja nimsalimie ila sikufanikiwa kumaliza hata sekunde 30 kuzungumza nae. Sijawahi kulishwa sumu juu yake ila ni vile tu nahisi nilishamtoa kwenye maisha yangu. Kwenye nyaraka zangu zote muhimu zinazohitaji taarifa za wazazi upande wa baba huwa naandika amefariki. Hata nikisema nikutane nae katika umri huu huwa naona ni suala la kinafiki tu nitazungumza nae kitu gani??. Hakuna bond.

Bond ni kitu muhimu sana kwenye familia
 
zz
Kwema Wakuu!

Sikuwepo zamani sana. Lakini miaka ya tisini mpaka elfu mbili hivi ilikuwa kawaida Baba kumtelekeza mtoto au watoto huku akiacha maneno ya shombo, jeuri na kiburi. Kuwa akikua atanitafuta mwenyewe.

Na kweli zamani hizo niliona watoto wengi wakifanya hivyo, wakitafuta wazazi wao hasa kina baba waliowatelekeza.

Sababu zilikuwa nyingi lakini kubwa zaidi ni Mambo ya mali (urithi) na michango ya maisha pamoja na Baraka(Radhi) kwani iliaminika zamani hizo kuwa huwezi kufanikiwa bila baraka za wazazi( jambo ambalo ni uongo wa wazi).

Sasa kuanzia miaka ya 2010 mpaka hapa ninapoandika mambo yamegeuka sio kidogo.
Siku hizi Wazazi hasa Baba ndio wanaotafuta Watoto wao(waliowatelekeza) na watoto hawana habari kabisa na kuwatafuta wazazi wao.

Ile kasumba ya Wababa waliyokuwa nayo kuwa Mtoto akikua atamtafuta kwa sasa ni useless, yaani ukijichanganya umekwisha.

Watoto hawategemei tena urithi, watoto hawategemei tena michongo kutoka kwa wazazi wao. Watoto siku hizi hawategemei ule uongo wa kizamani kuwa ili ufanikiwe itakupasa upewe sijui baraka sijui radhi za wazazi.

Wapo watoto maelfu kwa maelfu duniani kote ambao hawana mahusiano mazuri na Baba na wazazi wao na wanamaisha mazuri kuliko wale wenye mahusiano mazuri. Hii inatoa picha kuwa kauli zile zilikuwa uongo.

Nami kama Mtibeli nasema, ukitelekeza utatekelezwa tuu. Ukifanya wajibu wako na watoto watafanya wajibu wao. Watoto wa kizazi hiki wamevurugwa sio Pouwa.

Tufanye wajibu wet
Chai
 
Back
Top Bottom