Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Hii ni kutokana na karatasi za wagombea kutokuwapo pia picha za wagombea haziko sawa zimechanganywa...

Utafanyika jumapili ijayo tena
 
Uchaguzi umeahirisha kulingana na mapungufu yaliyojitokeza kwenye makaratasi yakupigia kura. Source: Chanel Ten
 
Me nimeichinjia baharini MAGAMBA tayari kwishneiii
 
Kwa hapa ifakara zoezi limeanza SAA 2 kamili vituo vyote vifaa vimewasili kwa wakati. Amani imetawala, hakuna malalamiko. Kura zinapigwa kwa utulivu mkubwa
 
Ni huku Dodoma ccm wamemteka na kumsihi atangaze kujitoa... Hadi sasa amepatikana na amekana kujitoa kabisa..

Wananchi wamegoma kupiga kura hadi mgombea huyo awe huru na aje kupiga kura yake..

Ccm wameshindwa sasa wanahujumu... Ni ktk mtaa wa kisasa Dodoma... Ntawajuza zaidi
 
Siasa za upinzani zinanishangaza sana kiukweli. Ukiwa unashinda hapa Jf nakusoma yanayoendelea juu ya kuchukiwa CCM utadhani uchaguzi ukiitishwa kesho hakuna tena CCM. Lakini ukipita huko mtaani watanzania hawana wanachojua zaidi ya CCM. Nimepita sehemu majuzi nikiwa tanga mjini watu/wanawake ndio wanajadiliana wanasema nasikia kuna chama kipya chaitwa UKAWA kimeunganisha CUF na CDM. Sasa huyu akienda kwenye sanduku la kura asipoikuta UKAWA ataichagua nini kama si CCM?

Brother, Tanga, Pwani na Morogoro ni misukule ya ccm hawana wanalolijua zaidi ya ccm hivyo usishangae.
 
hapa wilayani kwetu vifaa vimechelewa na uchaguzi umechelewa lakini mpaka sasa 50% ya raia wameishapiga kura
 
Inakuwaje baadhi ya vituo vingi vya kupigia kura hapa muheza hata karatasi za kupiga kura hazijafika mpaka sasa hivi? Watu hata hawajaanza kupiga kura, au ccm nd wanataka wawapigie watu kura.!! Inashangaza, vituo vimefunguliwa sa 1.30 ila hakuna vitendea kazi
 
Mtaani kwetu Kiseke PPF Mwanza nimeshawafuta CCM mim na jiranizangu wote tupatao 18! Vijana niwengi kweli kwenye foleni. RIP ccm
 
Hivi sasa amelazwa hospitali ya wilaya... Anadai amepigwa na wanna ccm wakati wakimpiga walikuwa wakimwambia kuwa kwanini amegombea na anawapeleka ligi?

Ccm wameshindwa ustaarabu wana apply ubabe hili..... Kutakucha
 
kwa kwel serikali ya ccm ni majizi na mashetani ya kutupwa hapa ruaha kilombero hali si nzuri maana majina ya wagombea yamekosewa na kinachoshangaza ni majina ya wagombea wa chadema tu ndo yamekosewa wa ccm yapo sawa wameweka watu ambao wanawajua wao wale ambao ndo walpitishwa na chama wamewatoa hii nchi sijui inakwenda wapi
 
Unaweza kusema CCM inalazimisha mapenzi kwa wananchi. Wananchi wameichoka. Wananchi hawaipendi CCM. Leo nimefika katika kituo changu nilichojiandikishia kupiga kura hapa jijini Mbeya, nikiwa na hamu kabisa ya kutumia haki ya msingi kumchagua kiongozi nimtakaye. Mbali na mimi niliwakuta pia wananchi wengine waliokuwa kituoni kwa lengo hilo hilo. Cha ajabu na cha kusikitisha tunaambiwa hakuna kupiga kura, kisa mgombea wa CCM amepita bila kupingwa. Kwamba mgombea wa UKAWA alienguliwa katika hatua za mwishoni kwa kutokutimiza taratibu za wagombea. Wananchi tukasema basi tumpigie kura huyo huyo wa CCM kuonesha kama tunamtaka yeye au la, wasimamizi wakasema kanuni haziruhusu kufanya hivyo! Tunajua hizo ni hila za CCM kuengua wagombea wa vyama vinavyounda ukawa kiujanja ujanja lakini naomba niwaambie kuwa kufanya hivyo ni sawa na kulazimisha mapenzi kwa wananchi! Kufanya hivyo ni sawa na mwanaume kulazimisha mapenzi kwa mwanamke ilihali hakutaki au kinyume chake! Naomba CCM wajue kuwa wakati wa kuongoza watapata shida kwani watakuwa wanaongoza wananchi wasiowapenda!
 
ukisikia eneo hakuna uchaguzi watu wamepita bila kupingwa ni jambo la kusikitisha sana wenyeji wajiulize wao ni jamii ya namna gani .Iliyofika tayari kwenye nchi ya mmaziwa na asali? ni fedheha .singepend hata kuishi katika jamii hiyo
 
Back
Top Bottom