Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Nipo hapa Mbeya, kada wa chama tawala. Hata hivyo pita pita ya ngu mitaani hadi kule Rungwe nimejionea mwenyewe hali ilivyo tete kwa CCM.

Ni kama CHADEMA wao wamejitayarisha vizuri, na wapo kila mahala. Huu si oungo ,maana wameteka vijana wengi na bendera hasa Ile pana ziko kila mahala.

Jana niliona magari kadhaa ya matangazo na uhamasishaji ya CHADEMA, lakini sikubahatika kuona hata moja la CCM.

Nimefika Kiwira ndo balaa! Mchana vijana walifunga barabara kwa mdundiko uliokuwa ukiongozwa na gari ya matangazo ya CDM!

CCM najionea huruma lakini tusubiri tu.
Mkuu twa masiku!
 
Mwanza:- mtaa wa mwembeni Chadema imeshinda nafas zote yaani uenyekit na ujumbe.

Mtaa wa Utemini:- Ndugu Hamza Yusuph Shido (cuf) UKAWA kashinda wajumbe wake sijapata matokeo yao.

N.B kwa waliopo Mwanza mnaweza kutune 90.2 City fm inatoa matokeo live.
 
Hapa Kijiji cha Ongoma Kata ya Uru Kaskazini Mkoani Kilimanjaro Mgombea wa Chadema ameshinda kwa kura 500 zidi ya 200 za CCM na ikumbukwe kijiji hichi kilikuwa Ngome ya CCM.
 
viva ukawa. Viva chadema morogoro kata ya kilakala chadema tumeshinda mitaa 3

haaaaaa morogoro?? Morogoro-kilakala, hoingereni sanaaa , hongereni sana... Mabadiliko yanawezekana, ila chadema moro iongeze nguvu, watu wa morogoro ni wagumu sanaaa...na hasa ni uduni wa elimu, waruguru kwao elimu si kipaumbele, lakini hongereni sanaaa...
 
UPDATES MATOKEO MAENEO MBALIMBALI,
Mtaa wa Msewe, Ubungo
CCM 356,
CHADEMA 683

Mtaa wa Mjini, Karatu
CCM 109
CHADEMA 281
Mtaa wa TFA, Karatu
CCM 179
CHADEMA 358.
Mwenye matokeo zaidi aweke hapa.!!
CHANGE ni mimi, ni wewe, ni sisi.. TUNAWEZA!

Asaaaaaaaante UKAWA-tumaini letu
 
Mtaa wa Lake Tanganyika katika kituo cha Jihad manispaa ya Kigoma Ujiji Chadema wakutwa wakigawa rushwa ya 5000 5000 kwa wapiga kura ili waichague CCM na waikatee ACT-TANZANIA inasikitisha sana ukawa hii mpya kuibukia Kigoma
Mwana mjaa laana wewe!
 
hvi hawa watu wa UKWAMA wanavutaga bangi kwanza au viroba ndo wanakuja Jf. ebu angalia post kama hii.
"hapa tunasubiri matokeo,mgombea wa cdm anaelekea kushinda" sasa kwa nini asubiri si aende akalale anajua "mshindi" wao.
NGOJA MATOKEO YA JUMLA YAJE WAANZE VISINGIZIO.
 
Hongereni Ukawa nguvu yenu imeonekana hapa ni kazi moja tu mpaka 2015 mpaka ccm wahamie uvunguni mwa meza
 
Mwanza mtaa wa pasiansi mashariki A:- ccm 335
Chadema :- 211 na wajumbe wote ccm imechukua.
 
Back
Top Bottom