Wito kwa Askari Polisi Barabarani tunaomba yule Dereva wa gari ya Simba SC anyang'anywe leseni yake

Kaka Yaoh

Senior Member
Sep 23, 2021
188
353
Habari yako kamanda mkuu wa Barabarani, Kuna video inasambaa ikionesha basi ambalo moja kwa moja linaonekana ni la timu ya Simba SC likiendeshwa kinyumenyume katika barabara kuu hapo Dar es salaam.

Mara tu baada ya kuona video hiyo nikiwa kama msamaria mwema katika nchi hii nimeamua nitoe taarifa kwako hili hatua kali zichukuliwe kwamaana hule sio uendeshaji sahihi alafu kinachouma zaidi askari wa barabarani nao wamelikalia kimya na kufumbia macho uzembe hule.

Nikiwa kama mtanzania na mmoja kati ya wananchi wachache ambao tunamiliki magari na Leseni ya uendeshaji wake nakemea na kukerwa sana na namna ya lile basi lilivyoendeshwa.

Natumaini Kamanda Mkuu wa kikosi cha Barabarani wewe ni msikivu na kwenye hili utalichukulia hatua kama zifuatazo:

(I) Kumfutia Leseni dereva yule pamoja na chuo alichosomea udereva wa kuendesha basi kwa namna hile.

(ii) Klabu ya Simba SC kupigwa faini ya kiwango kikubwa hili hiwe funzo kwa wamiliki wa mabasi wasirudie tena kosa kama Hilo maana kule ni kuhatarisha usalama wa abiria.

(ii) Abiria waliokuwepo ndani ya basi lile wakusanywe kwa pamoja na kupewa elimu juu ya usalama wao barabarani na nini wafanye mara tu waonapo usalama wao unahatarishwa.
Asante sana.

NB; Modes najua mnakawaida ya kuzifutaga mabandiko yangu na kwa kiukweli mnaibaka haki yangu ya kama mwanaJF kuleta hoja zangu humu ombi langu naombeni kabla hamjaufuta tena hili bandiko nitumieni ata meseji PM nione sababu za kuufuta, Asanteni sana.
 
Hii siyo kweli,kwanza basi la Simba kwa sasa sio linaloonekana kwenye hiyo video
 
Back
Top Bottom