Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 60
- 1,237
Je ni sahihi wananchi kujichukulia sheria mkononi wakamuua RPC wa Arusha? Kama sio sahihi basi tunataka kuona askari wa usalama barabarani Arusha waliojichukulia sheria mkononi kwa kumuua Omari Msamo wanafikishwa mahakamani. Huu ujinga wa polisi kujiona wako juu ya sheria na wanaweza kufanya chochote ukomeshwe sasa.
Sisi kama wadau wa haki na utawala wa sheria tutaanza kuchukua hatua ambazo tutaona zitaleta uwajibikaji kwa RPC wa Arusha na askari waliohusika na mauwaji hao. Tumepata taarifa ambazo bado tunazifanyia kazi kwamba RPC wa Arusha na maafisa wengine wanafanya juhudi za kuzima jambo hili ili lisijulikane.
Haya matukio ya watu kufia mikononi mwa polisi yamekuwa mengi. Huu ni uthibitisho kwamba askari wengi ndani ya jeshi la polisi wanatumia nguvu nyingi kuliko akili. Pengine tatizo hili linatokana na mafunzo ambayo hayakidhi vigezo na wala hayaendani na wakati kipindi hiki ambacho technology inakua kwa kasi. Ndio maana tangu mwanzo nasisitiza kuwa hili jeshi limekosa sifa za kulinda raia na mali zao, hivyo kuna ulazima wa kulifanyia Overhaul .
Nitaelekea Arusha kuhakikisha haya mabumunda yanachukuliwa hatua haraka sana.
Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Pia soma - Arusha: Polisi wawakamata Waliohusika na Mauaji ya Dereva wa magari ya Watalii Omari Msamo
Sisi kama wadau wa haki na utawala wa sheria tutaanza kuchukua hatua ambazo tutaona zitaleta uwajibikaji kwa RPC wa Arusha na askari waliohusika na mauwaji hao. Tumepata taarifa ambazo bado tunazifanyia kazi kwamba RPC wa Arusha na maafisa wengine wanafanya juhudi za kuzima jambo hili ili lisijulikane.
Haya matukio ya watu kufia mikononi mwa polisi yamekuwa mengi. Huu ni uthibitisho kwamba askari wengi ndani ya jeshi la polisi wanatumia nguvu nyingi kuliko akili. Pengine tatizo hili linatokana na mafunzo ambayo hayakidhi vigezo na wala hayaendani na wakati kipindi hiki ambacho technology inakua kwa kasi. Ndio maana tangu mwanzo nasisitiza kuwa hili jeshi limekosa sifa za kulinda raia na mali zao, hivyo kuna ulazima wa kulifanyia Overhaul .
Nitaelekea Arusha kuhakikisha haya mabumunda yanachukuliwa hatua haraka sana.
Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Pia soma - Arusha: Polisi wawakamata Waliohusika na Mauaji ya Dereva wa magari ya Watalii Omari Msamo