Babes;
Sijasoma report ya hii study lakini kwa ninavyoelewa, Serikali+wadau kupitia mashirika/mipango kama NASHCoP/TACAIDS etc wanakuwaga na afua mbalimbali ambazo huwa kuna aspect ya kutambua makundi maalumu/makundi ambayo yako vulnerable kulingana na intervention husika.
Makundi hayo hutambuliwa ili wasaidiwe katika changamoto zao (hapa naomba tusiende deep sana) Sasa katika utambuzi huo ndio hupatikana takwimu yao. Hii data nadhani imetokana na utayari wa respondents ndio maana watu wanashangaa iweje TMK iwe na takwimu ya juu kuliko kinondoni ambapo kiuhalisia wote tunaona Kino wanaupiga mwingi? Kwahiyo yawezekana Temeke hao KVP’s ndio wamerespond zaidi, wameonesha ushirikiano na pengine wamekuwa mbele kama “beneficiaries ” wa afua husika (utilization ya aspect za afua husika)
Naelewa Ubishani uliopo kwenye hii mada ni kuhusu actual prevalence vs recorded prevalence na hii haimaanishi kuwa TMK data imepikwa. Possible reasons za disperancy kati ya TMK na Kinondoni inaelezeka.
Kwenye interventions kama hizi inategemea zaidi na utayari wa respondents sababu ni mambo nyeti huwezi kwenda kuwaswaga watu watoke majumbani mwao waje wakupe ushirikiano. Na ndio maana “labda” kwa necha ya watu wa Kinondoni (wanajiweza) au wako rigid(wanajua) data yao haijapatikana kwa ukubwa.
Sasa kwenye reporting huwezi kuanza kujitungia tu kuwa kiuhalisia Kinondoni ndio kuna mashoga wengi kuliko TMK, utareport kile ambacho data yako imekupa.
Strategist7 Hello.