'Who created God' is an Illogical Question!

'Who created God' is an Illogical Question!

Usikwepe kujibu swali.Thibitisha ubaya uko vipi.Kwa nyenzo unayoiamini.
Wewe hujui hata uliposimamia.

Hata Quran huiamini wakati unasema ni Muislamu.

Ungekuwa unaamini Quran usingetaka uthibitisho kama kuna maovu.
 
The bible is full of contradictions. Why do you believe it is the word of God?
naona unahamisha goli. jibu kwa sababu all those statements are scientiffically correct. mbona unatoa majibu mepesi. rudi kwenye mtiririko if not God give me your assumptions. bible has never contradicted itself though it may look so according to your current knowledge . Jibu hoja kwa mtiririko urihamehame mkuu.
 
Kwa muislamu sio lazima aseme anaamini Qur'an,matendo yake ndio yatakayoambatana na kusema kama anaamini vitabu vya Mungu vyote.
Wewe matendo yako hayaoneshi kwamba unaamini Quran.

Unaomba uthibitisho kama mabaya yapo duniani wakati yameelezwa yapo katika Quran unayosema unaiamini.

Kwa nini unaomba uthibitisho wa kitu ambacho kimeelezwa katika kitabu chako mwenyewe cha dini?

Ina maana humuamini Mungu wako mwenyewe? Unataka mimi nithibitishe ubaya upo duniani wakati Mungu wako kasema hivyo katika Quran?

Huamini Quran?

Hivi unaelewa kama unaenda au unarudi wewe?

Unaamini Mungu yupo au huamini?

Unaamini Quran au huamini?
 
naona unahamisha goli. jibu kwa sababu all those statements are scientiffically correct. mbona unatoa majibu mepesi. rudi kwenye mtiririko if not God give me your assumptions. bible has never contradicted itself though it may look so according to your current knowledge . Jibu hoja kwa mtiririko urihamehame mkuu.
Halafu aseme kwa nini contradiction au lies ni vitu vibaya. Naona karuka kama hajaona vile 🙂
 
Hivi unanielewa lakin??? Binadamu akimfanyia jambo baya binadamu mwenzake ni kwamba anapata dhambi...ila kuku akifanya mabaya kwa kuku mwenzake huu utaratibu haiko applied kwao wala kwa viumbe vingine??? Je ni kwamba viumbe hivyo haviumii?? Havina nervous system??? Je kuna consistency...?? Mkiulizwa mnadai mnatumia akili za kufikiria sasa mimi na wewe tukiwa hatufikiri tungekuwa na tofauti gani na mtoto mchanga. Kuna vitu viwili kwenye maisha ya binadamu ni very powerful navyo ni arithmetic nd logic... mtu anaepossess vitu hivyo kwa kiwango cha juu zaidi.... he/she must be genius. it whether u tell a lie or truth.... any statement u made it either ni kweli au si kweli (this is what we call logic). Whatever u compute either kwa kukuambia nimezaliwa mwaka gani then ukaderive my age au nimekukopa kiasi cha sh 100k nikarejesha 80k...ili uweze kujua kilichosalia basi hapo una apply kitu kinaitwa mahesabu(arithmetic). Do u see how strong those two attributes are???
Hapo nakuachiwa swali najua nimeshakuuliza mengi hapo juu, mfano mtu amekupa statement ambayo kwa kutumia reasoning yako umeshindwa kujua kama ni kweli au si kweli nd u have to make decision. mfano unamwambia mtu ambae hajawahi kuiona bahari kwamba asilimia 75 ya dunia yetu ni maji, je akuamini kwa kumwambia tu au afanyeje ili ajue umesema ukweli?? Maendeleo ya kiteknolojia unayoyaona sasa yametokana na tafiti na zilikuwa na base ambayo ni vitabu vya dini.... mfano wale waliosema dunia iko stationary at the center na vingine vyote including jua vinaizunguka. Kama watu wangetuliza pumb* zao chini alafu wakawa na hoja kama za kwako ukweli ungeonekana ni huo kwa vile ukiwa hapa duniani hivyo ndivyo inavyoonekana....
Tunarudi kulekule unajuaje kuwa kuku akimfanyia ubaya mwenzake hapati dhambi? Dhambi ni nini?

Kwa nini unapenda kuwafanya watu special kiasi hicho? Ushawahi kuingia ndani ya akili za kuku na kujua wanachofikiri?
 
Kiranga huna uthbitisho wa ubaya,unajigonga.Unapoambiwa utoe uthibitisho,utoe uthibitisho,usio utoe maelezo.
 
Kiranga huna uthbitisho wa ubaya,unajigonga.Unapoambiwa utoe uthibitisho,utoe uthibitisho,usio utoe maelezo.
Ni aina gani ya ubaya ulikuwa unautaka akutajie ... Nadhani kiranga alikuwa akimaanisha mambo kama vimbunga vinavyoua watu, matetemeko,Ugonjwa n.k
 
Ni aina gani ya ubaya ulikuwa unautaka akutajie ... Nadhani kiranga alikuwa akimaanisha mambo kama vimbunga vinavyoua watu, matetemeko,Ugonjwa n.k
Amethibitisha vipi kama ni vitu vibaya ,kwa nyenzo anazoamini yeye au wewe.
 
Kwa nini Mungu mwenye uwezo wote aumbe ulimwengu uliyo na imperfections?

Kama Mungu yupo kwa nini umtetee wewe na siyo ajitete mwenyewe?
Kama mambo hayapo kama tutakavyo ndiyo tusema hakuna mungu?
 
Kama mambo hayapo kama tutakavyo ndiyo tusema hakuna mungu?
Kama Mungu ni mkamilifu mbona kaumba vitu visivyo kamilifu?

Ina maana hakuna Mungu mkamilifu anayeweza kuumba vitu kwa ukamilifu.
 
Hiki unachoeleza unauhakika kuwa ndio ukweli halisi na siyo mawazo yako?

Je wafia dini wengine wakiulizwa swali hili watatoa jibu kama la kwako ama watafikiria jibu lingine?
hiyo ni kazi yako kuchakata. sikujibu ili niwe na usambamba wa maoni na unaowaita wafiadini, wala sikujibu ili uje umuamini Mungu hiyo ni kazi yako kuchagua mimi sihusiki.
 
Kama Mungu ni mkamilifu mbona kaumba vitu visivyo kamilifu?

Ina maana hakuna Mungu mkamilifu anayeweza kuumba vitu kwa ukamilifu.
Kwanza hivyo vitu ambavyo sio vikamilifu ni vp ambavyo vimeumbwa?

Halafu nieleze mahusiani ya hivyo na kutokuwepo kwa mungu.
 
Sikubaliani na hitimisho lako wala flow ya arguments.
Hilo swali sio kweli halina mantinki (illogical) bali halina maana (meaningless) na mfu (self-defeating).
Katika kuuliza swali hilo kuna dhahania (assumptions) ndani yake kuwa kila kilichopo kinapaswa kuumbwa. Hii ni dhahania ambayo sio kweli kwa sababu hakuna mahali imethibitishwa kuwa ni kweli kuwa kila kilichopo kimeumbwa au kimetoka mahali. Kwa sababu dhahania husika haina mashiko basi hata swali lenyewe halina maana kabisa. na hivyo halihitaji majibu yeyote. Pili ni self-defeating kwa sababu wanaouliza huwa wana dhahania nyingine nyuma yake kuwa kila kilicho kweli lazima kiambatane na ushahidi. Lakini dhahania yao hii kuwa "kila kilicho kweli lazima kiambatane na ushahidi" haina ushahidi popote na hivyo kulifanya swali zima liwe mfu. kwa maana rahisi kama unasema "kila kilicho kweli lazima kiambatane na ushahidi" halafu hautoi ushahidi kuwa kila kilicho kweli lazima kiambatane na ushahidi basi unanipa fursa ya mimi kusema chochote bila ushahidi na kikawa sawia bila mawaa!
.
Hapana, swali lake lina mantiki, hata kama hajajieleza kimantiki. Katika metaphysics tunaulizana: Is God Omnitemporal or atemporal? Huu ndio msingi wa swali lake. Mjadala sasa uendelee.

Kuhusu ukweli, unachoongelea ni “first principles of logic” kwa mfano, “no statement can be true and false”. Mbali na hizo kanuni, kauli nyingine zote zinahitaji ushahidi. Katika philosophy, “God is an uncause D cause” sio self-evident.

Mjadala uendelee.
 
Kama Mungu ni mkamilifu mbona kaumba vitu visivyo kamilifu?
Kwa nini ni vibaya vitu kutokuwa vikamilifu?

Ina maana hakuna Mungu mkamilifu anayeweza kuumba vitu kwa ukamilifu.
Kipimo chako cha ukamilifu ni nini?
1. Kama ni akili yako Je yenyewe ni kamilifu?
2. Kama ni maandiko ya/watu wengine, je wao ni wakamilifu?

Ukamilifu ukoje? na unaupimaje?
 
hiyo ni kazi yako kuchakata. sikujibu ili niwe na usambamba wa maoni na unaowaita wafiadini, wala sikujibu ili uje umuamini Mungu hiyo ni kazi yako kuchagua mimi sihusiki.
Sasa huoni kuwa kuna hatari ya kuababudu na kuamini mawazo ya fikra zako nikisema ni Mungu?

Wewe umewahi kumuona, kumhisi, kumshika au kumsikia Mungu physically au unafuata fikra za watu wa kale zenye kukinzana kwenye kitabu kinachodaiwa kuwa cha Mungu?
 
Kwanza hivyo vitu ambavyo sio vikamilifu ni vp ambavyo vimeumbwa?

Halafu nieleze mahusiani ya hivyo na kutokuwepo kwa mungu.
Dunia siyo well designed na ndio maana kuna majanga asilia. Kwa hiyo hakuna Intelligent designer mnayedhania yupo.

Kwenye miili ya viumbe hai kuna -ve mutation zenye kusababisha matatizo kibao, hivyo sii kweli watu waliumbwa na Intelligent designer mnayedai yupo.
 
Lakini habari zenye contradiction hazipo logical. Habari kama kuna Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote ambaye kaumba ulimwengu huu ambao mabaya yanawezekana wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani kufanyika ina contradiction. Kwa nini Mungu huyu kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa nanuwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani? Je, alitaka kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani akashindwa? Kama ni hivyo, je, no kweli anaweza yote? Ama aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani ila hakuamua tu kuumba ulimwengu huo? Kama ni hivyo kweli ana upendo wote? Mbona Mungu huyu ana contradictions? Yupo at all? Au ni stories tu zilizotungwa na hayupo?
.
Umejieleza vema.
 
Back
Top Bottom