Lakini habari zenye contradiction hazipo logical. Habari kama kuna Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote ambaye kaumba ulimwengu huu ambao mabaya yanawezekana wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani kufanyika ina contradiction. Kwa nini Mungu huyu kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa nanuwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani? Je, alitaka kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani akashindwa? Kama ni hivyo, je, no kweli anaweza yote? Ama aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani ila hakuamua tu kuumba ulimwengu huo? Kama ni hivyo kweli ana upendo wote? Mbona Mungu huyu ana contradictions? Yupo at all? Au ni stories tu zilizotungwa na hayupo?