Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

Kwa wale waelewa...Vikwazo vya magharibi vina nia hizi pamoja na nyinginezo...
1)Kuitenga serikali na wananchi kwa kuwasababishia maisha magumu
2)Kuidhoofisha serikali husika ili iwe rahisi kuwavamia!
 
Sio kweli kwamba Mugabe anataka kushindana na Wazungu, au anaamini hali ya Zimbabe inatokana na nguvu za nje. Hana hiyo dhati.

Anachofanya Mugabe ni sawa na Osama bin Laden anaposema ujasusi ni juhudi za kutetea Uislamu unaotishiwa na Wamagharibi ikiongozwa na US. Hiyo inamsaidia kupata sapoti ya wapenda Uislamu, na wachukia ukoloni mamboleo wa US na siasa zao za kibeberu (imperialism). Kama unachukia ubeberu, na ukoloni mamboleo na pia ni mpenda Uislamu unaweza kujikuta unajiunga na kambi yake ya mafunzo, kumbe ukweli ni kwamba mzizi wa fitina haswa ni bifu yake na watu wa kwao huko Uarabuni ambao walikataa mawazo yake fulani fulani miaka kibao iliyopita.

Anachofanya Mugabe kunyooshea kidole Magharibi ni pretext kama hiyo hiyo ya kumsaidia kupata hurumu ya wote tusiopenda Ukoloni mambo leo na ubeberu wa Wamagharibi. Ni usanii wa kisiasa.


Hiki ni kichekesho. Ina maana Mugabe anafurahia kuongoza nchi iliyo na matatizo ya kiuchumi? Inamaana akina Mbeki, Mkapa na wengine ni wajinga kumkingia kifua Mugabe kwa vile tu analia waingereza-waingereza-waingereza? Naona mkuu stori za vyombo vya magharibi zimekushiba sana.
 
Mimi nawapa changamoto wale wote mnaobisha kuwa Waafrika Ndivyo Tulivyo kunionyesha mifano ya Sivyo Tulivyo na nitatoa ya kwangu ya Ndivyo Tulivyo ili kulinganisha lipi ni zaidi. Nawahakikishia mkinionyesha mifano kumi ya Sivyo Tulivyo mimi nitawaonyesha mifano 10,000 ya Ndivyo Tulivyo. Haya kazi kwenu......let's go for it.

Ngabu,

Mimi nakubaliana nawe kuwa waafrika ndivyo tulivyo. Watu kama Mugabe ndio wanathibitisha kabisa hili.
 
Hiki ni kichekesho. Ina maana Mugabe anafurahia kuongoza nchi iliyo na matatizo ya kiuchumi? Inamaana akina Mbeki, Mkapa na wengine ni wajinga kumkingia kifua Mugabe kwa vile tu analia waingereza-waingereza-waingereza? Naona mkuu stori za vyombo vya magharibi zimekushiba sana.

Kwani wewe mpaka leo hujajua kwamba Mbeki na Mkapa ni wajinga sana kuendelea kufumbia macho matatizo yaliyo wazi kwa sababu za uswahiba? Ndio wenzake ANC wamemtimua na anahesabu siku tu akapumzike.
 
Hiki ni kichekesho. Ina maana Mugabe anafurahia kuongoza nchi iliyo na matatizo ya kiuchumi? Inamaana akina Mbeki, Mkapa na wengine ni wajinga kumkingia kifua Mugabe kwa vile tu analia waingereza-waingereza-waingereza? Naona mkuu stori za vyombo vya magharibi zimekushiba sana.

Na hiki nacho ni kichekesho.

Mugabe angekuwa hapendi kuona moto wa kiuchumi unaowakuta Wananchi wake angeendeleza uhuni uliopelekea Zimbabwe kuwa mafukara wa kuchapwa viboko wasio na mfano?

Mbeki -anaeiambia Africa kwamba AIDS hailetwi na HIV ila ni Wazungu wanatuongopea- na Mkapa - ambae wakati anajaza fomu za kuandikisha kampuni alipokutana na swali "mahala pa biashara," akajaza "Ikulu," hao watu unaweza kuwatumia kama mifano ya watu waliotulia vichwani hao?

Nikiogopa kukemea uhuni wa utawala wa Zimbabwe eti kwa vile Mbeki na Mugabe wataniita kibaraka wa Magharibi nitakuwa nimekubali waninyweshe maji yao ya sharbati. Mugabe ni fidhuli.
 
Na hiki nacho ni kichekesho.

Mugabe angekuwa hapendi kuona moto wa kiuchumi unaowakuta Wananchi wake angeendeleza uhuni uliopelekea Zimbabwe kuwa mafukara wa kuchapwa viboko wasio na mfano?

Mbeki -anaeiambia Africa kwamba AIDS hailetwi na HIV ila ni Wazungu wanatuongopea- na Mkapa - ambae wakati anajaza fomu za kuandikisha kampuni alipokutana na swali "mahala pa biashara," akajaza "Ikulu," hao watu unaweza kuwatumia kama mifano ya watu waliotulia vichwani hao?

Nikiogopa kukemea uhuni wa utawala wa Zimbabwe eti kwa vile Mbeki na Mugabe wataniita kibaraka wa Magharibi nitakuwa nimekubali waninyweshe maji yao ya sharbati. Mugabe ni fidhuli.


Kwa Taarifa yako ni kuwa, Zimbabwe kuna hyper-inflation tu lakini sio kweli kuwa watu wake ni fukara kupindukia. Standard of living ya Zimbabwe bado iko juu sana na inashinda hata baadhi ya maeneo mengi ya TZ. Tatizo ni ukosefu tu wa bidhaa kutokana na kutokuwa na forex. Usidhani kuwa wako kama Congo au Somalia, nenda ukajionee mwenyewe. Zimbabwe sio mbali na bongo.

Kumkingia Mugabe kifua haina maana kuwa tunakubaliana na yote anayofanya, bali hatuwezi kukubali kutumiwa na hao weupe kuwakandamiza waZimbabwe kwa vile tu wamechukua ardhi yao.
 
Kwani wewe mpaka leo hujajua kwamba Mbeki na Mkapa ni wajinga sana kuendelea kufumbia macho matatizo yaliyo wazi kwa sababu za uswahiba? Ndio wenzake ANC wamemtimua na anahesabu siku tu akapumzike.

Sio kweli kuwa wamefumbia macho, in contrast ni kuwa wameyahangaikia sana lakini kwa vile MDC instruction zao zinatokea UK n.k., inakuwa vigumu kufikia compromise ya kiafrika ambayo inajumlisha kusameheana. Waingereza wanachotaka ni kichwa tu cha Mugabe kama ilivyokuwa kwa Sadaam na Millosevic.
 
Sio kweli kuwa wamefumbia macho, in contrast ni kuwa wameyahangaikia sana lakini kwa vile MDC instruction zao zinatokea UK n.k., inakuwa vigumu kufikia compromise ya kiafrika ambayo inajumlisha kusameheana. Waingereza wanachotaka ni kichwa tu cha Mugabe kama ilivyokuwa kwa Sadaam na Millosevic.

...you're out of touch!
 
I used to like Mugabe then................but now.......nooo........
Hivi karibuni nilikuwako harare kwa muda wa wiki moja, anayesema hali ya maisha ya Wazimbabwe ni nafuu.......he/she is out of touch kabisaaa........in short hali ni mbaya sana......its not that Zim ya wakati ule wa miaka mid 80s and early 90s that i visited.

Unyama unaofanywa na Mugabe na kundi lake uko wazi mno....nashangaa hapa watu wanaomtetea huyu Babu
 
Thursday 26, 2008

Addressing a campaign rally in Chitungwiza, south of Harare, Mugabe said: "We have some of our brothers in Africa making that call (to postpone the vote), pushing us to violate our own law and we have refused to do so, we are sticking to our law."

"I know some people are gearing themselves for an attack on Zimbabwe. I want to see any country which will raise its finger in the AU, our elections have been free."

Huyu mzee kweli ni Jongwe.
 
........freedom Is Coming Tomorrow....!
Lets Open Our Brothers & Sisters Konshas About Freedom.....from Oppression, Corruption, Invasion, Inferiority Complex.....!

You sound very revolutionary!
Latin America wameshaamka bado sisi waafrika!
 
Nyie watu mnaosema Mugabe this Mugabe that you are naive!

Kama kweli malikia wa Uingereza anaipenda Zimbabwe kwa kumpinga Mugabe...Then mjiulize maswali haya....Je wangemchukia Mugabe kama wasingenyanganywa Masahamba?

Swali la pili...Hivi munafikiri wakoloni waliondoka Zimbabwe na AFRIKA KWA KUPENDA?

Leo hii Malikia wa Uingereza kamvua Mugabe U KNIGHT!
Nani anataka heshima za wakoloni?

Hivi nyie watu mnajua historia ya Afrika?

Na kama mnadhani hii si PROX WAR...THEN MJIULIZE SWALI MOJA...Ni kwanini North Korea wametangaza leo RASMI KUWA WANA NYUKILIA?

Mchina ana intelligence zote kuwa Mmarekani anakwenda kumnyang'anya koloni lake...Akaibipu PYONGYANG...Sasa BUSH KESHAJUA NOMA!

Naomba mtafakari na muachane na hayo mambo kwani mpango wa MAFISADI WA KUTUTOA KWENYE HOJA YA UFISADI ITATIMIA!

HIVI VITA HAKUNA TENA!
 
KJ,
hapa msee umeteleza, yaani unataka ku-side na watu waajabu kabisa!! ktk watu woote wewe umeona Mkapa na Mbeki!!? Mbeki bado ana-hangover ya lile saga lake la ARV's, sijui anataka ku-prove point gani!! huyu Mkapa anajua kabisa, kwamba kama Jongwe akichukuliwa hatua basi kutakuwa na precedence ya kudili na watu mafisadi kama yeye!!

mwisho wa siku...!!! kazi kwako kubwajinga, uzalendo unamipaka kaka, oooohooo. Hii issue ni simpo, soln(s) zipo wazi, hakuna miujiza, Mugabe gotta go!!! hivi kwenye first round si alishapewa "pink slip," sasa nini tena??

Mkuu YNIM,
Ni wazi kabisa kuwa Mugabe has to go hili linajulikana na hata yeye analifahamu. Tatizo linakuwa ni aondokeje? Offcourse sio kwa vita kama alivyosema JK.

Kama usalama wake ungehakikishwa, huyu mzee alishakuwa tayari kuyamwaga manyanga siku nyingi. Shida ni kuwa wapo wanaotaka shingo yake ndio maana akaamua kufia madarakani? Niliwahi kusema hapo awali kuwa Tsvangirai anayo nafasi kubwa hivi sasa ya kuongea na huyu mzee na kumpa terms nzuri za kuondokea, kitu ambacho kingerahisisha mambo, shida ni kuwa amri za nini afanye Tsvangirai zinatoka kwa masponsa wake wasiotaka Mugabe akaritaya bila kufikishwa mahakamani. Hapo kazi ndio ilipo.

Mugabe alikuwa anaheshimu sana wajumbe wa Tanzania, lakini staments za Membe na JK zitakuwa zimeharibu kila kitu na kufanya azidi kuwa na roho ngumu.
 
Sasa BUSH KWASABABU ALISHAMUAHIDI BLAIR KUHUSU VITA..Wanajidai kuwapa shavu NK KWA KUJIDAI ETI WANAWATOA KWENYE LISTI YA MATAIFA YA KIGAIDI!

SIASA TU ILI WASIMPE SAPOTI CHINA!

MANDELA NAYE KAPIGA KIMYA NA TRUST ME ANAJUWA KUWA MAGHARIBI WANAWEZA KUANGUKA KAMA UKOMUNISTI...NYIE HAMJUI KUWA MCHINA SASA NDIYE BINGWA DUNIANI?

HAWA WATU WANAPAMBANA VIBAYA MNO!
HU JINTAO ALIKUWA NA ZIARA YA AFRIKA,ASIA NA MIDDLE EAST KUSAINI MIKATABA!

BUSH KUONA HIVYO NA YEYE AKAENDA KWENYE NCHI ZOTE ALIZOPITA JINTAO KWA KUANZIA NA INDIA!

WAMECHELEWA...MCHINA SASA NDIO BINGWA TAKA WASITAKE!
MCHINA MWENYEWE ANAITAWALA MAREKANI!
PESA ZOTE ZA VITA VYA IRAQ WANAKOPESHWA NA MCHINA!

KAMA VILE SISI WAAFRIKA TUNAVYODAIWA NA MAGHARIBI...BASI MMAREKANI ANADAIWA NA MCHINA PESA NYINGI KULIKO TAIFA LOLOTE LILE!

KWA HIYO MCHINA AKIDAI PESA ZAKE...MMAREKANI MWENYEWE AWEZA KUPOTEZA UHURU WAKE!
 
Wewe kama hujui hadi hivi sasa maana ya Waafrika Ndivyo Tulivyo basi ndio unazidi kunithiubitishia kuwa kweli ni Ndivyo Tulivyo!!

Kama unakubalian na misemo ya kumwonyesha kuwa mwafrika ni duni kiutendaji, kiuamuzi n.k., na kuwa habadiliki basi ujue kuwa wewe uko katika hali mbaya sana kifikra, na utaendelea kutawaliwa mpaka utakapodondoka.
 
Kama unakubalian na misemo ya kumwonyesha kuwa mwafrika ni duni kiutendaji, kiuamuzi n.k., na kuwa habadiliki basi ujue kuwa wewe uko katika hali mbaya sana kifikra, na utaendelea kutawaliwa mpaka utakapodondoka.

.....inferiority complex....!
 
...halafu kusema vyombo vya Magharibi this or that, haisadii kupata ufumbuzi wa tatizo la Zimbabwe!! hakuna mchawi hapa zaidi ya Mugabe mwenyewe.....puliz!


No! no! no! Vyombo vya habari vya magharibi ni muhimu sana katika ku-manipulate public opinions. Vinaweza kutengeneza au kubomoa sura ya mtu kulingana na wanavyotaka wao. Hivi sasa huko magharibi Mugabe ni caricuture fulani hivi, a zombie.

Chukulia tu mfano wa hiyo Troika iliyoketi ambapo wala haikutimia. Lakini wapo ambao tayari washaiita kuwa ni statement ya SADC. These people are tacktical and very powerful.
 
Back
Top Bottom