Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

i truly support huyo Mugabe anavyokuwa shujaa kutosikiliza westeners but at the same time, anawaumiza wananchi wake ambao wanakufa njaa, wengine kufa na political violence. sasa yeye hajali kama watu wake wanaumia ilimradi tu aonyeshe kuwa yeye ni mbabe kwa westeners.
[pia ile ya kunyang'ana mashamba na kugawa kwa waafrika wenzake was abrave thing..lakini hayo mashamba yanakufa kwasababu aligawa kwa watu wake na sio watu ambao they can manage ..which proves a point kuwa at times waafrika kwa ufisadi hatutafika kokote]
 
Mkuu Fundi Mchundo,

Naamini kwamba uwezo wako wa kuelewa ni mkubwa. Lakini nashindwa kuelewa unapojifanya kutokuelewa nini hasa maana ya rangi NYEUPE!!

Rangi NYEUPE kamwe haimanishi UZUNGU! ALMASI na PAMBA zote zina rangi NYEUPE lakini zinapatikana hapahapa Afrika ya WEUSI, tena Tanzania kwa WASUKUMA walalahoi wa nchi hii. Wasukuma huiita PAMBA kwa jina la DHAHABU NYEUPE kwa sababu ya WEUPE wa RANGI yake ya ASILI. Inamaana tuwambie hao wasukuma waache kulima pamba(dhahabu NYEUPE) kwa sababu FUNDI MCHUNDO anaamini WEUPE ni UZUNGU??!! Au tuwalazimishe waamini kwamba PAMBA ina RANGI NYEUSI wakati ni NYEUPE! Ajabu!

RANGI NI RANGI TU WALA HAINAUHUSIANO NA TAIFA AU DINI YA MTU!

MUNGU WASAIDIE WALIOATHIRIKA KISAIKOLOJIA KIASI CHA KUWAABUDU WAZUNGU!

Sasa mbona mnatumia rangi kujenga hoja yenu? Au hao wazungu mnamaanisha na wengine walioamua kuhamia ulaya na marekani?

Usijifanye naive, Mkuu. Mjadala wote umesimamia rangi na post colonial rhetoric. Rangi in the racial context. Sasa katika postcolonial rhetoric moja ya nguzo ni kuziandika upya association zote zilizohusishwa na rangi nyeupe na waliotutawala. Ambazo nyingi ni negative. Blackmarket, Black plague, Black mail, dark as sin, black deeds etc etc. Na mitazamo kama hii ikapelekwa kwenye race relations; kama mambo yote maovu ni meusi basi wenye rangi hiyo ni waovu na lesser than walio weupe, rangi ya mbinguni! Makovu yaliyoachwa na hizi associations tunayo mpaka sasa. Dada zetu kutumia mkorogo kwa sababu the ideal ya uzuri katika western media ni weupe. Sasa leo nakushangaa armchair revolutionary unaposimama na kusema umechagua rangi nyeupe kukuonyesha usafi wa matendo yako. Kwa mtazamo huo una maana kuwa weusi hauwezi kuwa msafi?

Haujui unachokisema.
 
Binafsi simpongezi Mugabe hata kidogo isipokuwa mnashindwa kusoma between the lines...Hivi kama Wazungu wangekubali matokeo ya kuchukuliwa ardhi bado mnafikiri kuwa Mugabe angekuwa huyu wa leo?... Na ilikuwaje ktk miaka yote toka 1982 hadi 2000 (18 yrs) Alikuwa akiitwa kiongozi bora Africa...While watu kama mimi nilifahamu kabisa kuwa Mugabe ni mmoja kati ya NDIVYO TULIVYO!
Kilichochukuliwa ni ardhi ambayo ilikuwa inamilikiwa na wazungu, hilo la mashamba ni lugha ya mzungu!...ardhi ambayo sio laqzima ilikuwa ikitumika ktk kilimo..
Kisha mnafikia kuamini ati vikwazo ni kuhusiana na vifaa vya kijeshi, lini Zimbabwe wamenunua vifaa vya kijeshi toka nchi za magharibi na hununua vifaa hivyo mara ngapi kwa mwaka! mara ati oooh kazuiwa kusafiri, Sii huyu Mugabe alikuwa New York (UN) na Italia majuzi tu..

Fundi Mchundo,
Mkuu endelea kuamini unavyoamini lakini mimi binafsi naamini kabisa kuwa kinachofanywa na nchi za magharibi ni kikubwa kuliko tunavyosoma. Binafsi nilitaka kununua Chicken egg incubator na hatchery machine toka Zimbabwe nilikataliwa na bank yangu kufanya transaction kwa sababu ya sanctions.. Kuna mshikaji wangu ambaye anasafirisha Pamba toka Zimbabwe nje kwa kupitia South Africa na kanihakikishia kwamba ni lazima deal lipitie Suoth laa sivyo hakiuziki kitu.
ZNI ujinga mkubwa kuamni kwamba Wazimbabwe hawawezi hata kulima mahindi wakati ni hao hao Wazimbabwe waliokuwa wakilima Mahindi kwa mzungu.. Hakuna mzungu aliyeingia shambani kuzalisha mahindi peke yake wote hao walikuwa na wafanyakazi Wazimbabwe..
Kisha kuhusu habari ya kuwekeshga Cuba nakuomba soma vizuri habari nzima usichague kipande cha NIKE... na lauikama ingekuwa rahisi kama unavyozungumza basi Tungeona maduka kama hayo Tanzania ambako kila kitu ni ruksa isipokuwa tunaona mitumba na vitu fake..
Mugabe ni kiongozi mbaya sana lakini hadi sasa hivi hamjatoa suluhisho zaidi ya kulaumu tuuuu. nimeomba maoni yenu toka jana nachokiona ni kuzunguka mbuytu hakuna mwenye jibu zaidi ya kulaumu...kitu ambacho hakuna anayekataa.. Huyo Morgan kajificha kwa wazungu, Ubalozi gani vile?...
 
ZNI ujinga mkubwa kuamni kwamba Wazimbabwe hawawezi hata kulima mahindi wakati ni hao hao Wazimbabwe waliokuwa wakilima Mahindi kwa mzungu.. Hakuna mzungu aliyeingia shambani kuzalisha mahindi peke yake wote hao walikuwa na wafanyakazi Wazimbabwe..


Mkandara,
Waliokuwa wanalima aliwatimua akawapa mashamba cronies wake! Angalau hata angewapa hao hayo mashamba yako. Mfano wako ni kama vile mimi nijione zaidi ya mhandisi aliyedesign structure kwa sababu mimi ndiye ninayemwaga zege site!

Wazungu wana matatizo yao bila shaka. Lakini nakataa kumtumia kama kisingizio kwa matatizo niliyoyasababisha mwenyewe.
 
Humility, Humility, Humility!. Mugabe anataka kushindana na wazungu, kuwaonyesha kwamba yeye ni kidume!. Kiongozi ni lazima uwe tayari kusacrifice kwa ajili ya watu. kuna raha gani kudindiana na wazungu wakati watu wako wanakufa kwa njaa, ukosefu wa dawa, na pia kuzidi kudidimia katika shimo la umasikini?.

hata kama Mugabe ana haki ya kutawala, lakini yeye binafsi ilibidi ajiondoe kwa sababu yeye ndo imeshafahamika kwamba amekuwa tatizo. ilibidi afikirie kwa moyo na akili aone kwamba kuwepo kwake kunasolve tatizo au kunazidisha tatizo?. umwamba wakati mwingine hausaidii!.

sasa kama Mugabe anadhani hali ngumu inatokana na vikwazo vya west, na wakati huo huo anafahamu fika kwamba vikwazo hivyo vimewekwa kwa sababu yake, kwa nini sasa asiondoke ili hivi vikwazo viondoke. na kama ni kuhusu hii land reform, mtu mwingine anaweza kuendelea na hiyo programu kwani lazima iwe Mugabe?
 
Mkuu endelea kuamini unavyoamini lakini mimi binafsi naamini kabisa kuwa kinachofanywa na nchi za magharibi ni kikubwa kuliko tunavyosoma. Binafsi nilitaka kununua Chicken egg incubator na hatchery machine toka Zimbabwe nilikataliwa na bank yangu kufanya transaction kwa sababu ya sanctions.. Kuna mshikaji wangu ambaye anasafirisha Pamba toka Zimbabwe nje kwa kupitia South Africa na kanihakikishia kwamba ni lazima deal lipitie Suoth laa sivyo hakiuziki kitu.

Mkandara, unachanganya maamuzi ya dola na wananchi. Ingawa serikali za uingereza na marekani hawajaweka trade embargo kwa Zimbabwe lakini nchi hiyo imekuwa demonised kiasi cha kuwa any self respecting business atachelea kufanya biashara nao kwa kuogopa ghadhabu ya wananchi akijulikana. Ingawa serikali ya Marekani haikuwawekea sanction utawala wa makaburu lakini wananchi wake, haswa wanafunzi wa vyuoni, walishinikiza vyuo vyao vi-disinvest kwenye makampuni yeyote yaliyokuwa yakifanya biashara Afrika Kusini. Makanisa nayo yakashinikizwa kufanya hivyo hivyo. Bila shaka hiki ndicho kinachoendelea kuhusu Zimbabwe. Sitashangaa kusikia watu wana boycott kununua passion fruits kutoka Zimbabwe. Lakini hauwezi kuita hizi ni sanctions za serikali.
 
Wazungu mtawalaumu mpaka YESU arudi without Africans getting any better!



Haya ndio maneno yanayotumiwa kumfanya mweusi asidai haki yake toka kwa mweupe. Ndio, tuna makosa yetu, lakini hiyo haiondoi makosa ya hao wazungu waliyotufanyia na mengine wanaendelea kutufanyia.
 
Humility, Humility, Humility!. Mugabe anataka kushindana na wazungu, kuwaonyesha kwamba yeye ni kidume!. Kiongozi ni lazima uwe tayari kusacrifice kwa ajili ya watu. kuna raha gani kudindiana na wazungu wakati watu wako wanakufa kwa njaa, ukosefu wa dawa, na pia kuzidi kudidimia katika shimo la umasikini?.

hata kama Mugabe ana haki ya kutawala, lakini yeye binafsi ilibidi ajiondoe kwa sababu yeye ndo imeshafahamika kwamba amekuwa tatizo. ilibidi afikirie kwa moyo na akili aone kwamba kuwepo kwake kunasolve tatizo au kunazidisha tatizo?. umwamba wakati mwingine hausaidii!.

sasa kama Mugabe anadhani hali ngumu inatokana na vikwazo vya west, na wakati huo huo anafahamu fika kwamba vikwazo hivyo vimewekwa kwa sababu yake, kwa nini sasa asiondoke ili hivi vikwazo viondoke. na kama ni kuhusu hii land reform, mtu mwingine anaweza kuendelea na hiyo programu kwani lazima iwe Mugabe?

nakukubali kabisa ganda la nyoka, halafu pamoja na hiyo naona anaibisha waafrika kwa kukataa kuachia ngazi baada ya zaidi ya miaka ishirini na kwenye uraisi kwani hakuna mtu mwingine kutoka chama chake ambaye anaweza akagombania uraisi ili wazimbabwe wasiteseke .
 
Mugabe anataka kushindana na wazungu....

sasa kama Mugabe anadhani hali ngumu inatokana na vikwazo vya west...,

Sio kweli kwamba Mugabe anataka kushindana na Wazungu, au anaamini hali ya Zimbabe inatokana na nguvu za nje. Hana hiyo dhati.

Anachofanya Mugabe ni sawa na Osama bin Laden anaposema ujasusi ni juhudi za kutetea Uislamu unaotishiwa na Wamagharibi ikiongozwa na US. Hiyo inamsaidia kupata sapoti ya wapenda Uislamu, na wachukia ukoloni mamboleo wa US na siasa zao za kibeberu (imperialism). Kama unachukia ubeberu, na ukoloni mamboleo na pia ni mpenda Uislamu unaweza kujikuta unajiunga na kambi yake ya mafunzo, kumbe ukweli ni kwamba mzizi wa fitina haswa ni bifu yake na watu wa kwao huko Uarabuni ambao walikataa mawazo yake fulani fulani miaka kibao iliyopita.

Anachofanya Mugabe kunyooshea kidole Magharibi ni pretext kama hiyo hiyo ya kumsaidia kupata hurumu ya wote tusiopenda Ukoloni mambo leo na ubeberu wa Wamagharibi. Ni usanii wa kisiasa.
 
Kama Mugabe ni mkombozi wa waafrika na kama anadai kuwa Tsa.. ni kibaraka, kwa nini asimwachie mtu mwingine kutoka kwenye chama chake ili agombee uraisi?

Ina maana Zimbabwe yote hakuna mtu mwingine but Mugabe pekee ndiye mwenye uwezo wa kupigana na "wakoloni"?

Grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr ..... watu wasiojali masilahi ya wananchi wao ni mafisadi na Mugabe ni fisadi mkubwa.
 
Sio kweli kwamba Mugabe anataka kushindana na Wazungu, au anaamini hali ya Zimbabe inatokana na nguvu za nje. Hana hiyo dhati.

Anachofanya Mugabe ni sawa na Osama bin Laden anaposema ujasusi ni juhudi za kutetea Uislamu unaotishiwa na Wamagharibi ikiongozwa na US. Hiyo inamsaidia kupata sapoti ya wapenda Uislamu, na wachukia ukoloni mamboleo wa US na siasa zao za kibeberu (imperialism). Kama unachukia ubeberu, na ukoloni mamboleo na pia ni mpenda Uislamu unaweza kujikuta unajiunga na kambi yake ya mafunzo, kumbe ukweli ni kwamba mzizi wa fitina haswa ni bifu yake na watu wa kwao huko Uarabuni ambao walikataa mawazo yake fulani fulani miaka kibao iliyopita.

Anachofanya Mugabe kunyooshea kidole Magharibi ni pretext kama hiyo hiyo ya kumsaidia kupata hurumu ya wote tusiopenda Ukoloni mambo leo na ubeberu wa Wamagharibi. Ni usanii wa kisiasa.

Asante mkuu! Ungekuwa karibu ningekupa hata bia moja pale Rose Garden kesho!
 
Binafsi simpongezi Mugabe hata kidogo isipokuwa mnashindwa kusoma between the lines...Hivi kama Wazungu wangekubali matokeo ya kuchukuliwa ardhi bado mnafikiri kuwa Mugabe angekuwa huyu wa leo?... Na ilikuwaje ktk miaka yote toka 1982 hadi 2000 (18 yrs) Alikuwa akiitwa kiongozi bora Africa...While watu kama mimi nilifahamu kabisa kuwa Mugabe ni mmoja kati ya NDIVYO TULIVYO!
Kilichochukuliwa ni ardhi ambayo ilikuwa inamilikiwa na wazungu, hilo la mashamba ni lugha ya mzungu!...ardhi ambayo sio laqzima ilikuwa ikitumika ktk kilimo..
Kisha mnafikia kuamini ati vikwazo ni kuhusiana na vifaa vya kijeshi, lini Zimbabwe wamenunua vifaa vya kijeshi toka nchi za magharibi na hununua vifaa hivyo mara ngapi kwa mwaka! mara ati oooh kazuiwa kusafiri, Sii huyu Mugabe alikuwa New York (UN) na Italia majuzi tu..

Fundi Mchundo,
Mkuu endelea kuamini unavyoamini lakini mimi binafsi naamini kabisa kuwa kinachofanywa na nchi za magharibi ni kikubwa kuliko tunavyosoma. Binafsi nilitaka kununua Chicken egg incubator na hatchery machine toka Zimbabwe nilikataliwa na bank yangu kufanya transaction kwa sababu ya sanctions.. Kuna mshikaji wangu ambaye anasafirisha Pamba toka Zimbabwe nje kwa kupitia South Africa na kanihakikishia kwamba ni lazima deal lipitie Suoth laa sivyo hakiuziki kitu.
ZNI ujinga mkubwa kuamni kwamba Wazimbabwe hawawezi hata kulima mahindi wakati ni hao hao Wazimbabwe waliokuwa wakilima Mahindi kwa mzungu.. Hakuna mzungu aliyeingia shambani kuzalisha mahindi peke yake wote hao walikuwa na wafanyakazi Wazimbabwe..
Kisha kuhusu habari ya kuwekeshga Cuba nakuomba soma vizuri habari nzima usichague kipande cha NIKE... na lauikama ingekuwa rahisi kama unavyozungumza basi Tungeona maduka kama hayo Tanzania ambako kila kitu ni ruksa isipokuwa tunaona mitumba na vitu fake..
Mugabe ni kiongozi mbaya sana lakini hadi sasa hivi hamjatoa suluhisho zaidi ya kulaumu tuuuu. nimeomba maoni yenu toka jana nachokiona ni kuzunguka mbuytu hakuna mwenye jibu zaidi ya kulaumu...kitu ambacho hakuna anayekataa.. Huyo Morgan kajificha kwa wazungu, Ubalozi gani vile?...

Bob heshima mbele,

Hivi niambie, hii violence kama kuwapiga wananchi, kuwanyanyasa wapinzani, arguments za Mugabe kwamba aliteuliwa na Mungu na yeye pekee ndo anaweza kumuondoa madarakani, kuwagawia mashamba marafiki zake, kuwachoma moto wasiokubaliana naye nk..WHAT HAS THAT GOT TO DO WITH WAZUNGU??? Uchaguzi wa Zim..waliopiga kura si ni wananchi? Common lets not be fooled to that extent!

Hakuna anayewatetea wazungu hapa. Wana issue zao ofcourse. Kinachogomba hapa ni will of the people! Kwa nini watu wauawe simply because hawajamchagua yeye? Na ni kitu gani haswa kinakufanya uone kwamba Morgan ni sell out? the fact kwamba Mugabe has demonized him, lets look the other side of the coin! Africa ni incumbent gani aliyeko madarakani ambaye amekubali kiustaarabu ushindi wa wapinzani? bila kusema kwamba wanapata support ya magharibi? remember Mseven in 2006? alichomfanyia Kiza Besigye? Hivi kweli kama Tanzania unategemea upinzani ushindane na CCM..wakati kuanzia kwa VEO wa kijiji mpaka rais wa nchi wanatumia raslimali za taifa kuifanyia kampeni CCM? Jamani mbona wapinzani Africa tunawademonize yet we expect them to be an alternative of the current system we have?

Kama Kuhani alivyosema, Mugabe is playing the "racial card" na "ant western card" kwa sababu anajua wote tulikuwa victims..kwa hiyo tutamuonea huruma. Lakini hapa tunaongelea kitu kingine kabisa! Tunapoleta hadithi za mashamba na wazungu we lose focus! hapa ni credibility ya jinsi Mugabe anavyojustify kukaa madarakani..simple!
 
ahsante Lakini Hapana Ahsante.

Unajuaje Mimi Ni Mlevi Kama Wewe Kunikaribisha Kilevi?

J/k

naomba Radhi Mkuu! Tafadhali Nisamehe Sana! It Was Just A Simple Gesture Of Appreciation! I Withdraw My Statement Ya Mwaliko Na Kukubali Kwamba Mimi Ni Mlevi As You Faithfully Branded Me.

Peace
 
Fundi,Mkandara,Kuhani,Masanja,Koba,....

..kiongozi yeyote yule wa dunia ya tatu akiwekewa VIKWAZO na wakubwa na akajaribu kuendesha UCHUMI kivyake-vyake matokeo yake ni hayo tunayoyaona Zimbabwe.

..hapa Tanzania Baba wa Taifa alijaribu kwa muda mfupi yale anayojaribu Mugabe, matokeo yake Mwinyi alipokea nchi ikiwa haina fedha za kulipia meli moja ya mafuta. sasa sembuse Mugabe aliyekuwa chini ya sanctions for how long now?

..kwa hiyo ukweli ni kwamba VIKWAZO ndivyo vinavyosababisha matatizo ya uchumi Zimbabwe. Lakini ni ukweli pia kwamba VIKWAZO vimewekwa kwasababu ya MUGABE.

..Mugabe akiondoka vikwazo navyo vitaondolewa mara moja. tena msije mkashangaa Wazimbabwe ndani ya muda mfupi wakaendelea kuliko Tanzania.

NB:

..kuna kipindi Mugabe alimpendekeza Mkapa awe msuluhishi kati yake na Waingereza.

..ninavyoelewa mimi MDC na Waingereza did not respond.

..ninavyoona mimi Mugabe alikuwa anatafuta pa kutokea[exit strategy] lakini kwasababu ya siasa za kukamiana za MDC na wafadhili wao nafasi hiyo ikapotezwa.
 
naomba Radhi Mkuu! Tafadhali Nisamehe Sana! It Was Just A Simple Gesture Of Appreciation! I Withdraw My Statement Ya Mwaliko Na Kukubali Kwamba Mimi Ni Mlevi As You Faithfully Branded Me.

Peace

Mkuu,

Uliona nilivyoweka "j/k" pale chini? Nilikuwa nakwambia "just kidding," ikiwa ni gesture yangu ya kukushukuru wewe pia kutumia a sense of humor of political correctness. Ka utani kenyewe ka political correctness ni kwamba huwezi kumkaribisha mtu bia kama hujui anakunywa. Lakini najua kabisa tusingekutana kunyeshana bia.

Na kumwambia mtu aliyekuunga mkono hoja yako kwamba ni mlevi kwa sababu kakukaribisha bia moja huo ndio ulevi. Nilikuwa nakutania tu Mkuu.

Naona hukunielewa. Samahani.
 
Mimi nawapa changamoto wale wote mnaobisha kuwa Waafrika Ndivyo Tulivyo kunionyesha mifano ya Sivyo Tulivyo na nitatoa ya kwangu ya Ndivyo Tulivyo ili kulinganisha lipi ni zaidi. Nawahakikishia mkinionyesha mifano kumi ya Sivyo Tulivyo mimi nitawaonyesha mifano 10,000 ya Ndivyo Tulivyo. Haya kazi kwenu......let's go for it.
 
..kiongozi yeyote yule wa dunia ya tatu akiwekewa VIKWAZO na wakubwa na akajaribu kuendesha UCHUMI kivyake-vyake matokeo yake ni hayo tunayoyaona Zimbabwe.

Mugabe alifanya nini cha "kuendesha UCHUMI kivyake-vyake" mpaka akawekewa vikwazo?

Na alianza lini?
 
Mimi nawapa changamoto wale wote mnaobisha kuwa Waafrika Ndivyo Tulivyo kunionyesha mifano ya Sivyo Tulivyo na nitatoa ya kwangu ya Ndivyo Tulivyo ili kulinganisha lipi ni zaidi. Nawahakikishia mkinionyesha mifano kumi ya Sivyo Tulivyo mimi nitawaonyesha mifano 10,000 ya Ndivyo Tulivyo. Haya kazi kwenu......let's go for it.

Ndivyo tulivyo ina maana gani? Au mwenzetu bado hujakomboka kimawazo?
 
Back
Top Bottom