WembeMkali
JF-Expert Member
- Jun 16, 2007
- 282
- 3
Mandela, Mandela. Mbona kaenda kuongelea Uingereza? Tena kasentensi kamoja. Halafu alikuwa wapi wakati waafrika wanauwawa na kuvamiwa South Africa? Hana dili huyo Mzee.
Kuhusu Zimbabwe, mimi namwelewa Mugabe (every african leader knows the score, but they also know that the only winner is mzungu who control africa's economy. Once africans decide to control their economies, this wont happen. But I cant see it happening, so this will be a vicious cycle. Today Mugabe, tomorrow maybe Tanzania). Ila ya uchaguzi, kachemsha. Yeye na Morgan Manundu, wote nawaona wachizi na hawafai. Kila mtu anacheza na propaganda zake. Mugabe is in so deep, its hard to turn back. Morgan is such a sell-out, he aint better either. The losers are Zimbambwe people.
Haya mambo yatakuja yatugeukie sisi siku moja........na ndio maana kina Zitto wanajihami. In truth, nyie upinzani shughulikieni matatizo ya nyumbani, kwani ishu ya Zimbambwe si nyepesi.
*Nyani Ngabu, waafrika ndivyo tulivyo. Kwani wewe unaweza kueleza kwanini waafrika walikuwa wanakusanywa kama watumwa kutoka Tabora mpaka Pwani wakisimamiwa na mwarabu ana kimjeledi au kigobole?
Asante sana mkuu...
Viongozi wengi wa kiafrika wanaelewa vizuri sana kiini cha matatizo ya Zimbabwe ila wanaogopa kusema ukweli kwa kuwa watawachukiza wazungu na kunyimwa misaada.
Namheshimu sana Mandela ila kwenda kusema maneno yale Uingereza tena mbele ya Waingereza na tena ka-sentensi kamoja na kushindwa kutumia busara zake,umaarufu wake,ujuzi wake,uafrika wake kuziita pande zote zinazopingana katika mgogoro huu na kufanya dialogue ili kuleta mema Zimbabwe naona naye anaingia kwenye group lile lile la kutowaudhi wazungu!! Ni lazima waafrika tukaelewa kuwa leo hii yametokea Zimbabwe na kesho yanaweza kabisa kutokea Afrika ya Kusini na sitashangaa yatatokea tena hata katika nchi zingine Afrika.Kwa hiyo nilazima tukemee kwa nguvu zote mtindo wa mataifa ya magharibi kuingilia,kuzivuruga,na kuchagulia viongozi nchi za kiafrika kwa manufaa yao na siyo manufaa ya wengi.
Wembe.