Website ya IKULU na miradi ya COMPUTER ya Serikali

Website ya IKULU na miradi ya COMPUTER ya Serikali

Ukipiga hesabu kwa watu 50 tu inaweza kufika.. labda kama kuna mtu anaweza kutuma ISP ya bongo ambayo inaweza kuwa chini ya hapo. Nadhani hapa issue siyo hiyo hela issue hapa ni kwa nini Internet ni ghali sana.
 
Mkuu hivi unajua Ikulu watumiaji wa Internet ni wangapi? na wana ofisi ngapi?

Nafikiri kwa Tanzania kama either wanamlipa ISP kwa mwaka mzima. Hicho kiasi nafikiri ni sawa kabisa.

Jamani hizo hela si za kwendea internet cafe...au nimeelewa vibaya!!
 
Jamani hizo hela si za kwendea internet cafe...au nimeelewa vibaya!!

Mkuu Gigo's

Unapokuwa unafanya planning ya kupewa service ya Internet kuna kitu kinaitwa quality of services

Kuna vitu vidogo unavyotakiwa kufikiria, kimoja wapo network itakuwa inatumika kwa services zipi, ni computer ngapi zitatakiwa kuwa zimefungwa kwenye internet(watu watumiaji), kuna mintanance, na sina uhakika kama je wana wana na W_LAN Ikulu nk.

Vigezo mbali mbali huwa vinatumika kuamua ni speed kiasi gani itatakiwa. Sitegemei kama link speed ya Ikulu inatakiwa iwe sawa sawa na ya vikampuni vidogo.

Kwa hiyo suala la watumiaji na matumizi yapi na ofisi ngapi zitakazokuwa zina access internet, pamoja na maintanance zinaweza kusababisha garama kufikia kiasi hicho.

Na pia kwa security purposes nafikiri Ikulu hawezi kuwa na services sawa sawa na watu wengine wa kawaida
 
Katika hili, hapana. Hicho kiasi kwa mwaka ni more than fair !
 

Kwanza ni ndogo, ilibidi iwe zaidi ya hapo. Mawasiliano kwa sehemu kama hiyo inabidi yawe ya hali ya juu
 
Jambo la kushangaza ni kuwa pamoja na ukweli kuwa Ikulu hawana hata website kwa kipindi chote hiki ila ni kuwa gharama za Internet zilizoombwa ni kiasi cha shilingi 38,400,000.

Hizi fedha zipo kwenye kifungu 2002 mawasiliano serikalini, kwenye kasma namba 260104 ya kitabu cha bajeti ofisi ya rais ikulu,

wameandika hivi ,nanukuu..Kasma hii hutumika kulipia gharama za mawasiliano ya mtandao kwa njia ya internet .katika mwaka wa fedha 2008-2009 zinaombwa shilingi 38,400,000.

Maswali ya kujiuliza ni kuwa kama kutuma tuu internet wanahitaji kiasi chote hicho kwa mwaka ni gharama halisi ama ni mchezo wa Salva et all?

Kwa ujumla gharama za mawasiliano ,habari na utoaji huduma zimeobwa kiasi cha shilingi 60,475,000. na hizi ni kwa ajili ya vitu kama gharama za simu 2,400,000,gharama za posta 500,000, Internet 38,400,000,uchapishaji 4,200,000, huduma za utangazaji 12,675,000 na tepu,rekodi na diski 800,000.

Hya angalieni wenyewe jinsi internet inavyokula pesa zetu je wakiweka na website si ndio tutakwisha kabisa?

MK,

Hizo ni pesa ndogo sana kwa matumizi ya internet kwa Ikulu. Hapo kunaweza kuwa na hardware kama switches, routers, modems nk. Lakini pia kunaweza kuwa na software mbalimbali kama kwa ajili ya kompyuta na pia vitu kama anti-viruses.

Pia kuna kulipa ISP na mambo mengine.

Kama Ikulu wanatumia pesa ndogo hivyo kwa Internet labda ndio maana wako nyuma hata kwenye mambo ya website.
 
Nafikiri kwa sababu tayari wana internet lakini hii bajeti kwa mawasiliano ya internet ya Ikulu ni kidogo sana na pia ukizingatia maintanance yake.

Uliza hata baadhi ya makampuni mengine msikie bajeti yake. Milioni Tshs 38?

Kwa mawasiliano ya internet ya Ikulu ya Tanzania ningefikilia yafikie hata 100-milioni kwa mwaka.
 
Naona waungwana walitaka kuanza kupiga porojo tayari...kuna vitu vingi vya kuconsider kwenye maswala ya mawasiliano ya sehemu nyeti kama ikulu...sio tuu just internet, vitu kama-Firewalls za kuzuia outside intrusions, speed, service ipo 24/7, maswala ya intranet..lakini kikubwa zaidi ni maswala ya security.
 
Tatizo ninaloliona hapa ni kwamba huenda Ikulu wanatumia hata pesa nyingi kuliko walizoomba.

Siamini kama milioni 38 zinatosha kwa Ikulu.

Huenda kuna mtu anajiandikia tu na kisha wanatumia hata zaidi ya hizo kwani nani anaweza kuwachunguza Ikulu?
 
Mtanzania.... kwa sababu mwaka jana/juzi tuliambiwa wanaandaa tovuti yao na watatengewa bajeti na kwa karibu miaka mitatu sasa hiyo website inayotengenezwa haijaonekana... lakini wana ujasiri wa kuomba fedha tena.... hiyo ni intaneti au intraneti ya wao kwa wao?
 
Hii ni hela ndogo sana kwa internet connection kwa nchi ya Africa Mashariki zinazotumia satellite... acheni ulimbukeni...

Hiyo sio fedha ya webhosting... surely webhosting is cheaper than internet connection...


sasa tumekosa ya kuongea... du!
 
Hii ni hela ndogo sana kwa internet connection kwa nchi ya Africa Mashariki zinazotumia satellite... acheni ulimbukeni...

Hiyo sio fedha ya webhosting... surely webhosting is cheaper than internet connection...


sasa tumekosa ya kuongea... du!


kasheshe... mwaka jana Ikulu walitengewa fedha za Intaneti.. na mwaka juzi pia.. hizo firewall, na vyombo, nk halafu kuna bajeti ya mawasiliano.. n.k hivi huoni tatizo? Kabla hawajapewa hatu hutu tusenti milioni 38 si wasema hizo nyingine walizopewa walizitumiaje?
 
kasheshe... mwaka jana Ikulu walitengewa fedha za Intaneti.. na mwaka juzi pia.. hizo firewall, na vyombo, nk halafu kuna bajeti ya mawasiliano.. n.k hivi huoni tatizo? Kabla hawajapewa hatu hutu tusenti milioni 38 si wasema hizo nyingine walizopewa walizitumiaje?


Mzee Mwanakijiji,

Huu utamaduni wa ku-question kwa hakika matumizi ya mambo ambayo hamuyajui yanawafanya muwe watu wa ajabu sana...

Shule kidogo;
1. Naweza kubajeti kutumia 5,000/- mwaka huu, alafu itokee nisiitumie ile 5,000/- kwa kuwa mwaka umeisha bila kuitumia... ni lazima ni budget tena mwaka unaofuata same amount of money ndio nitaruhusiwa kutumia...kama nisipobajeti mwaka unaofuata sina ruhusa ya kutumia... hata kama sikutumia mwaka jana... na hata kama kweli nahitaji nitumie mwaka huu...

2. Hizo cost kwa hali yoyote kama ni za internet access ni ndogo sana... elewa pia kwamba firewall etc... is one time charge... while internet access is monthly.

3. Ukiangalia bajeti 2007/08... serikali ili-expect kuuza shea za NMB,,, lakini kwa kuwa haikutokea... mwaka 2008/09 pia wame-bajeti kupata mapato kutokana na kuuza hisa za NMB....

Mwisho... jadili mambo ya msingi acheni vitu visivyo na tija na taifa... ati kwa kuwa hamupendi Rweimamu au Kikwete...
 
Naona Kila Kitu Kinakuwa Siasa Siku Hizi Hata Hii Nayo Imeshakuwa Siasa Kwa Sababu Tu Ccm Ndio Ipo Ikulu , Lakini Wanaoleta Siasa Wanatakiwa Wajue Pale Wafanyakazi Wote Wale Hawako Pale Kwa Sababu Ya Kadi Au Uwanachama Wao Wa Chama Fulani Wale Ni Raia Huru Kitu Chochote Wanachofanya , Kupanga Au Kupangua Wanafanya Kwa Masilahi Ya Sehemu Yao Husika Na Taifa Kwa Ujumla .

Hata Hizo Hela Walizoomba Wameomba Kutokana Na Mahitaji Yao Hapo Walipo Wao Nina Uhakika Watakuwa Wameonana Na Wataalamu Wao Wa Ict Katika Kupanga Mambo Hayo Pamoja Na Wataalamu Wengine Kabla Ya Kuja Na Kitu Kama Hicho

Tuache Zarau Na Kushoboka Hii Sio Siasa Ni Kitu Halisi
 
Naona Kila Kitu Kinakuwa Siasa Siku Hizi Hata Hii Nayo Imeshakuwa Siasa Kwa Sababu Tu Ccm Ndio Ipo Ikulu , Lakini Wanaoleta Siasa Wanatakiwa Wajue Pale Wafanyakazi Wote Wale Hawako Pale Kwa Sababu Ya Kadi Au Uwanachama Wao Wa Chama Fulani Wale Ni Raia Huru Kitu Chochote Wanachofanya , Kupanga Au Kupangua Wanafanya Kwa Masilahi Ya Sehemu Yao Husika Na Taifa Kwa Ujumla .

Hata Hizo Hela Walizoomba Wameomba Kutokana Na Mahitaji Yao Hapo Walipo Wao Nina Uhakika Watakuwa Wameonana Na Wataalamu Wao Wa Ict Katika Kupanga Mambo Hayo Pamoja Na Wataalamu Wengine Kabla Ya Kuja Na Kitu Kama Hicho

Tuache Zarau Na Kushoboka Hii Sio Siasa Ni Kitu Halisi

Hivi accountability ni siasa?
 
Nafikiri Shy unaweza kujibu vizuri maswali yaliyoulizwa hapa si wewe ni mtaalamu wa ICT?
 
Back
Top Bottom