Waziri Mkuu aelezea ubadhirifu wa mamilioni uliofanywa Bohari ya Dawa (MSD), asema ataenda akiongozana na Polisi na TAKUKURU

PPRA kazi yake kuu hasa ni nini naona haifanyi majukumu yake ipasavyo
Tatizo watumishi wengi wa serikali/umma hawafanyi kazi kwa kufuata taratibu/miongozo ya kazi zao, bali hufuata matakwa ya wanasiasa (wenye maslahi binafsi). Ndio maana hata kwenye kesi ya Mbowe ulikuwa unasikia afisa wa polisi anaulizwa kuhusu vifungu vya PGO ambayo ni muongozo wa utendaji wao wa kazi lakini anasema hajui
 
Hapa MSD ubadhirifu wote ulisababishwa na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu yule Mwanjeshi Gabriel Mhidize,yeye kila kitu alikuwa anataka kifanyike Kijeshi na kuweka taratibu pembeni,hivyo wale wataalam wote waliokuwa sehemu ya Menejimenti ambao walikuwa wanapenda kufuata taratibu walikuwa ni Maadui kwake na alifanya mpango akawaondoa wote,binafsi nilisikitika sana kuondolewa kwa mtaalam mmoja somebody Pondamali,alikuwa anapiga kazi hasa na kufuata taratibu kitu ambacho Mjeshi Mhidize hakukipenda,matokeo yake ndio kukawa na Wizi sana,sisi Wafanyakazi wengine tukabaki tunaangalia tu,yule Mwananjeshi alikuwa na matatizo sana
 
Hivi alishwahi kumchukulia hatua yeyote hapa nchini? Kama maneno yake yangekuwa kweli. Leo ingekuwa inakaribia mwaka tangu trein ya mwendo kasi kuzinduliwa
Huyu haaminikiki, ndiye aliyetuficha wakati Magufuli amekwisha kufa akatudanganya eti alikuwa ofisini!! Ni mbwekaji mzuri lakini hana meno.
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi amkute katika ofisi za Bohari ya Dawa (MSD) Jumatatu saa nne asubuhi, baada ya kubaini madudu katika ununuzi wa vifaa vya matibabu.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo katika ufunguzi wa Wiki ya Ununuzi wa Umma jijini Arusha ambapo ametaja gharama kubwa iliyotumika kununua vifaa hivyo tofauti na bei halisi za soko, na hivyo kupoteza fedha nyingi za umma na kuwakosesha wananchi huduma kwani vifaa vilivyonunuliwa ni vichache.

Akizungumza na wataalamu wa ununuzi na ugavi, ametaja baadhi ya manunuzi hayo kama vile ununuzi wa seti moja ya vitenganishi kwa ajili ya awamu moja ya kusafisha damu kwa shilingi 65,000, lakini wakanunua kwa shilingi 189,000.

Aidha, MSD walitakiwa kununua mashine ndogo ya kipimo cha haemolojia ya mwili kwa shilingu milioni 5, lakini wakanunua kwa shilingi milioni 14,045,000.

Ametoa mfano mwingine ambao ni kipimo kikubwa cha haiemolojia ya mwili ambacho ni shilingi milioni 37, lakini MSD wamenunua kwa shilingi milioni 147.9, pia walitakiwa kununua mashine ya kuchakata maji kwa ajili ya kusafisha damu ambacho kinauzwa milioni 32 lakini wamekinunua kwa shilingi milioni 129.

"Kwanini hili linatokea? kwa maslahi ya nani?" amehoji Waziri Mkuu

Kutokana na PSPTB kuwa na jukumu la kuwachukulia hatua wataalamu wa ununuzi na ugavi wanaokiuka sheria, Waziri Mkuu Majaliwa ameiagiza kufika ofisi za MSD akisisiitiza kuwa serikali haiwezi kukubali hali hiyo kuendelea.

"Na mimi sitasita kwenda na Kamanda Sirro, na Kamanda Hamduni, ili washughulike na watu. Lazima tuanze na watu hawa wanaofanya kazi hii, wakae nje, hatua nyingine zifuate," amesisitiza Waziri Mkuu Majaliwa

Ameongeza kuwa pengine wasimamizi wa vitengo vya ununuzi na ugavi wanahitaji kuapishwa, kutokana na unyeti wa nafasi zao katika kutoa huduma kwa Watanzania.
Asante Waziri mkuu
 
Enzi zimeshapita, mkwara kama huu wakati wa JPM tayari watu wangeshakimbia nchi. Lakini huyu wa kukunwa vizuri na kupapasa ndo wamekula kwa urefu wa kamba zao.
Eti wahalifu wamsubiri aende na siro na hamduni utafikiri huko hakuna polisi wa kuwaweka ndani.
Acha aupige mwingi.
January oyeee
Nape oyeee
Riz1 oyeee
Mama wa mafao ya wake za viongozi oyeee

Haya majizi msubirini katelefone anakuja na siro na hamduni.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Uzuri mmepewa bunge na Kila kitu kwanini msipeleke hoja ya dharura na maazimio yachukuliwe kushughulikia wizi as per report ya CAG??

Mmeachiwa Kila kitu ila Bado mnalia lia? Tulidhani upinzani na mabeberu ndio wanatuchelewesha kumbe CCM wenyewe mnatukwamisha!!

Tunawasubiri 2025
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi amkute katika ofisi za Bohari ya Dawa (MSD) Jumatatu saa nne asubuhi, baada ya kubaini madudu katika ununuzi wa vifaa vya matibabu.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo katika ufunguzi wa Wiki ya Ununuzi wa Umma jijini Arusha ambapo ametaja gharama kubwa iliyotumika kununua vifaa hivyo tofauti na bei halisi za soko, na hivyo kupoteza fedha nyingi za umma na kuwakosesha wananchi huduma kwani vifaa vilivyonunuliwa ni vichache.

Akizungumza na wataalamu wa ununuzi na ugavi, ametaja baadhi ya manunuzi hayo kama vile ununuzi wa seti moja ya vitenganishi kwa ajili ya awamu moja ya kusafisha damu kwa shilingi 65,000, lakini wakanunua kwa shilingi 189,000.

Aidha, MSD walitakiwa kununua mashine ndogo ya kipimo cha haemolojia ya mwili kwa shilingu milioni 5, lakini wakanunua kwa shilingi milioni 14,045,000.

Ametoa mfano mwingine ambao ni kipimo kikubwa cha haiemolojia ya mwili ambacho ni shilingi milioni 37, lakini MSD wamenunua kwa shilingi milioni 147.9, pia walitakiwa kununua mashine ya kuchakata maji kwa ajili ya kusafisha damu ambacho kinauzwa milioni 32 lakini wamekinunua kwa shilingi milioni 129.

"Kwanini hili linatokea? kwa maslahi ya nani?" amehoji Waziri Mkuu

Kutokana na PSPTB kuwa na jukumu la kuwachukulia hatua wataalamu wa ununuzi na ugavi wanaokiuka sheria, Waziri Mkuu Majaliwa ameiagiza kufika ofisi za MSD akisisiitiza kuwa serikali haiwezi kukubali hali hiyo kuendelea.

"Na mimi sitasita kwenda na Kamanda Sirro, na Kamanda Hamduni, ili washughulike na watu. Lazima tuanze na watu hawa wanaofanya kazi hii, wakae nje, hatua nyingine zifuate," amesisitiza Waziri Mkuu Majaliwa

Ameongeza kuwa pengine wasimamizi wa vitengo vya ununuzi na ugavi wanahitaji kuapishwa, kutokana na unyeti wa nafasi zao katika kutoa huduma kwa Watanzania.
Ccm ni mafiii tunataka rais FULL DICTATOR MZALENDO
 
Dawa aina moja bei ya iliyotengenezwa Kenya, Tanzania, India China nk zinatofautiana na ya UK ukubwa wa kifo na kusinzia. Sijui kwa mashine na vifaa vingine vya tiba kutoka hizo nchi ukinganisha na vya UK.
 
Kassim utauawa mapema! MSD, TANESCO, Bandari, nk ni vyungu vya asali alivyosema Makamba Sr.
 
Kwani hizo zabuni hazikushindanishwa? Hawakutumia mfumo WA manunuzi?
Kama hawajafanya hayo Wana shida.
 
Hawa Panya Road wangejua umuhimu wa katiba mpya wangekuwa na sababu ya kustrike kwakua ushujaa wanao.
 
Kuna uwezekano wa kuwa na matumizi mabaya ya fedha MSD lakini turudi nyuma na tuache kuwalaumu sana kwa kazi ngumu wanayo ifanya. Siku zote, Sera ya serikali imekuwa kuhakikisha kwamba huduma za afya zinawafikia wananchi katika makundi tofauti ambapo huduma huwa bure kwa watoto chini ya miaka mitano, wazee waliozidi miaka 60 na kadhalika. Kama taasisi MSD inatakiwa ipokee malipo kutoka kwa hospitali na vituo vya afya baada ya kuhakikisha kwamba wanapata dawa na vifaa tiba. Tatizo la MSD linaweza lisihusishwe sana na matumizi mabaya ya fedha bali ni shirika kushindwa kujiendesha lenyewe kwasababu ya kuidai serikali mabilioni ya fedha. Afya bure kwa wote ni maneno ya kutafutia kura, hali halisi haipo hivyo
 
Hivi alishwahi kumchukulia hatua yeyote hapa nchini? Kama maneno yake yangekuwa kweli. Leo ingekuwa inakaribia mwaka tangu trein ya mwendo kasi kuzinduliwa
Nikuongezee

1. Report ya Kuungua Soko la Kariakoo

2. Kuungua soko la Karume

3. Mauaji ya kijana mfanyabiashara wa madini Mtwara yaliyofanywa na Mapolisi
 
Back
Top Bottom