Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Itakubidi ui-download, halafu inakubidi uwe na software ya kufungulia ZIP FILES.

Kama vipi Invisible aiweke kwenye PDF. Au..?
kama unashindwa ku download pengine hustahili kusoma nyaraka za siri.Nenda kwa mwansheria wa seikali akuapishe kwanza itafunguka
 
kama unashindwa ku download pengine hustahili kusoma nyaraka za siri.Nenda kwa mwansheria wa seikali akuapishe kwanza itafunguka


Sisi wananchi ndo waajiri wa hao watu wanaojiita collectively.."SERIKALI".

Sasa ni ajabu mimi muajiri niambiwe sina haki ya kusoma nyaraka ya kijakazi niliyemuajiri, yaani nampa kazi halafu anataka kunipanda kichwani!!.Kama nyaraka ni ya siri mimi bosi ndio wa kuamua, na sio kijakazi Ndo maana mawazo ya siasa na dhana nzima ya 'serikali' kwangu is fallacious.

Ndo maana nikasema solution ya matatizo ya nchi yetu ni kwa sisi mabosi kuwatimua kazi 'vijakazi' wetu, na kila bosi kushika njia yake. See post #112
 
......

1.Open tender............(i.e all are invited....kuna kuwa na post pre-qualification........)
........

whatever that is.... you all tender and then you post prequalify?.. ongeza Kilimanjaro au ni "Gulda" unakunywa huko?... if you are trying to talk about TZ procurement rules, then your expertise leaves much to be desired...
 
....same thing iliyoleta disaster and loss of billions kwa ubabe and favoritism za Lowassa kulazimisha na kuingilia kazi za bodi zilizokuwa zinaamua umeme ndio kinachofanyika hapa na huyu Masha,huyu hana tofauti na alichofanya Lowassa kwenye Richmond na anataka kutuletea incompetent company kwa ajiri ya 10% or for whatever reason ambayo cost yake still tunalipia in billions every month kwa makampuni kama IPTL,Richmond etc,this is abuse of power and corruption...he must go,fisadi mkubwa huyu!

Bwana Koba, tofauti kubwa sana moja ni kwamba tuko hapa hadahrani tunaongelea mambo haya...na kwa niaba ya nani? Masha! ..Do you see the difference? Angeamua kukaa kimnya mambo yote haya yangepita halafu ukaja kulia machozi baadaye kama kwenye mambo ya RDC....Na masha mwenyewe asingeitwa Dodoma, magazeti ya Mengi yangekosa uchafu ya kumkosoa nae...mambo yangekuwa poa na Masha mwenyewe ungekua na ulafi angesubiri dili nyingine ambapo angekula kilaini..... take is easy and try support someone who is actually working for the nation..
 
You spotted right Kelly, Kuhani is a juggernaut. The thread has lost direction.

Unajua Wadanganyika wanapenda ujinga kama muuza sura wetu. If anyone had the balls to say that Masha was wrong wanashindwa. The purpose of this letter to the PM was to cover his behind. The criteria he used to explain " non-material deficiencies" should have been enough to give him Kudos for not following the status quo. Kama kampuni ambayo imeshindwa ku-submit financial stmts inakua short listed while a company which failed to provide an MOU for a joint venture is excluded kwenye process hiyo basi wote kwenye hiyo bodi ni wapuuzi/wajinga na hawaitakii TZ mema. The above mentioned excuse should apply to every company.

Kama hii tender ingepita kama ilivyo na baadaye yakaonekana haya mapungufu mtu wa kwanza to blame ni yeye. Ndio maana akasema "Collective responsibility" hataki. Kosa alifanya ni kunukuu Sagem verbatim on whatever they wrote him. Lakini the bottom line ni kwamba the double standard is evident and we should thank him for being vigilant. Kama amevuta mimi simo!

My 2 Cents
 
whatever that is.... you all tender and then you post prequalify?.. ongeza Kilimanjaro au ni "Gulda" unakunywa huko?... if you are trying to talk about TZ procurement rules, then your expertise leaves much to be desired...


.......tell me about what you know (your procurement expertise).....na sio kuleta vioja........hivi umeshawahi kufanya hili zoezi..........i doubt.........!!
 
Last edited:
New member, I dont see the file you are talking about! How do I go about to access it?
 
Sauti za umeme zitakuja hivi: bla bla bla bla bla.........Lau kwa hili bado hajawa guilty ......nimeongea nae kwa simu sasa hivi kasema kuna more dataz anazo anasubiri aitwe na mkulu.......bado nampa Lau benefit of dought....."

- According to the dataz za leo, ni kwamba Dodoma kumechafuka sana tena sana, mafisadi wameshika hatamu, kuna mkakati mzito wa kumuokoa Masha na unaeleka kufanikiwa, Lowassa bado anavuta plugs tena big time.....jana usiku kikao maalum rais na baadhi ya mawaziri kuanzia saa 12 jioni mpaka saaa sita usiku, matokeo Makamba, Kingunge, na Almeir the fronts kumsafisha Masha by anymeans necessary......haiwezekani katika muhula mmoja tu wa utawala wa hii serikali Waziri Mkuu amejiuzulu, mawaziri wawili wamejiuzulu, mawaziri wengi wametemwa kwa mashinikizo ya wabunge, sasa bado tena waziri mwingine na katibu mkuu wa CCM watoke pia, ....sasa next wananchi watadai nani ajiuzulu kama sio rais mwenyewe? hilo according to the mafisadi sasa hapana, Masha ni lazima aokolewe by anymeans necessary!

- According to the dataz za kikao........mafisadi wamemcharukia mbunge Beatrice kuwa ndiye chanzo cha the leak....wamemuita na kumpa ujumbe mzito kwamba wanajua kuwa ndiye aliyempa Mengi nyaraka za siri za ishu ya Masha na Mengi ndiye aliyempa Dr. Slaaa......ingawa huu sio ukweli maana aliyempa Dr.Slaa ninamjua kua ni mwingine kabisaa wala hakuhusika na Mengi kwenye hili mafisadi wako off the balance...wamemuahidi mbunge malipo mazito sana kwenye uchaguzi.....!

- Another victim hapa anayetafutwa na mafisadi ni Membe, ambaye wameapa kwamba lazima amalizwe mapema, Dodoma kumechafuka sana, msimamo wa kuyumba wa rais aliyekua Dodoma jana usiku kwa kisingizio cha kutembela chuo kikuu kipya kumbe ana yake mengine kabisaa umewakatisha tamaaa kabisa wabunge wengi, infact mbunge mmoja ameniambia kua kuna kazi kubwa sana imefanyika in the last 48 hours ya kumsafisha, kwamba leo ikiletwa hoja ya kumuondoa Masha uwaziri kwenye floor ya bunge, wabunge wanaopinga watakuwa wengi kuliko wanaounga mkono,

- Mafisadi wanaendelea kuwatisha wabunge wote wapiganaji kwa kuwapelekea wagombea kwenye majimbo yao tayari, wakijitayarisha kwa kura za maoni, baadhi ya wabunge hawa tayari inaelekea kutakuwa na uwezekano mdogo sana wa kurudi tena bungeni, mkazo mzito unawekwa kwenye jimbo la Mama Makinda na Spika, maana hawa wawili ndio tatizo hasa la mafisadi bungeni na cc, Dodoma pamechafuka sana kiasi kwamba mbunge mmoja ameniambia kuwa hili bunge sasa ni bure kabisa, labda tusubiri la 2010 maana hili la sasa Lowassa ameshalivuruga, inasmekana kivuli cha Lowassa bado kinalitesa sana bunge maana kuna mgawanyiko mkubwa sana ndani ya bunge na sio rahisi tena kuwa na msimamo, Pinda naye ni another target ya mafisadi ambao tayari naye wameanza kumchafua ndani ya bunge.....!Infact katika huu mchakato mpya wa kumsafisha Masha, leo gazeti moja maarufu sana limeandika maneno mengi sana.

- Mpaka leo asubuhi tayari wajumbe wa kamati ya ulinzi walikwua wameshavurugana......! Hizi ndio dataz za leo asubuhi na mchana, tunazitafuta za jioni na kesho tena.

Thanxs!

- Mkulu Invisible, vipi kuna njia yoyote nyingine ya kufungua hii kitu yako maana so far ninakwama? na nimeshindwa kuifungua, au?

Baharia FMES, wazee wa meli!
 
Last edited by a moderator:
Bwana Koba, tofauti kubwa sana moja ni kwamba tuko hapa hadahrani tunaongelea mambo haya...na kwa niaba ya nani? Masha! ..Do you see the difference? Angeamua kukaa kimnya mambo yote haya yangepita halafu ukaja kulia machozi baadaye kama kwenye mambo ya RDC....Na masha mwenyewe asingeitwa Dodoma, magazeti ya Mengi yangekosa uchafu ya kumkosoa nae...mambo yangekuwa poa na Masha mwenyewe ungekua na ulafi angesubiri dili nyingine ambapo angekula kilaini..... take is easy and try support someone who is actually working for the nation..

.......tumejiwekea utaratibu ili ufuatwe........na si vinginevyo........hii mambo ya kuendekeza kuvunja vunja utaraitibu ndio maana tuna mambo kama RDC ya akina Lowassa.......
 
- By the way, naomba kusema neno moja dogo sana, ni kwamba ninawaomba wananchi hapa JF tufike mahali tuelewe sababu ya kuwepo kwetu hapa JF, mimi ninaamini kwamba ni taifa na sio anything else, na ninaamini kwamba wananchi wote tulioko hapa JF tuna uchungu ulio sawa kwa taifa letu na besides hapa ni mahali pa mapambano ya fikra pia, lakini lengo ni kulisaidia na ili tulikomboe taifa letu kutoka mikononi mwa viongozi wachache waliotusaliti wananchi wa taifa hili Tanzania.

- Ninasikitishwa sana na baadhi yetu wananchi kushindwa kuelewa kwamba kila kitu kwenye maisha kina wakati wake na msimu wake, katika mapambano ya fikra za kisiasa kama ilivyo hapa JF, sio ajabu kuwepo na patashika za hapa na pale, lakini tatizo linakuja pale wengine wetu wanaposhindwa ku-let it go, kuna msimu wa kucheka na msimu wa kulia, lakini haiwezekani ikawa mkisha pitia msimu wa kulia tu basi iwe kila siku kurudia rudia yale yale ya msimu wa kulia, tunapoteza focus wakuu yaani taifa.

- Mambo mengi yanafanyika na kutupita wakati tunapoteza muda, hivi unajua sasa hivi ni marufuku kwa wafanyakazi wa serikali kufungua JF? Hivi unajua kua ni marufuku kwa wafanyakazi wa serikali kukutwa na kijarida cha Fikra za cheche? Hivi unajua mafisadi sasa wanakaribia kulishika taifa tena maana hapa kati kati walianza kuishiwa nguvu? Lakini finally nguvu zimeanza kuwarudia tena, huku sisi tukipoteza muda hapa kusifiana na kuchekana wakuu tuamke!

- Hivi ni nani anakuwa na sifa kubwa hapa JF, kwamba ni mchambuzi makini, kwamba ni bingwa this or that? Nani huyo ambaye wananchi wetu wa mijini na vijijini wamemsikia na kumjua kua ni mkombozi wao mkubwa? JF tulikuwa na sifa kubwa sana huko nyuma kwa sababu we were working together kwa manufaa ya taifa, kwenye kila hotuba ya rais in the first two years in power tulikuwa hatukosi kuwemo, akituita "watu wa internent" tulikuwa hatukosi kwenye hotuba za rais, mara ya mwisho tulitajwa kwenye hotuba yake bungeni mwaka jana, that was it hajarudia tena kututaja, WHY? ni kwa sababu tumeanza kukosa muelekeo, tumeanza kuwa mimi, mimi, mimi, na me myself and I, tumeanza kukalia ya jana tu yaani mambo ya Jumapili mpaka leo bado tuu, vipi wakuu tunarudi nyuma sasa amukeni twende mbele.

- Ndugu zangu lets get serious tena, hakuna wa kusifiwa hapa wakati taifa linadidimia huku bongo, acheni wananchi wa nje ya forums wasifie iwapo wanaguswa na kinachoendelea hapa, lakini haya ya kuvunjiana heshima na maneno mengi yasiyosaidia taifa sidhani kama yanaweza kutusadia kwenye long run, sawa hatuwezi kuzuia malumbano, lakini yakiisha yaishe tusonge mbele sio kukalia yale yale tu ya jana inakatisha taamaa wananchi walio serious wakuu, zamani tulikuwa tunasifiwa na magazeti na hata viongozi wetu, lakini sasa tumegeuka kutafuta sifa tu wenyewe tena sometimes kwa nguvu nguvu na ujanja ujanja as if wananchi wa vijijini wanafadika anything na hizi sifa, please lets work together wakuu, too much division hapa sasa,

- I mean hatuwezi wote kua na msimamo sawa, lakini ni lazima tuheshimiane kwamba lengo letu ni moja nalo ni kulikomboa taifa, tunakua na nguvu sana tukiwa pamoja, lakini sio tukigawanyika kama tulivyo sasa, we are losing this war na mafisadi wakuu, tulumbane lakini yakiisha yaishe yakija yaje, lakini yakipita yapite na tusonge mbele ndugu zangu, taarifa nilizoazipata leo kutoka Dodoma zinasikitisha sana wakuu, hebu tupunguze yasiyokuwa na faida kwa taifa na hasa wananchi wanaotuangalia sana hapa JF kama darasa la kuwakomboa kimawazo, maana ni wengi sana kuliko wengi wetu tunavyofikiri.

Haya ndugu zangu sana Fundi Mchundo, Kuhani, Uwiano Maalum, Nyani, Yoursnameismine, na wengineo wote tukaze buti sasa taifa linadidimia hili, ya jana ya jana, ya kesho ya kesho, lakini one day at a time.

Ahsante Wakuu wote, na Mungu Aibariki JF.

Baharia - FMES!
 
Wakuu hapa kazi ipo, mimi nimeona matatizo yafuatayo:-

1) uandishi wa barua siyo makini kabisa. Mhe. ni msomi (Masters holder) tena mwanasheria aliyebobea, inakuwaje aandike barua shallow hivyo! 60% ya barua ni malalamiko kutoka sagem, nilitegemea kuona kiambatanisho A, kiwe malalamiko ya sagem.

2) Sagem walipata vipi taarifa mpaka wakalalamika? Kwanini sagem hawakuilalamikia bodi ya zabuni au katibu mkuu wa wizara?

inaonekana Waziri wa mambo ya ndani hana taarifa kabisa kama kuna chombo cha serikali kinachoitwa Mamlaka ya udhibiti wa manunuzi ya serikali na Bodi ya rufaa ya manunuzi ya Taifa.

Waziri Masha zaidi ya kujua kuwa hana mamlaka ya kuingilia maamuzi ya Bodi ya zabuni alitaiwa pia kujua kuwa hana mamlaka ya kushughulikia rufani za waombaji wa zabuni... Angeielekeza hiyo kampuni kwa wanaohusika na appeals na mambo yake angekuwa fresh tu.
 
Bwana Masha akaandika barua hii kwa Pinda ktk style ya kujitetea kwa kile anachokiita "kuonekana kuitetea SAGEM SECURITE " .Utaona ametambua kuwa amegosea kwa kusema "najua sina mamlaka wala madaraka kisheria kuingilia mchakato huu" baada ya kusema hayo akaendalea na kuanza ku-justify kwa nini kafanya kinyume na sheria.

Ujinga ninao uona katika utetezi wake ni kuwa SAGEM SECURITE imetolewa kwa kutokuwa na kigezo ambacho Bw.Masha anaita " NON MATERIAL DEFECIENCIES " inakuwaje Masha kusema Company hiyo inaonekana tishio? kama tishio kwa nini kwa nini ktk mchakato imeonekana kuwa haina vigezo hata kama vigezo vyenyewe ni non material defeciencies.Ili iwe tishio kwa Alitakiwa kusema kuwa Company hii ina zigezo vyote kisha /kwa nini imetolewa hapo ndio angeweza kusema kuwa imetolewa kwa kuwa ni tishio kwa zingine kama anavyodai.
 
inaonekana Waziri wa mambo ya ndani hana taarifa kabisa kama kuna chombo cha serikali kinachoitwa Mamlaka ya udhibiti wa manunuzi ya serikali na Bodi ya rufaa ya manunuzi ya Taifa.

Waziri Masha zaidi ya kujua kuwa hana mamlaka ya kuingilia maamuzi ya Bodi ya zabuni alitaiwa pia kujua kuwa hana mamlaka ya kushughulikia rufani za waombaji wa zabuni... Angeielekeza hiyo kampuni kwa wanaohusika na appeals na mambo yake angekuwa fresh tu.



ahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa safi sana imekaa vema
 
.......ndg yangu.....uandishi Cabinet paper ni solely responsiblity ya PS sana sana anaweza ku-delegate kwa DPS..........Material inputs kwenye cabinet paper inatoka kwa senior technical/Administration staff........na hii Cabinet paper inapoandaliwa.......kunakuw ana constant liaison kati ya PS na Waziri husika kwani hata Waziri naye anakuwa na input yake ikibidi.........na isitoshe yeye ndiye atakayei-present mbele ya Cabinet.

....cabinet paper ikishakamilika.......PS huiwakilisha kwa CS.....CS ndiye muandaaji wa muhtasari/ajenda ktk Cabinet........CS ndio huandaa extract ya Cabinet resolutions (hii ni SIRI) na kutuma kwa PS........kwa further utekelezaji..........

Unachanganya habari!

Wananchi hawataki kusikia, na cabinet meeting haina muda wa kuchambua, ni bureaucrat gani wa wizara amechangia nini katika paragraph ipi ya ukurasa gani wa taarifa ya Wizara. Waziri anawajibika na ile ripoti nzima nzima, anayoenda kuiwakilisha kwenye cabinet meeting. Simple as that!

Mambo yakiharibika katika waliyoyaripoti au kama kuna uongo fulani, kwa mfano, Waziri hawezi kusema hizo sections za uongo sio input yangu, au eti aseme sikuwa na input popote this time around! Atafukuzwa, atafungwa!

Masha amekataa upuuzi wa kupewa wajibu, mzigo, maswali, lawama na sifa za Waziri halafu kuna underlings wanamzunguka under his nose kupeleka vi-ripoti, kama sio umbea, kwa Katibu Mkuu Kiongozi. Masha anasema - na nilisema yoooote haya jana, almost neno kwa neno, kabla ya hii barua kufumuliwa humu na Invisible - Masha essentially anasema huyo Luhanjo huyo sio bosi wake. Hatakiwi kuingilia kazi za Wizara bila kumshirikisha yeye Waziri. Masha ndio mwisho wa siku anawajibika na hii wizara. Luhanjo hapa ndio ameingilia. Ajifunze namna ipasayo ya ku intervene in ministry's business or keep off!
 
Unachanganya habari!

Wananchi hawataki kusikia, na cabinet meeting haina muda wa kuchambua, ni bureaucrat gani wa wizara amechangia nini katika paragraph ipi ya ukurasa gani wa taarifa ya Wizara. Waziri anawajibika na ile ripoti nzima nzima, anayoenda kuiwakilisha kwenye cabinet meeting. Simple as that!

Mambo yakiharibika katika waliyoyaripoti au kama kuna uongo fulani, kwa mfano, Waziri hawezi kusema hizo sections za uongo sio input yangu, au eti aseme sikuwa na input popote this time around! Atafukuzwa, atafungwa!

Masha amekataa upuuzi wa kupewa wajibu, mzigo, maswali, lawama na sifa za Waziri halafu kuna underlings wanamzunguka under his nose kupeleka vi-ripoti, kama sio umbea, kwa Katibu Mkuu Kiongozi. Masha anasema - na nilisema yoooote haya jana, almost neno kwa neno, kabla ya hii barua kufumuliwa humu na Invisible - Masha essentially anasema huyo Luhanjo huyo sio bosi wake. Hatakiwi kuingilia kazi za Wizara bila kumshirikisha yeye Waziri. Masha ndio mwisho wa siku anawajibika na hii wizara. Luhanjo hapa ndio ameingilia. Ajifunze namna ipasayo ya ku intervene in ministry's business or keep off!

Kuhani heshima mbele,

Ni mawazo na fikra kama hizi ambazo zimetufikisha hapa tulipo watanzania. Kuona kwamba we can always sideline the rules because we know better what are the "national interests". YAANI KWELI MKUU UNAONA MASHA KUKIUKA UTARATIBU NI HAKI, SIMPLY BECAUSE YEYE NI WAZIRI? NASEMA HAPANA!

MBONA WATANZANIA TUNAKUWA WEPESI WA KUSAHAU? JUZI JUZI LOWASSA ALIFANYA EXACTLY THE SAME STUFFS NA KUAMURU TENDA WAPEWE RICHMOND...KISA UMEME ULIKUWA NI URGENT NA KWAKE ILIKUWA NI JUSTIFICATION TOSHA YA KU-SIDESTEP SHERIA. YES, WE ALL KNOW WHAT HAPPENED WITH RICHMOND. UMEME HATUKUPATA, NA MPAKA LEO TUNALIPA MILLION 152! KILA SIKU! POOR WE TANZANIANS!

JAMANI, HIVI KWELI LEO TUNAWEZA KUDIRIKI KUJA KWENYE HII BODI TUKUFU TUKATETEA UOZO KAMA HUU? YAANI SIAMINI KWAMBA WATANZANIA NI WEPESI WA KUSAHAU NAMNA HII! NO WAY! WE CAN DO BETTER!

AU NI YALE YALE YA NYANI KWAMBA WAAFRIKA NDIVYO TULIVYO..TUMESHAKATAA TAMAA..KWAMBA THERE IS NOTHING GOOD WHICH CAN EVER COME OUT OF OUR THINKING?

MASHA ALIKOSEA KABISA! HAPA HAKUNA CHUKI WALA NINI. HAKUNA ANAYEMCHUKIA MASHA, AS SOME PEOPLE WOULD LOVE US TO BELIEVE! PEOPLE CAN SPIN IT THE WAY THEY WANT..ILA UKWELI NI KWAMBA MASHA ALIKOSEA NA INABIDI AWAJIBIKE KIKAMILIFU.

UKIISOMA HII BARUA YAKE..ALIKUWA ANATAFUTA MLANGO WA KUTOKEA, AND ONLY FOOLS CAN TAKE THIS LETTER AT ITS FAC VALUE.

YEYOTE ANAYESEMA KWAMBA HIZI NI CHUKI ZA KISIASA, SITASITA KUSEMA HUYO NI MFINYU WA MAWAZO. YAANI NA LOWASSA KUTUCHEZEA AKILI NA RICHMOND, BADO TUNAONA KWAMBA WAZIRI CAN DISPENSE WITH THE LAW..BECAUSE YEYE NI WAZIRI? DUH! WABONGO KAZI TUNAYO!

WHAT IS STUPIDITY? ITS DOING THE SAME THING OVER AND OVER AGAIN, WHILE EXPECTING DIFFERENT RESULTS. AND THATS WHAT WE ARE DOING.
 
Unachanganya habari!

Wananchi hawataki kusikia, na cabinet meeting haina muda wa kuchambua, ni bureaucrat gani wa wizara amechangia nini katika paragraph ipi ya ukurasa gani wa taarifa ya Wizara. Waziri anawajibika na ile ripoti nzima nzima, anayoenda kuiwakilisha kwenye cabinet meeting. Simple as that!

Mambo yakiharibika katika waliyoyaripoti au kama kuna uongo fulani, kwa mfano, Waziri hawezi kusema hizo sections za uongo sio input yangu, au eti aseme sikuwa na input popote this time around! Atafukuzwa, atafungwa!

Masha amekataa upuuzi wa kupewa wajibu, mzigo, maswali, lawama na sifa za Waziri halafu kuna underlings wanamzunguka under his nose kupeleka vi-ripoti, kama sio umbea, kwa Katibu Mkuu Kiongozi. Masha anasema - na nilisema yoooote haya jana, almost neno kwa neno, kabla ya hii barua kufumuliwa humu na Invisible - Masha essentially anasema huyo Luhanjo huyo sio bosi wake. Hatakiwi kuingilia kazi za Wizara bila kumshirikisha yeye Waziri. Masha ndio mwisho wa siku anawajibika na hii wizara. Luhanjo hapa ndio ameingilia. Ajifunze namna ipasayo ya ku intervene in ministry's business or keep off!

Kuhani,
Kwa muda mrefu Makatibu wakuu wa Kiongozi wanajiona kuwa wao ni next baada ya rais. Hili sasa limekuwa ni kama tatizo la kurithishana. Mara nyingi Katibu Kiongozi hufanya maamuzi au kutoa maelekezo yaliyo nje ya kazi zake. Nakumbuka mzozo kati ya Waziri wa Mambo ya Ndani (Mrema) na CS (Rupia) juu ya kupatiwa hatia ya ukazi daraja 'A' kwa Chavda. CS Rupia ndiye aliyekuwa key player katika suala la kumbeba Chavda kupitia watendaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani. Hali ilikwenda na kuwa mbaya kiasi cha Kumfanya Mrema aonekane kama Waziri boya huku mambo yakipita baina ya CS na PS wa mambo ya ndani. Nadiriki kusema kuwa Masha amejaribu walau kutumia wakati huu kubainisha mapungufu yaliyopo katika utendaji ndani serikali.
Katika hili CS ninahisi ndiyo key player kwani yeye ndiye mhimili mkubwa wa ajira za wale wote waliopo katika tender committe. Umafia ulikuwa unaendelea na huenda Masha alikwishaugundua na hakusita kuweka mambo katika macho ya watu. Sidhani sana kama katika hali hii Masha atapenda akubali kuendelea kuitwa waziri wa Mambo ya Ndani 'jina' asiyeweza kulinda na kutetea maslahi ya taifa na hasa akiwa ndiye Waziri Mwenye dhamana. Ninakumbuka kuwa JK wakati anatembelea wizara za serikali alitamka kuwa kiti chake cha Urais hana ubia na mtu mwingine yeyote na kuwataka Mawaziri kutokuwa na ubia na mtu yeyote katika kufanya maamuzi ya mwisho yahusuyo wizara zao.

Mwisho, bado ninaendelea kuisoma na kuangalia kwa kina uandishi wa barua ile ya KM-MNN ambao unanipa mashaka, kuna kitu nyuma yake.
 
Aliingia kupitia dirishani, sasa anaoneshwa mlango...
 
Back
Top Bottom