Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

..........assuming kweli Masha alikuwa na nia nzuri kwa Taifa........, yet kwa approach aliyotumia.......tena kwa singleout SAGEM.......ndio inamfanya aonekane bwege mtozeni kweli kweli kwani kajiweka kikaangoni........na sasa anajikaanga kwa mafuta yake mwenyewe...........tunashukuru tumepata taarifa.....however kijana Masha...............kalikoroga....period

Kuhani......
.....kuna mtu aliomba nimuleweshe kuhus hizi cabinet paper na maswala mengine........
kuhusu Luhanjo......just check his jurisdiction ya mawasiliano yake na ma-PS.........kama hujui sema uambiwe.........
.....Hata kama Waziri akishindwa kujibu baadhi ya maswali.........wakati wa Cabinet meeting.......watu walioshiriki (hata technical officers ikibidi) huitw akutoa ufafanuzi.......ni normal practice........wala hakuna kitu cha ajabu........


Pundamilia..............
.......Masha hajaoyesha mapungufu ya utendaji serikalini..............ila yeye ndio kaonyesha UDHAIFU katika utendaji wake............
 
..........assuming kweli Masha alikuwa na nia nzuri kwa Taifa........, yet kwa approach aliyotumia.......tena kwa singleout SAGEM.......ndio inamfanya aonekane bwege mtozeni kweli kweli kwani kajiweka kikaangoni........na sasa anajikaanga kwa mafuta yake mwenyewe...........tunashukuru tumepata taarifa.....however kijana Masha...............kalikoroga....period

Kuhani......
.....kuna mtu aliomba nimuleweshe kuhus hizi cabinet paper na maswala mengine........
kuhusu Luhanjo......just check his jurisdiction ya mawasiliano yake na ma-PS.........kama hujui sema uambiwe.........
.....Hata kama Waziri akishindwa kujibu baadhi ya maswali.........wakati wa Cabinet meeting.......watu walioshiriki (hata technical officers ikibidi) huitw akutoa ufafanuzi.......ni normal practice........wala hakuna kitu cha ajabu........


Pundamilia..............
.......Masha hajaoyesha mapungufu ya utendaji serikalini..............ila yeye ndio kaonyesha UDHAIFU katika utendaji wake............

Sidhani kama Masha alihitaji kutoa maelezo yake kwa kutokuwa straight forward kwenye issue. huyu ni mwanasiasa wa kizazi hiki, kama kuna spade anatakiwa aiite spade na wala si vinginevyo. Hii mambo ya kusema kuwa alitaka kuipendelea Segem sioni kama lina uzito katika stage hii ya mwanzo. Katika maelezo yake Masha ambayo aliyatoa kabla ya hao baadhi ya wapenyezaji kufanya hivyo, alibainisha wazi nini nafasi yake kwenye wizara na wajibu wake kama Waziri mwenye dhamana katika wizara ya mambo ya ndani. Angalizo la Masha ni muhimu kwake kama Mkuu wa wa Wizara, kwa vyovyote vile mambo ambayo yangeweza kumkuta Masha huko mbele ya safari labda hata kama ni baada ya miaka 5 nadhani ingekuwa ni mbaya.
hata hivyo intervention ya Masha, haipo kwa ajili ya kuzuia process ya tender zaidi ilikuwa inataka kuimarishwa kwa uwazi katika zoezi zima.
I support him kwani he was right kama Waziri wa MNN.
 
Mfumo tulionao tumeutoa kutoka kwa waingereza. The civil service imetengwa na utawala wa kisiasa kwa sababu zifuatazo:

1. Utendaji wa serikali usitumiwe kisiasa. Waziri asihamishe resources ( watu na mali) kutokana na sababu za kisiasa. Kwa vile Katibu Mkuu ndiye mwenye mamlaka ya kufanya hivi ni wajibu wake kukataa kutekeleza maagizo ya waziri kama anaona kuwa sabau ni siasa na si ufanisi. Kwenye hili makatibu wakuu wengi walisinzia na kukubali maamuzi ya mawaziri ambayo dhahiri yalielekea katika kujijenga kisiasa na si ufanisi. Wakati mwingine maamuzi haya yaliongozwa na sababu binafsi ( mwamishe fulani kwa sababu simpendi n.k.) na si ufanisi.

2. Kuweka continuity wakati wa mabadiliko ya utawala wa kisiasa. Civil service ni ya kudumu kwa hiyo hata kama chama tofauti cha kisiasa kitaingia, uendeshaji wa serikali utaendelea bila kuyumba.

Kwa hali hiyo, ingawa KM anapokea maagizo kutoka kwa waziri ( Kwa hali hii unaweza kusema kuwa waziri ni bosi wake) ni wajibu wake kuhakikisha kuwa taratibu na sheria zinafuatwa katika utekelezaji. Waziri ni kama board chairman katika kampuni binafsi.

Kwenye suala tunalozungumzia, ni dhahiri kuwa K.M alikuwa na wasiwasi kuwa waziri wake ana sababu nyingine nje ya kutaka ufanisi katika zoezi zima. Kwa hali hiyo ni wajibu wake kupata ushauri kutoka kwa bosi kiutendaji ambae ni Katibu Mkuu Kiongozi. Kuingilia kwa waziri kwenye hili zoezi ni ku-taint the whole process. KMK alikuwa sahihi kumwagiza KM aendelee tu na zoezi maana tofauti na hivyo wataonekana kutumika kisiasa. Na wote tunajua matokeo ya wanasiasa kuingilia technocrats katika utendaji kutokana na sababu za kisiasa. Sababu zinazovishwa koti la maslahi ya taifa.

Suala la waziri kuingilia katika zoezi zima halihitaji kwenda PPRA. PPRA wanatoa ushauri katika namna mchakato ulivyofanyika. Mathlani, je ilikuwa haki kumuengua mzabuni? Hata kama watasema haikuwa haki, kwa maoni yangu hii haimsafishi waziri. Alikosea kuingilia kwa jinsi alivyofanya. Full stop.

Amandla...........
 
Hivi uwazi wa tenda process ni lazima umhusishe Sagem? Kwangu mimi swali la msingi ( hiki ni kitu ambacho hakiwekwi wazi) ni Sagem walijuaje kuwa wameenguliwa? Mimi ninavyofahamu kuwa taarifa ya nani hakupat inatoka BAADA ya zoezi zima kukamilika. Wanaojua awali ni wale ambao wanaonekana mwanzo kabisa kuwa hawakutimiza masharti muhimu. Hawa tenda zao zinarudishwa BILA kufunguliwa. Lakini wazabuni wanaoingia kwenye hatua ya evaluation hawafahamishwi mpaka zoezi linapoisha. Masha kwa kusema wazi kuwa ametaarifiwa na mzabuni inaonyesha kuwa ana uhusiano na huyo jamaa. Kwa hali hii, ni haki kwa KMK kumruka katika mawasiliano yake na K.M. Nina wasi wasi vile vile na madai ya masha kusema kuwa KMK alimwagiza KM apeleke taarifa kwenye Cabinet. KM hawezi kupeleka taarifa yeyote kwenye Cabinet ambako yeye si mjumbe. Kinachowezekana ni kuwa KMK alimwagiza awasilishe taarifa kwenye kikao cha makatibu wakuu wenzake (kinachofanyika Ikulu) ambacho KMK ni mwenyekiti. Kwa kufanya hivi hakuwa na sababu ya kumhusisha waziri maana hiki ni kikao cha utekelezaji. Na hasa ukizingatia kuwa bila shaka moja ya vitu ambavyo vingejadiliwa ni nafasi ya waziri katika zoezi zima.

Kuhani. Katibu Mkuu si underling wa waziri.
 
Ni mawazo potofu kufikiri kuwa open tenda ndiyo itakayo hakikisha kupata the best. On the contrary, mara nyingi makampuni yenye uwezo hayaingii kwenye open tenda. Hii ni kutokana na ukweli kuwa ku-participate kwenye tenda ni gharama na ni kamari. Kwenye open tenda kwa vile vikampuni vya kila namna vinaweza kuingia na ku-ofa the earth basi yale makubwa hayaingii. Makampuni yanayopenda tenda hizi ni yale machanga na yale ya kitapeli. Ya kitapeli yanapenda kwa sababu kutokana na uwingi wa wazabuni basi kuna tumaini na uwezekano wa kutofanyiwa due dilligence ya uhakika. Vile vile nayo yanajua kuwa makampuni ya uhakika hayatajipeleka.

Kwenye specialised case kama hii, ni bora zaidi kufanya restricted tenda. Hii inatokana na ukweli kuwa makampuni yenye utaalamu huu yanajulikana. Ni vizuri kuyaalika ( kutoka na uzoefu wao) ili ya submit tenda. Tenda ya namna hii inakubalika nao maana wanajua kuwa wanashindana na watu wa saizi yao. Mfano rahisi. Kama unataka kuagiza simu za mkononi kwa wingi ( mamilioni), hautangazi open tenda. Unawakaribisha Nokia, Samsung, Sony Ericsson, LG, Apple, BenQ kutenda. Ukitangaza ya wazi kuna hatari ya kuingia mtu atakaekuletea product fake kwa bei ya chini kuliko ya watengenezaji wenyewe.

Kwa kuzania open tenda, siasa ilitawala kuliko ufanisi. Na hiki ndicho kilichotufikisha hapa na mwisho wa siku kutuacha na majuto.

Zoezi na mradi mzima ufutwe. Hauna maslahi kwa taifa.

Amandla......
 
Ukiisoma barua ya Masha kwa makini sana, kwa kiasi kikubwa ilikuwa imelenga ku-counter allegations kwamba kitendo cha yeye kuanza ku-question kwanini SAGEM wametolewa kwenye mchakato alikuwa na nia ya kuibeba hiyo kampuni, hisia ambayo hata sisi hapa tungeipata kama tungekuwa kwenye hiyo Bodi ya Zabuni na hatimaye kuanza kuulizwa maswali ambayo hayana kichwa wala miguu.

Mimi si mtalaam wa sheria, lakini kwa uelewa wangu JOINT VENTURE AGREEMENT (JVA) ni muhimu sana kuliko hata Audited Financial Report ya Kampuni. JVA inaonyesha legal existence ya hiyo kampuni, sasa kama kwenye maelezo yao walisema wanashirikiana na kampuni fulani na hakuna JVA, si tutarudi kule kule kwa akina Richmond ambapo watu walipewa business card na wakaamini kwamba Richmond ilikuwa na uhusiano na hiyo kampuni nyingine na kumbe ni utapeli mtupu. Leo tunataka kurudi huko huko kwa marehemu Richmond, hivi jamani hatujifunzi kutokana na makosa yaliyopita? Financial Report inaonyesha financial status ya kampuni kitu ambacho external auditors wa kampuni wanaweza kufunika bovu na watu wakalishwa kasa.

Ukisoma barua ya Mh. Masha utagundua kwamba yeye kwa mawazo yake anaona JVA ni kitu minor sana. Tunaweza kujikuta tunaingizwa mkenge na kampuni ikidai ina ushirikiano na kampuni yenye jina kubwa na kumbe hakuna ushirikiano wowote.

Je, SAGEM walijuaje kwamba wametolewa kwenye mchakato katika hatua za awali na kiasi cha kwenda kwa waziri kulalamika? Pinda alisema Bungeni kwamba kuna swala la siri kuvuja, nani alivujisha siri? Masha akiwa kama Waziri wa Mambo ya Ndani, kwanini hakutaka kuchunguza hao SAGEM walipataje taarifa hizo ili kama wajumbe wa Bodi ya Zabuni wamevujisha basi ingekuwa nafasi yake nzuri sana kuwa-deal.

Ninachokiona hapa ni kwamba mzizi wa barua ya Masha ni utetezi baada ya kuona Bodi ya Zabuni wameshikilia msimamo wao kwamba hawaoni tatizo kwenye mchakato mzima. Kitendo cha Masha kuanza kuuliza kwanini SAGEM walitemwa kiliwapa hisia hao wana Bodi ya Zabuni kwamba huenda Masha ana nia ya kuibeba kampuni ya SAGEM. Ili kujilinda ndipo akaamua kuandika barua hiyo ambayo naona imejaa utetezi na kulalamika kwamba Luhanjo anamwingilia kwenye wizara yake. Sijaona hata sehemu moja ambayo Masha ametetea maslahi ya serikali ama taifa, kama ni nia njema hata Lowassa alikuwa na nia njema kabisa na alitupatia "BEST DEAL" ya richmond ambayo bado inaendelea kutu-deal mpaka leo hii.
 
Fundi Mchundo na Keil.........

shukrani kwa ufafanuzi wa ziada you are very correct..........kama kuna mtu mpaka sasa hivi haelewi............basi tena

............Unajua kuna watu wameamua kubisha tu ili mradi wanaweza kubisha bila hata kujua wanachobishia..............

ndio maana nilimkubali ndg yangu mmoja aliyeandika......inabidi watu wafundishwe

ba be bi bo bu, a e i o u................
 
Mkuu Keil.
A very very very good point. Mara nyingi kampuni za kitapeli zinadai kuwa zitashirikiana na kampuni inayoaminiwa ( angalia Richmond) ku-legitimise tenda yao. Kama hiyo JVA ( inayoifunga hiyo kampuni nyingine kwenye tenda) haipo basi nini kitamzuia mzabuni kuingiza kampuni nyingine ya kitapeli mara wanaposhinda? Kutoweza kui-submit ni dalili kuwa haukuwepo na makubaliano ya awali. Hapa walitaka kutuingiza mkenge na tenda bodi wanastahili pongezi kwa kuliona hilo badala ya kushutumiwa kuwa wana personal agendaz!
 
Sijasoma chochote kwenye thread hii... lakini jambo lililowazi ni kwamba SAGEM wako juu sana kwenye technologia ya vitambulisho... sitashangaa huyo atakayeshinda kwenda kununua mitambo ya SAGEM kufanya kazi ambayo SAGEM ameambia anaweza...

Mimi niko upande wa MASHA.
 
Sijasoma chochote kwenye thread hii... lakini jambo lililowazi ni kwamba SAGEM wako juu sana kwenye technologia ya vitambulisho... sitashangaa huyo atakayeshinda kwenda kununua mitambo ya SAGEM kufanya kazi ambayo SAGEM ameambia anaweza...

Mimi niko upande wa MASHA.

Sasa kama wako juu kiasi hicho, hiyo joint venture ilikuwa ya nini? Ni dhahiri waliona wana upungufu mahala fulani ambapo hiyo kampuni nyingine ingewasaidia!

Amandla.....
 
Sasa kama wako juu kiasi hicho, hiyo joint venture ilikuwa ya nini? Ni dhahiri waliona wana upungufu mahala fulani ambapo hiyo kampuni nyingine ingewasaidia!

Amandla.....

Nasema hivi... fanyeni uchunguzi mdogo sana... uliziieni makampuni ya Tanzania ya biashara tu... makubwa ambayo yanatumia technology ya access control, ambayo ndiyo hiyo hiyo ambayo itatumika... all most yote yana vifaa vya SAGEM...

Mimi simo.... endeleni na siasa zenu... mheshimiwa Masha kama unasoma thread hii... nipe PM... nikupatie dada za kusema ukweli... Watanzania wakuhukumu kwa kukataa ujinga wa kufuata kanuni hata kama hazilisaidii taifa....

It is just a bullshit.... Masha you are very right brother... kwenye taifa la... ajabu kama hili ukionekana hivyo ujue ndio uko sawa.
 
Nani ana list ya wajumbe wa ile tender committee?

Ninataka kuangalia je, kuna yeyote ambaye si presidential appointee?
 
Sijasoma chochote kwenye thread hii... lakini jambo lililowazi ni kwamba SAGEM wako juu sana kwenye technologia ya vitambulisho... sitashangaa huyo atakayeshinda kwenda kununua mitambo ya SAGEM kufanya kazi ambayo SAGEM ameambia anaweza...

Mimi niko upande wa MASHA.

Mhhh tech ya corruption?......Nigeria watu walifungwa, kwetu je? tusubiri tuone kwani huenda kweli Masha kamkamata mkono kipofu maana hawa jamaa zetu hawaaminiki na kila jambo walifanyalo ni lazima uwe na shaka nalo, hivi Luhanjo si ndio alikuwa KMK enzi za BWM? na ndiye alikuwapo wakati wa Richmonduli? na wakati wa kibali class 'A' cha Chavda? au.......
 
Nasema hivi... fanyeni uchunguzi mdogo sana... uliziieni makampuni ya Tanzania ya biashara tu... makubwa ambayo yanatumia technology ya access control, ambayo ndiyo hiyo hiyo ambayo itatumika... all most yote yana vifaa vya SAGEM...

Mimi simo.... endeleni na siasa zenu... mheshimiwa Masha kama unasoma thread hii... nipe PM... nikupatie dada za kusema ukweli... Watanzania wakuhukumu kwa kukataa ujinga wa kufuata kanuni hata kama hazilisaidii taifa....

It is just a bullshit.... Masha you are very right brother... kwenye taifa la... ajabu kama hili ukionekana hivyo ujue ndio uko sawa.

Bia zake zitakuua mzee
 
Mhhh tech ya corruption?......Nigeria watu walifungwa, kwetu je? tusubiri tuone kwani huenda kweli Masha kamkamata mkono kipofu maana hawa jamaa zetu hawaaminiki na kila jambo walifanyalo ni lazima uwe na shaka nalo, hivi Luhanjo si ndio alikuwa KMK enzi za BWM? na ndiye alikuwapo wakati wa Richmonduli? na wakati wa kibali class 'A' cha Chavda? au.......

wakati wa Chavda katimku mkuu kiongozi alikuwa Rupia, wakati wa BWM , katibu Mkuu kiongozi alikuwa Lumbanga ambaye alipitisha deal la Mahalu kununua Jengo la ubalozi italy
 
Sasa kama wako juu kiasi hicho, hiyo joint venture ilikuwa ya nini? Ni dhahiri waliona wana upungufu mahala fulani ambapo hiyo kampuni nyingine ingewasaidia!

Amandla.....

Joint venture ili kumpata mwekezaji wa Bongo. Ndio mtindo wa kisasa Serikali yetu imejiwekea inapoingia kwenye mradi na makampuni ya kigeni.
 
Joint venture ili kumpata mwekezaji wa Bongo. Ndio mtindo wa kisasa Serikali yetu imejiwekea inapoingia kwenye mradi na makampuni ya kigeni.

Nadhani hapa CS na genge lake walifikiri kuwa Masha ange-bow out halafu ingekuwa business as usual. Lakini kitendo cha Masha kuandika kwa PM kimewaudhi sana wakuu. Kwa hiyo kinachofanyika ni kuhakikisha wanamgeuzia Masha kibao. Trust me, kama masha angekubali kukaa kimya wala tusingejua nini kinaendelea.

Bravo Masha
 
Watu bwana, yaani kwa vile kuna thread nyingi hapa zinasema Masha fisadi, basi na hapa wameng'ang'ana Masha has to go bila kuwa na sababu which is clearly stated.

Hiyo barua haimweki Masha kwenye hatia, na kama kuna hatia basi kuna mawili, either Masha has to Go or hao Makatibu wakuu wawili. What if Katibu Mkuu ndio ali-leak-isha info kwa Sagem? if not what prevailed had Sagem wakalalamika? hili hakuna mtu anayetaka kuliongelea.



Kwa hiyo Masha angesubiri tu taarifa akaisome bungeni, hajui background; then akiulizwa maswali ajibu nini? If that is the system it is more than rotten, bogus and no wonder mambo yanakwenda ndivyo sivyo kila leo.

Kama hamtakubali kubadili hilo lisystem lenu la uongozi, mtaendelea kulia sana...na endeleeni kuendesha nchi kwa mazoea na sio kufuata taratibu.

Hapa hypothesis nyingine inakuwa derived kuwa huko kwenye system kuna cold war between wazee waliozoea kuendesha nchi kwa uzoefu na vijana 'labda' wanaotaka kuendesha nchi kwa kufuata organisational ranks na taratibu.

Sielewi bado bwana Ogah, inakuwaje Katibu Mkuu apeleke taarifa kwa Katibu Mkuu Kiongozi, na Katibu Mkuu Kiongozi atoe rulling on the way forward bila kushauriana na Waziri husika?


Sikatai kwamba Masha has to go, but there is a need to know he has to go on which grounds.

Tatizo la Masha naliona hapa. Kuwa, kama alilalamikiwa kwa mdomo hakutakiwa kuanza kuwasiliana na wengine kwa maandishi kwa sababu akiulizwa hao SAGEM walilalamika wapi atakosa la kueleza. Angewaelekeza SAGEM wapi pa kulalamika, na taratibu zinazotakiwa kufuatwa. Kama SAGEM walilalamika kwa maandishi, Masha asingekurupuka kuanza kuwasiliana na Katibu Mkuu hatimaye Waziri Mkuu. Kwa kawaida barua ya SAGEM angeipeleka kwenye vitengo husika; ama kwa mwanasheria wa wizara au kwa mkuu wa PMU kupata ushauri. Jibu kutoka kwa wataalamu hao lingekuwa kuwa malalamiko yote kuhusu zabuni yanatakiwa kuwepo baada ya mshindi wa tenda au walio-pass pre-qualification kutangazwa (sio wakati wa mchakato). Malalamiko ya kwanza baada ya matokeo kutangazwa yangepelekwa kwa aliyetangaza zabuni ambaye ni Katibu Mkuu, ambaye angeshughulikia malalamiko hayo na kutoa majibu ndani ya muda maalumu kulingana na sheria ya manunuzi. Wasiporidhika wangekata rufaa PPRA.
Masha akiwa mwanasheria hakutakiwa kukurupuka haraka kiasi hicho na hapo ndio anahisiwa kuwa ana self interest. Angetumia wataalamu wake (akalivalia njuga kama EL alivyofanya)
Kwenye sheria ya manunuzi "the best deal" anayoizungumzia Masha, iko kifungu gani cha sheria?
Halafu, zabuni hii ni kubwa, nashindwa kuelewa kampuni inayoomba zabuni kubwa namna hii haijui taratibu za kupeleka malalamiko mpaka wamwandikie waziri! Kwani waliomba kwa waziri? Hapo ndio walakini wa kampuni na Masha unapoanza. Inaonekana kampuni hii iliomba kama "joint venture" na sheria ya manunuzi iko wazi kuwa kama hukuweka hati moja, au hukugonga muhuri pale panapotakiwa unatolewa mwanzo kabisa. Hata hao walioruhusu "audited accounts " za miaka 5 kupelekwa wakati hazikuwepo wakati wa ufunguzi wa tenda walifanya kosa.
Katika taratibu za zabuni zilizo kwenye utaratibu wa "Pre-qualification" hakuna utaratibu wa "conditional pre-qualification. Kwa utaratibu huu wazabuni wanatakiwa kuwa evaluated na kuwekwa kwenye makundi mawili tu. "Pass or Fail". Basi. Kundi lililo "pass" ndilo litakalopelekewa zabuni rasmi za ushindani. Wakati huu itakuwa ni kuangalia the "lowest evaluated bidder".
 
Back
Top Bottom