Ndugu zangu ktk JF, nadhani hapa kuna tatizo la ushabiki na la pili ni kutokujua mfumo wa uongozi ktk wizara. Waziri anawajibika na masuala yote ya kisera na kisiasa ktk wizara, bosi wake ni Rais. Katibu Mkuu anawajibika na masuala yote ya kiufundi na kiutendaji, bosi wake ni Katibu Mkuu Kiongozi.
Watumishi wote wa serikali wapo chini ya Chief Secretary. Sheria za manunuzi ziliwaondoa wana-siasa kujihusisha na mchakato wa manunuzi. Hii ni kutokana na ukweli kuwa wao sio watendaji ktk serikali, ndio maana vigezo vya kumpata Diwani au Mbunge havizingatii elimu au uzoefu alionao.
Tatizo la waziri Masha ktk sakata hili ni kuwa, yeye alizuia mchakato wa kumpata mzabuni, kwa sababu tu, eti kampuni ya Sagem iliondolewa ktk hatua za mwanzo. Ikumbukwe ya kuwa, ktk tenda hii kulikuwa na makampuni 104 yaliyochukua tenda document, na 54 pekee ndio yaliyorudisha.
Utaratibu wa Open enda ni kuwa, kila kampuni iliyoomba itafahamishwa kwa maandishi sababu za kuondolewa kwao, na wale wote walioshinda watafahamishwa kujiandaa na hatua ya pili.
Kila kampuni inaruhusiwa kupinga sababu za kuondolewa kwao. Hatua ya kufanya hivi ni kuwa, kwanza wanamuandikia barua ya kupinga katibu mkuu wa wizara, na kama hawataridhika na majibu, basi watapeleka malalamiko yao kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA), kama hawataridhika na uamuzi wa PPRA basi watakata rufaa PPAA (Public Procurement Appeal Authority). Kila hatua imepewa muda wake kushughulikiwa, hivyo hakuna suala la ucheleweshaji hapo.
Kama kweli Masha alitaka kuisaidia Serikali anayoitumikia, angewashauri Sagem wafuate taratibu hizo za kisheria. Haki ya mtu huwa haipotei, bali huwa inacheleweshwa tu.
Baada ya kutokukubaliana na maamuzi ya Katibu Mkuu wake na tenda bodi yake inayowashirikisha watu mahili toka idara ya usalama wa Taifa na TAKUKURU, Katibu Mkuu aliiamuru tenda bodi iapitie malalamiko ya Masha tena. Baada yakuyapitia na kuichambua vizuri kampuni ya Sagem, bodi ikagundua makosa mengine zaidi, ikayaweka bayana ktk taarifa yao kwa Katibu Mkuu minajili ya kumfikishia Waziri Masha. Kwanini hili halisemwi?
Kwanini Masha alipoambiwa na Sagem kuwa wameenguliwa alikurupuka na kusimamisha mchakato ilhali akijua kuwa kufanya hivyo ni kosa la kisheria?
Kamati ya Bunge inayoshughulikia suala hili mpaka sasa haijamuhoji mtendaji yeyote ktk mradi huu. Ili kuwa sahihi kwa maamuzi stahili, ilitakiwa Kamati imuhoji vizuri Katibu Mkuu aliyepita kwani yeye aliondoka akiwa ameishafana maamuzi yote, Katibu na M/Kiti wa tenda bodi, na Consultants wa mradi.
Suala hili tusifikirie ni dogo kama linavyosomeka. Hapa kuna sheria zimekiukwa, LAZIMA HATUA zichukuliwe.