Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Jamani am experiencing shida kulog in na kufungua JF,hasa mzee invisible kuweka hii kitu!! tatizo lipo kwangu tu ama wote!! wakati mwingine napata page can not be displayed!! mhhhh

Mas
 
Jamani am experiencing shida kulog in na kufungua JF,hasa mzee invisible kuweka hii kitu!! tatizo lipo kwangu tu ama wote!! wakati mwingine napata page can not be displayed!! mhhhh

Mas
That was a technical error, we've corrected.

Thanks to someone who gave me a shout.
 
Kweli hii ndo JF. Ninaikubali sana! Duu!
 
Nasubiri ma pundit waanze kujadili......maana barua imejaa swangishi
 
Fundi, huyu Masha hana rekodi nzuri ya uongozi. Inawezekana kabisa alitaka kufanya ufisadi hapa.

Lakini nakuomba unifanyie hisani moja mzalendo. As hard as it may be, hebu assume kwamba Masha sio fisadi, assume hana rekodi ya erratic pronouncements wala uchafu wowote ule. Let's hypothesize briefly kwamba hapa pia nia yake ilikuwa ni nyeupe kama mwana kondoo, yani kuhakikisha mzabuni atakaeshinda tenda ni wa haki na kweli. Halafu tuangalie, je, alotenda ni sawa? Okay? Thank you.



Sasa bosi wa Katibu wa Wizara ni nani? Well, kwani huo utendaji huo, maagizo anayapata kwa nani? Anatekeleza na kutenda mipango na mwongozo wa nani? Nadhani sio jibu bovu nikisema ni waziri! Luhanjo haamki asubuhi kutuma daily projects kwa makatibu wakuu wa wizara. Na ukikubali kwamba Masha ndio msimamizi na mwongozaji mkuu wa kazi zote za wizara, huoni kwamba Masha yuko sahihi kuulizia na kufuatilia kazi zinazofanywa na wafanyakazi wake, akiwemo mtendaji mkuu, Katibu ? Halafu Masha akiulizia kitu akaona kuna tenda zinaenda kimizengwe (nilikuomba u-assume kwamba Masha alikuwa ana moyo mweupe) halafu akajaribu kuziwahi kabla tenda hajapewa Richmond mwingine wa vitambulisho hapo kosa litakuwa lake au ni mfumo mbovu wa itifaki?

Wewe unaona hakuna tatizo, unasema Makatibu Wakuu walikuwa wamefunikwa na mawaziri. Well, under your model, or the prevailing model, mimi naona ni mgongano wa majukumu kwa sababu organizational entity yeyote lazima iwe na itikafi, mfumo wa ngazi ya utawala, liwe kanisa, liwe duka la wachaga, iwe nchi, uwe msikiti, iwe familia ya kimafia.

Timu yetu ya uchochoroni ilikuwa na kapten, mweka hazina, na katibu. Wote tulikiwa chini ya mwenyekiti.

Nadhani hapa katibu mkuu wa Waziri alikosa, huwezi kumzunguka boss wako. Kitendo cha Katibu mkuu wa waziri Masha kupata maelekezo kutoka kwa Katibu Mkuu kiongozi bila ya Masha kujua, ni sawa na kumzunguka.

Huyo Katibu Mkuu wa Waziri Masha anatakiwa ajieleze inakuwaje anawasiliana na Katibu Mkuu Kiongozi pasipo Waziri kuhusishwa? Na inakuwaje Katibu Mkuu Kiongozi amsikilize Katibu Mkuu wa Wizara bila kuhoji kama Waziri husika alikuwa aware.

Something is wrong somewhere.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nimeiona na nimekupata,Bwana mdogo ameondoka! Dodoma hakukaliki jana usiku nilipishana naye akienda kwa kasi mwendo wa jua ndani ya gari binafsi-Jeusi, namba sikuishika kwani nilishamshamkuta nalo viwanja wakati fulani.

Mwaacheni arudi kijiweni kwake tu.Sasa Jimboni sijui kama kutaendeka tena kweli.!!Wapiga kura wake poleni sana.Bwana mdogo amewaangusha kwa makeke ya kutaka cha juu...............................
 
Wakuu hapa kazi ipo, mimi nimeona matatizo yafuatayo:-

1) uandishi wa barua siyo makini kabisa. Mhe. ni msomi (Masters holder) tena mwanasheria aliyebobea, inakuwaje aandike barua shallow hivyo! 60% ya barua ni malalamiko kutoka sagem, nilitegemea kuona kiambatanisho A, kiwe malalamiko ya sagem.

2) Sagem walipata vipi taarifa mpaka wakalalamika? Kwanini sagem hawakuilalamikia bodi ya zabuni au katibu mkuu wa wizara?

3) Mhe. ameingilia zoezi kwa makusudi huku akijua fika kuwa anafanya kosa kwa kuwa hana mamlaka hayo tena anakiri hilo wazi.

4) Je katibu alifanikiwa kuandika taarifa ya utekelezaji na kupelekwa baraza la mawaziri? Nadhani huo ndo ulikuwa uwanja mzuri kwa mheshimiwa kujimwanga na kutoa sera zake mbele ya Rais, Waziri Mkuu na mawaziri wenzake.
 
Mkuu Invi, shabash..... Hii maneno nzito sana!!!

Mungu Ibariki Tanzania na watu wake!!
 
Wakuu hapa kazi ipo, mimi nimeona matatizo yafuatayo:-

1) uandishi wa barua siyo makini kabisa. Mhe. ni msomi (Masters holder) tena mwanasheria aliyebobea, inakuwaje aandike barua shallow hivyo! 60% ya barua ni malalamiko kutoka sagem, nilitegemea kuona kiambatanisho A, kiwe malalamiko ya sagem.

2) Sagem walipata vipi taarifa mpaka wakalalamika? Kwanini sagem hawakuilalamikia bodi ya zabuni au katibu mkuu wa wizara?

3) Mhe. ameingilia zoezi kwa makusudi huku akijua fika kuwa anafanya kosa kwa kuwa hana mamlaka hayo tena anakiri hilo wazi.

4) Je katibu alifanikiwa kuandika taarifa ya utekelezaji na kupelekwa baraza la mawaziri? Nadhani huo ndo ulikuwa uwanja mzuri kwa mheshimiwa kujimwanga na kutoa sera zake mbele ya Rais, Waziri Mkuu na mawaziri wenzake.


Ukiacha kuingilia mchakato wa zabuni, kama aliingilia (hatujui detailed background, as ilikuwaje waziri akalalamikiwa na Sagem) lakini hadi hapa alikuwa na kila sababu ya kulalamikia kuzungukwa na Katibu Mkuu wake. Inakuwaje katibu Mkuu awasiliana na Katibu Mkuu kiongozi bila Waziri kujua? Walimtega? Pili, Masha alikuwa na kila sababu kulalamika, yaani taarifa iandaliwe bila yeye kuhusishwa, halafu yeye ndio akaiwasilishe kwenye baraza la Mawaziri....angekuwa mbu mbu mbu mzungu wa reli kweli kweli.

Masha had all the rights kulalamika!
 
Last edited by a moderator:
Sure your really ''INVISIBLE SIR'' if these people are smart enough they short relinquish authority and give rooms for others and opportunity for them to learn more about the system for they actually know nothing about what is happening despite being in power since independence.
 
Mkuu dah ulivyo iweka iweka.
Mpaka nimechoka watu bado hawajang'amua kunani huko!
Tunashukuru mkuu kwa DATAZ.
 
Back
Top Bottom