Wazee na uchawi wa mapenzi. Hii imekaaje?

Wazee na uchawi wa mapenzi. Hii imekaaje?

Kwa mwanaume dawa ya mapenzi ya uhakika ni Tigopesa. Hayo mambo ya uchawi wa mapenzi wanatakiwa kufanya wanawake na sio wanaume

. Hao wazee ni mamwinyi na hawanaga akili hao. Kule Liwale kuna mganga mmoja wa mapenzi anatumia UCHAWI WA MTO ( Huu unatajwa ndio uchawi wenye nguvu sana kwenye kumuita mpenzi. Ni uchawi unatengenezwa kwa kutumia tope za kwenye mto unao tembea. Tope zinachukuliwa kwenye pande mbili za mto kulia na kushoto then zinakaushwa na madawa ya porini na panzi walionaswa wakiwa wanajamiiana wakafungwa wakafa hivyo hivyo wakiwa wamenasana wakifanya mapenzi.. Huu uchawi hutumika kumchomea mpenzi anakufuata kesho yake)

Ila sasa kwa huyo mganga ukienda kwake mwanaume halafu akagundua shida yako ni mapenzi ata kwambia ukasubirie nje ukae sehemu ambayo wateja wake wanawake wanasubiria zamu ya kuingia Kilingeni.. Hapo kwake ana wateja wengi sana ,wanawake kwa wanaume. Wanawake wanasubiria sehemu Yao na wanaume wanasubiria sehemu Yao.. Msaidizi wake anakuwa anakuja kuita majina kwa namba ataanza na wanawake watatu kisha baadae wanaume watatu hivyo hivyo Hadi usiku. Sasa wewe kidume ukienda kwa ajili ya dawa ya mapenzi anakuweka pamoja na wanawake na zamu yako inakuwa mwishoni kabisa na usipo angalia zamu yako inaweza kuwa baada ya siku tatu..


Anakuweka ukae pamoja na wanawake kwa sababu amekudharau amekuona wewe akili zako ni kama za wanawake na haustahili kuchangamana na wanaume.


Ni mwanamke ndio anaenda kwa mganga kutafuta dawa za mapenzi. Mwanaume anaenda kutafuta dawa za biashara
Duh hatari.. Kukaa na wanawake hiyo lazima ikuharibu kisaikolojia pakubwa sana
 
Bongotunacheza Ikitokea umemchoka humuitaji tena unamfungua au unamuacha na ndumba zako?

Na wewe unajiwekea ndumba usitamani wengine au hiyo ni upande mmoja tu? Mi naona huo ni ubinafsi.

Kwanza nitakuwa naona kama naishi na msukule. Heka heka za mapenzi zitakuwa hmna. Nikichelewa kurudi ye hewala, akinifumania ye hewala. Kuna uhalisia wa mapenzi utapotea jambo ambalo huenda hata likakufanya mlozi umchoke mapema huyo msukule wako hata kama ulimpenda kwa dhati.
 
Kuna jamaa boda boda mwenzetu alioa demu vidato vingi kichwani wakawa wanasumbuana kuna wazee wakamwambia hao tunaishi nao hivi....kwa namna flan nje nliona mambo iko 'swita swita' sikujua ni alizingatia ushauri au bas tu demu aliamua kutulia.
Yes wanawake bana hawatulii kabisa mpaka najiuliza babu zetu walifanyaje kuwatuliza
 
Jana mtaani kwetu kulikuwa na mechi ya timu ya mtaani kwetu vs timu kutoka Mbande. Sasa Upande nilio kuwa nimekaa kulikuwa na wazee wa kiislamu kadhaa wakawa wanapiga story kuhusu wanawake.. Mada ikawa kuhusu uchawi wa mapenzi..

Kati Yao kuna mmoja ana kama miaka 60 akawa anasema anawashangaa vijana wa siku hizi wanateswa na mapenzi wakati uchawi wa mapenzi upo. Kumchomea mwanamke anakufuata mwenyewe na kumdhibiti kwako asitoke nje ya ndoa maisha yake yote.

Anasema mwanamke huwezi Kukaa nae bila kumdhibiti kwa uchawi.. Wenzake wakawa wanaongea kuonyesha kwamba ni jambo la kawaida. Ndivyo inavyo kuwaga hivi? Je uchawi wa mapenzi kweli upo?
Athari mojawapo ya kutokuwa ndani ya Kristo Yesu ni kuishi maisha ya kutangatanga kama hivi
 
Nimewakuta kwenye maongezi wao kwa wao..
kuna uwezekano mkubwa sana hao wote ni wale wazee wapigaji,
hizo stori walizokua wanapiga lengo ni ili wewe kijana uvutike na kuwapa tension,

wazee na mapenzi wapi na wapi bana, hao wameshafanya sana mapenzi na hakuna wasichokiju kwenye mapenzi,
wanajua tamaa za vijana wengi kwasasa ni mapenzi na kwahivyo wao kama wazee wakionyesha ikiwa wana suluhisho la dawa ya kumpata pisi kali bila kutumia, kijana ukisikia hivyo utaingia tu kwnye18 zao,

but kiukweli hakuna uchawi kwenye mapenzi :NoGodNo:
 
Kanda ya ziwa ndio zao hizo
Kuna mzee mmoja mganga wa kisukuma alimpa kijana wake wa darasa la saba dawa ili apendwe na binti ya mwalimu mkuu. Yule kijana akaimwaga dawa mlangoni mwa darasa, so wasichana wote wakaikanyaga. Wasichana wote wa darasa wakaanza kumpenda kijana, wanamfuata kila anapoenda, yaani kundi zima. Huku wakimwambia "TWINAGI" yaani TUPATIE 😆😆😆
🤣🤣🤣🤣
 
Acha kukaa na wazee wanakuharibu kaa na vijana wenzio gademit😎
Haya mambo ya uchawi wa mapenzi yapo, sema mjini waganga matapeli ni wengi

Mwanaume unaeza ukawa na pesa nyingi, na wanawake wasikutake, wakaishia kukuchuna tu..

Hujawahi ona kizee Cha miaka 55, hakina uchumi mzuri, ila kinalamba vibinti vya miaka 25, 24, saa nyingine ni dawa..


Hapo ndo uchawi unapoingia ShesRise_1
 
Haya mambo ya uchawi wa mapenzi yapo, sema mjini waganga matapeli ni wengi

Mwanaume unaeza ukawa na pesa nyingi, na wanawake wasikutake, wakaishia kukuchuna tu..

Hujawahi ona kizee Cha miaka 55, hakina uchumi mzuri, ila kinalamba vibinti vya miaka 25, 24, saa nyingine ni dawa..


Hapo ndo uchawi unapoingia ShesRise_1
Uongooo 😅
 
Back
Top Bottom