Wazazi acheni uhuni na visingizio, toeni urithi kwa watoto. Elimu sio urithi!

Urithi ungekuwa ujinga hii nchi ingekuwa Yenu??

Itashangaza mtu ni msomi asielwe concept ndogo niliyoieleza, pia itashangaza Kama mtu anaumri wa zaidi ya miaka 25 asielewe mantiki ha kile kilichozungumzwa hapa.
Now mkuu tofautisha Nchi na urithi wa mali these are two different things ni impossible kufanya kuwa mfano wa kuthibitisha ulichoandika ni sahihi in anyway.

Na Nchi sio urithi sababu sio mali ya mtu mmoja bali kila mtu aliyekuwepo nchini basi na yeye ataitwa mwananchi, au unataka kusema kuna mtu mmoja ambaye ameturithisha nchi?

Na ili kukuprove wrong vizuri na mfano wako wa nchi kama kithibitisho cha mtoto kupewa urithi.
Ni hivi yoyote aliyezaliwa nchini ni mwananchi na kuwa mwananchi haaimaanishi kwamba unaimiliki nchi bali ni mshiriki tu na ndio maana unalipia kodi ya ardhi, kodi za vichwa na kodi za aina nyingine, kuna viongozi na serikali, kuna sheria na kanuni.
Na pia ukifanya Utumbo wowote basi unahukumiwa, kifo, kifungo cha maisha nk

Mpaka hapo unaona hiyo nchi ni yako au bure?
Kwanini ufanyi unachokitaka kama ni yako ambayo umerithishwa sijui na nani?

Sababu nchi haiwezi kuendelea bila ya wananchi kufanya chochote ili kuongeza chochote kwenye nchi yao.
Ni lazima ufanye kazi ulipe kodi ili zijengwe shule, hospitali, maji na huduma nyingine za kijamii ambazo zitafanya nchi iendelee na kuweza kusurvive au Nchi itakufa kwa umasikini wa kutisha.

Na kama ilivyo nchi ndivyo ilivyo familia na mali ya urithi.
ni lazima isimamiwe means ipate uongozi na watoto wafanye chochote ili kuendeleza na kukuza hizo mali za urithi ili familia ikue.
Au kila mtu akipewa na kufanya anachokitaka lazima mali ipotee na umasikini kushamiri kwenye familia.

In simple terms as possible ni kuwa mali haitakiwi kurithishwa bali inatakiwa kuendelezwa na watoto.

Ni kama zile familia tajiri ambazo baba akifa na kugawa urithi kwa watoto basi ghafla familia inageuka masikini.
Again urithi ni ujinga unaofanya familia izidi kuwa masikini hii sio opinion bali ni fact na ukweli. utakataa only kama umeamua kukaza kichwa sababu ndivyo ulivyoamua kuamini.
 
Uko sahihi Elimu inaweza isiwe Urithi.

Kwangu mimi mambo ya urithi naona ni ujinga unaofanya familia zizidi kuwa masikini hivyo hakuna kitu nakichukia kama urithi kwenye mambo ya familia...
Familia zote zenye nguvu ya kiuchumi Duniani zinarithisha mali kwa vizazi vyao.
Hii mantiki yako uliyoielezea haina mashiko pia inapingana na uhalisia.
Mfano wa familia zenye mafanikio zaidi ni hizi
The Rothschild family(bankers)
Bush family(politicians)
Sinclair(nobles)
Toyoda family (Toyota)
Lee family(Samsung)
Waltons family
Mars family
Al Saud family
Ambani family
Koch family
Hizo familia zote zimefika hapo zilipo kwa kurithishana mali, kurithi ni suala na uumbaji na muendelezo wa maisha ya binadamu na urthi pekee ulio halali ni ule mtoto kurithi kwa mzazi wake (BABA).
 
Familia zote zenye nguvu ya kiuchumi Duniani zinarithisha mali kwa vizazi vyao.
Hii mantiki yako uliyoielezea haina mashiko pia inapingana na uhalisia...
Sawa mkuu, wamerithi.

Lakini hawajarithi kwa kugawana kila mtu na chake asepe afe kivyake, sababu hivi ndivyo watanzania wengi wanafikiria wakisikia neno urithi. Na ndicho kinachofanyika mpaka leo.

Bali wamerithi kwa kuendeleza kile kilichoachwa na wazazi, wanapambana kwa nguvu zao wenyewe kuendeleza kilichoachwa na waliopita. na bila shaka waliambiwa nini cha kufanya na waliopita ili kuziendeleza au kuna vitabu kabisa na darasa la jinsi ya kukuza mali na utajiri waliorithishwa.

Na sio kwamba wamegawana tu hovyo'hovyo na kila mtu kwenda kivyake au usingesikia wala kujua kama zilikuwepo. na ndio maana mpaka leo unazisikia zinaitwa "family" hata wewe umeziita hivyo, unaona? unarudia kilekile nilichokiandika?

Sasa hiki ndicho ninachokiongelea hapa.
 
Mungu wa Isaka na Yakobo na akujaalie uyatimize maono yako. Urithi kwa vizazi vyetu ndo jambo muhimu. Na hongera kwa kuwa mmojawapo wa wachache tuliolielewa somo hili.
Ni jambo muhimu na wajibu kutoka kwa Mungu, na baraka ndipo zinapoanzia, imagine mzazi anapenda mtoto wake apate zawadi au mambo makubwa kutoka kwa watu wengine wakati yeye mwenye mtoto na wajibu wa kumpa Mali anaona wivu kumpa mtoto wake Sasa hizo bahati anazoomba zimshukie mtoto kutoka kwa watu wengine zitakujaje?
 
Sawa mkuu, wamerithi.

Lakini hawajarithi kwa kugawana kila mtu na chake asepe afe kivyake, sababu hivi ndivyo watanzania wengi wanafikiria wakisikia neno urithi.
Na ndicho kinachofanyika mpaka leo...
Sasa madingi zetu hapa bongo hawapo hivyo mkuu, ukumbuke urithi sio mali pekee bali huambatana na maarifa ya urithi husika ambavyo kwa pamoja hubeba tabia ya familia husika.

Kama alivyosema mtoa mada kwamba maarifa(elimu) sio urithi bali ni siraha/mbinu za kuendeleza urithi. Katoa mfano mtoto wa mkulima atafundishwa kilimo kisha atarithishwa shamba ili atumie maarifa yake kuendeleza maisha.

Leo hii wazee wengi wa kichaga kwa mfano wanawaambia watoto wao hakuna mali ya kurithi wakati huo huo mzee huyo anamiliki kipande cha ardhi kule Kilimanjaro alichokirithi kwa baba yake mzazi na anakitumia kwenda kupumzika kila mwisho wa mwaka.

Wazazi waache uhuni, wahakikishe wanawarithisha mali watoto wao.
 
Nihitimishe kwa kusema tu mtoto wangu lazma nimpe mali aisee! Huu msoto naopitia sio kitoto. Kama ataziharibu atauza atajua mwenyewe ila lazma nimpe njia ya kuishi bila stress
Huu ndio mtazamo chanya aisee, ni lazima mtoto aanzie nilipoishia mimi. Tena kwangu mm kama nisingeachiwa kaurithi sijui hata ningekuwa na hali gani mana mzee wangu alikufa nikiwa bado mdogo sina nijualo kuhusu maisha.
 
Familia zote zenye nguvu ya kiuchumi Duniani zinarithisha mali kwa vizazi vyao.
Hii mantiki yako uliyoielezea haina mashiko pia inapingana na uhalisia.
Mfano wa familia zenye mafanikio zaidi ni hizi
The Rothschild family(bankers)
Bush family(politicians)
Sinclair(nobles)
Toyoda family (Toyota)
Lee family(Samsung)
Waltons family
Mars family
Al Saud family
Ambani family
Koch family
Hizo familia zote zimefika hapo zilipo kwa kurithishana mali, kurithi ni suala na uumbaji na muendelezo wa maisha ya binadamu na urthi pekee ulio halali ni ule mtoto kurithi kwa mzazi wake (BABA).


Hawatakuelewa
 
Ukiona kijana amepata elimu na maarifa halafu bado anaongelea mambo ya urithi maana yake amefilisika kimawazo. Kwani huyo mzazi alipata wapi hizo mali? Kizazi hiki cha Wagalatia kinasikitisha sana, ukiwepo urithi sawa hakuna shida, lakini sio wakung'ang'ania urithi mpaka wengine wamewauwa wazazi wao ili tu wapate urithi. Unaelimu unaujuzi pambana utafute chakwako nawewe uwarithishe wanao na sio kuwazia kupata urithi kwa nguvu kutoka kwa wazazi wako. Nasema Elimu na ujuzi ni Urithi kama urithi wa mali. Kwavile elimu na ujuzi ndio vinaweza kukupatia mali
 
Ukiona kijana amepata elimu na maarifa halafu bado anaongelea mambo ya urithi maana yake amefilisika kimawazo. Kwani huyo mzazi alipata wapi hizo mali? Kizazi hiki cha Wagalatia kinasikitisha sana, ukiwepo urithi sawa hakuna shida, lakini sio wakung'ang'ania urithi mpaka wengine wamewauwa wazazi wao ili tu wapate urithi. Unaelimu unaujuzi pambana utafute chakwako nawewe uwarithishe wanao na sio kuwazia kupata urithi kwa nguvu kutoka kwa wazazi wako. Nasema Elimu na ujuzi ni Urithi kama urithi wa mali. Kwavile elimu na ujuzi ndio vinaweza kukupatia mali

Mtumwa anawaza Kama wewe!

Watawala, wanasiasa, wafanyabiashara Wakubwa na matajiri Wakubwa wanawaza kuacha urithi mpaka Kwa vitukuu alafu Kapuku mmoja anadhani kielimu chake sijui cha degree kitamfikisha wapi😃😃

Elimu bila Rasilimali ni Sawa na Masai mwenye ugoro mdomoni
 
Mtumwa anawaza Kama wewe!

Watawala, wanasiasa, wafanyabiashara Wakubwa na matajiri Wakubwa wanawaza kuacha urithi mpaka Kwa vitukuu alafu Kapuku mmoja anadhani kielimu chake sijui cha degree kitamfikisha wapi😃😃

Elimu bila Rasilimali ni Sawa na Masai mwenye ugoro mdomoni
Hujitambui ndio maana unashindwa kupambanua na kuelewa hoja, unaishia kutukana. Kutukana haikusaidii chochote, sana sana inaonyesha jinsi ulivyomtupu kichwani kwako na hujakomaa. Nilidhani una busara kumbe ni zero kabisa. Na hata elimu yako inaonekana ni ya kubabaisha ndio maana hujiamini. Kutofautiana mitizamo au hoja sio sababu ya wewe kutoa matusi, kwanza huna adabu na hujui unaongea na nani, wengine hapa tumekuzidi kila kitu, hata kiumri wewe ni sawa na mtoto kwangu. Jifunze kuheshimu wakubwa. Hoja inajibiwa na hoja sio matusi kijana wewe. Uwe na adabu kwa wakubwa
 
Hili ni moja ya Bandiko lako Ambalo Sitakaa nilielewee!! Watu tupo makabila na Imani tofauti....Hivi Unafahamu kuna makabila yana utaratibu wao wa kugawa mirathi na Serikali inatambua hilo?
.Hivi Unafahamu katika Dini Kiislamu kuna Utaratibu mzima Umepangwa kuhusu mirathi,Una uhakika gani km unaendana na Huo utaratibu unaotuwekea hapa?? Jaribu kufanya tafiti kwanza kwenye Jamii tofauti Ndio ulete bandiko km Hili hapa....
 
Hujitambui ndio maana unashindwa kupambanua na kuelewa hoja, unaishia kutukana. Kutukana haikusaidii chochote, sana sana inaonyesha jinsi ulivyomtupu kichwani kwako na hujakomaa. Nilidhani una busara kumbe ni zero kabisa. Na hata elimu yako inaonekana ni ya kubabaisha ndio maana hujiamini. Kutofautiana mitizamo au hoja sio sababu ya wewe kutoa matusi, kwanza huna adabu na hujui unaongea na nani, wengine hapa tumekuzidi kila kitu, hata kiumri wewe ni sawa na mtoto kwangu. Jifunze kuheshimu wakubwa. Hoja inajibiwa na hoja sio matusi kijana wewe. Uwe na adabu kwa wakubwa

Sasa wapi nimekutukana?

Kutofautiana Kwa watu ndio unaita matusi?
Hujui kuna wenye mtizamo wa kitumwa kwani Hilo ndilo kwako umeona Tusi?
 
Nikisema kwamba umezaliwa katika familia maskini, unawaonea wivu watoto wa matajiri wa rika lako nitakuwa nimekosea mkuu??. Vipi nikisema wewe una mali ila umezidisha uchoyo, unapenda starehe kuliko kujali watoto. Sustainablity in family wealth should be maintained over the present and future generations. One generation should get its share of wealth or income without limiting the future generations to get wealth. Sijapinga ulichokiongea ila nakushauri uukuze msimamo wako ufahamu kwamba pamoja na hayo uliyoyasema (Kama watoto kuwa komavu kwa kujua kujipambania) mali uliyonayo siyo yako peke yako bali vizazi vyote vya sasa na vya baadae.
Uko sahihi Elimu inaweza isiwe Urithi.

Kwangu mimi mambo ya urithi naona ni ujinga unaofanya familia zizidi kuwa masikini hivyo hakuna kitu nakichukia kama urithi kwenye mambo ya familia.

Urithi unafanya watoto wabweteke wasichangamshe akili kutafuta vyao na kutengeneza mategemezi, hii inapelekea familia kuwa masikini zaidi sababu watoto watakaa kusubiria ufe wachukue chao (kama mzazi ulivyowaaminisha).

Na urithi wa mali ni mpaka mmiliki afe au kama wakikurithisha wakati yeye yupo hai then atabaki na nini?
Pia urithi wa mali unagawanya familia sababu kila mtu atakuwa anachomoa chake na kuondoka na kama hakuna umoja na ushirikiano then hakuna familia wala hakuna nguvu tena.

Na wewe umeshawahi kujiuliza kwanini baba yako haishi kwa wazazi wake?
Unajua jinsi gani baba yako alipata alivyonavyo sasa hivi? Je alitegemea urithi?
Kama hakutegemea urithi kwanini wewe ulilie urithi?

Maana ya Familia ni kukusanyika pamoja ili kuleta ushirikiano na umoja ili kuzalisha nguvu.
Kama ule msemo maarufu wa "umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu"..

Sasa badala ya wazazi kugawa urithi.
Cha kufanya ni kumwambia kila kima mmoja atafute chake na baada ya hapo basi aende kuongezea kwenye mali za familia.
Hii italeta umoja na ushirikiano kwenye familia na kwenye umoja na ushirikiano kuna Nguvu.
Nguvu hii itatumika na itafanya Familia izidi kuimarika kila uchwao badala ya kugawanyika na kudhoofika baada ya kugawana urithi.

Mtu unayempa ugali kila siku lazima atakuja kwako kila siku kufuata ugali, badala ya kumpa ugali mpe njia ulizotumia kuupata huo ugali ili atafute wake.

Mtu ukimpatia urithi haijarishi ni kiasi gani cha mali basi hazitofika popote lazima zitapotea tu na kuisha kabisa.
Sababu hajui jinsi gani umezipata au mangapi umepitia na kuhangaika kiasi gani, hana uchungu nazo wala hajui moto wa jiwe.
Na hiyo ndio sababu familia tajiri huwa masikini ghalfa baada ya mmiliki kufa na kurithisha mali kwa watoto.

Lakini ukimwambia na kumfundisha njia ulizopita mpaka kupata vya kwako na yeye apite hizo'hizo mpaka kupata vya kwake.
Basi lazima atakuwa na uchungu wa mali zake kutokana na msoto aliopitia na atakuwa na nidhamu nazo na kamwe hatojaribu kuzichezea na kuzipoteza kizembe. hivyo hata zile za kwako atakuwa na uwezo wa kuziendeleza.

Kulilia Urithi ni dalili ya Uvivu wa kimwili, kufikiri na kiakili na ni vibaya zaidi ukimfundisha hivi mtoto wa kiume sababu ataamini ni haki yake kupewa now that's really bad.
Sababu mtoto wa kiume anatakiwa afundishwe kupambana na kutafuta vyake mwenyewe no matter what.

Wanangu nitawaambia jinsi ya kupamba na maisha na kuwa adaptable na mazingira yoyote huku wakiendeleza nilichokianzisha kwa kuongeza vya kwao juu yake haijalishi ni wakike au wakiume wote nitawakazia kibabe ila wakiume itakuwa more severe..
Ni kufight till you drop dead hakuna cha bure hata kama nnilikuz
 
Hili ni moja ya Bandiko lako Ambalo Sitakaa nilielewee!! Watu tupo makabila na Imani tofauti....Hivi Unafahamu kuna makabila yana utaratibu wao wa kugawa mirathi na Serikali inatambua hilo?
.Hivi Unafahamu katika Dini Kiislamu kuna Utaratibu mzima Umepangwa kuhusu mirathi,Una uhakika gani km unaendana na Huo utaratibu unaotuwekea hapa?? Jaribu kufanya tafiti kwanza kwenye Jamii tofauti Ndio ulete bandiko km Hili hapa....

Ukiona Jambo nimeandika elewa nimeshalihakiki
 
Back
Top Bottom