MONEY LAUNDERING BADO BONGO SIO KITU CHA MUHIMU.
Nakumbuka kuna mwaka mmoja muheshimiwa Mbowe kipindi hicho akiwa mbunge wa Hai,alisema hatari ya money laundering,kwa kweli kile kitu kiliniingia sana na bahati mbaya waandishi wetu wa habari hawakona umuhimu hilo jamabo.Sijui ni kutoelewa au basi wameona aliyeongea hana maana.
Walichoshindwa elewa ni kwamba Mh Freeman mbowe katembea na ni mfanya biashara wa kimataifa, kaona mataifa mengine, kaona wafanya biashara wanavyohamisha fedha kwa njia haramu kiasi cha kuicha serikali ikikosa fedha za kigeni.
Sasa hapa kuna njia nyingi za kucheza na hii money laundering.Hapa wachumi wetu ndio inabidi waonyeshe thamani ya elimu yao.
Leo nimewawekea hii link kuwafikisha ilipo article ambayo pia inaelezea mambo mengi kuhusu nchi zetu za SADC na uporaji unaoendelea,kupitisha madawa ya kulevya ,kutoroshwa madini na utdahifu wa mifumo yetu ya usalama wa mipaka,mamlaka ya kodi,na vyombo vya sheria.
http://www.iss.org.za/pubs/Monographs/No90/Chap3.pdf
Nategemea watakuwepo watu watakaoangalia hay yote kwa makini na kufanya mabdiliko kwa ukombozi wa nchi.