Watu wa Dar es Salaam muache hii tabia, mnakera

Watu wa Dar es Salaam muache hii tabia, mnakera

Kwanza sioni umuhimu wa kumlazimisha mtu muonane.
 
Hayo ni maono yako. Wewe ni miongoni mwa waliozaliwa Aghakhan au Marie Stoppes. Kama umejitahidi sana labda umezaliwa Ocean Road au Muhimbili. Sijui kama unaijua Sewa Haji Hospital. Sanasana unajua, kama unajua, kuwa Sewa haji ni wodi mojawapo pale Muhimbili kwa sasa.

Endelea kukua kijana. Maana huwezi jua labda mama yako alikuwa girlfriend wangu, kama alikuwa kashafika mjini.

Hahah uwezekano huo upo ingawa nahisi kipindi hicho baba yako bila kubustiwa alikua hawezi kula mzigo nadhan nilimbust baba yako ili jogoo aweze kupanda mzigo ndio ulipopatikana wewe
 
mkuu ukiona wewe unalala, usifikiri kila mtu anapo pa kulala. kuna watu hawajui kesho watakula nini huko majuuu...nishaombwa sana hela na diaspora nikiwa huko, ikabidi nianze kuwakimbia, kila nikimwona nakula kona.

inaonyesha wewe una hela sana....maanake badala ya kwenda SOCIAL SECURITY wanakuja kukuomba wewe hela.
 
Mie cna roho mbaya mliotoswa na ndg zenu hapo Dar, karbu sana kwangu ntawapokea japo naishi nyumba ya kupanga.
 
Maisha ya Dar ni magumu sana kwa watu walio wengi ss anajua akikupokea kuna gharama ataingia usiwalaumu kaka!!!!!!
 
Kuna jamaa yangu anayeishi Dar nilimkopesha tsh 200,000 mwezi desemba 2012 kwa ahadi ya kurudisha ndani ya mwezi 1.
Nina jaribu kumwomba anirudishie anakua mkali,anasema hana fedha kama polisi nimpleke,kwanza yeye ni mtoto wa mjini (dar), hakuna mtu yeyote wa mkoani anambabaisha wa mkoani wote washamba tu na vijidudumtu.

wanaJF uyu bwana katumia defence mechanism ili nisimdai,na mbaya zaidi hatukuandikishia kwani nilimuamini.

je Kuna mbinu yoyote ya kumfanya uyu bwana anilipe? au niandike maumivu? the american dream likes this.
 
Wapo bussy kuuza vichwa, miguu, firigisi na utumbo wa broila
 
Duu mi ndo nimerudi mkoani full mapokezi asubuhi kabla ya chai tunapata kahawa kidogo jioni tunaenda kupata uji kidogo, najiuliza wakinitembelea nitarudishaje hizi fadhila maana mie ni MTU wa ratiba Kali nikiwa jijini
 
Watu wa Dar bwana,

Kabla hujaenda ukimpigia simu anakwambia karibu sana kaka ukija usiache kunitafuta.

Ukifika ukampigia kwanza anakuuliza umefikia wapi, unamwambia nipo Kawe, utaskia nipo Kibaha kuna issue nashughulikia ntakuchek kesho. Kesho ndo hutaiona simu yake ng'oo.

Ukimpigia simu kumwambia kesho naondoka, utaskia mbona fasta kaka, daah sema umekuja bahati mbaya sa hiv nipo taiti kiaina ila ukija tena tutamit tu.

Wote sound zao hzo hzo, utadhani mwalimu wao mmoja.

Afu wao wakija huku wanapopaita mikoani, anataka uwe nyuma yake 24/7, utadhani mnatafuta wadhamini. Stori zake sasa.

Hivi huku mikoani mnaishije? hakuna mzunguko wa hela kabisa.

Hiyo mizunguko ya hela huko Dar ingekuepo si wote mngekua Bakhressa.

Tusiharibiane swaum asee. Acheni hizi tabia, mnatukera sana sisi wakuja.
 
Kula like yako. Ni wahuni sana na inakera sana, kimoyomoyo wanakuita kimeo. Hata kama mmekua pamoja wanafanya ujinga huo huo. Wanajifanya wapo busy sana
 
Wako hivyo hivyo hao , utawasikia mara pesa mkoani taabu, ndorooooobo zenu. Mnaishia kumiliki gari mikweche na nyumba za kupanga

aaahh! isiwetabu mjini watu wanatafuta pesa hatutafuti mtu..by theway Ndoroooobo mwenyewe na wenzako wa mkoani wanaopenda kutafutwa.
 
aaahh! isiwetabu mjini watu wanatafuta pesa hatutafuti mtu..by theway Ndoroooobo mwenyewe na wenzako wa mkoani wanaopenda kutafutwa.

Hua napenda sana mtu akighafirika kwa kuambiwa ukweli, kwakuwa unakuwa umempiga jiwe la gizani na kilio ni ishara limempata. Hakuna mwenye njaa njaa na visenti vya madafu vya mtu, maisha ni social network. Wanatafuta nn, wakati kila kesho yao ni nafuu ya Jana! Kwa takwimu hapa dar kuna maskini wa kipato kuliko mikoa mingi tu. Waganga njaa ndivyo mlivyo, nani anashida na wewe, si viherehere vyenu, Mara tutafutane bana. Be real, uongo uonngo wa nn? Ndorooobo nyieeeee
 
Kumkaribisha mgeni Dar kama mgeni sio mwelewa ni gharama,and then Dar maisha kwa majority ni ya kuunga unga.Watu Dar tunakaa mke na watoto chumba kimoja,au viwili kuanza kutafutana ni kuumbuana,otherwise awe ni close friend,ambaye anajua kila kitu.Then wa Dar wakienda mikoani they are likely kujitegemea na kiasi cha wageni wanaopokelewa mikoani au vijijini au mkoani ni kidogo kuliko wa Dar.Sasa we jifanye mwema kuwa ndio mpokea wageni Dar.Wageni kila siku wapo
 
Mimi mwenyewe nimeishia Dar kwa miaka mingi, kwasasa niko mkoani, na nakiri majibu yangu yalikuwa ya namna hiyo kwa ndorobo wanaoleta kujuana sana wanapokuja mjini
 
Watu wa Dar bwana,

Kabla hujaenda ukimpigia simu anakwambia karibu sana kaka ukija usiache kunitafuta. Ukifika ukampigia kwanza anakuuliza umefikia wapi, unamwambia nipo Kawe, utasikia nipo Kibaha kuna issue nashughulikia ntakuchek kesho.

Kesho ndo hutaiona simu yake ng'oo. Ukimpigia simu kumwambia kesho naondoka, utaskia mbona fasta kaka, daah sema umekuja bahati mbaya sana hivi nipo taiti kiaina ila ukija tena tutamit tu.

Woote sound zao hizo hizo, utadhani mwalimu wao mmoja.

Halafu wao wakija huku wanapopaita mikoani, Anataka uwe nyuma yake 24/7, utadhani mnatafuta wadhamini. Stori zake sasa. Hivi huku mikoani mnaishije? hakuna mzunguko wa hela kabisa.

Hiyo mizunguko ya hela huko Dar ingekuepo si wote mngekuwa Bakhressa. Tusiharibiane swaumu aisee, acheni hizi tabia.

Kweli aisee watu wa Dar mnazinguana sana.
[/QUOTE
hii post ina ukweli kabisa.
 
Back
Top Bottom