Watoto 19 wafa kwenye disco la Idi Tabora

JF counsels must open up case against the owner and NSSF for the families of the deceased to be compensated handsomely.

But though, money can not replace the lost life. Some of these kids would have been the Sittas and the Lipumba!

Asha

Mi nadhani tumtume "freelance investigator" wetu akachunguze ili tuone kama kuna uwezekano wa lawsuit....
 
Hakuna kiasi cha pesa kinachoweza kuwa sawa na thamani ya uhai wa mtoto. Namsikitikia sana Dr Makelele ambaye tunafahamiana, ameumia sana kwa hakika, kupoteza watoto wawili kwa mpigo ambapo ni wiki 3 tu zimepita tangu mama yao alipofariki.

Hapo kuna mambo mengi ya kushughulikia, ikiwa ni pamoja na masuala ya usalama katika majengo yetu na ile kitu wanaimba kila siku ya "disaster preparedness". Hivi tuna mikakati ya uhakika ya kutambua potential disasters kama hiyo na kuzishughulikia preventively kabla hazijatokea? Hapo ndipo pa kuanzia. Walioumia wakisaidiwa kupona kuna maana kubwa, lakini hakika kwa waliokufa hakuna kiasi cha malipo kitakachokaribia thamani ya uhai uliopotea.
 
Hakuna kiasi cha pesa kinachoweza kuwa sawa na thamani ya uhai wa mtoto. Namsikitikia sana Dr Makelele ambaye tunafahamiana, ameumia sana kwa hakika, kupoteza watoto wawili kwa mpigo ambapo ni wiki 3 tu zimepita tangu mama yao alipofariki.

Hapo kuna mambo mengi ya kushughulikia, ikiwa ni pamoja na masuala ya usalama katika majengo yetu na ile kitu wanaimba kila siku ya "disaster preparedness". Hivi tuna mikakati ya uhakika ya kutambua potential disasters kama hiyo na kuzishughulikia preventively kabla hazijatokea? Hapo ndipo pa kuanzia. Walioumia wakisaidiwa kupona kuna maana kubwa, lakini hakika kwa waliokufa hakuna kiasi cha malipo kitakachokaribia thamani ya uhai uliopotea.

Kithuku, search google au yahoo kwa mada hii "Taifa lisilojiandaa kwa majanga"...
 
Binafsi sikutegemea kusikia au kuona watoto wa miaka 7 - 15 wanakwenda night club. Hii ni habari mbaya kwa kweli.
 
Binafsi sikutegemea kusikia au kuona watoto wa miaka 7 - 15 wanakwenda night club. Hii ni habari mbaya kwa kweli.

Nziku haikuwa night club, ni lile disco la mchana. Wengine tunakumbuka pale Tanga kulikuwa na ile Twiga Club (sijui kama bado ipo) na kila Jumapili kulikuwa na disco la mchana kuanzia saa nane hivi. This is what happened. Haikuwa usiku bali disco la mchana siku ya mapumziko ya idi.
 
Yaani kwa kweli hainiingii akilini watoto kujaa hadi kukosa hewa!Hii ni hatari sana mambo ya kupenda pesa!sasa hizo laki tano zitasaidia nini?any way lakini uhai wa mtu huwezi kuulinganisha ni kiasi cha pesa yoyote!lakini ndo laki tano jamani!inauma sana!Hii nchi hii balaa!
 
Yaani kwa kweli hainiingii akilini watoto kujaa hadi kukosa hewa!Hii ni hatari sana mambo ya kupenda pesa!sasa hizo laki tano zitasaidia nini?any way lakini uhai wa mtu huwezi kuulinganisha ni kiasi cha pesa yoyote!lakini ndo laki tano jamani!inauma sana!Hii nchi hii balaa!

Now...this whole tragedy is sinking in me....and it hurts.....and I'm starting to get upset.....and pissed....and livid....
 
Jamani Mhindi katunzwa ili hasira za wadanganyika ziishe .Wahindi hawa ndiyo wafadhili wa CCM kila mkutano utaona Vijana CCM na Kamba toka Chamani wanawaitwa wahindi mzee .Leo hii hili kutokea ni sinema zile zile hakuna cha amri wala uchunguzi .Sisi JF ndiyo tutaipa Serikali ukweli kwa maana wao hawaweza kuusema kwa kuwa watajinyima pesa za kampeni .Amini usiamini kesi hii haina kasi wa nguvu kwa kuwa mwenye pesa ndiye kapatwa na hilo .
 
Now...this whole tragedy is sinking in me....and it hurts.....and I'm starting to get upset.....and pissed....and livid....

duh.. tatizo ni watu hawajaangalia the issue at hand na badala yake wajanja wachache wakawa "lets get Mwanakijiji".. they missed the whole severity of the tragedy. Hili ni kubwa kweli. Mara karibu nne mwaka huu mabweni kadhaa ya watoto wa kike yamenusurika kuchomwa moto; hatukujifunza kwenye vifo vya Shauritanga, na nawahakikishia hatutajifunza kutoka hili kwani baada ya muda si mrefu (within hours) ule wimbo usio na kibwagizo wa "mapenzi ya Mungu" utaanza kuimbwa na wananchi wataitikia kama maroboti "yatimilike".

Tukianza kuchambua tukio hili tutaambiwa waacheni marehemu wapumzike jamani, kifo ni kifo. Tutaambiwa na watetezi wa uzembe na waamini wa kutokuwajibika kuwa tusimlaumu mtu, taasisi, au chombo chochote kwani "Bwana ametoa, na bwana ametwaa".

Nakataa rasmi wimbo huo, na waimbe wao waliolaaniwa wao na uzao wao na malipo yao yawe humu humu duniani!
 
WanaJF

Sidhani watanzania wanaosoma makala kama za akina M.M na wengineo wanafika hata asilimia 10. Hata hawa viongozi hawasomi na kama wangekuwa wanasoma leo hii wakurugenzi wa idara zao wangejivunia sana sana maana hao ndo wataalamu. sidhani kama wato wanafurahia mishahara tu ila unapoona umeweka milestone kwenye hili taifa utakuwa happy na kujivunia. siku zote huwa wanaenda kufuatana na matukio, they are not pro active hata siku moja.

Naamini kabisa kila tume inayoundwa inakuja na maoni ambayo yanakosoa mfumo ili kusiwe na chansi ya kufika maafa haya. I used to ask myself maswali haya;
- Kombe alisema magari yote yawekewe milango ya dharura, Je ni mabasi mangapi yamewekewa? Basi la kutoka Korogwe kwenda Magoma lina emergency door? standard yake ikoje?
- Dereva taksi anakamatwa eti hajafunga seat belt, abiria wake je?
- Kuna ugumu gani kwa mabasi ya abiria kuwa na seat belt? Kizimia moto? First Aid Kit? Je, hata kama vizimia moto vipo na hizo huduma za kwanza nani amewafundisha? aliwafunidsha wakaelewa?
- Je, hizi kumbi za starehe ina maana imepatiwa leseni kupitia wapi? si kuna conditions za sehemu kuwa butcher na kadhalika?
- Sawa hatua kali zichukuliwe kwa wale waliohusika, kwa lipi? Kwa sheria mbovu? Kama ni kwa watu kufa basi wawachukue wali walioona kiingilio was much better kuliko maisha ya wale watoto.
- Mwanakijiji, tuna sheria nyingine ni nzuri sna. Je zinatumika? Zina kanuni? Guideline nani anakumbuka kuzitengenezea?

Hizi laki ngapi ni changa la macho lakini TUTAFAKARI, TUCHUKUE HATUA.

Lakini wengi bado tunaamini kuwa haya ni mipango ya Mungu, viongozi wa dini kutoka vyuo vikuu ya kidini kule wapi kuleee na makumira, what are you doing? Better take out all holy buildings mana ndo chanzo cha ujinga huu.

Asanteni sana
 
Tume lazima itaundwa, JK bwana...........Inasikitisha mno kuona kwamba wakuu wetu huwa wanadeal zaidi ya namna gani watakuwa perceived kuliko utatuzi wa tatizo...Sasa tuataanza kusikia kauli za kukurupuka muda si mrefu!!!!!!

All in all Mungu apumzishe salama roho za malaika hawa.
 
Tanganyika Nchi ya amani na utulivu mashida tunakufa nayo , Nchi ya usanii na wasanii wa aina zote , Nchi ya wajanja wa kuandikla report na hotuba tamu lakini wanaongoza kwa rushwa, ujuha, wizi, Umimi, na ujambazi kama huu wa tarime sasa
 
duh.. tatizo ni watu hawajaangalia the issue at hand na badala yake wajanja wachache wakawa "lets get Mwanakijiji".. they missed the whole severity of the tragedy. Hili ni kubwa kweli. Mara karibu nne mwaka huu mabweni kadhaa ya watoto wa kike yamenusurika kuchomwa moto; hatukujifunza kwenye vifo vya Shauritanga, na nawahakikishia hatutajifunza kutoka hili kwani baada ya muda si mrefu (within hours) ule wimbo usio na kibwagizo wa "mapenzi ya Mungu" utaanza kuimbwa na wananchi wataitikia kama maroboti "yatimilike".

Tukianza kuchambua tukio hili tutaambiwa waacheni marehemu wapumzike jamani, kifo ni kifo. Tutaambiwa na watetezi wa uzembe na waamini wa kutokuwajibika kuwa tusimlaumu mtu, taasisi, au chombo chochote kwani "Bwana ametoa, na bwana ametwaa".

Nakataa rasmi wimbo huo, na waimbe wao waliolaaniwa wao na uzao wao na malipo yao yawe humu humu duniani!

Na hizo laki 5 bado hazijakatwa kodi na wajanja! Wimbo tutaimba na hakuna litakalofanyika.

Idadi ya watu wanaoruhusiwa kwenye kumbi ni kutokana na uwezo wa kubali hewa na milango ya kutokea ya tahadhari. hauwezi kuwa na ukumbi wenye mlango mmoja wa tahadhari! Milango ya tahadhari ni lazima iweze kufunguka lakini angalia tunavyowekea grilli kuzuia vibaka na wapenda dezo!

Wahusika hapa ni wengi. Kuanzia mwenye jengo, mwenye ukumbi na aliyetoa kibali cha chumba hicho kutumika kwa burudani.

Hapana. Tutalia leo lakini kesho kama kazi mpaka mauti mengine yatukute!
 
Na hizo laki 5 bado hazijakatwa kodi na wajanja! Wimbo tutaimba na hakuna litakalofanyika.

Idadi ya watu wanaoruhusiwa kwenye kumbi ni kutokana na uwezo wa kubali hewa na milango ya kutokea ya tahadhari. hauwezi kuwa na ukumbi wenye mlango mmoja wa tahadhari! Milango ya tahadhari ni lazima iweze kufunguka lakini angalia tunavyowekea grilli kuzuia vibaka na wapenda dezo!

Wahusika hapa ni wengi. Kuanzia mwenye jengo, mwenye ukumbi na aliyetoa kibali cha chumba hicho kutumika kwa burudani.

Hapana. Tutalia leo lakini kesho kama kazi mpaka mauti mengine yatukute!

Fundi Mchundo, watu wakiacha kumfikiria mtoa hoja na kupima uzito wa tukio wataona kuwa kilichotokea ni kikubwa mno na kinauma mno. Watoto wanahitaji uongozi wa watu wazima, tunapowaona watoto na kuwatendea kama watu wazima tunawanyima haki yao ya utoto. Kama tunashindwa kutengeneza mazingira mazuri ya watoto wetu kufurahia utoto wao, siyo tu tunawanyima nafasi ya kufurahi lakini naamini hatuwatendei haki. NSSF na wamiliki waliuandaa ukumbi huo kwa kiasi gani kuwa wa kuchezea watoto?
 
Na wazazi nao wanamakosa kwa nini wawaruhusu watoto wao kwenda kwenye huo ukumbi wakati wanaufahamu kuwa hauna sifa ya kuwa ukumbi wa disko?Majuto ni Mjukuu!
 
Na wazazi nao wanamakosa kwa nini wawaruhusu watoto wao kwenda kwenye huo ukumbi wakati wanaufahamu kuwa hauna sifa ya kuwa ukumbi wa disko?Majuto ni Mjukuu!

umejuaje kuwa wazazi walikuwa "wanaufahamu kuwa hauna (huo ukumbi) sifa ya kuwa ukumbi wa disko"?
 
umejuaje kuwa wazazi walikuwa "wanaufahamu kuwa hauna (huo ukumbi) sifa ya kuwa ukumbi wa disko"?

Ukumbi wa mikutano leo wa disco wazazi lazima wanafahamu!wewe huwezi kumpa pesa mwanao akaingie sehemu ambayo huifahamu?au huna watoto nini MKJJ?
 
Na wazazi nao wanamakosa kwa nini wawaruhusu watoto wao kwenda kwenye huo ukumbi wakati wanaufahamu kuwa hauna sifa ya kuwa ukumbi wa disko?Majuto ni Mjukuu!

Usianze kulaumu wazazi wa watoto waliopoteza maisha yao!! Wazazi hao wana muda gani kwenda na kuanza kuchunguza kama ukumbi huo una sifa wakati kuna watu walioajiriwa kwa madhumuni hayo na pengine kuna sheria inayo address code za majengo na matumizi yake. Jamani, hili janga linauma na tafadhalini acheni kulifanyia mzaha. Lazima kuwepo na uwajibikaji hapo.
 
Na wazazi nao wanamakosa kwa nini wawaruhusu watoto wao kwenda kwenye huo ukumbi wakati wanaufahamu kuwa hauna sifa ya kuwa ukumbi wa disko?Majuto ni Mjukuu!

Ni wajibu wa mamlaka husika ( hapa ni manispaa) kuhakikisha kuwa hao wanaopewa leseni kuendesha hiyo biashara wanaifanya katika sehemu salama. Wananchi wa kawaidi wao wanachukua tu kilichopitishwa ni salama. Ni lazima hizi mamlaka za miji ziangaliwe kwa undani na tuhakikishe kuwa kuna sheria zinazoongoza matumizi ya public space.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom