Mazuri ya Rais Samia na Mabaya ya Hayati Dkt. Magufuli

sifi leo

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
5,013
8,369
Serikali sijui mna waza nini dhidi ya historia nzuri za watu hawa kwa waliyo yafanya enzi za uhai wao hapa Duniani. Ni kweli Dr Samia na viongozi walio pita mmejenga malaibrary ya wapendwa wetu huko waliko zikwa

Lakini ni.watanzania wangapi watafunga safari kutoka Sumbawanga,katavi au hata kateshi kusoma historia ya Mwalimu Nyerere?

Nani atakwenda chato kutoka nangurungo kwenda kusoma historia nzuri ya Hayati John pombe Magufuli?

Kwa nini siku ya kumbukizi ya VIFO vyao ndo mnaziunganisha na matukio mengine ambayo hayausiani kiserikali?

Mfano kuunganisha siku cha Mwenge na siku au tarehe ya kifo cha Baba wa Taifa uku mkifanya sherehe zilizo jaaa uzinifu na ubadhilifu wa fedha za Umma kuna uhusiano gani na kifo cha Raisi wa awamu ya kwanza?

Kwa nini siku hiyo vyombo vyote vya habadi visielekezwe kuonesha tu mazuri ya Hayati Nyerere ili watoto wetu watakao kosa nauli za kwenda Makitaba wasikie na waangalie ili waendelee kuwaenzi viongozi wetu?

Tarehe 17/03/2024 watu wamekodi ukumbi pale Mlima City, malaya wamejazana pale nje ya ukumbi wanasubilia watu watakao tokea kwenys kongamano la mama anaupiga mwingi wanunue NYUCHI ZAO.

Kulikuwa na umuhimu gani wa waziri kuwa mgeni rasimi katika kongamano la Mama ameupiga Mwingi ndani ya Miaka mitatu leoo hii siku ya kumbukizi ya hayati Magufuli?

Kibaya zaidi kilichonikera watu wamejaa ukumbini kumsikiliza Mh Waziri hata baada ya waziri kufika hakukumbuka kama leo ni gani walauh awanyanyue walio fika hata dakika moja kumwombea aliyekuwa amemteua kwa nafasi ya Naibu waziri wa kilimo yaani kwa ufupi hakuwa tayari kuchanganya uji na SODA.

Ninayasema haya leo hii naweza onekanika ni mshambenga la hasha ni vyema tuyaenzi mabaya na mazuri ya viongozi tulio pewa hapa Tanzania.

Kabla hatujaanza kusherekea siku ya kifo cha Hayati Mwinyi Mwakank tujisahihi katika ili tunawakosea marehemu

Yawezekana unae soma hapa huwezi nielewa ila ukitaka kujua ubaya wa kuunganisha matukio wewe nenda siku ya kilele cha Mbio zo mwenge uone yanayo fanyika usiku huo na kiwango cha kondomu kinachosanbazwa siku hiyo alafu ukiusishe nishe na historia mbaya na nzuri ya hayati Nyerere.

Ikulu nayo iko kimnya kana kwamba haitambui yakuwa hata walio leo hapo kesho kutwa nao hawatokuwepo

Je, tukiunganisha historia za wanayo yafanya leo wakiwa ikulu na SIKU YA KUMCHEZA MWALI watafurai?au siku kuwatoa wamasai jando watafurahi?

Viongozi wote wenye maono waliyaona haya ndio maana wameamua kuandika vitabu vyao kabla ya vifo vyao mathalani Hayati Mkapa, Hayati Mwinyi, wapo ambao hawajaandika watu kama akina Membe, Lowasa na wengine vijana wa kisasa wanasema imekula hiyo hawatakaaa wakumbukwe maana kama Nyerere tununganisha sherehe ya kifo chake na siku ya kuzima mwenge ambapo mchana miradi uzinduliwe na vigeregere kede kede ila ikifika usiku uzinzi mwanzo mwisho sasa hawa wengine tutawapa ZAWADI YA KUUNGANISHA MATUKIO GANI?

Labda Hayati Lowasa tuunganishe kumbukizi ya siku ya kifo chake na siku ya Maji Duniani au siku Ya elimu Duniani kama haipo tushauri.iwepo kwa sababu alisimamia ujenzi wa.shule za Kata.

Kwa upande wa Membe labda tuunganishe siku ya kifo chake na siku ya kuenz kuzaliwa kwa.viongozi wa.ACT WAZALENDO POLITICAL PARTY.

Najaribu kuwaza historia nzuri za viongozi wetu zinafunikwa kwa masilai gani?hivi kweli unaweza team ya mpira iliyoshinda kwa kumsifisa mfungaji tu paspo kumuunganisha na wenzake kwa maana ya kwanza huyo alie funga alianzia kucheza kutoka gorini kwake mpaka gorini kwa timu pinzani kisha akafunga?

Tunaunganishaje siku ya kifo cha Magufuli na Mafanikio ya utendaji wake?kipi kipya amekianzisha mama kama sio kumalizia miradi aliyoiasisi Hayati Magufuli?unaelezeaje Mafanikio yake pasipo kumpongeza mtangulizi wake?

Hivi kama sio Magufuli kutukinga na maradhi ya Corona kwa kauli zake za kishujaa Dr Samia angeongoza Ng'ombe hapa Tanzania si tungeisha?

Hivi unadhani kama sio hayati Magufuli kuanzisha ujenzi wa Bwawe la Nyerere Nape na Wenzake wangelikaa wawaze kulijenga? Kama sio Raisi Hayati Mahufuli kuanzisha ujenzi wa Daraja la Busisi Ingekaa itokee Raisi Samia afikirie kulijenga?

Nakwambia ukweli maomaji wa kona hii ya JAZA UJAZWE
sikutaniii ni Rais Sana Mh Nape kumshauri Rais Ajenge Daraja kati ya Tanganyika na Zanzubari na sio Busii kigongo sijui kama mnanielewa? Kuweka kumbuku sawa mpaka inafika tarehe 17/03/2020 Dr Samia halikuwa hajawa Raisi wa Tanzania.

Katiba ya nchi ipo wazi alitakiwa kuapishwa kuwa Rais wa nchi ndai ya masaa 24 lakini wakubwa waliikanyaga kwa sababu walikuwa wakikanyagana ilihali katiba iko wazi kabisa sjui walitaka wamzime na Mama wa watu mimi na wewe hatujui

Sitaki kuambanisha haya yanayo endelea na kuunganisha sukari na soda na kauli za wazuri hawafi, ila wabaya ndo wanao kufa, sasa jamani Mtu kama Mzee wetu Ally Hassani alikuwa na ubaya gani Mzee amepumzika akiwa na umri mkubwa unao mnyima hata fursa ya kucheza na malaika kama kweli wapo uko mbinguni sina hakika maana hakuna aliyekwenda na kurudi na majibu na hata Mwana wa Mungu Yessu Kristo hakuna alipo tamka yakuwa wapo mbinguni ila nina jua kitu muhimu alitamka ni kuwa mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa.

Najua utajiuliza kuoa na kuolewa vimeingiaje hapa, Ngoja nikueleze hivi watambua wakati Hayati Magufuri anakata roho hakuwa hata na mkewe pembeni akimfuta kijasho chembamba kilichomtoka wakati anakata roho?

Hiyo ndiyo tafisiri sahihi yakuwa mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa yaani Hayati Magufuli wakati anakata roho akuwa na Baba yake Mzazi hakuwa na mama yake mzazi na hakuwa hata mwanae wa kiume wala hakuwa na Mkewe,inasemekana mkewe alikuwa akiomba Mungu kupitia Rozari Mungu amponye lakini siku za msanadamu imeisha andikwa yakuwa zinahesabika hata uombeje lazima aende kwa Mungu Muumba,sitaki kuwa shahidi wa uongo au ukweli yaani kusema Hayati Magufuli alienda Kwa Mungu Baba maana mimi naamini Mungu yupo kila pahala.

Nina jaribu kuwaza Hayati Mwinyi yeye mtaunganisha siku ya kifo chake na kitu gani ili naliacha kwa msomaji wa kona hii mpya ya JAZA UJAZWE nitafurahi kupitia no zangu hapo chini ukiniandikia na kunieleza siku yake iunganishwe na sherehe ya nini ili kuficha historia yake

Kuhusu Mkapa huyo vijana wanasema imepita hiyo siku yake ikifika anakumbukwa na.familia yake paroko wa kanisa lake alipo kuwa anasali siku hiyo Paroko wa kanisa anavaa joo zuri liliro nyooshwa pasi na kujiandaa kuonekana kwenye Television au tweeter maana yawezekana siku hiyo na wale wakina Umoja Daima media au Jamii forum wakawa wamelala usingizi wa pono au wakaona habari haiuzi tena kwa sababu hata ukienda kuripoti kumbukizi hiyo bahasha ya kaki inaweza kuwa empty ukijikuta wewe mwanahabadi ndo unawatoa wajane wa marehemu kama wasemavyo vijana.

Nina jaribu kuwaza sana sana najiuliza kwa mzee wangu, kipenzi Jakaya Mrisho Kikwete yeye tutasherekea siku yake kwa kuiunganisha na siku ya YANGA DAY? Au Tutaiunganisha na siku ya uzinduzi wa crown media ya mwanamziki Alikiba?maaana ndo tukio nilimwona akicheka.

Najaribu kuwaza siku nikifa mimi Mzee wa JAZA UJAZWE mtasherekea kumbukizi ya kifo changu kwa kununua sana gazeti la Umoja Daima mkute pale kwenye ukurasa wa ZEE LA JAZA UJAZWE mkute mapicha yangu na rafiki yangu Jerome kileo alie niunganisha na Gazeti ili pendwa la Umoja daima tukiwa kwa Manka tunagonga Mvinyo?

Najaribu kuwaza ikiwa kwa Mama yangu Dr na Rais wa Sasa itakuaje?

Najua ndugu msomaji unajiuliza nimewa nini mpaka nikaandika makala hii ila naomba sote tuwaze uwa tunawaenzi vipi ndugu.na jamaa zetu walio tangulia mbele ya haki?je mbinguni ni sehemu haki?
 
Mkuu umemuenzi vizuri, umetimiza wajibu wako. Mengine yaachwe kama yalivyo!
 
Huu utumbo uliovunda hauna soko hapa. Umetupotezea muda tu kusoma, japo sijafika mwisho
 
Back
Top Bottom