annito
JF-Expert Member
- Aug 13, 2013
- 888
- 464
Nyerere, dr slaa, kikwete, uislaam hayo ndo maneno pekee ninayoyaona yakiandikwa na kilaza FF
Teh teh
Amepaona hapa au kapita kimya kimya
Nyerere, dr slaa, kikwete, uislaam hayo ndo maneno pekee ninayoyaona yakiandikwa na kilaza FF
Soma post namba moja halafu nioneshe hayo uyasemayo. Ukishindwa ujuwe kuwe ni fataani. Unajuwa maana ya fataani?
Wazo zuri? HILI NI WAZO MFU!!!Wazo zuri sana. Vipi wakichakachua kura? Vipi wakiwaapisha wawapendao wao wenye chama dola?
Soma post namba moja halafu nioneshe hayo uyasemayo. Ukishindwa ujuwe kuwe ni fataani. Unajuwa maana ya fataani?
Hakuna chama ni taasisi na ccm imeamua kuwa taasisi ya mafisadi hata akishushwa malaika lazima afuate sheria za taasisi ya chama alichopo kuku kuku tu jogoo jina.
Mfano hai ni mwaka 1995 wakati Kikwete alipowania kuwa Rais kwa mara ya kwanza, hakuna asiyejuwa kuwa alishinda ndani ya chama lakini wenye chama hawakutaka, matokeo unayajuwa.
bora alivovyokatwa 1995 mana tumeshuhudia sasa asivofaa kuwa hata katibu tarafa
Wakati tunaingia kwenye mwaka wa heka heka za uchaguzi wa Wabunge na wa Rais.
Nawaasa Watanzania wasichaguwe chama bali wachaguwe kiongozi.
Mfano mzuri ni kama tuliouonesha mwaka 2005, wakati tulipomchaguwa Kikwete kuwa kiongozi mkuu wa nchi hii. Ushindi alioupata Kikwete wa zaidi ya kura 80% ni dhahiri ulikuwa si kwa kuchaguliwa na wana CCM bali hata wa upinzani na wasio na vyama.
Mfano mwingine ni wa John Shibuda, pale alipoihama CCM na kuhamia Chadema, wana CCM wa jimbo lake wengi walimpa kura zao bila kujali yupo chama kipi. Huo ni uzalendo na unaonesha jinsi Tanzania tunavyoweza kufanya maamuzi bila ya kuburuzwa na chama au wenye chama.
Viongozi wazuri tunao, tena tusingoje wale wanaojitokeza tu kuzitaka hizi nyadhifa kwa udi na uvumba. Tutazame katika jamii, tunapomuona anaefaa kuongoza, hata kama si mwanasiasa, bali tukimuona kuwa haa huyu anafaa kuongoza, tumlazimishe, tumsimamishe, tumchaguwe.
Tukianza kuchaguwa viongozi na si chama tutakuwa sisi wenyewe tumeshakuwa viongozi.Tuanze kwa kujiongoza wenyewe kwa kuchaguwa tukitakacho na si kuburuzwa na wakitakacho wenye vyama.
Tukianza hivyo, hata vyama vyetu vitaweka viongozi tuwatakao na si wawatakao wenye vyama.
Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama. Hii si demokrasia tuitakayo na huleta uvunjifu wa amani.
Ni wakati muafaka sasa Watanzania tusikubali kuchaguwa wamtakae wenye vyama, tunataka tuwe na viongozi tuwatakao wananchi tulio wengi. Tunataka na wagombea huru, wasio na vyama pia wawepo, ili tuwachaguwe tuwaonao wanatufaa na si wanaowafaa wenye vyama.
Upo huru na mawazo yako na wengine pia tupo huru na mawazo yetu. Hapa kwenye mada siongelei chama, nnaongelea tutakaowachaguwa.
Punguani wahed.
Safari tuwe makini Rais mwenye wake wengi na maconcubines wa.kutosha si kuchagua.Humu wengine ni concubineswewe kila kitu kikwete.....duh!
Mwambie kesho aweke mada ya tuchague watu tusichague diniSafi sana siku nyingine unakuwa na point nzuri sana dada mwenyezi Mungu akupe Baraka ubaki na busara zako ulizokuwa nazo leo usibadilike sawa.
leo natamani tuwe na undugu, nataman tukumbatiane hata kwa dakika tatu, umetema madiniWakati tunaingia kwenye mwaka wa heka heka za uchaguzi wa Wabunge na wa Rais.
Nawaasa Watanzania wasichaguwe chama bali wachaguwe kiongozi.
Mfano mzuri ni kama tuliouonesha mwaka 2005, wakati tulipomchaguwa Kikwete kuwa kiongozi mkuu wa nchi hii. Ushindi alioupata Kikwete wa zaidi ya kura 80% ni dhahiri ulikuwa si kwa kuchaguliwa na wana CCM bali hata wa upinzani na wasio na vyama.
Mfano mwingine ni wa John Shibuda, pale alipoihama CCM na kuhamia Chadema, wana CCM wa jimbo lake wengi walimpa kura zao bila kujali yupo chama kipi. Huo ni uzalendo na unaonesha jinsi Tanzania tunavyoweza kufanya maamuzi bila ya kuburuzwa na chama au wenye chama.
Viongozi wazuri tunao, tena tusingoje wale wanaojitokeza tu kuzitaka hizi nyadhifa kwa udi na uvumba. Tutazame katika jamii, tunapomuona anaefaa kuongoza, hata kama si mwanasiasa, bali tukimuona kuwa haa huyu anafaa kuongoza, tumlazimishe, tumsimamishe, tumchaguwe.
Tukianza kuchaguwa viongozi na si chama tutakuwa sisi wenyewe tumeshakuwa viongozi.Tuanze kwa kujiongoza wenyewe kwa kuchaguwa tukitakacho na si kuburuzwa na wakitakacho wenye vyama.
Tukianza hivyo, hata vyama vyetu vitaweka viongozi tuwatakao na si wawatakao wenye vyama.
Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama. Hii si demokrasia tuitakayo na huleta uvunjifu wa amani.
Ni wakati muafaka sasa Watanzania tusikubali kuchaguwa wamtakae wenye vyama, tunataka tuwe na viongozi tuwatakao wananchi tulio wengi. Tunataka na wagombea huru, wasio na vyama pia wawepo, ili tuwachaguwe tuwaonao wanatufaa na si wanaowafaa wenye vyama.
Mfano hai ni mwaka 1995 wakati Kikwete alipowania kuwa Rais kwa mara ya kwanza, hakuna asiyejuwa kuwa alishinda ndani ya chama lakini wenye chama hawakutaka, matokeo unayajuwa.
Hivi, Shibuda ni mfano wa kutoa kwa uongozi uliotukuka? Bi Mkubwa? naomba jibu kwa heshima na taadhima