50thebe
JF-Expert Member
- Mar 10, 2011
- 4,139
- 4,119
Mpaka sasa hivi nakisapoti chama. Chama sera zake husimamiwa na nani? Fikiri.
Nimeona unavyohangaika kuhalalisha hoja yako iliyopwaya na inayoendelea kupwaya.
Kwa wakati huu tulionao, wapiga propaganda za Chama ukiwamo wewe dada'ngu ndio mnapaswa mfikiri zaidi jinsi ya kukinasua Chama kutoka hapa kilipokwama.
Hoja hii uliyoianzisha haikijengi Chama unachokitetea. Ni bahati mbaya sana Chama kinakutumaini wewe na wenzio waliomo humu barazani ili kukirejeshea nuru yake inayofifia.
Nikutakie kazi njema. Pia nikuagize UFIKIRI vizuri ili kukikwamua Chama hapa kiliponasa. FIKIRI sawasawa. Maana wanachama wa Chama unachokitetea ambao baadhi yao ni viongozi ndani ya chama na serikali ndio "bora viongozi" kwani kila uchao wanafanya mambo ya hovyo yanayoiangamiza jamii na kubomoa misingi jadidi ya taifa. "Bora viongozi" hawa hawajui kwa nini Tanzania ni masikini wa kutupwa. Ama hujasikia hili pia?
Alamsiki.