Watanzania, Msichaguwe Chama Chagueni Kiongozi

FaizaFoxy

Platinum Member
Apr 13, 2011
93,048
109,404
Wakati tunaingia kwenye mwaka wa heka heka za uchaguzi wa Wabunge na wa Rais.

Nawaasa Watanzania wasichaguwe chama bali wachaguwe kiongozi.

Mfano mzuri ni kama tuliouonesha mwaka 2005, wakati tulipomchaguwa Kikwete kuwa kiongozi mkuu wa nchi hii. Ushindi alioupata Kikwete wa zaidi ya kura 80% ni dhahiri ulikuwa si kwa kuchaguliwa na wana CCM bali hata wa upinzani na wasio na vyama.

Mfano mwingine ni wa John Shibuda, pale alipoihama CCM na kuhamia Chadema, wana CCM wa jimbo lake wengi walimpa kura zao bila kujali yupo chama kipi. Huo ni uzalendo na unaonesha jinsi Tanzania tunavyoweza kufanya maamuzi bila ya kuburuzwa na chama au wenye chama.

Viongozi wazuri tunao, tena tusingoje wale wanaojitokeza tu kuzitaka hizi nyadhifa kwa udi na uvumba. Tutazame katika jamii, tunapomuona anaefaa kuongoza, hata kama si mwanasiasa, bali tukimuona kuwa haa huyu anafaa kuongoza, tumlazimishe, tumsimamishe, tumchaguwe.

Tukianza kuchaguwa viongozi na si chama tutakuwa sisi wenyewe tumeshakuwa viongozi.Tuanze kwa kujiongoza wenyewe kwa kuchaguwa tukitakacho na si kuburuzwa na wakitakacho wenye vyama.

Tukianza hivyo, hata vyama vyetu vitaweka viongozi tuwatakao na si wawatakao wenye vyama.

Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama. Hii si demokrasia tuitakayo na huleta uvunjifu wa amani.

Ni wakati muafaka sasa Watanzania tusikubali kuchaguwa wamtakae wenye vyama, tunataka tuwe na viongozi tuwatakao wananchi tulio wengi. Tunataka na wagombea huru, wasio na vyama pia wawepo, ili tuwachaguwe tuwaonao wanatufaa na si wanaowafaa wenye vyama.
 
Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama. Hii si demokrasia tuitakayo na huleta uvunjifu wa amani.

Umeandika vizuri FF hasa hapo kwenye red.

Unaweza kutoa mifano hai kuhusu chama chako kuhusu hilo?
 
Umeandika vizuri FF hasa hapo kwenye red.
Unaweza kutoa mifano hai kuhusu chama chako kuhusu hilo?

Mfano hai ni mwaka 1995 wakati Kikwete alipowania kuwa Rais kwa mara ya kwanza, hakuna asiyejuwa kuwa alishinda ndani ya chama lakini wenye chama hawakutaka, matokeo unayajuwa.
 
Ni Wazo Zuri.

What if Huyo Wamtakae wananchi (aliyeshinda katika Kura za Maoni) ikiwa ameshinda kwa sababu ya kutoa Rushwa, Je aachwe tu Agombee kwa Kuwa ndilo hitaji la wananchi wa Eneo husika?
 
Naam mawazo endelevu yasiyo na upendeleo wa upande wowote ule.

Safi sana, naamin wamekusikia na watayafanyia kazi mawazo yako. Kila la kheri Double F.
 
Wazo zuri sana. Vipi wakichakachua kura? Vipi wakiwaapisha wawapendao wao wenye chama dola?

Ndiyo inabidi wananchi tusiburuzwe na wenye vyama. Tusikubali kuchaguliwa kiongozi na chama, tuliweza kwa Kikwete, tuliweza kwa Shibuda, kwanini tushindwe sasa?
 
Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama. Hii si demokrasia tuitakayo na huleta uvunjifu wa amani.

Ni wakati muafaka sasa Watanzania tusikubali kuchaguwa wamtakae wenye vyama, tunataka tuwe na viongozi tuwatakao wananchi tulio wengi. Tunataka na wagombea huru, wasio na vyama pia wawepo, il tuwachaguwe tuwaonao wanatufaa na si wanaowafaa wenye vyama.
umeongea jambo la maana,nakubaliana na wewe.
 
nafarijika umelegeza msimamo..si mhafidhina tena...

Kama unanisoma humu JF ungejuwa kuwa kama ningekuwa mhafidhina basi kwanza ningekuwa namsifia Nyerere na hata nisingeyaona makosa yake. Fikiri.

Tundu Lissu kwa kutokuwa mhafidhina na kwa kuweza kuyaona na kuyasema wazi makosa ya Nyerere namkubali, lakini ananikera pale anapoiga sauti za wachungaji wa Jangwani anapowasilisha hoja zake.
 
Huyu ndie anaitwa FaizaFoxy mwanamke anayeipenda ccm pamoja na katiba iliyopendekezwa na wahununi wenye malengo machafu na nchi yetu.

mwana mama huyu baada yakuona mahakama yake ya kiislam(mahakama ya kadhi) ccm hawataki kuyatekeleza, sasa naona amepata akili nakuona ukawa ndio mkombozi wake.

taratibu lile jinamizi la ccm limeanza kumtoka.

hongera sana, leo umekuja na mada zuri sana, lakn kaa ukielewa kwamba mgombea tutakayempendekeza wanainchi ni dr.slaa ukate ukumbali ukweli ndio huo.
 
Last edited by a moderator:
kama tukifuata mtu badala ya chama ccm kuna mtu gan mwenye sifa ya kuchaguliwa ? maana wote wameshindwa kutatua matatizo ya watanzania sasa ni zamu ya wapinzani
 
Ni Wazo Zuri.

What if Huyo Wamtakae wananchi (aliyeshinda katika Kura za Maoni) ikiwa ameshinda kwa sababu ya kutoa Rushwa, Je aachwe tu Agombee kwa Kuwa ndilo hitaji la wananchi wa Eneo husika?

TAKUKURU wapo na kila mwaka wanazidi kupata uzoefu na sisi wenyewe inabidi tuwe macho. Tunapoona kuna kutoa na kupokea rushwa tusifumbe macho.
 
Back
Top Bottom