Kiingereza ni Lugha tuu... Maarifa hayana Kabila dini wala lugha.. wewe ukijua engine inafanyaje kazi ..kwa kifupi umejua... ueleze kwa kijapani kwa kiingereza au Kisukuma unaelezea namna engine inavyofanya kazi periodt.
Nice.
Sasa tatizo sio kwamba English ni lugha tu.
Bali tatizo English ndio lugha inayotumika kimataifa.
Kuna wachina wanakuja hapa kila siku, na uwezo wao wa kuongea kiswahili ni sifuri na uwezo wao wa kuzungumza kiingereza ni zero.. ila wanakuja na wanatalii na kurudi kwao... Maswala ya wakalimani hayajaanza leo na hayataisha leo
So unadhani ni kawaida kwa mtu kutumia almost 10 years kujifunza kwa English then anatoka mweupe kwenye English.
Sababu wachina hawawezi kumudu English wala kiSwahili na wanatumia wakalimani.
Wachina hawatumii English wala Kiswahili kwenye mifumo yao hivyo hakuna cha ajabu wao kushindwa kumudu Kiswahili wala English.
Ila ingekuwa ajabu wao kushindwa kumudu kichina.
Na mkuu watanzania sio wachina.
Kujifunza kwa kiswahili ninamaanisha Watu wazungumze kwa uhuru usio na mipaka wa kimaarifa. Mtu akikuelezea juu ya mji wake, timu yake ya mpira au akiuliza kwa lugha yake ya kiswahili huulizwa kwa urefu na upana na kwa namna huru.. Hii inamfanya mtu kuelewa kwa uharaka na urahisi...na kwa namna inayohusisha mazingira yake..humfanya kukumbuka haraka
Well mpaka leo bado kuna watu hawajaweza kumudu Kiswahili.
If you name 3nations that has become successful kwa kuendekeza mapokeo nitakuelewa... Maana I can guarantee you there is none
Mapokeo kivipi kama wao ndio walichangia kwenye uanzilishi?
knowledge is simply contextualized information. Wewe kujua A definition of kinetic energy na huwezi kuiweka into context to solve your problem or enhance your environment..is nothing but an information au umbea... And probably you shouldn't be receiving such info. Its a waste of time.
Well hapo blame mfumo wa elimu.
Na kama ni hivyo hata ukibadilisha tusome masomo yao kwa Kiswahili still itakuwa umbea as you said.
Sababu hutoweza kuapply hayo kivyovyote vile.
English ni essential kwenye ulimwengu wa sasa hizo sababu nyingine hazina mashiko.
Achana na umuhimu wa English duniani.
Haimake any sense mtu atumie 10 years kujifunza kwa English then atoke mweupe.
hilo ni tatizo linalohitaji solutions na sio justifications.
Kama wameshindwa kujifunza na kuitumia lugha tu then hata ukiweka Kiswahili sidhani kama wataweza kutumia hayo maarifa kama lugha tu imewashinda.
Definitely something is wrong.