Nasikitika sana haya nayasikia kutoka kwa mtu ambaye ni muislamu,kama ni muislamu asiye na elimu ya kutosha basi sikulaumu
Ila kama unaelimu yako basi unachofanya ni ujinga,nawe umeingia kwenye mtego na nyimbo zile zile za watu kuisema vibaya Bakwata pasina hoja madhubuti,kwahiyo leo hii wagalatia watupangie lini itskuwa eid? Au tupange eid siku fulani kwakuwa tu eti tunadhalilika?
Umesahau aya hii:
“Wala Mayahudi na Manasara hawatakuwa radhi nawe mpaka ufuate dini yao. Sema: Hakika uongofu wa Mwenyezi Mungu ndio uongofu (wa kweli). Na ukifuata matamanio yao baada ya yale yaliyokujia katika elimu, hutakuwa na mlinzi wala msaidizi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.”
(Surah Al-Baqarah 2:120)
Ikiwa sisi waislamu tuna elimu juu ya mwandamo wa mwezi ,je utawafuata ambao hawajui figh ya dini yetu? Kwahiyo kwako wewe kuwafurahisha watu ni bora zaidi kuliko kufuata misingi ya dini?
Swali kwako dogo la kutafakari,kama wote tunafuata mwezi wa kimataifa,mbona Saudi Arabia hawafuati mwezi mwengine wowote ule usipokuwa ule unaotoka kwao??? Je wao hawajui elimu ya mwandamo wa mwezi?
Usiwe mjinga na kufuata miluzi ya watu,bali fuata haki siku zote,hitilafu ya kuuona mwezi imekuwepo hata kabla ya Bakwata kuwepo ,imeanzia karne nyingi sana huko nyuma,na itaendelea mpaka kiama,usiwe miongoni mwa wajinga