Wapangua ''Vizinga'' tupeane mbinu mbalimbali

Wapangua ''Vizinga'' tupeane mbinu mbalimbali

Kuna kidemu bhana juzi kati kinaliaa liaa shida niliwah piga one time nikapotezea ikabak tu chatin za kawaida

Sasa juzi kinasema nina shida ya laki tatu baba kalazwa MOI nikajajibu sipo vzur sana ila ukija kuleta msosi nishtue tuonane siwez kukosa kitu cha kukupa kama msaad kidog mpka navoandika hapa itakuwa chakula hakijaivaa😂😂😂

Kalitaka kunipiga mzinga pasipo kujua muhimbili ndo mitaa yangu hapaa ngomaa ika fail
 
Mbinu kiboko kuliko zote ni kumuwahi mpiga kizinga kabla hajakupiga. Yaani ile unapokea simu yake tu unamuuliza kulikoni mbona ulikuwa hupatikani? Akianza kujitetea unamkatiza kwa kumwambia nilikuwa nakutafuta nikukope. Au unaanza kumlilia shida kabla hajasema zake hadi anaishiwa pozi.
Hii mbinu nzuri sana.

Kuna jamaa mmoja yeye alikuwa na tabia ya kuombaomba kila akikukuta,basi wadau wakabuni njia wakionana nae tu baada ya salamu wanamchomekea "kaka hauna buku ya karibu hapo nna shida" jamaa anajibu kinyonge hata sina hapa buku basi huyoo anakuwa ushamuwahi.
 
Jibu rahisi ni kusema SINA PESA.
Kwani atakufanya nini?
Wewe simama hapo hapo tu, sina pesa, sina pesa, sina pesa. Hakuna kumuonea huruma wala aibu.

Blah blah zingine zote zitakufanya uingie kwenye mtego wa yeye kukusumbua utadhani anakudai, kumbe wapi.
 
Unajibu tu sina hela, basi. Ukijibu hivyo atajua una hela ila hutaki kumpa kwa hiyo kwa ethics za taaluma yao atajiongeza.

Hapo kwa watoto wa bweni/vyuoni kama unazungumzia hawa wa kuwazaa, mzinga haukwepeki. Mzazi ukiwa mkoloni mtoto anakupiga kwenye michango hewa.
Hapo list ya mahitaji inaandikwa mpaka photosynthesis 30,000 hippopotamus 25,000😀

Everyday is Saturday................................😎
 
Kuna mshikaji wangu mmoja huwa tunasaidia kwenye hizo mambo, tume-create kbs zile auto reply text tumeiandika "nipigie jifanye unanidai" akitokea tu mtu ninaona huyu uelekeo ni huo namsukumia jamaa text ananipigia anaanza kunida kwa vitisho na mikwara. Basi mi najibu kinyongeee lkn kumbe ndo nampoteza maboya yule anataka kunipiga vizinga.
 
Back
Top Bottom