Wapangua ''Vizinga'' tupeane mbinu mbalimbali

Wapangua ''Vizinga'' tupeane mbinu mbalimbali

Weka kisa chako na jinsi gani ulivyo fanikiwa kwepa kizinga au kukidhibiti.

Iwe katika mausiamo,bishara hata kwa watoto wakiwa bweni au vyuoni mana nao wameingia kwa kasi.

Nb:Ni kwa faida ya kujikinga kuvunjwa goti.
Utaskia
Niaje ofisa,namna gani?
Niko na ishu nakimbizana nayo nimepelea sh 50 elfu ,nitoe mzazi keshokutwa nakurefund.

Unajibu

SINA , huu ni ukatili haha
 
Me nshawai kushuhudia Niko bar ,then pembeni amekaa msela na demu. .wameagiza kitimoto sasa katkati ya story jamaa akamuuliza demu
Vipi tukitoka hapa tunaenda home?
Demu akagoma akasema siku ingine ,bhac yule jamaa akaongea kwa sauti Hiyo kitimoto funga ntaenda kulia nyumbani doh! Dada aliona aibu Sana lakini muhuni alikua serious
Kuna watu wagumu Sana kwenye Pesa zao
Mwamba atakuwa anaishi Kimara bonyokwa au buza
 
Kuna baadhi ya mbinu huwa zinakuwa ngumu kuchomoka.

Ila mimi ukiniruhusu nikaongee na simu nje ya eneo la tukio...ujue utasubiri mpaka kukuche, labda unisindikize.

Naenda kubeulia ofa zako home kwangu.
Kuna Uzi humu uliletwa,jamaa amefanya utafiti wake akagundua kuwa wanawake wanapenda pesa zaidi kuliko ng.ono, na bado watu wakabisha.
 
Utaskia
Niaje ofisa,namna gani?
Niko na ishu nakimbizana nayo nimepelea sh 50 elfu ,nitoe mzazi keshokutwa nakurefund.

Unajibu

SINA , huu ni ukatili haha
Apo kuvaa ubinadamu nawe ndo unatumia formula ya kumuwahi mpiga kizinga na kumwonyesha nawe unashida vibaya mnoo

"Kiongozi uwezi amini apa natoka marejesho siunaelewa aya mamikopo ya bank kunadi kibanda changu siku yoyote chif

Na hivi TRA wanachanganya,biashara haiendi"
Alafu unasikiliza respond itakuwavipi
 
Nimetoka kukopa sasa hivi hali mbaya ndugu yangu


Nimetuma nyumbani sasa hivi mama anaumwa


Mi mwenyewe nilikuwa nataka nikukope sina kitu sema we umeniwahi


Au zima laini anayoijua kama unazo mbili



Akikupigia simu jifanye kama humskii kata akituma message usiijibu .utaijibu baadae ungeniambia mapema mi hela nishaitumia



Nitaendelea ......
 
Nimetoka kukopa sasa hivi hali mbaya ndugu yangu


Nimetuma nyumbani sasa hivi mama anaumwa


Mi mwenyewe nilikuwa nataka nikukope sina kitu sema we umeniwahi


Au zima laini anayoijua kama unazo mbili



Akikupigia simu jifanye kama humskii kata akituma message usiijibu .utaijibu baadae ungeniambia mapema mi hela nishaitumia



Nitaendelea ......
iyo ya mwisho kiboko yani Kama unamleta mgipa kizinga alafu unamkataa tena
 
Kiini cha tatizo ni nini???

Kwanini kumekuwa na vizinga vingi kila uchao????

Ni ukata wa pesa au nini....???

Jibu ni: The rate of dependence ratio is high than working population

Ndio...watu tegemezi ni wengi kuliko wazalishaji...

Ukinipiga kizinga kama nawewe nakupigaga au nanufaika na wewe kwa namna yoyote kuna walakini wa kukupa kinyume na hapo ni hola

Quid pro quo....

Economic point of view...
 
Kiini cha tatizo ni nini???

Kwanini kumekuwa na vizinga vingi kila uchao????

Ni ukata wa pesa au nini....???

Jibu ni: The rate of dependence ratio is high than working population

Ndio...watu tegemezi ni wengi kuliko wazalishaji...

Ukinipiga kizinga kama nawewe nakupigaga au nanufaika na wewe kwa namna yoyote kuna walakini wa kukupa kinyume na hapo ni hola

Quid pro quo....

Economic point of view...
"Friend with benefits"
Nzuri hiyo
 
MREJESHO:

Nimefanikiwa kuzima vizinga vitatu kwa mkupuo
(1)
Cha mtumishi mwenzangu; huyu huwa tunawita Yahaya si jina lake halisi kaja na gia ya niazime 80k nitarejesha nikamuwahi fasta "unakumbuka January nilikupa mchongo nataka kufungua mradi wa ufugaji kuku apa uwezi amini nimetoka kopa mifuko 5 ya chakula na yote inanisubiri kulipa mwisho wa mwezi huu wakigain weight na kuwatoa ikumbukwe jamaa huwa ni mzee wa mizinga office nzima inamjua.hii njia tunaita muwahi mpiga mzinga kabla hajakomaa

(2)
Ni mchepuko: kamekuja na gia ya pesa ya saluni na pango
Huyu sikupoteza muda nikamwambia SINA
hii ni maususi kwa uliye mla tayari kwani " umeona wapi samaki wa kwenye mtumbwi akapewa chambo tena?"

(3)
Mzinga toka kwa class mate:
Huyu nimepokea simu hajanza kuzungumza tuu nikakata nikawasha airplane mode
Ikumbukwe alianza na txt so ikawa rahisi kubaini simu hii Ni ya mzinga
 
Me nshawai kushuhudia Niko bar ,then pembeni amekaa msela na demu. .wameagiza kitimoto sasa katkati ya story jamaa akamuuliza demu
Vipi tukitoka hapa tunaenda home?
Demu akagoma akasema siku ingine ,bhac yule jamaa akaongea kwa sauti Hiyo kitimoto funga ntaenda kulia nyumbani doh! Dada aliona aibu Sana lakini muhuni alikua serious
Kuna watu wagumu Sana kwenye Pesa zao
 
Kama hiviii
IMG-20210206-WA0084.jpg
 
Hii kitu imemkuta jama yangu mmoja
Mtoto kamchapa kizinga cha field 800k
Kuhamaki kumbe kijana na boom anapokea kabaki kusikitika bao langu linanipanda kichwani.
Kuna rafiki yangu analipiwa kodi ya mwezi kazidisha 50k kwahiyo mzee wake analipa zaidi. Bado anadai hana boom wala ada wakati vyote anavyo na hela ya field anayo. Mwishoni anakusanya pesa nyingi ila anazitumia kwa mademu na hana kitu cha maana ukiachana na gadgets kali.

Atleast kuna wengine wamepiga vizinga wazazi wakaanzisha Juice bar Kigamboni, ila wengi hutumia kwa bata tu. Hasahasa wale ambao baba na mama waliachana na wana uwezo, unakuta hawana mawasiliano mazuri kila hela inalipwa mara mbili.

Wale watoto wa wanyonge hata ada wanaimalizia kwa kutumia boom.
 
Back
Top Bottom