Wanene kuongezewa marupurupu

Wanene kuongezewa marupurupu

sawa! lakini wakiyatoa mawazo hayo hadharani, ni haki yetu kuyakosoa na kuonesha upungufu wake kama vile wao wana haki ya kukosoa na kuonesha upungufu wa mawazo na fikra za wale wanaowakosoa... Kwa vile inaonekana unataka kujua for the sake of kujua tu.. sina la ziada carry on!
 
Double standard ya JF. Sio mara ya kwanza na watu wengine wamelalamikia hili.

Inabidi muangalie! Narudia I am not interested kujua mambo ya ndani ya watu. Rudia hata ile thread ya Zitto Vs Chifupa, sikuwa mchangiaji mkubwa. Lakini as a matter of principle ilibidi kukaa upande wa pili na kutetea consistence kwenye hili.

I hope precedence mliyoiweka hapa mtaiheshimu kwa mijadala mingine yote inayofuata na wengine tutakuwa tayari kuwakumbusheni.

Mambo binafsi ya mtu msiyajadili hata kama huyo mtu ni kiongozi wa taifa. Mumeonyesha kwa Zitto kwamba kuna mambo binafsi na I really hope mutakuwa waungwana na kuwapatia watu wengine heshima hiyo hiyo bila kujali ni Malecela, Sumaye au Muungwana.
 
Halafu kusema "Hawa ndio viongozi wa chama M-badala! kuongoza jimbo tu mnamaliza wake za watu je mkifika huko Ikulu si mtafungua madunguro? heri ya hao wanaofanya biashara Ikulu..."... ni maneno yasiyo na umakini yakipinduliwa upande wa pili. Hivi kuna wana CCM wangapi ambao wamekula wake za watu? Je hujawahi kusikia jamaa ambaye mke wake alichukuliwa na Waziri na yeye mwenyewe akapewa Ukuu wa Wilaya? Hujasikia habari za Kiongozi mmoja ambaye kila akija US wakati huo akiwa waziri alivyokuwa akijifungia ndani na mtu asiye mke wake hadi kukosa vikao muhimu vilivyomleta? Kama tungetaka kuwapigia kelele, mbona tungepiga kelele sana! Siyo kwamba hatujui, tunajua kuna mambo mengine ni ya binafsi na tukianza kuyazungumzia yanataka kutupoteza kwenye mambo muhimu!

In that tone now two wrongs makes one right!... Huyo alyechukuliwa mkewe na kupewa ukuu wa wilaya is as victim as Mpakanja... na huyo Kiongozi alikukuja US is as culpit as Zitto... Kama hukuweza kuanika uozo wake huo ni udhaifu/woga wako mwenyewe na usiutumie kuhahalisha ufuska wa Zitto hapa.

Tuzungumze mambo ya muhimu kitaifa. Swali la usalama wa wake za watu au waume za watu ni masuala ya wenzi wao! Kama ungetuhumiwa kubaka, kunajisi n.k ningekuwa wa kwanza kupigia kelele jambo hilo, hili ni udadisi wa kisiasa tu na kulia chabo (voyerism) maisha ya mtu ambaye tunafikiri "tunamjua". Kama kuna mtu anayetaka kuzungumzia suala hili binafsi wanaweza kukupigia simu na ukazungumza nao kiutu uzima.

Yaani Mbunge kuvunja ndoa ya mtu ni suala binafsi tuliache na tuzungumzie masuala muhimu ya kitaifa! Kwa taarifa yako ktk hili Zitto, kaiba, kazini, kavunja ndoa, kaharibi malezi ( ya mtoto Abdulrahman ) na kaongopa kwa kweli I feel very sorry for young Rahmaninho.

Hili haliwezi kuachwa kwa kisingizio cha masuala muhimu ya taifa. Haya ndio wanaotaka ridhaa ya kutuongoza baadae lazima tuwajadili wapende wasipende. Kama kathubutu kuiba mke wa mtu na kupelekea kuvunja ndoa, atashindwa nini kutuibia hazina yetu tukimpa madaraka. Mwizi ni mwizi tu hata ukijaribu kupindisha kwa tafsiri yeyote, (mambo binafsi, mambo muhimu ya kitaifa nk)


Hivi kuna lolote atakalosema Zitto litakalowaridhisha? Kama mmeshaamua "uroda ale yeye kwa raha zake" sasa kinachotakiwa kujulikana ni nini? Mimi ni mhalisia, siyo mwota njozi. Mnachotaka kujua ni je tunda lilikuwa tamu au la! na ilikuwa kuwaje... Kwa vile Zitto ni mwanachama hapa basi tumefikia mahali pa kuamini kuwa tuna haki na tunastahili habari za maisha yake binafsi. Kwa vile tunahisi tunamjua Zitto basi atuambie sisi washkaji zake mambo yalivyokuwa. Akisema ndiyo amekula, tutaridhika? Akisema hakula tutaridhika? akisema nizungumze kwa wakati wangu muafaka, tutaridhika?

This is more than suala binafsi acha kupotosha, huyu ni kiongozi anatakiwa awe kioo cha jamii. Kufanya ufuska kwa kiwango cha kuvunja ndoa ni jambo lisilo mithilika. Mwenyewe kakiri hapa ktk surgery yake jimboni anahudumia wa wastani wa watu 70 kwa siku, kati ya hao kutakuwa na wake za watu halafu unatuambia mambo binafsi..


Zitto akiamua kuzungumzia sasa hivi sina tatizo ni uamuzi wake, akitaka kuzungumzia mwezi ujao sawa sina tatizo, akigoma kulizungumzia kabisa sina tatizo...ni uamuzi wake! kati ya vitu vilivyoko mawazoni mwangu suala la Amina na Zitto liko mbali kweli!

I hope u could provide the same concession to Mkapa in the doing business from Ikulu saga. Wat a double standards!


amani, watu wote mnaotaka Mheshimiwa Zitto awataarifu kuwa alikula yule mtoto, mnataka atumie lugha gani hadi mfahamu. Kuwa ndiyo nilimtafuta? Ameshatoa jibu ambalo liko wazi kabisa. Kumbukeni kuwa Kabwe ni msema ukweli na katika sakata hili ana majibu mawili tu:

Jibu lipi?

Ingawa ni jambo la kukatisha tamaa kabisa hasa kwa vile kuna watu walikuwa wanamtegemea Mheshimiwa Zitto kuwa na standard kubwa sana na hivyo kutoa mfano wa aina ya uongozi tunaotegemea, ndiyo hivyo tena, maji yaliyomwagika hayawezi kuzolewa tena. Wakati sakata hili bado lina nguvu, niliwahi kuongea na ndugu yangu mmoja pale Dar aliyehappen kuwa anamfahamu sana huyu dada kwa vile walifanya kazi pamoja pale redioni; jamaa huyu anasema mtoto yule ni moto sana, anapenda sana yale majambo ya sirini, na anaweza kumfuatilia mwanamme yeye mwenyewe akimtaka. Jamaa huyu hakushangaa kabisa alivyosikia tuhuma zile kwa vile alitegemea kuwa kuna wabunge kadhaa wanatinga tu na hasa vijana. Kwa vile Zitto naye ni kijana it becomes obvious.

Kwa kama maji yamemwagika huturusiwa hata kujadili? U r now bringing a new twist on this! shifting the burden to AC kwamba amejilengesha? huu usanii at it best....

Ushauri wangu, JF tumwache Mheshimiwa Zitto ajisahaulishe na mambo yale kusudi aweze kuconcetrate kwenye kazi za umma. Pamoja na purukushani ile, bado ana nguvu na uwezo wa kuleta mabadiliko katika mfumo wa bunge letu kama tutamsaidia kuyasahau yale mambo. Yeye siyo wa kwanza kukumbwa na mikasa ya aina hii. Hapa Tanzania wabunge na wanasiasa wengi wanafanya hivyo hivyo, tatizo tu hawajashikwa. President Clinton na President Kennedy walifanya mambo hayo hayo lakini yalikwisha na leo hii legacy yao ni kubwa tu katika historia ya marekani.

This is a very advice.. but why dont we extend it to cover the Lowassa's, JK's Karamagi's etc so as we can give them more time to concetrate on kazi za umma? between Zitto and those afore-mentioned who has more kazi za umma?

Hii ni precedence mbaya sana tunaijenga hapa JF. It sound to me kuna untouchable one humu.

Zitto kafanya ufuska wa kupindukia, kavunja ndoa lakini kwa standards za JF hilo ni suala binafsi tuliache!

Kumbe there one rule for Chadema and another rule for other parties....!!!!!!!!
 
Masatu,

Umeandika vizuri sana. JF ina wenyewe, wanaotaka kuburuza wengine, bahati nzuri kuna watu ambao hutakubali ujinga huo wa double standard.

Nimesikitishwa na double standard ya Mwanakijiji juu ya hili. Kutaka kuwanyamazisha watu wasiseme kwa kisingizio cha mambo binafsi wakati
yeye alirusha mpaka kwenye matangazo yake ya redio ni double standard ya hali ya juu sana.

Watu hao hao kwa wakati tofauti wamemwandika Amina Chifupa utafikiri ni
wao wanamvua nguo kila siku, leo kwa Zitto wanakuja na mambo binafsi.
 
Masatu,

I think you are trying to bit around the bush here. You better come foward and rise your point instead of confusing matters. Kwa ninavyokusoma umeshachagua upande wako halafu unataka watu wandike kama unavyofikiria wewe. Watu wameomba majibu kutoka kwa Mh. Zitto na amesema tumpe muda atazungumza kwenye muda mwafaka. What's wrong with that? Hao wengine unaowasema hawapo humu kujibu hoja zetu ndiyo maana tunapiga kelele ili wapambe wao wawapelekee taarifa. If they could be replying like Hon. Zitto we could not be disscussing one issue for days!!! Anayway, hayo ni maoni yangu.
 
Masatu, nataka nikujibu mambo uliyoelekeza kwangu kama ifuatavyo:

Kwa kama maji yamemwagika huturusiwa hata kujadili? U r now bringing a new twist on this! shifting the burden to AC kwamba amejilengesha? huu usanii at it best....

Maji yameshamwagika baba, hayawezi kuozolewa. Hata ukiuliza mara mia huwezi kubadili kuwa hawakufanya tendo lile kama kweli walilifanya, siyo wizi wa fedha kuwa ukimbana atarudisha fedha hizo. Hii ni kati ya matendo ambayo ni irreversible, hata kama inakuuma vipi itabaki hivyo hivyo. Mimi kuandika hivyo sijamtetea Zitto kwa kufanya hivyo, ila ndio ukweli ambao lazima tuishi nao na wala sijatwist kuweka lawama kwa AC. Dada yule anasemekana ni mwanamke mzuri sana na yuko sexually active. Mimi simfahamu zaidi ya kuona picha zake tu. Rafiki yangu mmoja hapo Dar ndiye alinisimulia habari zake nyingi zaidi ya nilivyoandika pale kwa vile nyingine hazikuwa relevant. Pamoja na hayo ya AC, haikuwa ni vizuri kimaadili kwa Mheshimiwa Kabwe kufanya jambo lile huku kuelewa kuwa yule ni mke wa mtu. Lakini kama nilivyosema, maji yameshamwagika. Maswali mengi hayafuta ukweli kama ni kweli walilalana kama invyoonekana baada ya Zitto kushindwa kukanusha emphatically.

This is a very advice.. but why dont we extend it to cover the Lowassa's, JK's Karamagi's etc so as we can give them more time to concetrate on kazi za umma? between Zitto and those afore-mentioned who has more kazi za umma?

Kuna ya makosa na makosa. Ndiyo maana watu wengine hufungwa miezi miwili na wengine hunyongwa. Kama kweli Zitto alitenda vile basi alifanya makosa na wala sijamtetea. Lakini makosa yake huwezi kuyaweka katika callibre moja na makosa hayo mengine. Kulala na mke wa mtu kwa hiari hakulingani na kuliibia taifa hili mamilioni ya dola ingawa yote ni makosa.

Zitto kafanya ufuska wa kupindukia, kavunja ndoa lakini kwa standards za JF hilo ni suala binafsi tuliache!

Kumbe there one rule for Chadema and another rule for other parties....!!!!!!!!

Masatu, umekwenda mbali sana dhidi ya Zitto. Binafsi simjui na wala sina haja ya kujua ameshalalala na wanawake gani zaidi ya hili la Chifupa tulilotangaziwa. Unaposema kafanya ufska kupindundia unakuwa umelikuza sana hili. Kwanza hata hili la AC, hakuna anayejua kama kweli alifanya ufuska, hakuna ushahidi uliowahi kutolewa zaidi ya kusema kuwa Amina alionekana na Zitto kwenye baa pale Dodoma katika muda awakward huku Amina akiwa amevaa koti la Zitto. Sasa kama wewe ulikuwa unaingia nao chumbani na kurekodi matukio yote hadi kuona kuwa sasa ufuska huu umezidi kipimo umekuwa wa kupindukia basi tuambie, ama sivyo usikuze jambo usilokuwa na uhakika nalo.


Siku nyingine ukinijibu mimi, tafadhali sana nijibu kama kichuguu. Usinihusishe na uanachama wenu wa CCM au CHADEMA. Usipokubaliana nami, ujue hukubaliani nami kama Kichuguu usiseme hukubaliani nami kama CHADEMA. Mimi siyo mwanasiasa na wala siyo mwanachama wa chama chochote hapo Tanzania.
 
Kichuguu

Maji yameshamwagika baba, hayawezi kuozolewa. Hata ukiuliza mara mia huwezi kubadili kuwa hawakufanya tendo lile kama kweli walilifanya, siyo wizi wa fedha kuwa ukimbana atarudisha fedha hizo. Hii ni kati ya matendo ambayo ni irreversible, hata kama inakuuma vipi itabaki hivyo hivyo. Mimi kuandika hivyo sijamtetea Zitto kwa kufanya hivyo, ila ndio ukweli ambao lazima tuishi nao na wala sijatwist kuweka lawama kwa AC. Dada yule anasemekana ni mwanamke mzuri sana na yuko sexually active. Mimi simfahamu zaidi ya kuona picha zake tu. Rafiki yangu mmoja hapo Dar ndiye alinisimulia habari zake nyingi zaidi ya nilivyoandika pale kwa vile nyingine hazikuwa relevant. Pamoja na hayo ya AC, haikuwa ni vizuri kimaadili kwa Mheshimiwa Kabwe kufanya jambo lile huku kuelewa kuwa yule ni mke wa mtu. Lakini kama nilivyosema, maji yameshamwagika. Maswali mengi hayafuta ukweli kama ni kweli walilalana kama invyoonekana baada ya Zitto kushindwa kukanusha emphatically.

Kichuguu,

Suala hilo ni zaidi ya Zitto kulala na AC huyu mtu kavunja ndoa na ni kiongozi, he has to be accountable 4 what he has done. The least we can do hapa JF ni kujadili, unfortunately inaonekana taboo.

Hilo la maji yakishamwagika hayazoleki ni majibu mapesi kwa maswali magumu.. lets extends the line of reasoning there akija mtu akisema suala la Richmond maji yamemwagika hayazoleki je atakuwa right?


Kuna ya makosa na makosa. Ndiyo maana watu wengine hufungwa miezi miwili na wengine hunyongwa. Kama kweli Zitto alitenda vile basi alifanya makosa na wala sijamtetea. Lakini makosa yake huwezi kuyaweka katika callibre moja na makosa hayo mengine. Kulala na mke wa mtu kwa hiari hakulingani na kuliibia taifa hili mamilioni ya dola ingawa yote ni makosa.


Hii inaji contradict na jibu lako la hapo juu! Why dont we use the same pretext , maji yamemwagika!


Masatu, umekwenda mbali sana dhidi ya Zitto. Binafsi simjui na wala sina haja ya kujua ameshalalala na wanawake gani zaidi ya hili la Chifupa tulilotangaziwa. Unaposema kafanya ufska kupindundia unakuwa umelikuza sana hili. Kwanza hata hili la AC, hakuna anayejua kama kweli alifanya ufuska, hakuna ushahidi uliowahi kutolewa zaidi ya kusema kuwa Amina alionekana na Zitto kwenye baa pale Dodoma katika muda awakward huku Amina akiwa amevaa koti la Zitto. Sasa kama wewe ulikuwa unaingia nao chumbani na kurekodi matukio yote hadi kuona kuwa sasa ufuska huu umezidi kipimo umekuwa wa kupindukia basi tuambie, ama sivyo usikuze jambo usilokuwa na uhakika nalo.

Ufuska ni kosa kubwa sana, hususan unafikia kiwango cha kuvunja ndoa na kuhatarisha malezi ya mtoto. Kama kwako ni jambo dogo tu let be it...


Siku nyingine ukinijibu mimi, tafadhali sana nijibu kama kichuguu. Usinihusishe na uanachama wenu wa CCM au CHADEMA. Usipokubaliana nami, ujue hukubaliani nami kama Kichuguu usiseme hukubaliani nami kama CHADEMA. Mimi siyo mwanasiasa na wala siyo mwanachama wa chama chochote hapo Tanzania.

Sijasema kuwa wewe Kichuguu ni Chadema unless unataka ieleweke hivyo. Niliposema there is one rule for Chadema and another for other parties lilikuwa ni hitimisho la posting yangu lililojumlisha yote niliyoyasema

I think you are trying to bit around the bush here. You better come foward and rise your point instead of confusing matters. Kwa ninavyokusoma umeshachagua upande wako halafu unataka watu wandike kama unavyofikiria wewe.

Nionyeshe mahali niliposema watu waandike nitakavyo mimi.


Watu wameomba majibu kutoka kwa Mh. Zitto na amesema tumpe muda atazungumza kwenye muda mwafaka. What's wrong with that? Hao wengine unaowasema hawapo humu kujibu hoja zetu ndiyo maana tunapiga kelele ili wapambe wao wawapelekee taarifa. If they could be replying like Hon. Zitto we could not be disscussing one issue for days!!! Anayway

Ur misiing the point zero... suala sio kumlazimisha Zitto ajibu, bali suala ni hawa madalali na watetezi wa Zitto wanaodai hili ni suala binafsi na liachwe. cha kushangaza wakati Afisa wa ubalozi wa UK aliposemwa kuwa ana mkuwadia JK hakuna aliesema ni mambo binafsi, EL amehusishwa na wanawake kibao akiwemo waziri wa ofisi yake (Bunge) tena huyu Mama ana mume na anajiheshimu sana, hakuna aliesema ni mambo binafsi the list is endless, I can go on and on..... kibaya zaidi hakuna aliesema ni mambo binafsi tuwaache wajenge taifa.

Tatizo lilipomkuta Zitto ma bush lawyers tele ooh hayo mambo ya chumbani, hayana umuhimu kwa taifa..nk

Hapo ndio wadau tunaposema hapa JF kuna double standards na hususan suala linapohusu Chadema.
 
Masatu,

Ukirudia ile post yangu ya kwanza kabisa utaona nilisema kuwa Zitto alikuwa na option mbili. Option ya kwanza ingekuwa kusema kuwa sikufanya mambo yale ila jamaa wamenisingizia tu; hata hivyo details za zinzohusiona na jambo hili sitazitoa hadi nikiona muda ni mwafaka. Hii ingekuwa anakunusha uvumi huo bila kutoa taarifa zaidi. Option ya pili ndiyo hii aliyochukua, kushindwa kukanusha uvumi huo lakini vile vile hawezi kukiri kutokana na fedheha ya jambo lenyewe. Baada ya kuorodhesha hivyo ndiyo nikasema kuwa hiyo ni dissapointment kwa wale waliokuwa wakimtegemea kama kiongonzi mzuri, hata hivyo basi maji yamekwishamwagika.

Sasa ndugu yangu Masatu, kutokana na hoja zako dhidi ya CHADEMA umebadilisha maneno yangu na kuyapa maana tofauti. Hata hivyo, ukweli ndio huo, hayo ni maji yaliyomwagika hayawezi kuzoleka. Kujaribu kulinganisha swala la Zitto/AC na wizi unaofanyika serikalini ni kukosa mwelekeo; ni kama kulinganisha machungwa na mapera. Katika sheria, kosa la wizi wa fedha za serikali ni criminal case, na hili kosa la kulala na mke wa mtu kwa hiari ni civil case, litakuwa criminal case tu kama inaonekana kama alilala naye kwa nguvu.

Mimi nimeona jibu la Zitto likiashiria kukubaliana na shutuma zile kwa vile hakuzikanusha. Sasa mvutano wa nini tena; unataka ailipe nchi kutokana na hasara aliyosababisha kwa kulala na Amina? unataka ajiuzulu? unataka aseme ndiyo nilikula AC? unataka afanye nini litakalokuridhisha uachane naye. Wengi tulikuwa dissapointed kuwa hakutoa majibu kama tulivyotegemea, lakini sasa tufanye nini?
 
Kichuguu,

Kwenye option yako ya pili, angekaa kimya, mimi nisingeandika tena. Lakini hili
la kwamba atakuja kujibu on his own terms, binafsi naona JF haitakiwi kukubaliana au ku entertain mambo kama hayo.

Zaidi ya hapo nakubaliana na mengi uliyoandika hapo juu.
 
Wabongo kwa chini jamani?... eeeeh ndio maana wa Nordic wanaongoza ktk Utalii nchini!... Mimi naona wizara ya Utalii ingeongeza idara moja...Ngono!

Mwanakijiji,
Rudi nyuma fikiria kwa nini mawaziri wetu wanakuwa viburi?...hali ni haohao wabunge lakini ubunge wao hauna kazi kabisa utamwajibisha vipi mtu ambaye kachaguliwa na rais?.. huduma kwa bwana inatangulia. Hivyo hivyo ma Rc na Dc, kwa hiyo lazima itafutwe mbinu, hao Halmashauri za wilaya na miji tumeshindwa toka Uhuru. Mabadiliko ya Miji yetu yanaletwa na wananchi wenyewe kujenga majumba tena maeneo mengine hata hayajapimwa na wizara ya ardhi!
 
Cha ajabu wote wanaotaka Zitto 'awaridhishe" tayari wameshatoa hukumu kuwa anahatia ya kuzini kisa wameambiwa Amina alionekana amevaa koti la Zitto. Mbona hata langu nikimwona nitampa avae tena ndani ya ukumbi wa bunge acha mambo ya Dodoma hotel....mhhh nimesahau la kwangu sio la kiheshimwa....na linanuka uvundo wa kabatini.....anyway nitapulizia deodoranti..

Kaka Zitto hata kama na mimi hii hadithi inaniumiza haka kamoyo kangu lakini kwa kweli nakuvulia kofia kwa kuibuka humu ukijua wazi "wanamaadili" wa Tanzania yetu wanakusubiri kukumaliza....

Tanzanianjema
 
Unajua hata topic imebadilika kutoka Bunge kuwa Zitto. Swali alilokuwa ameuliza Mzee ES lilikuwa linatosha sana. Mhesimiwa Zitto kachangia ukuzwaji wa jambo hili baada ya kukataa kulijibu. Ni afadhali angejibu evasively na inconclusively kuliko kudictate kuwa hatajibu sasa hivi. Baada ya hapo waliokuwa na usongo na jambo hilo wangelimfuata kule kwenye "Vibweka vya Wakubwa."

Tangu sakata hili lianze, hakuna anayejua kikamilifu what transpired. Taarifa iliyokuwepo ni ile ya video ikionyesha Amina na Zitto wakiwa kwenye bar kikonakona huku Amina amevaa koti la Zitto. Ushahidi huo una reasonable doubts nyingi sana kiasi kuwa ulikuwa hautoshi, lakini Zitto naye anazidi kulifanya kuwa issue.
 
Kichuguu, nakusikia mzee.. let assume for a second kuwa Zitto anakuja na kusema "wana JF yote mliyosikia kuhusu suala hili hayana ukweli wowote ule. Mimi na Amina nimemfahamu kama Mbunge mwenzangu na tumekuwa tukishirikiana katika mambo mengi ya kikazi. Uhusiano wote haukuwa wa kimapenzi hata chembe licha ya tetesi na tuhuma zilizotolewa. Nasikitika tu kwa maneno ya watu ndoa ya watu imeharibika. Hilo siyo kosa langu wala siwajibiki kwa hilo. Naomba nirudie tena, sikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mhe. Chifupa. Uhusiano wetu ulikuwa ni wa kikazi na urafiki wa jumla kama nilivyo na urafiki na waheshimiwa bla bla bla. Asanteni kwa kunisikiliza". Je jibu la namna hiyo litatosha kunyamazisha wanaotaka kujua zaidi?
 
Kichuguu, nakusikia mzee.. let assume for a second kuwa Zitto anakuja na kusema "wana JF yote mliyosikia kuhusu suala hili hayana ukweli wowote ule. Mimi na Amina nimemfahamu kama Mbunge mwenzangu na tumekuwa tukishirikiana katika mambo mengi ya kikazi. Uhusiano wote haukuwa wa kimapenzi hata chembe licha ya tetesi na tuhuma zilizotolewa. Nasikitika tu kwa maneno ya watu ndoa ya watu imeharibika. Hilo siyo kosa langu wala siwajibiki kwa hilo. Naomba nirudie tena, sikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mhe. Chifupa. Uhusiano wetu ulikuwa ni wa kikazi na urafiki wa jumla kama nilivyo na urafiki na waheshimiwa bla bla bla. Asanteni kwa kunisikiliza". Je jibu la namna hiyo litatosha kunyamazisha wanaotaka kujua zaidi?

Exactly, jibu hilo lilikuwa linatosha sana na kama kulikuwa na details zaidi ambazo angependa kuzileta hapa baadaye angeongezea tu kuwa "taarifa nyingine zaidi zinazotokana na wale wachonganishi nitazileta hapo baadaye katika muda mwafaka." Mtu ambaye angemfuata kwa maswali zaidi baada ya jibu kama hilo angeonekana ana lake jingine.
 
Kichuguu nadhani wengi wetu tusingeridhika na hilo jibu, tungeanza kujiuliza kati ya wabunge wote kwa nini yeye. Ila jana nilikuwa naangalia kipindi cha Face 2 face cha Channel 10 walikuwa wanamhoji bwana Zitto naona kasema kuwa yuko Committed kwa fiancee wake.
 
Kwa upande wangu kitu ambacho sikutaka ni mtu kukaa katikati akitegemea upepo utavuma upande upi. Angekanusha tayari mnaweka kwenye kumbukumbu kwamba mheshimiwa kakanusha na mnaendelea mbele ila kama kadanganya na huko mbele ukweli unakuja kujulikana ndio mnarudisha mafile ya nyuma.

Mtu mkweli hata siku moja hakai katikati. Hapo ndio wengine tulipo na matatizo napo, kwamba hata baada ya zaidi ya mwezi hawezi kusema sentensi moja ambayo ni definite kama anakanusha au anakubaliana na hayo madai.

Tumeshayaona ya akina Clinton na kukaa katikati akitegea sijui Monika atamsaliti au la. Ukisoma cases mbalimbali, hiyo lugha aliyotumia Zitto ndio
inatumiwa na watu ambao kuna kitu wanataka kuficha kwasababu moja ama nyingine. Sisemi anadanganya lakini kwa maandishi yake najua kuna kitu anaficha, why? Anajua yeye mwenyewe.

Mimi nimeelewa na tuendelee, mheshimiwa Zitto ameshindwa kukanusha kama hahusiki na hiyo kashfa, the jury is still out.
 
Wanabodi,
Mimi na Amina nimemfahamu kama Mbunge mwenzangu na tumekuwa tukishirikiana katika mambo mengi ya kikazi. Uhusiano wote haukuwa wa kimapenzi hata chembe licha ya tetesi na tuhuma zilizotolewa. Nasikitika tu kwa maneno ya watu ndoa ya watu imeharibika. Hilo siyo kosa langu wala siwajibiki kwa hilo. Naomba nirudie tena, sikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mhe. Chifupa. Uhusiano wetu ulikuwa ni wa kikazi na urafiki wa jumla kama nilivyo na urafiki na waheshimiwa bla bla bla. Asanteni kwa kunisikiliza

Aliyosema Mzee Mwanakijiji ndiyo maneno alosema Zitto hapo awali katika magazeti...kuna tofauti gani kati ya taarifa ile na hii ambayo mnaisubiri hapa?. Kama kuna swali la nyongeza nadhani washtaka ndio wanatakiwa waiweke ile video hadharani.
Kwanza nataka kujua habari za ile barua ya mashtaka kwa spika ili-leak vipi toka kwa spika?. Je, sio jukumu la mshtaka kuonyesha ushahidi tosha kumkumu mshtakiwa Zitto ila leo imegeuka na kuwa mtuhumiwa Zitto anatakiwa kujikosha kabla hajawekewa ndoo ya maji!...

Bwana harusi mwenyewe kisha shtukia kuwa alipandishwa mkenge aachie mali wajanja wapate ubwete!, kesha tuma washenga kibao kumaliza matatizo yao ambayo hayakuanza jana. Angalia basi Zitto alivyokuwa mstaarabu, kawaacha wajikanyage wenyewe waliokianzisha!
Zitto hana haja ya kujibu lolote lile! That's the best weapon ya Udaku...wekeni madai yenu mezani na ushahidi tosha laa sivyo korti hii inatupialia mbali madai!
 
Sasa ndugu yangu Masatu, kutokana na hoja zako dhidi ya CHADEMA umebadilisha maneno yangu na kuyapa maana tofauti. Hata hivyo, ukweli ndio huo, hayo ni maji yaliyomwagika hayawezi kuzoleka. Kujaribu kulinganisha swala la Zitto/AC na wizi unaofanyika serikalini ni kukosa mwelekeo; ni kama kulinganisha machungwa na mapera. Katika sheria, kosa la wizi wa fedha za serikali ni criminal case, na hili kosa la kulala na mke wa mtu kwa hiari ni civil case, litakuwa criminal case tu kama inaonekana kama alilala naye kwa nguvu.

Kichuguu kwako wewe hili linaishia kwenye kuiba mke wa mtu tu, sisi wahafidhina tunaangalia bigger picture, ikiwa ameweza kuiba mke wa mtu hutashindwa kuliibia taifa given a chance! we call it LOGIC!
 
Hili jambo la Mh. Zito ni vyeti sana. Sidhani kwa mtu mwenye akili zake naweza kulizungumzia hili swala kweny JF. Hivyo kumforce Zito ni kupoteza muda tu ni bora ku-concerate kwenye masuala ya muhimu kwa taifa.
 
Nadhani tumeandika sana juu suala hili. Kwa kweli haikuwa nia ya mtu yeyote kuanzisha tena mjadala huu.

Katika hali ya kawaida mimi siwajibiki kwa JF. Hivyo sitakiwi kujieleza mbele ya bodi hii kwa lolote lile. Natakiwa kuwajibika kwa matendo yangu mbele ya Wananchi wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, wanachama wa CHADEMA Tanzania nia nzima kupitia vikao vya chama na pia Bunge kwa mambo yanayogusa Kanuni za Bunge, Sheria na 3 ya 1988 na Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Hata hivyo, nilijiunga JF kwa hiari yangu. Hivyo nikajifunga na "mkataba wa kijamii", kwamba JF ni jamii ya watu fulani wanaoamini katika mijadala na hoja juu ya masuala ya Tanzania. Ni kwa sababu hii ndio maana wanachama wa JF wanapata uhuru wa kutaka maelezo yangu.

Nimewahi kusema huko nyuma kuwa sihusiki na kadhia iliyotokea na siwajibiki kwa matukio yaliyofuatia. Maelezo yangu yalinukuliwa katika gazeti la Tanzania Daima. Maelezo yale bado yanasimama kwa sababu sijayakanusha.

Mzee Es, kwa kutumia fursa ya kwamba mimi ni mwanachama wa jamii hii akataka nimpe maelezo zaidi kwa niaba ya wanaJF. Nikamwambia muda mwafaka ukifika nitaeleza maelezo zaidi. Kwa sasa niachwe kwanza.

Sasa, sijui wanaotaka niseme wanataka niseme nini? Maana msimamo wangu niliutoa kitambo sasa. Kama mwanachama mwenzenu mnataka mpate faida ya details. Nimesema mungu akipenda nitasema zaidi. Nitasema vipi, nadhani ni juu yangu.

Mtu yeyote anayetaka niseme kwa terms zake, kwa vyovyote vile ana ajenda nyingine. Sio ajenda ya kujua kutoka mwanaJF mwenzake nini kilisibu.

Matokeo yake mjadala wa awali umehama kutoka nyongeza ya maslahi ya wabunge kwenda kwa ndugu Zitto. Mimi nahisi, hisia zangu tu, kuwa labda huu ni ujanja wa kutuhamisha kutoka katika mada. Kuna mtu humu ndani, nadhani ni mama lao, alipendekeza mada hii (call it a petition) ya kumtaka mwanachama wa JF ndugu Kabwe Zitto (ambae kwa concidence ni Mbunge) ajieleze kwa matendo yake iwe na thread yake.

Turudi kwenye mada yetu muhimu sana. Je, sahihi kwa walipa kodi wa Tanzania kutoa pesa zaidi kwa wawakilishi wao? Je, kazi ya wawakilishi hawa inalingana na thamani ya malipo? Je, ni sahihi kuwapa wabubge fedha za maendeleo na hivyo kuwa watendaji?

Muswada wa kuanzisha CDF unaletwa under certificate of urgency katika Bunge hili ie mkutano wa nane.

Katika historia ya Bunge la Tanzania, inasemakana, hii ni mara ya kwanza miswada kujadiliwa Bungeni wakati wa Bunge la Bajeti isipokuwa finance Bill na Appropriation Bill.
Je kuna udharura katika kuleta muswada wa CDF. Je, wananchi watapata muda kuujadili na kutoa mawazo?

Mjadala uendelee
ZK
 
Back
Top Bottom