Wanene kuongezewa marupurupu

Wanene kuongezewa marupurupu

Zitto,

Kabla sijauliza maswali yangu ningependa kutoa maelezo yafuatayo;

Tunafahamu na kuheshimu uamuzi wako (kuzungumza/kutozungumzia) kuhusu jambo hili.

Hata hivyo ukiwa kama mdau muhimu sana ktk forum hii na kwa kweli tunajivunia kuwa na mtu wa calibre yako hapa na hususan kwa michango yako makini, yenye kina na ujasiri wako wa kupambana na uozo ktk nchi yetu ukiwa ndani na nje ya bunge.

Na kwa kuwa wewe ni miongoni mwa wanasiasa vijana na wenye mvuto ktk contemporary politics za Tanzania. Maswali yangu kwako ni haya;

1. Je Mh Zitto utakubali kuchukua pongezi zangu za dhati kwa niaba ya wana JF wote?

2. Je Mh kwa kukataa kutupa hii habari nyeti ( Breaking newz) sisi wana JF hapa huoni kuwa unainyima forum nafasi muhimu ya kujitangaza na kupata wasomaji wengi? na nafasi ya kujivunia kama miongoni mwa vyanzo muhimu vya habari ndani na nje ya nchi?

3. Kama namba 2 ni kweli. Je Mh utakuwa tayari kubadili uamuzi wako na kutupatia habari hii ambayo itakuwa ni hot sana (scoop)

4. Kama utaamua kubaki na msimamo wako wa kusubiri wakati "muafaka" kuelezea ukweli wote. Je huoni kuwa wakati unasubiri huo wakati hadhi na hishma yako kwa jamii itakuwa imeporomoka zaidi beyond repair?

Masatu,

Thats Ok labda tu niongezee maswali mengine...

5. Je Zitto wapiga kura wako wa kiume wa Kigoma Kaskazini utawa hakikishia vp usalama wa wake zao wanapokuja kukuona ktk surgery yako? Vilevile na wakazi wa Dodoma ambako utapiga "kambi" wa miezi miwili kuanzia mwezi ujao nao utawahakikishia vp usalama huo?

6. Je Zitto ktk mperampera ule na Amina ulitumia kinga?

Mheshimiwa naomba kutoa hoja......
 
Zitto,
Bravo mjomba bravo, hakika umekuwa sana kisiasa...
Maamuzi yako yote nayapongeza na ndio mwanasiasa aloiva hutumia lugha kama yako. Nashukuru pia kwa kutupa mwanga ktk maswala mengi ambayo binafsi yalikuwa yakinitatanisha hasa hilo swala la kuongezwa marupurupu kupitia Bunge!...
Maswali yangu mengine naona umeya ruka na kuyaacha kiporo....nitafanya subira.
Binafsi ndugu Zitto, mimi naamini kabisa kuwa wabunge ndio watu waliokuwa karibu na wananchi na ndio fedha za maendeleo zinatakiwa ziwe mkononi mwao badala ya wakuu wa wilaya (untouchables) watu ambao wamechaguliwa na rais. Sina taabu na malipo yoyote ikiwa wataweza ku-deliver!.
Naamini sana kuwa kila mbunge akiwa ndiye hazina ya wilaya ama mkoa kuna kila uwezekano wa kupata huduma bora kwa sababu wananchi wenyewe ndio watamhukumu huyu mtu. Nguvu ya kura za wananchi itaanza kuonekana through wabunge kwani mfumo huu wa RC na DC ni mfumo ambao umeshindwa kutusukuma mbele. Ni mfumo batir ktk mazingira yetu hivyo hatuna budi kukubali mabadiliko ya uongozi na kiutendaji kazi! mabadiliko ambayo yatasukuma kila wilaya kuwa na umuhimu kwa wananchi kumchagua mbunge mwenye elimu zaidi ya siasa peke yake.
Na kikubwa zaidi rais hatakuwa na uwezo wa kuwaambia wananchi vitisho kama vile vya huko wilayani mwako!...Sura nzima ya maendeleo yao itakuwa wazi na kwa mara ya kwanza wananchi watajifunza umuhimu wa kumchagua Mbunge mwenye uwezo na sio mwenye Umaarufu!
 
Mheshimiwa Zitto,

Ninjua kuwa wewe ni mwanasiasa mwenye vision, kwa hiyo unajua umuhimu wa "timing" katika siasa, kwa hiyo nitavuta subira mpaka utakapokuwa tayari, labda sasa ndugu zangu turudi kwenye ishu,

Isipokuwa ndugu yangu, kama Salim alivyosema, baada ya Chimwanga, uongo wa siasa usipojibiwa kwa muda mrefu, hugeuka kuwa ukweli wa siasa!

Heshima Mbele Mkuuu!
 
Mzee Es,

Dr. Salim alisema uongo ukirudiwa rudiwa bila kuijbiwa hugeuka ukweli.
Let me do this on my own terms.

Fedha za mfuko wa maendeleo ya jimbo ni suala linalohitaji mjadala mkali sana. Na mimi nakubaliana kabisa na Mama Meghji kuwa tujiandae vya kutosha kabla ya kuingia katika mpango huu.
Mpango ukitekelezwa kama tutakavyo sisi wabunge, uhuru wa serikali za mitaa utakuwa kitanzini. Baraza la madiwani litapoteza mamlaka yake na hivyo wananchi kujenga loyalty kwa mbunge badala ya taasisi iitwayo halmashauri ya wilaya/jiji/manispaa.

Hebu tujadili kwa makini dhana hii maana mwelekeo ni kutenga asilimia 2 ya bajeti ya serikali kila mwaka katika mfuko huu. Mfano mwaka huu zingetengwa asilimia 2 ya 6.1 Tr. ambayo ni 122 Bn. kuna majimbo 232 ya uchaguzi, hivyo kila mbunge kwa mwaka atapata angalau shs 530m kwa mwaka. duh,mapesa mengi sana haya. Mnajua,wabunge wakitaka kitu chawa!

Swali, Mbunge ni mwakilishi au mtendaji? Je, ni kazi ya mbunge kujenga barabara? je, ni sawa kuweka fedha za maendeleo kwa mwanasiasa ambae baada ya miaka 5 ataomba tena kura?

Mpango ni kumpa kila mbunge, kwa kuanzia, shs 60m kila mwaka. je, ni sahihi kugawa sawa kwa sawa kwa wabunge wote bila kujali ukubwa wa majimbo? Baadae baada ya sheria kupita itakuwa ni asilimia 2 ya bajeti. Kenya ni asilimia 7 ya bajeti yao.


mkandara------- hebu tujadili hili. Mapesa haya katika mikono ya mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini. No,let me put it this way- katika mikono ya mbunge wa Iramba Magharibi/Ilala/na kama hao. Kitila anagalia hii. Tujadili kisha tupige kelele. Kama hatuwezi japo tunune
 
Zitto, hili suala la binafsi kama utalizungumzia utalizungumzia on your own personal terms siyo kwa kufurahisha JF au watu wachache wanaotaka kuridhisha udadisi wao tu. NI kweli jambo hili lilivuta hisia za watu wengi na mambo ya kitaifa n.k. Kama tulivyosema awali kama CCM na wahusika upande huo hawataki kuzungumzia kwanini tukulazimishe wewe ulizungumzie ilimradi tu tujue "nini kilitokea". Ukisema ndiyo ilikuwa kweli, utaulizwa "mlilala hoteli gani" ukisema hizo ni njama za kisiasa utaambiwa "tukuamini vipi wewe wakati ilishasemwa...". In any case hakuna atakayeridhika kwani majibu yatazua maswali zaidi ambayo yatahitaji majibu zaidi yakakayo zua maswali zaidi, na gurudumu la maswali yasiyoisha na majibu yasiyotosheleza litazidi kubingirishwa.

Tuzungumze mambo ya muhimu kitaifa. Swali la usalama wa wake za watu au waume za watu ni masuala ya wenzi wao! Kama ungetuhumiwa kubaka, kunajisi n.k ningekuwa wa kwanza kupigia kelele jambo hilo, hili ni udadisi wa kisiasa tu na kulia chabo (voyerism) maisha ya mtu ambaye tunafikiri "tunamjua". Kama kuna mtu anayetaka kuzungumzia suala hili binafsi wanaweza kukupigia simu na ukazungumza nao kiutu uzima.

Back to the mada!

Zitto, kumpa shilingi milioni 60 mbunge mmoja kila mwaka na kushindwa kuwalipia shilingi milion 70 wanafunzi wanaolilia haki ya kusoma huko Ukraine ni suala liligeuzwa kipaumbele. Kama serikali haina shilingi milioni 60 kwa mtu mmoja, inawezaje kupata shilingi milioni 60 kwa watu 320? Na kama Rais akiamua kujaza zile nafasi tatu, serikali itaweza kupata shilingi nyingine milioni 180!!

Unafikiri hapa kuna haki yoyote ile?
 
Mzee Es,

Dr. Salim alisema uongo ukirudiwa rudiwa bila kuijbiwa hugeuka ukweli.
Let me do this on my own terms.

Fedha za mfuko wa maendeleo ya jimbo ni suala linalohitaji mjadala mkali sana. Na mimi nakubaliana kabisa na Mama Meghji kuwa tujiandae vya kutosha kabla ya kuingia katika mpango huu. Mpango ukitekelezwa kama tutakavyo sisi wabunge, uhuru wa serikali za mitaa utakuwa kitanzini. Baraza la madiwani litapoteza mamlaka yake na hivyo wananchi kujenga loyalty kwa mbunge badala ya taasisi iitwayo halmashauri ya wilaya/jiji/manispaa.

hebu tujadili kwa makini dhana hii maana mwelekeo ni kutenga asilimia 2 ya bajeti ya serikali kila mwaka katika mfuko huu. Swali, Mbunge ni mwakalishi au mtendaji? Je, ni kazi ya mbunge kujenga barabara? je, ni sawa kuweka fedha za maendeleo kwa mwanasiasa ambae baada ya miaka 5 ataomba tena kura?

Mpango ni kumpa kila mbunge shs 60m kila mwaka. je, ni sahihi kugawa sawa kwa sawa kwa wabunge wote bila kujali ukubwa wa majimbo?

mkandara------- hebu tujadili hili



Kinachofanyika ni kurudisha takrima kwa mlango wa nyuma na kurasimisha ubunge na uongozi wa kisiasa kuwa uchifu wa milele...

Tanzanianjema
 
Kinachofanyika ni kurudisha takrima kwa mlango wa nyuma na kurasimisha ubunge na uongozi wa kisiasa kuwa uchifu wa milele...

Tanzanianjema

Tanzanianjema
Mapesa haya katika mikono ya mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini. No,let me put it this way- katika mikono ya mbunge wa Iramba Magharibi/Ilala/na kama hao. Kitila angalia hii.
Tujadili kisha tupige kelele. Kama hatuwezi japo tunune
 
Zitto,

Nionavyo mimi hapa sio swala la kutumia tena taratibu za kitabuni. Maendeleo yameshindikana chini ya RC na kulkikuwepo na hatari kubwa ya haohao viongozi wa ngazi za mitaa kufa ktk mfumo huu zaidi ya Mbunge.

Binafsi namtazama Mbunge kama waziri tu, kuna watendaji kazi, waajiriwa wa serikali kama wizara..lakini inapofikia maswali hujibiwa na waziri. Kwa hiyo Kila wilaya inakuwa kama wizara vile na katibu mkuu wake wakishiurikiana na Halmashauri ya jiji/wilaya/ manispaa.
halmashauri za miji yetu na wilaya zimeshindwa kufanya kazi hadi sasa. tena basi ukienda mikoani huko utawakuta hawa makatibu wa chama CCM wamechukua majumba, mali na kusimamamisha miradimingi tu. Pia kuna madiwani wamesimamisha miradi iliyokuwa imetangulia diwani aloachia ngazi kwa sababu kila diwani anakuja na mawazo yake mwenyewe ktk ujenzi wa taifa zima.
Yaani Utendaji kazi nchini umekuwa wa kichama na mapendekezo ya mtu na sio ya wananchi.
Binafsi nadhani hili sio swala la mfumo zaidi ila linatokana na nafasi za watu ktk mshiko wa ngawila. Kwa hiyo tulitazame kwanza kulingana na nafasi za watu kuliko mfumo maanake Ubinafsi ndio adui yetu mkubwa!.. Ni mbinu ipi ambayo itamwajibisha kiongozi mweka hazina wa wilaya ikiwa DC, Halmashauri za wilaya/jiji/ manispaa zote zimekuwa zikikwama kumaliza mipango ya maendeleo yao.
Nilichojifunza mimi huko mikoani sio tatizo la uvujaji wa pakacha ila tatizo kubwa ni mbebaji tofauti na Kitaifa ambacho pakacha lavuja!. Kidogo kinachopatikana hupigwa ktk sinia moja la pilau sasa hapo mjomba kuna wageni wa heshima wao huwa ndio wa kwanza kukaa mkekani!.
 
Mapesa haya katika mikono ya mbunge wa Iramba Magharibi. Kitila angalia hii.


Tuna kazi mno na huyu RAIS kivuli......mwakilishi maalumu wa maslahi ya mahafidhina kwa kichaa Kichaka na wale wa mashariki ya kati.....

Kitila usijiumize kichwa hapo waachie wenyewe wenye nchi labda wanaweza kuucheza huo mpira...

Tanzanianjema
 
Back to the mada!

Zitto, kumpa shilingi milioni 60 mbunge mmoja kila mwaka na kushindwa kuwalipia shilingi milion 70 wanafunzi wanaolilia haki ya kusoma huko Ukraine ni suala liligeuzwa kipaumbele. Kama serikali haina shilingi milioni 60 kwa mtu mmoja, inawezaje kupata shilingi milioni 60 kwa watu 320? Na kama Rais akiamua kujaza zile nafasi tatu, serikali itaweza kupata shilingi nyingine milioni 180!!

Unafikiri hapa kuna haki yoyote ile?

Mwanakijiji, nani kakwambia kuwa sisi tuna vipaumbele? unajua bajeti yetu ya 6.1tr, 2.6 ni OC ambayo maana yake ni semina, warsha, makongamano na safari?

Hebu fikiria, nini maana ya sera ya mambo ya nje ya nchi kwa raia binafsi wa nchi aliyepo nje? Hivi serikali inaposhindwa kulinda raia wake walio Ukraine, kwa mfano, kuna haja gani raia hao kujidaia uzalendo?
Watoto wamejipeleka,ndio. hawakwenda kwiba kule. wameenda kutafuta elimu. wasaidiwe. wapewe mikopo na baadae warudi kujenga li nchi hili. Bila aibu mkuu wa nchi anasema, wamejipeleka serikali haiwezi kufanya kitu.

Ofcourse, ukisema tutawasadia unaweza ukafungua pandoras box ya kila mtu kukimbila nje na kisha kuomba kusaidiwa. Saidia kwa siri kwa basi.

Tuone....
 
Safari ni ndefu..

Mhe Zitto, wacha mimi nipate somo hapa japo kidogo. Hivi kwa utaratibu wa sasa fedha hizi za maendeleo zinapitia channel gani kumfikia mwananchi wa kawaida...kwa njia ya shule, zahanati n.k Maana hapa mnazungumzia kubadili utaratibu wa kuzipitisha kwa wabunge.

Tafadhali
 
Wana JF,

Hakuna haja ya kupeana sifa za kudanganyani hapa, mheshimiwa Zitto anatakiwa kujibu maswali ya wana forum kama hataki aseme pia hataki kujibu na kila mtu atakuwa na nafasi ya kutafsiri maana ya maneno hayo.

Je Mkapa akisema atajibu maswali kwa muda wake mtakubali? Zitto kwa wakati mbalimbali amekanusha hii habari magazetini, sasa kama ni kweli magazeti yalimnukuu mheshimiwa Zitto kuna ubaya gani kukanisha hiyo habari
hapa ili tujue kama kweli hahusiki na hiyo kashfa.

Inawezekana wengine mnaona mheshimiwa Zitto kuwa na kashfa ya kutembea na mke wa mtu ni jambo binafsi, hilo si jambo binafsi hata siku moja.

Kuamua kuchagua maswali ya kujibu sidhani kama kunamsaidia yeye au kunatusaidia sisi, kama hapa JF tunashindwa kuwawajibisha hawa waheshimiwa wetu, itakuwaje huko mitaani TZ?
 
Zitto,

Nionavyo mimi hapa sio swala la kutumia tena taratibu za kitabuni. Maendeleo yameshindikana chini ya RC na kulkikuwepo na hatari kubwa ya haohao viongozi wa ngazi za mitaa kufa ktk mfumo huu zaidi ya Mbunge.

Binafsi namtazama Mbunge kama waziri tu, kuna watendaji kazi, waajiriwa wa serikali kama wizara..lakini inapofikia maswali hujibiwa na waziri. Kwa hiyo Kila wilaya inakuwa kama wizara vile na katibu mkuu wake wakishiurikiana na Halmashauri ya jiji/wilaya/ manispaa.
halmashauri za miji yetu na wilaya zimeshindwa kufanya kazi hadi sasa. tena basi ukienda mikoani huko utawakuta hawa makatibu wa chama CCM wamechukua majumba, mali na kusimamamisha miradimingi tu. Pia kuna madiwani wamesimamisha miradi iliyokuwa imetangulia diwani aloachia ngazi kwa sababu kila diwani anakuja na mawazo yake mwenyewe ktk ujenzi wa taifa zima.
Yaani Utendaji kazi nchini umekuwa wa kichama na mapendekezo ya mtu na sio ya wananchi.
Binafsi nadhani hili sio swala la mfumo zaidi ila linatokana na nafasi za watu ktk mshiko wa ngawila. Kwa hiyo tulitazame kwanza kulingana na nafasi za watu kuliko mfumo maanake Ubinafsi ndio adui yetu mkubwa!.. Ni mbinu ipi ambayo itamwajibisha kiongozi mweka hazina wa wilaya ikiwa DC, Halmashauri za wilaya/jiji/ manispaa zote zimekuwa zikikwama kumaliza mipango ya maendeleo yao.
Nilichojifunza mimi huko mikoani sio tatizo la uvujaji wa pakacha ila tatizo kubwa ni mbebaji tofauti na Kitaifa ambacho pakacha lavuja!. Kidogo kinachopatikana hupigwa ktk sinia moja la pilau sasa hapo mjomba kuna wageni wa heshima wao huwa ndio wa kwanza kukaa mkekani!.

Kaka,

Tanzania kuna three levels of governance only.

1. Kijiji
Hapa unakuta serikali ya kijiji chini ya mwenyekiti wa kiiji na mtendaji ni Afisa Mtendaji wa Kijiji-VEO. Serikali ya kijiji ni serikali tosha ina mamlaka ya kukusanya kodi na kutunga sheria ndogondogo katika kijiji.

2. Halmashauri ya Wilaya/Mji/Manispaa/Jiji
Hili ndio twaita baraza la madiwani chini ya Meya na mtendaji ni Mkurugenzi MTENDAJI-DED etc. wana mamlaka ya kukusanya kodi na kutuga sheria.

3. Taifa
Hapa unakuta Bunge na baraza la mawaziri chini ya Rais.

Hivyo ngazi ya Kata na ngazi ya Jimbo la uchaguzi ni ngazi tu kuchagua. Tena afadhali ya Kata ambapo kuna kamati ya maendeleo ya Kata na afisa mtendaji-WEO, jimbo la ubunge ni kasha tupu ambalo kazi yake ni uchaguzi tu.

Kiutawala ni kosa kubwa kumpa mbunge pesa ya maendeleo maana hana ngazi ya utawala. Hana watendaji huyu, ni mtu.

Kama twataka kuwa serious na pesa hizi za umma, then tuwe na marekebisho ya sheria za serikali za mitaa ili kuweka ngazi ya utawala katika eneo la Jimbo la uchaguzi na hivyo kuwa na kitu kama kamati ya maendeleo ya Jimbo chini ya uenyekiti wa Mbunge.

Mkandara-RC na DC ni extension ya serikali kuu katikangazi za chini. Nafasi hizi zifutwe tu. Tunahitaji uimara na ubora katika halmashauri.

Kuwapa wabunge fedha za umma bila chombo cha uwajibikaji ni ubadhirifu wa fedha za umma.
 
Safari ni ndefu..

Mhe Zitto, wacha mimi nipate somo hapa japo kidogo. Hivi kwa utaratibu wa sasa fedha hizi za maendeleo zinapitia channel gani kumfikia mwananchi wa kawaida...kwa njia ya shule, zahanati n.k Maana hapa mnazungumzia kubadili utaratibu wa kuzipitisha kwa wabunge.

Tafadhali

Kwa sasa fedha zinpitia halmashauri za wilaya na miji. hii ya fedha kwa wabunge ni nyongeza kufanya mambo hayo hayo. Halmashauri bado zitaendelea na kazi pia
 
samahani, nilisahau kuwa mkopo wa magari tunaopewa 50% inalipwa na serikali na 50% ndiowanalipa wabunge.

tumeomba 80% ilipe serikali. sijui imekubalikaaaaaaaaaa
 
Mmhhh!!! hiyo ya asilimia 50 kulipiwa na serikali naona hapo ni tatizo. Hii ina maana minimum 20M mbunge anapewa bure. Nasema minimum kwasababu bado kuna exemption kwenye kuingiza gari, kwahiyo serikali inapoteza pesa zaidi ya asilimia 70 kwa ajili ya magari ya Waheshimiwa.

Mkandara, kwasasa wilayani mkuu wa wilaya hana madaraka tena kwenye matumizi ya pesa. Hizo halmashauri na madiwani ndio wenye pesa pamoja na madaraka. Ila tu cha kusikitisha ni kwamba capacity yao ni ndogo mno, pesa nyingi zinapotea kwa ujinga ujinga. Kama tunataka halmashauri ziwe ndio serikali za wilaya, kuna haja ya kuendesha trainings za hali ya juu mno.

Halmashauri wana budget kubwa sana ambayo kwa mawazo yangu hailingani na uwezo wao. Wanahitaji ushauri wa nguvu kuweza kuzitumia hizo pesa vizuri. Hiyo ndio weakness kubwa ya kupeleka madaraka kwenye halmashauri za wilaya. Japo idea ni nzuri lakini mafanikio katika utekelezaji wake ni mdogo mno hasa kwa wilaya za vijijini ambako zaidi ya asilimia 80 ya madiwani
wana elimu ya form four au chini ya hapo.
 
Zitto,

Sawa kabisa nakuelewa lakini hapa naona unaacha kitu kimoja. Unaacha kutazama kuwa kumpa madaraka Mbunge ni lazima kuandamane na kazi zake!.. huwezi kumpa mbunge jukumu la fedha bila kuongeza ngazi ya Utawala na ndio nilivyosema hapo awali nikitoa mfano wa utendaji kazi wa waziri.
Binafsi nataka kumtazama Mbunge kama waziri ktk sehemu aliyochaguliwa na hii pia itaondoa tu sio ma RC na DC bali pia wabunge watakuwa sio Mawaziri wetu tena. Baraza la mawaziri litajumuika watu wengine kabisa kwani wabunge wameshika wilaya zao. Nitapenda sana kuutazama uwezo wa Mwandosya akiendeleza Mbeya, kabla sijafikia kumpa kura yangu ktk maendeleo ya Tanzania kama rais mterajiwa. Lakini hivi sasa ktk mawaziri ni mparaganyo mtupu, na hawa halmashauri za wilaya na miji wanatumbua tu mafedha...

Itazame Dar inavyozidi kuharibika kila siku ya Mungu, yaani maendeleo makubwa yanayofanyika ni kutimua machinga mabarabarani..majumba hayajapakwa rangi toka mwaka 1982, ni nyumba za watu binafsi tu utaziona zikipewa ukarabati tena baada ya kuuzwa.
Kabla sijafika Bongo niliambiwa kuwa nenda Bongo mjomba, ile Bongo ya 1900 kweusi sii hii tena....
Looooh! kumbe maendeleo ya Mtanzania ni maghorofa!..barabara mbili tatu kuu yaani tunafagia na kuficha uchafu uvunguni. Wee mwenyewe unajua kwamba wenzetu Ulaya ukiwa mjini huwezi kabisa kuona mchanga mtupu kando ya barabara. Yaani ukiunguliwa na gari mpango wa kuzima na mchanga mjomba utakesha! hakuna mchanga... sasa leo hii Bongo mchanga kila kona mvua ikinyesha mitaro yote imeziba!.. distruction ya hapo itagharimu city budget ya miezi sita.. kama wakijaribu kushughulikia, kwa hiyo wanamwachia Mungu.

Wabunge wetu wanapiga kelele kila siku katika maeneo yao lakini hakuna mtu anayewasikiliza kabisa kwa sababu wao ni ktk kundi hilo ulosema. Kundi la Uchaguzi!.....for what?...I mean Zitto nambie hivi wabunge wa nini hasa ikiwa sheria za nchi hazina thamani ktk taifa letu. katiba haifanyi kazi wala uwezekano wa kuundwa upya hakuna!..
Sasa hivi Tanzania ni Punda aliyegoma kwenda, we need changes! nafikiri wabunge wanaweza kabisa kushika nafasi za Rc na Dc wakiundiwa utawala kupitia halmashauri za wilaya na miji. lazima kuwepo ushirikiano wa karibu sana kati ya Mbunge na Halmashauri zetu.
Kwa uharaka hayo ndio mawazo yangu.
 
Sasa tutategemeaje mbunge aikosoe serikali ambayo tayari inamlipia 80% ya manunuzi ya gari lake? Si ni kama serikali imeshanunua yes vote ya kila mbunge? No wonder Kaburu karudi CCM.
 
Lita ya mafuta = 1500/Lt
Lita 1000 x 1500 = 1,500,000
Idadi ya wabunge = 320
Gharama kwa wabunge wote kwa mwezi: 1500000 x 320 =480,000,000
Gharama ya wabunge wote kwa mwaka 480,000,000 x 12 = 5,760,000,000 (bilioni tano na nusu)
Gharama ya mafuta kwa miaka mitano 5.760 bilioni x 5=28.8 bilioni

Wakati huo huo shule hazina madarasa ya kutosha wala madawati, hospitali zetu hazina madawa, vifaa na vitanda vya kutosha, uptikanaji wa maji na umeme bado una hitilafu kubwa sana pamoja na kuwa huru miaka 46 iliyopita.

Sioni ari, nguvu mpya na kasi mpya yoyote ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania. Ninachoona ni yale yale ya kudanganya wadanganyika. Jamaa yuko madarakani zaidi ya mwaka sasa pamoja na kuwa aliingia madarakani na matatizo ya umeme, ujambazi na upungufu mkubwa wa chakula hakuna ahueni yoyote kwa wanachi. Waswahili walisema nyota njema huonekana asubuhi...sasa hivi tunakaribia mchana.
 
Back
Top Bottom