Mzee Kichuguu,
Usiweke maneno mdomoni mwangu, nimesema nina ushahidi juu ya hii ishu, sikusema kuwa Zitto amefanya kweli, ndio maana ninataka kumuuliza maswali yeye mwenyewe,
kama vile nilivyowaambia hapa forum kuwa Mbunge Malima aulizwe kama sio mkurugenzi wa kampuni ya Manji, alipoulizwa kila mwenye akili alielewa jibu lake ni nini, na ninasema on the same token, nina data kibao on Zitto's ishu ndio maana ninataka kumuuliza mwenyewe, ili nikate mzizi wa fitina kujua kama ni kweli, au anasingiziwa, na tuweze ku-move forward,
Sasa badalala yake nasikia hadithi nyingi za kumtetea, tena na watu very prominent hapa forum, ninarudia tena kwamba kwa mara ya kwanza I am ashamed kuwa mwanachama wa hii forum, majuzi nilikuwa ninalala macho kutafuta data za Richmond, mpaka nimetumiwa ujumbe na wanaohusika kuwa ni-slow down maana nilikuwa tayari ninaelekea kuwafichua uovu wao, sasa tunalala macho kwa ajili ya credibility ya hii forum, halafu mnasema eti ni uroda sijui, na mambo ya binafsi?
Zitto, anawakosoa viongozi wa serikali hapa kila siku, yeye kwa nini asiulizwe? Yeye ni nani? Msilete dhihaka wazee, ndio maana tutatawaliwa na kina Ridhiwani, mpaka mwisho wa maisha yetu, ni kwa sababu ya mchezo wa kujificha kama huu wa eti alikula uroda, ala tumeandikiwa barua na mzito mmoja wa nchi akiomba tuache kuandika on Richmond na anakubali kuwa anapagopa sana hapa forum maana hakuna mchezo hapa, sasa leo kuna mnaotaka kuleta busara za spika hapa, yes maneno ya kula uroda, oooh ameshajibu aseme nini tena, ndio hizo hizo busara za spika tulizozinunua kwa shillingi millioni 100!
Huuu ni unafiki usiokuwa na mfano, na wale wote mnaohusika nao shame on you, ndio maana CCM wanapata kura 80%, mwaka 2006 ni kwa sababu wananchi walishashituka kuwa wale tunaojifanya kuwa na exposure za majuu kuwa ni kina "Malinzi Type", hatuna lolote zaidi tu ya kuwa wasemaji wa viongozi uchwara, and I mean it maana sijui nitaitoaje hasira yangu na huu unafiki, tumejaa unafiki wabongo, wewe mtu mzima wa kimataifa rais wa benki ya dunia amepumzishwa kazi ya dunia kwa sababu ya uzinzi, leo unasema eti ni uroda?
Ninasema kuwa nimenawa mikono, maana uchunguzi wa Richomnd nusura unifikishe pabaya, na nina info kibao nimeshindwa kuzitoa nilikuwa tu nasubiri the right time, sasa leo kiongozi wa nchi, tena kijana tuko naye hapa kumkoma nyani, halafu anatuhumiwa kwa kashfa ya kijinga badala ya kutuonyesha how responsible au tall he is, anajificha na kuna wanaomtetea?
Usaniii maana yake ni nini? Hiii ndio hasa maana ya Boys 11 Men, usaniii usaniii tu, ndio maana kina Ridhiwani wanataka fomu za uongozi, maana sisi ndio wananchi wenyewe, ninarudia tena kuwa I am ashamed kuwa mwanachama wa hii forum, na siwezi kuona kiongozi yoyote wa serikali akikosolewa tena hapa, maana ni kufukuza upepo tu wa baharini,
Tuko uchi tunajaribu kufukuza mwenda wazimu, nasema bravo kwa wale owte waliosimama kidete kulinda heshima ya forum, kwako Mheshimwa Zitto, ninasema kuwa you are not bigger kuliko hii forum, NO WAY na over our dead bodies, hatutakubali kabisa huu unafiki mpaka utakapojitokeza na kuliweka hili jambo linapotakiwa kwenye hii forum ambapo wewe kwa hiari yako, ni mwanachama, tutakukumbusha tu hata kama ni one year from now, ninaema dawa ni kuja Clean hapa forum kwa wananchi walalahoi, ujibu shutuma ambazo so far ni accusations tu, mpaka tukapokuja clean, sio gazeti wala radio za uchwara, mambo ni hapa hapa forum!
Tutakusubiri mpaka utakapokuwa tayari!, kwa wale wapambe kina 'Malinzi" tumewasikieni, sasa muachieni Mheshimiwa Zitto aje hapa!