Wanene kuongezewa marupurupu

Wanene kuongezewa marupurupu

posho ya mafuta ni kwa wabunge wote. hakuna justification kwanini wabunge wakuteuliwa walipwe posho hii, lakini ccm imegawa wabunge wake wa viti maalumu kimikoa. hivyo wana majimbo hawa. kikatiba hawana majimbo, lakini chama tawala jamani, lililo si la katiba lawa na lilo silo.

hakuna justification yeyote ni kwa nini kuwe na flat rate. serikali inasema ni kurahisisha mahesabu.
 
Vipi kuhusu fedha za kuwalipa wasaidizi? Na zile za kununulia "mashangingi" kwa milioni 40 flat? Natumai nazo hamjajiongezea!!!!

Tanzanianjema
 
mukandara?
kupokea marupurupu kabla ya muswada? muswada wa sheria gani?

mshahara wa mbunge unatokana na waraka wa katibu mkuu kiongozi. pamoja na posho zote.

mpaka sasa hatujaanza kulipwa nyongeza. kilichopo mezani ni mapendekezo tu. huhitaji uswada wowote kupitishwa kuwa sheria ili wabunge walipwe zaidi. kama kuna mtu alisema hivi huyu hajui sheria za bunge na kanuni zake.
 
wabunge waliomba wasitozwe kodi kama majaiji. wengine tulikataa na hapakuwa na consesus. serikali ikapata nguvukukataadai hilila aibu la wabunge. hivyo mpaka sasa twalipa 30 PAYE.
 
Hivi na ile hadithi ya "mfuko wa maendeleo jimboni" inaendeleaje.........

Tanzanienjema
 
Tanzania njema,
mkopo wa magari,the so called shangingi, ni hiariya mbunge. Huu ni mkopo na hakuna anaelazimishwa. mkopo hauwezi kuongezwa kati kati kwani mkataba wake ni wa malipo katika kipindi cha uhaiwa bunge.
suala hilila mkopo, kwa mwonbowangu mimi si suala la mjadala maana ni lazimazilipwena zinalipwa.

mbunge yeyote makini anataka tuwezeshwe kuajiri wasaidizi wenye kiwango ili kufanisishakaziza bunge
 
mfuko wa maendeleo wa jimbo bado upo. hauj kutengewa fedha katika bajeti hii
 
Mheshimiwa Zitto,

Mkopo wa magari ya wabunge ni kiasi gani? Kuna mtu anasema 40M wakati wengine wanasema mpaka 100M. Je ni lazima ununue gari linaloendana na huo mkopo?

Suala hapo sio kukopa maana kama kukopa ni kwa interest asilimia 0, mkopo wa namna hiyo kila mtu atauchangamkia
 
kitila,
ni makosa kulinganisha malipo ya wabunge across countries. ni vema kulinganisha ndani ya nchi.

maswali ya msingi, je wabunge kutokana na kazi yao wanastahili kulipwa kiasi hiki wanacholipwa? ie malipo vs tija.

je, huduma tunayopata ni sawa na fedha tunayolipa? ie value for money.

jambo la kuzingatia, muhimu sana: changamoto za bunge kutokana na matatizoya watu ni kubwa mno. mfano ni nadra daktari kumkuta kila asubuhi anashughulikia matatizo binafsi ya raia. peak days mbunge anapata wageni 70 kutaka msaada kwa siku. tuzingatie sana hili. Tanzanianjema,naamini anajuahili. lizingatiwe katika mjadala wote.

hoja ya wabunge wasijipangie mishahara ni hoja muhimu mno. tuanze kuifanyia kampeni. mwanakijijiji,tupe concept paper wana jambo kisha tuamue
 
mkopo ni shs 40m tu. unapewa pesa na wala sio gari. unaamua mwenyewe gari utakayo. pamoja nayo mbunge anapata customs duty exemption. tupo wabunge ambao hatujanunua mashangingi kwa mkopo huo. kuna wabunge wamenunua mashine za kusaga nk. la muhimu ni kulipa tu
 
Mheshimiwa Zitto,

Asante kwa ufafanuzi wako na imesaidia kujua ukweli wa mambo
 
Mheshimiwa Zitto,

Heshima mbele ndugu yangu, maneno mazito ila kama unavyojua hapa kuna kiporo, ambacho wana-JF tumekuwa tukikusubiri kwa hamu, tumeshasema sana kuwa tunaheshimu sana your presence hapa, na hasa mawe yako na pia the most important your vision kama kiongozi, tumekufagilia sana hapa kuwa tuna imani na wewe kama kiongozi mwenye vision, mimi ninakuomba tu-switch the subject,

Tunajua kuwa kuna mchezo mchafu uliochezwa na DR. NCHIMBI, katika kumpiga vita Amina Chifupa, mbunge wa CCM, asiwe mwenyekiti wa CCM-Vijana, in the process ya hiyo operation, kwa mshituko mkubwa hapa forum tukasikia ukihusishwa na kashifa nzima ya kumuangamiza Mbunge, Mwanamama Amina Chifupa, kisiasa, na sisi hapa forum sio wajinga wa kutojua kuwa jina lako kisiasa, sasa limechafuliwa kwa kiasi fulani, lakini tuliwahi kukuombea na kutabiri kuwa iko siku uta-bounce back,

Sasa tusingependa unafiki au umbeya, kama sio udaku, mimi kama mtu niliyekuwa ninakufagilia sana, na bado ninaendelea kukufagilia as a matter of principle, ningekuomba uiweke hii ishu to the rest, by coming clean hapa forum nyumbani kwako, na sisi tuta-spread the good and the bad news,

Wana-Forum, tungependa kujua exactly, What happened? WHY? na WHERE? kama sio WHY YOU?

Na ninakuhakikishia what ever you say, we will take it na case close, please come clean mheshimiwa!

Ahsante kwa kunielewa, ingawa ni nje ya hii topic ila the best time and place, ni sasa na hapa forum!!
 
Mzee Es,

Kila jambo lina wakati wake. mungu akipenda na wakati ukifika ukweli juu ya jambo hili utajulikana. Kwa sasa mniruhusu kukaa kimya. Sitaki kujitetea. Nataka hapo mudea ukifika kusema ukweli, ukweli mtupu. Vuteni subira.

nimeitokeza hapa kufafanua tu baadhi ya hoja za malipo ya wabunge ili mjadala uwe mzuri.
 
Mzee Es,

Kila jambo lina wakati wake. mungu akipenda na wakati ukifika ukweli juu ya jambo hili utajulikana. Kwa sasa mniruhusu kukaa kimya. Sitaki kujitetea. Nataka hapo mudea ukifika kusema ukweli, ukweli mtupu. Vuteni subira.

nimeitokeza hapa kufafanua tu baadhi ya hoja za malipo ya wabunge ili mjadala uwe mzuri.
Karibu tena Mh. Zitto, wiki 5 ulikuwa muda mrefu sana kukaa kimya.

Wana JF wanasubiri kwa hamu maelezo yako; kwa wengine kukaa kimya kunafanya waamini habari hizi kama zilivyo na ukizidi kukawia maelezo yako hayatabadili kitu.

Ajali hizi kwenye siasa hutokea, jaribu kulinganisha hili suala na ile ishu ya DC wa Kibondo mwaka 1999 kuhusu mwanamke mzungu wa Concern; ilikuwa hot lakini yule mpiganaji alijitokeza na akasafisha hali ya hewa, hadi leo bado yuko kazini.
 
Karibu tena Mh. Zitto, wiki 5 ulikuwa muda mrefu sana kukaa kimya.

Wana JF wanasubiri kwa hamu maelezo yako; kwa wengine kukaa kimya kunafanya waamini habari hizi kama zilivyo na ukizidi kukawia maelezo yako hayatabadili kitu.

Ajali hizi kwenye siasa hutokea, jaribu kulinganisha hili suala na ile ishu ya DC wa Kibondo mwaka 1999 kuhusu mwanamke mzungu wa Concern; ilikuwa hot lakini yule mpiganaji alijitokeza na akasafisha hali ya hewa, hadi leo bado yuko kazini.

This is Zitto, i set my own terms.
Kakalende, imeandikwa wapi kuwa wiki 5 ni nyingi?
Lini na kwa style gani nitaeleza, ni maamuzi yangu mimi mwenyewe Kabwe Zitto, Mb, former student leader!.......... tuendelee na mada
 
Mheshimiwa Zitto,

Nafikiri haitoshi kusema kwasasa tukuruhusu ukae kimya bila ya maelezo kwanini unataka kukaa kimya? Kama kuna case mahakamani tutakubali lakini kutuambia tukae kimya kwasababu wewe hutaki kutueleza nini kimetokea, nafikiri hakuna mwana JF ambaye atakubali huo ushauri.

Mheshiniwa nafikiri huu ni wakati wa kusema ukweli juu ya hilo jambo, maana kashfa ya kutembea na mke wa mtu ni kubwa sana na kuna haja ya kueleza hilo kwanza badala ya kukimbilia hoja zilizo rahisi kuzijibu.

Naungana na wana JF wengine, tunataka majibu, ilikuwaje ukahusishwa na kashfa ya kutembea na mke wa mtu?
 
Zitto,

Kabla sijauliza maswali yangu ningependa kutoa maelezo yafuatayo;

Tunafahamu na kuheshimu uamuzi wako (kuzungumza/kutozungumzia) kuhusu jambo hili.

Hata hivyo ukiwa kama mdau muhimu sana ktk forum hii na kwa kweli tunajivunia kuwa na mtu wa calibre yako hapa na hususan kwa michango yako makini, yenye kina na ujasiri wako wa kupambana na uozo ktk nchi yetu ukiwa ndani na nje ya bunge.

Na kwa kuwa wewe ni miongoni mwa wanasiasa vijana na wenye mvuto ktk contemporary politics za Tanzania. Maswali yangu kwako ni haya;

1. Je Mh Zitto utakubali kuchukua pongezi zangu za dhati kwa niaba ya wana JF wote?

2. Je Mh kwa kukataa kutupa hii habari nyeti ( Breaking newz) sisi wana JF hapa huoni kuwa unainyima forum nafasi muhimu ya kujitangaza na kupata wasomaji wengi? na nafasi ya kujivunia kama miongoni mwa vyanzo muhimu vya habari ndani na nje ya nchi?

3. Kama namba 2 ni kweli. Je Mh utakuwa tayari kubadili uamuzi wako na kutupatia habari hii ambayo itakuwa ni hot sana (scoop)

4. Kama utaamua kubaki na msimamo wako wa kusubiri wakati "muafaka" kuelezea ukweli wote. Je huoni kuwa wakati unasubiri huo wakati hadhi na hishma yako kwa jamii itakuwa imeporomoka zaidi beyond repair?
 
pamoja na nia njema ya wanaforum ya kutaka kujua maelezo ya mh. zitto kuhusu kizungumkuti alichohusishwa nacho, nadhani ni vyema tukaheshimu uamuzi wake wa kutoa maelezo muda atakaoona yeye kwamba ni muafaka kwake.

inabidi tukumbuke haya yote ni mapambano ya kisiasa na katika hili mkakati utakaotumia ndo utahakikisha muelekeo wa mpambano huo. naamini mh. zitto anamkakati wake na labda anafahamu mkakati wanaotumia wapinzani wake wa kisiasa ndio maana anasita kutoa maelezo kwa sasa.

waheshimiwa hapa nadhani kuna suala la survival ya kisiasa hivyo tuendelee kumshauri njia ya kufanya ila uamuzi ubaki kwake na tuuheshimu uamuzi wake.

wale wanaotaka kuendelea kujadili hili suala nadhani hawazuiwi kufanya hivyo.

nawasilisha hoja
 
waheshimiwa hapa nadhani kuna suala la survival ya kisiasa hivyo tuendelee kumshauri njia ya kufanya ila uamuzi ubaki kwake na tuuheshimu uamuzi wake.

Naona wewe unatupeleka mchomo sasa
 
Back
Top Bottom