Mswahili,
Wee muhuni sana unapojitia una huruma! mhadaifu kumwonea huruma Chifupa hali wewe ni kiwembe. Aaaah angesema Mtazania labda ningeamini lakini wewe? heeee heee! na huyo senti 50 akukalie mbali kabisa! kwanza hii kujibu jibu anasogelea ndoana ya mvuvi!
Umesema sina huruma!....
Hapana ndugu yangu namwonea huruma sana AC pamoja na Zitto! Why? kwa sababu hawa wote wawili wamesema nani mgonvi wao na dunia ya wadanganyika haitaki kuamini. Dr. Nchimbi mbona hajatoa maelezo yake? kama yeye ndiye shuhuda wa haya maswala nadhani inabidi wananchi tuweke madai yetu mbele kuhakikisha kwamba huyu jamaa haleti majungu Bungeni!..
Dr. Nchimbi hakuwapaka Amina na Zitto peke yake kalipaka Bunge zima!..
Ebu tuangalie maneno yameanzia wapi kisha tumalizie kipande kinachosema hivi:-
Mwanasiasa huyo mchanga ameonja machungu ya kisiasa hadi kusababisha ndoa yake kuvunjika hivi karibuni. Amina anamshutumu mmoja wa vigogo ndani ya CCM kuwa ndiye amekuwa chanzo cha kuvuruga ndoa yake hadi ikavunjika.
Hata hivyo kumekuwapo na mchanganyiko wa mawazo kuhusu kuvunjika kwa ndoa yake, wengine wakibainisha wazi kuwa imetokana na masuala ya kifamilia huku wengine wakidai kuvunjika kwa ndoa hiyo kumetokana na nia ya Amina kutaka kugombea moja ya viti vikubwa ndani ya CCM.
Tangu kuvunjika kwa ndoa yake Amina amekuwa haonekani kwenye majukwaa ya kisiasa na hata simu yake ya mkononi ambayo imeandikwa kwenye kitabu cha orodha ya wabunge imekuwa haipatikani.
Kwa hiyo Amina kisha sema nani mgonvi wake tunachotaka sisi ni yeye aje hadharani mpate kumuumbua, hakuna zaidi.
Link hii hapa
http://www.dailynews-tsn.com/habarileo/page.php?id=2218