[SIZE=3 [USER=47929]Excel[/USER] wajua hata Braza
kiwatengu nae anataka kujua hili...
mimi ni mwalimu kwa profesheno japo sijakaa huko muda mrefu kivile hasa kuchaangiwa na suala la kwenda shule mara kwa mara katika vipindi tofauti, mkizingatia watu wengi wanapitia kada ya uwalimu ikiwa daraja la kwenda unapotaka, japo na hayo yote nimekaa nikiwa mwalimu mtendaji kwa miaka 8-kwa maana muajira, kwa hiyo najua mambo mengi ya walimu kuanzia maisha yao kwa kuwa hadi sasa naishi katika makazi ya walimu kwa maana wifi yenu ni mwalimu, matarajio yao pindi wapatapo kazi kama hawa walioajira juzi, na mengi zaidi.
sasa kwenye suala la mke bora kwa malezi na maisha kwa ujumla kwangu mimi ni mwalimu, sisemi kwa kuwa nina mwalimu hapana, ila kiukweli ni kazi ambayo haimpi stress kubwa sana zikamchanganya kuhudumia watoto (ikiwa Allah amewaruku watoto), wajua muda wake wa kurudi na kwenda kazi, kazi za ziada (mkukuta) zinajulikana na muda pia.
Pia hawa watu mnaweza kufanya mengi ya maendeleo kwa pamoja kwa kuwa anaweza akawa na muda mwingi wa ziada wakufanya kwa ufanisi indi baba unapomjengea uwezo, na maanisha nini, walimu wengi wakike kwa wa kiume ni waoga, uwoga huu wanafundishwa au wanawekewa mazingira tangu wakiwa vyuoni kuanzia wa Diploma na Digirii, ikiwa sivyo pindi pale wanaporipoti kwenye vituo vyao vya kazi, sasa yahitaji
Excel na
kiwatengu kufanya kazi ya ziada ya kumolde mwalimu wako.
sasa kwenye suala la tabia ni issue nyingine,
Excel walimu waliopitia dip niwazuri kitabia zaidi kuliko wale wengine samahani lakini, sababu hawa wanaangaliwa kwa ukaribu zaidi kuliko, wale kwa hiyo hata wale wenye matabia mabaya wakuta ualimu wanamshape sio kwa wadada hata kwa wakaka, mimi nakiri kabisa ualimu umenibadilisha sana....
ukimkuta mwalimu kicheche ah huyo kicheche haswa, lakini hachukui muda mazingira ya kazi ya mbadilisha.
Excel ukiwa unataka kuoa mwalimu usichelewe kufanya hivyo pindi tu anapopata ajira, maana akili yao yote inabaki katika kuanzisha familia suala la kuendelea kielimu hilo ni baadae, baadae sana....
inatosha, au unataka na jinsi wavyocheat....?[/SIZE]