Wanawake wanamaliza sana hela Kwa bodaboda

Wanawake wanamaliza sana hela Kwa bodaboda

Acha tu. Imefikia hatua mtu akikuona unatembea anahisi huna hela ya bodaboda. Wengine kutembea ni mazoezi na ni hobby lakini utakavyosumbuliwa na watoa lift, huwa hawaamini kama kuna mwanamke anatembea kwa hiari yake. Unawahakikishia kwamba huna shida lakini watakulazimisha wakupe lift. Wanakuambia mtu kama wewe sio wakutembea. Wtf???
Wanawake wenzangu tusipende kukaa kizembe tutembee na kufanya mazoezi ili kuepusha magonjwa. Finale uzeeni, kisukari presha nk. kisikie kwa mwenzio.
Kunywa juice ya miwa nakuja kulipa
 
Bodaboda kazi zao sijawai sikia wakilalama maisha magumu ,,,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Wanajua siri za wake za watu kila kona na mitaa wanaijua sijui wanalala saa ngapi 11 wapo macho
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Ndy maana siku hizi unaweza ukapiga nae shoo kimoja Tu,anahema utadhani amepandisha mlima. kutoushughulishisha mwili inachangia

Au nasema uongo cocastic
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Dr una nini wee? Hebu muache wifi ale pesa zako, tena umtafutie boda wake kabisaa.

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Jamii ya sasa kwa ujumla kizazi cha wakati huu chote kimekua na uvivu, sio kwenye boda boda tu hata kwenye dala dala

Kituo hapa hadi pale mtu yupo radhi atoe 300 apande daladala,wakazi wa Dar mtu anapanda daladala Kimara Mwisho

anaenda kushukia Stop Over, au Mtu anapanda Kimara suka Anaenda shukia Temboni sehemu ambazo ukisema unatembea

hata dk 10 humalizi, sishangai watu kuumwa magonjwa yasio na kichwa wala miguu kwasababu ya kutotaka ishughulisha miguu yetu.

Ila nimeandika yoteeee, mimi ni nambari 1 kupanda hiz boda sehemu ya kwenda kwa miguu,mjue sazngine boda inawahisha mambo,dala dala kadhalika Ki ufupi ulimwengu wa sasa watu tunajali MUDA bana eboooo..

Halafu nyie wadada wapanda boda boda mimi nawashukuru maana heri yenu,kuna wale majini wana aleji na boda boda wao ni UBER tu..

Mkuuu usiombe ukutane na majini UBER bwana bwana bwana , ana App zote za online transport mzeee kuanzia UBER,BOLT hao viumbe ukikutana naoooooooo Mkuu hao wanaenda sokoni kwa uber TU..

Anakaa Makumbusho sokoni anaenda manzese chezea wewe.. anakwambia anarahisisha mizunguko ataptia kabisa na saloon kuosha nywele kubandka kucha kwa Athanas mambo kede kedeee.

Sema nini Mkuu, Mtafutie mpenzi/mke wako biashara ili hela ya boda awe anaitoa mwenyewe kupitia biashara yake Hata akitaka kwenda kariakoo na Ndege shauri lake si hela yake mwenyewe. Hela yako jibaneeeeeee Mfungulie kitu apendacho cha kumpa hizo hela za Boda Boda. Mengine achana nayo maana hawachungiki hao wala hawazuiliki n waamue tu wenyewe kubadilika.
Umemalizaaaaah.

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Boda boda wako kazini, kwa hiyo wewe ukisikia unabaniwa na kukandiwa kazi yako utafurahi mkuu??

Leo boda boda tutafanya kikao jioni.
 
Endeleeni kutuachia bajeti za bodaboda..msimsikilize huyo mleta Uzi na Uzi wake batili😜
 
wanawapa biashara na wana wala kweli maana kila siri za jeshi wanajua wao msiwaonee wivu kama vipi na nyie endesheni bodaboda
 
Mbona wanakula hela za wanaume [emoji1][emoji1]hakuna hela ya mwanamke inaliwa hapo, ingekuwa wanalipa wao wasingethubutu kuendekeza huo ujinga
[emoji23][emoji23][emoji23]kweli kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom