Wanawake wanamaliza sana hela Kwa bodaboda

Wanawake wanamaliza sana hela Kwa bodaboda

Bodaboda kazi zao sijawai sikia wakilalama maisha magumu ,,,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Wanajua siri za wake za watu kila kona na mitaa wanaijua sijui wanalala saa ngapi 11 wapo macho
Utasikia ,Amsha popo.
 
Itakuwa ulikuwa haumtaki ulimtafutia sababu tu, hauwezi kuachana na mwanamke kisa amekwambia ana bodaboda wake ,jamii imejenga mtazamo mbaya kwa bodaboda
Hawa ni wanaume wasiojiamini, kuna wanawake wamenunuliwa magari na bado wanawatuma bodoboda sokoni, na jamaa zao wala hawamaindi.

Boda ni usafiri nafuu
 
Mwanamke anakunywa uji wa ulezi wenye "blueband",mtori au supu halafu anashushia na juisi nzito ya embe na parachichi na hataki kutembea afanyishe mwili zoezi na mmeng'enyo upate nafasi.Matokeo yake ni kupata vitambi na magonjwa yatokanayo na aendeshavyo maisha yake.
zoezi la kule naniliu linatosha haya ya kukimbia/kutembea tunawaachia nyie
 
Maisha ndio haya haya, ya nini uungue jua sasa!
 
Mazoezi ni ya jioni jua likishashuka.

Mie kama sina mishe sizururi hata kwa fimbo.

Sina urafiki na boda naogopa sana kupanda ila kuwaagiza fasta tu wanaenda.
Naomba niwe bodaboda wako
 
Kwa hiyo leo mnatunyoosha kisa boda?

Mnajua gharama za kutembea juani nyie?

Lazima tupake moisturiser, toner na sunscreen.

Si bora aende boda tu fasta kuliko ngozi zetu zichakae?

Hebu acheni ubahili.
Ndy maana siku hizi mna vitambi tofauti na zamani..mmekuwa wavivu Sana wa kutembea
 
Jamii ya sasa kwa ujumla kizazi cha wakati huu chote kimekua na uvivu, sio kwenye boda boda tu hata kwenye dala dala

Kituo hapa hadi pale mtu yupo radhi atoe 300 apande daladala,wakazi wa Dar mtu anapanda daladala Kimara Mwisho

anaenda kushukia Stop Over, au Mtu anapanda Kimara suka Anaenda shukia Temboni sehemu ambazo ukisema unatembea

hata dk 10 humalizi, sishangai watu kuumwa magonjwa yasio na kichwa wala miguu kwasababu ya kutotaka ishughulisha miguu yetu.

Ila nimeandika yoteeee, mimi ni nambari 1 kupanda hiz boda sehemu ya kwenda kwa miguu,mjue sazngine boda inawahisha mambo,dala dala kadhalika Ki ufupi ulimwengu wa sasa watu tunajali MUDA bana eboooo..

Halafu nyie wadada wapanda boda boda mimi nawashukuru maana heri yenu,kuna wale majini wana aleji na boda boda wao ni UBER tu..

Mkuuu usiombe ukutane na majini UBER bwana bwana bwana , ana App zote za online transport mzeee kuanzia UBER,BOLT hao viumbe ukikutana naoooooooo Mkuu hao wanaenda sokoni kwa uber TU..

Anakaa Makumbusho sokoni anaenda manzese chezea wewe.. anakwambia anarahisisha mizunguko ataptia kabisa na saloon kuosha nywele kubandka kucha kwa Athanas mambo kede kedeee.

Sema nini Mkuu, Mtafutie mpenzi/mke wako biashara ili hela ya boda awe anaitoa mwenyewe kupitia biashara yake Hata akitaka kwenda kariakoo na Ndege shauri lake si hela yake mwenyewe. Hela yako jibaneeeeeee Mfungulie kitu apendacho cha kumpa hizo hela za Boda Boda. Mengine achana nayo maana hawachungiki hao wala hawazuiliki n waamue tu wenyewe kubadilika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom