Tangu nimefika Dar angalau sasa hivi ndio naona kuna hali nzuri ya hewa ambapo ninaweza hata nikavaa shati ya mikono mirefu.
Angalau sasa hivi hata matumizi ya feni yamepungua na bill ya umeme nayo imepungua.
Angalau sasa hivi ninaweza kujifunika shuka usiku nikilala, hapo awali sikuwahi kujifunika shuka usiku.
Angalau sasa hivi hata nikipanda mwendokasi sikutani na harufu za ajabu ajabu za watu wanaonuka jasho sababu ya joto.
Kwa ufupi tu hii hali ya hewa ya Dar kwa sasa ndio inafaa kwa mtu kma mimi.
Na hakuna baridi, bali kuna kaupepo tu fulani amazing ambako ndio kanafanya watu wavae masweta hasubui.