Mzigua90
JF-Expert Member
- Sep 23, 2014
- 38,405
- 88,864
- Thread starter
- #181
We dada ningekuona ningekwambia uache kulilia maziwa yaliyomwagika. Ukijikuta kwenye hali kama hiyo kitu cha kwanza unajisamehe upuuzi uliofanya kisha unajipanga kuanza kutembea njia mpya. Usitafute tu mtu wa kumlaumu kana kwamba wewe hukuvurunda. Huyo mwanaume msamehe, muache aendelee na maisha yake. Ukikaa kumfikiria utakuwa unapalilia hasira, uchungu na kinyongo. Mhanga wa kwanza wa hicho kisirani ni mtoto wako. Mzazi mwenye mizigo moyoni hawezi kutoa nuru kwa mwanae. Kwa faida yako na mtoto wako kubali kuwa mko wawili ujipange ufurahie maisha.
Unaweza usielewe nikikwambia ushukuru huyo mwanaume kaondoka. Watu wengine wanakuja kwenye maisha yetu kwa kusudi fulani na kuondoka. Utakuja kuelewa baadae sana kwa nini hili limetokea hivi kama tu utatulia. Ingawa Obama hakukataliwa na babake, kutengana na baba yake na kulelewa marekani na mama na bibi zake ndo kulimpeleka kuwa Rais wa kihistoria Marekani. Baba yake aliporudi Kenya aliishia kwenye ulevi na baadae kufa. Sasa angekuwa amerudi Kenya na Barak sidhani kama Barak wa leo angekuwa hata mwenyekiti wa serikali ya mtaa huko Kenya. Hata huyo Diamond sidhani kama baba yake angekubali bibi Sandra kumpeleka diamond kwenye matamasha na mashindano ya muziki usiku.
Mifano ya watu waliotelekezwa na wazazi na kutelekezwa kwao kukawa ndo njia ya mafanikio ni wengi. Tanzania wapo na dunia nzima. Kuwa single parent mwenye matumaini na bidii kama mama wa Dr Ben Carsons. Badala ya kuwaza mwanaume aliyekuacha waza utakavyomtoa mwanao. Huyu mama katika umaskini wake aliweza kutoa mtoto mcha Mungu, mnyenyekevu, mwenye bidii, daktari bingwa duniani wa upasuaji wa mishipa ya fahamu na vingine ongezea.
Kuna baba anaitwa Chris Gardner ambaye kisa chake kilitengeneza movie ya "pursuit of happyness". Huyu alitelekezwa na baba yake na akanyanyaswa na baba wa kambo, na yeye akaja kuzaa kabla ya ndoa na akaachiwa mtoto wa chini ya miaka miwili akiwa hana ajira. Alikataa kulaumu kama wewe. Akakomaa na mwanae - kulala nae kwenye magari mabovu, stendi, kanisani mpaka kikaja kueleweka. Ni milionea aliyeacha biashara na sasa anazunguka dunia kuwatia moyo watu kama wewe na wanaume wanaokimbia watoto. Maisha yale yale ya kutelekezwa ndo yalimfanya akawa baba bora na mmoja wa wanaume waliofanikiwa duniani. Kwa hiyo kukata tamaa au kuvaa ujasiri na kufurahia au kuombelezea hayo maisha yako mapya ni chaguo lako. Amua unataka nini. Mungu huwa si mchoyo. Ukivurunda ukakubali na kumrudia anakupa nafasi ya pili na ya tatu na ya nne.
Thank you.