Wanaume tuoneeni huruma dada/mama zenu

Wanaume tuoneeni huruma dada/mama zenu

Hayo ni mawazo yako mkuu. Kama angekua kitega uchumi ningeanza nae kwenye mimba. Toka nimepata ujauzito hela pekee aliyonipa ni hela ya kwenda kutolea mimba. Na kuna kipindi nilikua sina hata 100 ila sikuwahi kumuomba hela hata ya kwenda clinic. Hata Mungu ni shahidi kama nilishawaza nitaishi kupitia hela za huyu mtoto. Bora angekua ananipa hata kipindi hicho angesema basi nilizuzuka na hela zake ila sikuwahi kuzuzuka nae. Na hata huu ujauzito niliupata kimaajabu tu.


Wewe wajiweza kiuchumi?? Kama ungelikuwa unajiweza kiuchumi usingelikuja na kilio kikali kihivyo. Tulia tu dada, wanaume kwa hasira hufanya upuuzi baadaye wakapata akili wakageukza hasira. Endapo akijua umekuja jf ataongeza umbali uliopo.
Kaeni chini myazungumze. Hiyo hela ya kuitoa hiyo mimba alikupa ukala au?? Huenda ulimwambia umeitoa, halaf akashtukia tena unamwambia bado ipo.
Sifurahii kutoa mimba wala siungi mkono ila kama alifikia hilo, kuna sababu na sababu kama haijatolewa, hamtaelewana. Akimwona huyo malaika, damu zinamsisimka kwani anajiona kuwa tiyari alishamhukumu kifo mtoto.
 
msaidie kwenda ustawi wa jamiii bna
Your wish is my command hun!

Kama yuko willing mimi nampeleka "right place at a right time" tena naanzia Dawati la jinsia na watoto pale Polisi HQ hopefully atapata stahiki yake hapo kabla hata ya kufika ustawi. Si unajua polisi ni shuruti na ubabe kwa mbaaali.

Sema yuko ana willingness!?
 
Just imagine, unaamini mtoto ni wako, lkn hukabidhiwa hadi ulipe:-
1. Ngwekwe
2. Misango
3. Na ulipe mahari hata kama humegi tunda, eti kisa tu umiliki mtoto.

Kwa nini nisikupe uhuru wa kulea? Siku akijua yeye siyo Yesu, atanitafta tu
 
We dada ningekuona ningekwambia uache kulilia maziwa yaliyomwagika. Ukijikuta kwenye hali kama hiyo kitu cha kwanza unajisamehe upuuzi uliofanya kisha unajipanga kuanza kutembea njia mpya. Usitafute tu mtu wa kumlaumu kana kwamba wewe hukuvurunda. Huyo mwanaume msamehe, muache aendelee na maisha yake. Ukikaa kumfikiria utakuwa unapalilia hasira, uchungu na kinyongo. Mhanga wa kwanza wa hicho kisirani ni mtoto wako. Mzazi mwenye mizigo moyoni hawezi kutoa nuru kwa mwanae. Kwa faida yako na mtoto wako kubali kuwa mko wawili ujipange ufurahie maisha.

Unaweza usielewe nikikwambia ushukuru huyo mwanaume kaondoka. Watu wengine wanakuja kwenye maisha yetu kwa kusudi fulani na kuondoka. Utakuja kuelewa baadae sana kwa nini hili limetokea hivi kama tu utatulia. Ingawa Obama hakukataliwa na babake, kutengana na baba yake na kulelewa marekani na mama na bibi zake ndo kulimpeleka kuwa Rais wa kihistoria Marekani. Baba yake aliporudi Kenya aliishia kwenye ulevi na baadae kufa. Sasa angekuwa amerudi Kenya na Barak sidhani kama Barak wa leo angekuwa hata mwenyekiti wa serikali ya mtaa huko Kenya. Hata huyo Diamond sidhani kama baba yake angekubali bibi Sandra kumpeleka diamond kwenye matamasha na mashindano ya muziki usiku.

Mifano ya watu waliotelekezwa na wazazi na kutelekezwa kwao kukawa ndo njia ya mafanikio ni wengi. Tanzania wapo na dunia nzima. Kuwa single parent mwenye matumaini na bidii kama mama wa Dr Ben Carsons. Badala ya kuwaza mwanaume aliyekuacha waza utakavyomtoa mwanao. Huyu mama katika umaskini wake aliweza kutoa mtoto mcha Mungu, mnyenyekevu, mwenye bidii, daktari bingwa duniani wa upasuaji wa mishipa ya fahamu na vingine ongezea.

Kuna baba anaitwa Chris Gardner ambaye kisa chake kilitengeneza movie ya "pursuit of happyness". Huyu alitelekezwa na baba yake na akanyanyaswa na baba wa kambo, na yeye akaja kuzaa kabla ya ndoa na akaachiwa mtoto wa chini ya miaka miwili akiwa hana ajira. Alikataa kulaumu kama wewe. Akakomaa na mwanae - kulala nae kwenye magari mabovu, stendi, kanisani mpaka kikaja kueleweka. Ni milionea aliyeacha biashara na sasa anazunguka dunia kuwatia moyo watu kama wewe na wanaume wanaokimbia watoto. Maisha yale yale ya kutelekezwa ndo yalimfanya akawa baba bora na mmoja wa wanaume waliofanikiwa duniani. Kwa hiyo kukata tamaa au kuvaa ujasiri na kufurahia au kuombelezea hayo maisha yako mapya ni chaguo lako. Amua unataka nini. Mungu huwa si mchoyo. Ukivurunda ukakubali na kumrudia anakupa nafasi ya pili na ya tatu na ya nne.
 
Nakubaliana na ww 100%, lilishawahi kunitokea, mwanamke niliekuwa nae kwenye mahusiano bahati mbaya alipata ujauzito wang, nikakubali kugharamia ujauzito mpaka anajifungua mwaka 2002 kila mwezi nilikuwa natoa tshs50, 000/=, baada ya kujifungua ndo mtihani ulipoanza, ukituma tshs100, 000/= baada ya siku tatu unaambiwa hela imeisha, ukihoji imetumika vp anakuwa mkali kwelikweli, ukumbuke mwaka 2003 tshs100, 000/= ilikuwa ni pesa kubwa unaweza nunua kiwanja au shamba, ikafikia kipindi nikamwambia siwezi ongeza pesaila nitatuma hiyohiyo tshs 100,000/= mungu wangu nilichambwa balaa, "kati ya wanaume na ww unajiona mwanaume? kwanza mtoto sio wako", hiyo kauli iliniuma nikaamua kusitisha utoaji wa pesa, ndo matusi yakazidi mi kimyaa sijibu chochote, ikapita miaka10 nikapata taarifa kuwa mwanao anapata shida sana kijijini analima vibarua ndo apate kula, dah roho ikaniuma sana nikajiuliza mmm niko dsm nafanya kazi, naishi vizuri, nakula vizuri naishi kwangu inakuwaje mwanangu apate shida? nikalianzisha sekeseke la kudai mtoto lakini mama mtoto mkali balaa, nikapiga mkwara kama ni mwanangu kweli namhitaji vinginevyo akipata tatizo usinihusishe kwa lolote, akakaa akajifikiria mwisho akasema tuma nauri nikuletee mwanao, nikatuma tshs80000/=toka iringa kuja dsm lakini nayo ikaliwa, nikatulia kimya kama miezi miwili akanitafuta na kunieleza kuwa ile pesa ilitumika kumtibu mama yake kwa hiyo anaomba samahani, nikatuma tena tshs80, 000/=akasafirishwa kijana hadi dsm mpaka ss niko nae home anaendelea na masomo, mida mingine huwa tunavumilia mengi ila baadhi ya wanawake huwa wanajiwahi kulaumu tu bila kujua kuwa chanzo cha matatizo mengine husababisha wao.
Pole mkuu,
 
Kwa kweli hapo pande zote zina husika! Kwanini ulibeba mimba ikiwa mtu uliyenaye haeleweki? Je ulijipanga na kuwaza how will you rise your child kabla hujabeba mimba just incase anything happen btn you two? Ulibeba mimba kwa kutaka wewe au yeye alitaka ubebe kisha akasepa? The problem is kuna wakt mwanamke akifika umri fulani anatamani kuitwa mama sasa kwa kuwa hajaolewa pia kajilinda asibebe mimba huko nyuma sasa hajui kama kweli mbegu inaota ikipandwa au bila ikitokea tu anajaribu na matokeo yake sasa kushika kwakwe mimba ndio iwe njia yake ya either muingie kwenye familia au kumfany mtot ndio awe njia ya kuwaleta pamoja wkt pengine mwanaume hakuwa tayr kuitwa baba na bado anandoto zake anazoziandaa kwaajili ya yake na familia atakayokuwa nayo so unadhani atafanya nini kama sio kuchapa ndala? Sikos upande wowote but yyt anaweza kuwa chanzo cha mwingine kusepa
 
Nikiwa kama mhanga wa mwanamke alieachiwa matunzo ya mtoto bila msaada wa baba naumia sana.
Hivi wanaume huwa mnawaza nini mnapotupa adhabu ya kulea watoto peke yetu na wewe baba ukiwa hai na unajiweza? Hata kama hujiwezi basi kumjali mtoto wako japo kwa kuulizia maendeleo yake mtu anashindwa kabisa. Hivi kina kaka mmejiuliza nyie baba zenu wangewakimbia mngekuwa wapi sasa hivi? Mnajua ni chuki gani mnaweka kwa watoto wenu mliowakataa? Mnajua ni laana gani mnapata kwa Mungu kwa kukataa kutimiza wajibu wenu kama wazazi? Au mnatukomoa kwa sababu mama hawezi kumuacha mtoto wake nyuma hata apate tatizo gani? Labda wewe na mama wa mtoto hamko sawa lakini ile hasira ya ninyi kutokua sawa baba usimkomeshe mama kwa kuacha kumtunza mwanao ukijua unamkomoa mama, pale unaemkomoa ni mtoto wako ambae ulimtafuta kwa mapenzi/tamaa zako mwenyewe.
Naandika nikiwa na uchungu mwingi sana moyoni. Mwanaume usiemtunza mwanao ona aibu na muogope Mungu wako kwa kitendo unachokifanya.
Jiulize ingekua ni dada yako au mwanao ameachwa na mwanaume alee mtoto peke yake ungejisikiaje?
KARMA IS A BITCH. Ukinifanyia mimi leo wakati unao dada na watoto wa kike jua itakuumiza na wew kwa mmoja kati ya hao kufanyiwa kama unavyofanyia wengine.
Baba mtoto wangu nimeshamlilia Mungu juu yako na nina hakika huyu mtoto ulieniachia nimlee peke yangu atanifuta machozi siku moja na utatamani akutambue kama baba yake utakua umeshachelewa.
Kaka/baba zangu baba Diamond akawe mfano kwenu, Obama aliekataliwa na baba yake mwishoni alikuja kuwa Rais wa marekani/dunia.
Pole sana Dada, kwa kwelo siungi mkono wanaume wanaokataa
Nikiwa kama mhanga wa mwanamke alieachiwa matunzo ya mtoto bila msaada wa baba naumia sana.
Hivi wanaume huwa mnawaza nini mnapotupa adhabu ya kulea watoto peke yetu na wewe baba ukiwa hai na unajiweza? Hata kama hujiwezi basi kumjali mtoto wako japo kwa kuulizia maendeleo yake mtu anashindwa kabisa. Hivi kina kaka mmejiuliza nyie baba zenu wangewakimbia mngekuwa wapi sasa hivi? Mnajua ni chuki gani mnaweka kwa watoto wenu mliowakataa? Mnajua ni laana gani mnapata kwa Mungu kwa kukataa kutimiza wajibu wenu kama wazazi? Au mnatukomoa kwa sababu mama hawezi kumuacha mtoto wake nyuma hata apate tatizo gani? Labda wewe na mama wa mtoto hamko sawa lakini ile hasira ya ninyi kutokua sawa baba usimkomeshe mama kwa kuacha kumtunza mwanao ukijua unamkomoa mama, pale unaemkomoa ni mtoto wako ambae ulimtafuta kwa mapenzi/tamaa zako mwenyewe.
Naandika nikiwa na uchungu mwingi sana moyoni. Mwanaume usiemtunza mwanao ona aibu na muogope Mungu wako kwa kitendo unachokifanya.
Jiulize ingekua ni dada yako au mwanao ameachwa na mwanaume alee mtoto peke yake ungejisikiaje?
KARMA IS A BITCH. Ukinifanyia mimi leo wakati unao dada na watoto wa kike jua itakuumiza na wew kwa mmoja kati ya hao kufanyiwa kama unavyofanyia wengine.
Baba mtoto wangu nimeshamlilia Mungu juu yako na nina hakika huyu mtoto ulieniachia nimlee peke yangu atanifuta machozi siku moja na utatamani akutambue kama baba yake utakua umeshachelewa.
Kaka/baba zangu baba Diamond akawe mfano kwenu, Obama aliekataliwa na baba yake mwishoni alikuja kuwa Rais wa marekani/dunia.
pole sana my dia. Kwa kweli siungi mono wanaume wasiohudumia watoto wao
 
Pole sana Mom. Wala sitakimbilia kukulaumu kwa kubeba uja uzito.

Cha kufanya ni kutambua kuwa sisi ni wanawake. Hatupo sawa na wanaume. Sisi ni zaidi yao. Tunaweza zaidi yao.

Futa machozi na amua moyoni kwako hutalia tena wala kuwa na machungu ama huzuni na utamlea mtoto mwenyewe.

Sio rahisi of course but inabidi ufanye kwa ajili ya mtoto wako. Mtoto hana hatia. Piga kazi/ biashara mpe mahitaji yake ya msingi. Ipo siku Mungu atakujaalia wepesi.
 
sio akina baba tu, hata nyie pia mnamatatizo! mbona mwanamke mwenzio juzi kakitupa kichanga ziwa victoria? au yule pia ni baba? tena nyie ndio hamna hata chembe ya huruma!! jitathmin kwanza dada yangu huenda ww ndio chanzo cha mwanaume kukimbia?
 
Asante kaka. Tatizo sio hilo, kuna watoto wamezaliwa utasema ni copy ya baba zao lakini huyo baba bila aibu anashindwa kumuhudumia mwanae.
copy hata pesa wanafotoa cha msingi kaa pembeni angalia wapi umekosea hadi ukimbiwe, then rudi back on track
 
Back
Top Bottom