Wanaume tuoneeni huruma dada/mama zenu

Wanaume tuoneeni huruma dada/mama zenu

Wale Sauti Sol wa Kenya hawakataagi mtoto hata Nerea walimsisitiza awapelekee mtoto wao watamlea..labda jaribu kwao ila hawa wa kibongo ni Pasua kichwa dadangu.

Ila kwa jinsi ninavyotafuta mtoto kwa gharama yeyote..huyo mwanamke atakenizalia si nitamkopea mkopo wa Saccos hapa wizarani ale na mwanangu na apumzike na uchovu wa uzazi..yani ndo maternity leaves yake hiyo..!

Afu napendaga wanawake wenye watoto....they are very easy to start a relationshio with them..yaani hapa nikianza kumcare na kumpenda mtoto kwa kiwango cha dunia basi automatically na mama yake ananipenda and voila! Abracadabra!

Anyways!! Sorry can I adopt her Mzigua90?
hivi baby tunazaa lini?
 
Let say sikua smart mimba ikaingia, bado nitakua nastahili kulea mtoto peke yangu sababu sikua smart kuzuia mimba?
Halafu sio kila mimba inaingia mtu akiwa anajua leo inaingia au leo lazima nimbebee mimba huyu. Nyingine zinaingiaga bahati mbaya hata ukijitahidi vipi kuizuia. Mimi yangu nilihakikisha mwanaume amevaa kinga sababu hatukua serious kiasi cha kusema niwe comfortable nae kumuachia tu bila kinga lakini at the end of the day nilijikuta mjamzito, sasa kwa kuwa nilimuona hatuna future ningeenda kuitoa ile mimba?
Unajua hata mama awe tajiri kama Folorunsho na baba awe kama matonya lakini ile hali ya baba kumnunulia mtoto hata pipi tu huwa inafariji. Kweli kipato changu sio kikubwa kusema kinanitosha kuishi na kusave lakini bado haikua sababu ya mimi kutoa kiumbe kilichoingia sababu sijajipanga ungekua ni ubinafsi.

Kama kinga ilitumika ilipasuka au aliitoa katikati ya game!?

Pole sana
 
ukikimbia mtoto adhabu nitakayokupa huta kaa unisahahu milele... nawaambiaga watu hivi wanaiambia na roho mbaya but not easy in such ... ila dada pole sana muache kuwa na mioyo ya huruma na kususa kama unahakika ni mtoto wake ana anauwezo kifedha chukua hatua mpeleke kwenye vyombo vya sheria ni jukumu lake kulea no matter anakupenda hakupendi hilo halimuhusu mtoto...... hakuna swala la kumuachia Mungu

Tatizo tulishaongea tukakubaliana kila kitu kuhusu kumlea mtoto. Tatizo ni kwamba baada ya kuongea hayo akapotea na simu hapokei tena. Nilichomwambia tu ahesabie amekufa kwenye maisha ya mtoto wangu. Yani ajue ana mtoto ila asitegemee mtoto atakuja kumjua kama yeye ni baba ake sababu nitamwambia mtoto baba ake alikufa na akiujua kweli kuwa baba yake yuko hai nitamwambia ukweli baba yako hakupendi alikukataa ili asije kuwa kama baba Diamond baadae. Nimemtumia msg kumwambia yote hayo akabaki kimya hata kusema ok kashindwa.
 
Nipigie tuyamalize ndo nini sasa kuja kuniaibisha huku
We mwanamke wewe.... Mungu anakuona
 
Kila mtu ana malengo yake kwenye maisha tena nyie ndo unakuta mnategesha mimba ili muolewe.Mkikataliwa mnaishia kuwalaani wakati chanzo ni nyie.Wewe kama upo tayari kuzaa tafuta aliye tayari sio kumzalia asiye tayari na ukilazimisha kila mtu atabeba msakaba wake utatiwa mimba the rest utajua mwenyewe

Usihukumu mkuu. Sio kila mtu anategesha mimba makusudi. Sikua tayari kuzaa kabla ya ndoa ila yaliyotokea yametokea. Nimeubeba msalaba wangu wa kulea mtoto mwenyewe.
 
madada wakati mwengine huwabambikia wanaume watoto sio wao!! mkiambiwa suala la DNA mnaruka mita 100, ufanano wa sura si kigezo cha mtoto kuwa wako kwa maana inawezekana hilo njemba jengine pia limefanana na hiki kidume!!! msibebeshe watu mizigo sio yao kwani nanyi pia mnakuwa na majukumu! na pengine unakuta mwanamme wako amekufumania upo na njemba nyengine ndiyo akakuacha kisha unadai wakati anakuacha alikuwa na ujauzito wako

Najua yanatokea hayo ya kubambikia mtu mtoto ila ni dhambi sana kumpa mtu akulele mtoto ambae sie wake.
 
Nikiwa kama mhanga wa mwanamke alieachiwa matunzo ya mtoto bila msaada wa baba naumia sana.
Hivi wanaume huwa mnawaza nini mnapotupa adhabu ya kulea watoto peke yetu na wewe baba ukiwa hai na unajiweza? Hata kama hujiwezi basi kumjali mtoto wako japo kwa kuulizia maendeleo yake mtu anashindwa kabisa. Hivi kina kaka mmejiuliza nyie baba zenu wangewakimbia mngekuwa wapi sasa hivi? Mnajua ni chuki gani mnaweka kwa watoto wenu mliowakataa? Mnajua ni laana gani mnapata kwa Mungu kwa kukataa kutimiza wajibu wenu kama wazazi? Au mnatukomoa kwa sababu mama hawezi kumuacha mtoto wake nyuma hata apate tatizo gani? Labda wewe na mama wa mtoto hamko sawa lakini ile hasira ya ninyi kutokua sawa baba usimkomeshe mama kwa kuacha kumtunza mwanao ukijua unamkomoa mama, pale unaemkomoa ni mtoto wako ambae ulimtafuta kwa mapenzi/tamaa zako mwenyewe.
Naandika nikiwa na uchungu mwingi sana moyoni. Mwanaume usiemtunza mwanao ona aibu na muogope Mungu wako kwa kitendo unachokifanya.
Jiulize ingekua ni dada yako au mwanao ameachwa na mwanaume alee mtoto peke yake ungejisikiaje?
KARMA IS A BITCH. Ukinifanyia mimi leo wakati unao dada na watoto wa kike jua itakuumiza na wew kwa mmoja kati ya hao kufanyiwa kama unavyofanyia wengine.
Baba mtoto wangu nimeshamlilia Mungu juu yako na nina hakika huyu mtoto ulieniachia nimlee peke yangu atanifuta machozi siku moja na utatamani akutambue kama baba yake utakua umeshachelewa.
Kaka/baba zangu baba Diamond akawe mfano kwenu, Obama aliekataliwa na baba yake mwishoni alikuja kuwa Rais wa marekani/dunia.
Tatizo kubwa linalowasumbua vijana wengi ni kutokuwa na uhakika juu ya baba wa mtoto kutokana na tabia zenu na kauli zenu za masimango

Pia wanashuhudia mifano katika jamii zao na kushuhudia namna ambavyo wanaume wenye moyo unaouhitaji wanavyo nyanyasika kwa kejeli kama MTOTO AMEKUA NDO LEO UNAAMBIWA SI WAKO.
Walaumu wanawake wenye midomo kama hiyo
 
Mwanamke unatakiwa uwe smart pia, usichukue mimba huku ukiwa unamtegemea mtu asiyeeleweka na sio mume... au kuwa na kazi ya kukupa kipato cha kumtunza mwanao kabla ya kuchukua mimba nje ya ndoa.. japo wanaume wana makosa ila mnaweza kupunguza extent ya watoto kulelewa kwenye umasikini kwa kuwa makini
true that
 
Nikisikiaga hizi kauli namkumbuka binti mmoja aliyempiga kofi daktari baada ya kuambiwa anaujauzito, alikuwa makini sana ila ikatokea, kwahiyo ndugu haya mambo hutokea tu hata kwa walio ndoani, cha msingi ni mkumbuke tu hizo damu zenu muwe part of their lives no mata what!! Hebu ufikirie tu ingekuwa ni wewe umetelekezwa hivyo ungejisikiaje?
"alikua makinj sana,ila ikatokea" how?????
 
tutazunguka sana lakini lililokubwa hapa ni kwamba tatizo kubwa ni la kimaadili.
sio kwamba zamani hali hii haikuwepo lakini kwa sasa mambo yamekuwa tofauti zaidi.
wazazi hawana vikao na watoto wao wanafikiri watoto wanahitaji shule tu na vingine si vya msingi.
matokeo yake ni mmomonyoko wa maadili kwa jamii nzima.
tekinolojia staili ya maisha tunayoishi sasa imefanya uhitaji wa ngono uwe mkubwa sana na hasa kwa vijana.
weekend moja niliingia bar moja kwa chakula cha mchana nikakuta kundi la vijana wa kiume wakila chips tena walio ingia na kukaa meza tofauti likanistua sana jambo hili tena wakiwemo "wasukuma"! hii ni dalili ya kutengeneza kizazi cha watu wavivu wasiofikiria mbali na haya ndio matokeo yake.
ni vigumu kusema kitu nikaeleweka lakini tuelewe kuwa kinacholalamikiwa tusipokuwa makini kwa watoto wetu pia kina kuja.
zaidi ya asilimia hamsini (50%) ya wachangiaji na wanachama wa jamii forum wameumizwa na wazazi wao nikiwemo mimi japo hatuko tayari kueleza ukweli lakini wengi wamekuwa ndio watu wa kuumiza wanawake hawa.
hivyo nashauri tuwe na michango ya kutosha kwa jamii na tuwe mfano wa kukaa na kuongea na watoto wetu.
najua wengi tumebadilisha lugha za kuongea kwenye nyumba zetu tunaongea kithungu ili mtoto waende na kasi ya shule lakini tunashindwa kujua kuwa hatuna maneno mengi ya ushawishi ya kizungu yanayoweza kujenga hoja ya kumjenga mtoto tunaishia na sentence tatu mpaka tano kama ifuatavyo:-
mtoto:good evening dady!
baba: huku ukiwa umetengeneza uso wa mtoto asiendelee sana unaitika good evening!
baba:did you done your home work?
mtoto: Yes dady
baba😱k go to sleep tomorrow school.
mtoto:dady.....
baba:talk to your mummy!
sasa hapa inakuwaje hakuna uhusiano mzuri na mtoto matokeo yake mtoto analelewa na dada wa ndani na jamii na haya ndio matokeo wakiharibikiwa tnawaita malaya!
hali ni mbaya sana ndugu zangu hebu tuhamie huku siasa tuiache kwa muda tupike kelele na jamii yetu kwa sasa!
 
Let say sikua smart mimba ikaingia, bado nitakua nastahili kulea mtoto peke yangu sababu sikua smart kuzuia mimba?
Halafu sio kila mimba inaingia mtu akiwa anajua leo inaingia au leo lazima nimbebee mimba huyu. Nyingine zinaingiaga bahati mbaya hata ukijitahidi vipi kuizuia. Mimi yangu nilihakikisha mwanaume amevaa kinga sababu hatukua serious kiasi cha kusema niwe comfortable nae kumuachia tu bila kinga lakini at the end of the day nilijikuta mjamzito, sasa kwa kuwa nilimuona hatuna future ningeenda kuitoa ile mimba?
Unajua hata mama awe tajiri kama Folorunsho na baba awe kama matonya lakini ile hali ya baba kumnunulia mtoto hata pipi tu huwa inafariji. Kweli kipato changu sio kikubwa kusema kinanitosha kuishi na kusave lakini bado haikua sababu ya mimi kutoa kiumbe kilichoingia sababu sijajipanga ungekua ni ubinafsi.
mmmhhh hii ngum kumeza asee...labda kwasababu haijanitokea...
 
Haya mambo si rahisi kama tunavyofikiri. Wanawake ni pasua kichwa anakueleza kuwa wewe achana na Mtoto wangu nitamlea hata kwa kuuza k sishindwi. Baadaye anaanza kulalamika! Hakuna Mwanaume anamtupa mtoto wake bila kuchoshwa na kejeli za mama yake. Hii inawahusu wanawake wa Tanga Mzigua90
 
Back
Top Bottom