Alvin Slain
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 6,375
- 3,665
Vijana kuchezea maisha ni jambo linakuja automaticaly so huwezi kupita ujana bila kujirusha.tatizo linakuja pale mtu anapojisahau kuwa anapoteza muda
sina uhakika na hesabu zako. kama kima cha chini kilikuwa ni shilingi elfu tatu na yeye alipewa elfu ishirini ina maana alipewa mshahara wa miezi saba. sasa sijui kama mishahara ya miezi saba ilikuwa inatosha kujenge nyumba na kumaliza. ila kama ulimsikia vizuri alisema alinunua kiwanja na kuanza ujenzi wa nyumba yake anayoishi sasa hivi.
Lazima mjue mazingira ya kipindi kile kwa kiongozi tu kuwa na nyumba binafsi ilikuwa ni dhambi. maana maswali yangekuja umepata fedha wapi za kujenga nyumba.
ukija kwenye masuala ya hatimiliki ndiyo ulikuwa usipime kabisa. nyimbo zote ni mali ya redio tanzania hupewi hata sumni. hakuna tapes wala cd wala show binafsi. bendi zote zilikuwa ni za mataasisi. mwanamuziki unalipwa mshahara kama mfanyakazi. wachache kama akina mbaraka mwinshehe ndiyo walikuwa wanafurukuta wanaenda nairobi wanauza master tape kwa mhindi kwa ujira mdogo.
elimu na ari ya ujasiriamali haikuwepo kama zama hizi. enzi hizo utaifa na uzalendo ulikuwa namba moja. wengi wao walikuwana vipaji vya hali ya juu kuliko hawa wa kurekebishiwa vyombo na sauti kwenye mastudio lakini hawakufaidi kazi za mikono yao. haya mazingira ya sasa hivi ya mapromo redio binafsi matamasha na kufunguka kwa soko huria na soko la nje hayakuwepo enzi hizo. mambo yalikuwa yamebana sana.
mi nikiwawaza hawa madingi zetu nakosa raha sana....Wanajisahau mno
wakati kila kitu kwao ilikuwa easy
mashamba ya kuomba tu serikalini
viwanja hununui,unalipa tu ardhi unapimiwa
mi nikiwawaza hawa madingi zetu nakosa raha sana....
life yao ilikua affordable sana, sasa hivi hawana hata cha kutupa....zaidi ni lawama na kutuona sisi ndo tunakosea sana kuendeleza maisha yetu.
anyway back to your topic we have to learn and act though it will be tough enough to make us crazy.....
wababa wengi wametawaliwa na mfumo dume, kwao kisa hela ni zao basi wanataka matumizi yao wayasimamie wenyewe. Wazzazi kama hawa huwaga wanatafuta mtu wa kumlaani baadae.gombaneni nae sasa hivi
atawasumbua mno huyo baadae...
Atawatolea laana msipompa pesa...hapo baadae
mngeanza kugombana nae sasa
bora tunakubaliana kwa hili.....Unavyopenda mambo ya hivyo, hata sijui unajisikiaje... Lol!
Ila ni kweli, mtu ukipata mke wa hovyo imekula kwako!
ha haaa, umenichekesha tunapoongea pale nyumbani (mbele ya watoto wetu) kuwa tunajiandalia maisha yetu ya baadae....Wanaudhi watu wa aina hii. Halafu usipowasaidia walalamishi hawakumbuki kabisaa walikotoka kweli watu husema mla kunde husahau lkn mzoa maganda huwa hasahau.Tena hujisifia kwamba bila mimi usingezaliwa , basi mwenzio nashangaaga sana na kusema kwani usingezaa wewe mtoto huyo si angezaliwa kwingine tena ulimpotezea opportunities nyingi tu. Ifike mahala wazee wa kesho wasiige hii tabia ya wazee wetu .
bora tunakubaliana kwa hili.....
yale mengine ambayo huyakubali basi nimeamua kuyapotezea, lol!
Hahahahahaaaa...... I wish uwe president wewe, alaf mimi waziri wa kilimo na mifugo!
That's right! Unalala vibarazani, kutwa kwenye vijiwe vya majungu, hata kufuga kuku wawili wa kienyeji wasio nagarama kubwa ya madawa na vyakula unashindwa, hata kuweka bustani ya mchicha uani, kupunguza garama ya fedha ya chakula huwezi!
Unapokuwa na nidhamu na bidii kwa vitu vidogo ndivyo Mungu naye anakupa maarifa ya mambo makubwa!
Yaani Eiyer umeeleza vzr haswa! Ni dini Fulani ivi ndiyo inawadumaza watu kutokufanya kazi kwa bidii, wala kutopanga future eti Mungu akipenda ndio utakuwa tajiri!
Dini zingine ni za hovyoo na ni za Shetani mwenyewe manake Mungu si dhalimu wala hana upendeleo.
Kama ulivyosema Mungu ameweka kanuni, na ukizifuata huwezi kubaki maskini!
ha haaa, hapo kwenye kutaka kukimbia nyumba ndo balaa, lol!Kwenye hili sina ubishi mkubwa mwenzangu....
Mwenzenu hadi sasa, karibia vitu vingi sifanyi bila ruhusa ya bibi....ila wakati mwingine anakaba sana hadi natamani kukimbia nyumba....
Mwanamke wa hovyo ni zaidi ya kiroba cha misumali.....
Ndiyo maana nawakubali na kuwaheshimu akina na mama wenye busara zao, wakiongozwa na Bibi DC, mama yangu mazazi na wengine kibao....!!
Babu DC!!
Mara ya kwanza niliposikia Mzee Gurumo wa Msondo Ngoma
anadai ameimba zaidi ya miaka 50 na maisha yake bado
ya 'kimaskini mno' niliona kuna kitu hakiko sawa..
sikuwa na ushahidi tu lakini nilikuwa na uhakika kwa vyovyote vile
'atakuwa alichezea maisha ujanani'
Sasa jana walioona akifanyiwa interview na Salama kipindi cha MKASI
watakubaliana na mimi huyu Mzee na wengine wengi tunaosikia
wakihojiwa na vyombo vya habari ..wakilaumu serikali kwa kutowajali.
wengi wao walipata 'golden opportunities' za kuwa na maisha bora
lakini 'walichezea pesa' na 'opportunities hizo' so many times...
mfano Mzee Gurumo jana alisema alilipwa 'elfu ishirini'
mwaka 1978 ili kuhamia bendi ya Sikinde...kumbuka
kuwa Mshahara wa Rias mwinyi mwaka 1992 ulikuwa 'elfu ishirini na saba tu'
sasa pata picha huyu mzee alikuwa na pesa kiasi gani?
na mshahara wake ulikuwa 'shilingi elfu tatu' mwaka hu0 1978..
wakati kima cha chini mpaka mwaka 1987 kilikuwa hakijafika 'shilingi elfu saba'
Kuna Mzee mwingine alitunga kitabu riwaya 'Simu ya Kifo' alilipwa
'elfu kumi na mbili ' miaka hiyo nyumba Kariakoo zinauzwa shilingi 'mia nne'
na alikufa bila nyumba wala kibanda..
Orodha ni ndefu...na wapo wengine Baba zetu,Wajomba,babu na kadhalika
ukiwaona uzeeni wanavyolalamika na kuomba wasaidiwe....utasema hawakupata chochote ujanani
kumbe anasa,starehe na kuhonga wanawake ndo sababu....
ukweli ni kwamba watu 'huchezea maisha mno' halafu uzeeni hutafuta wa kumpa lawama
mara watoto,mara serikali na kadhalika....
huyu Mzee Gurumo alikuwa sio mtu wa kupewa gari na Diamond...
angekuwa na magari na majumba tele ya kuwarithisha watoto na wajukuu...