Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Vijana kuchezea maisha ni jambo linakuja automaticaly so huwezi kupita ujana bila kujirusha.tatizo linakuja pale mtu anapojisahau kuwa anapoteza muda
 
sina uhakika na hesabu zako. kama kima cha chini kilikuwa ni shilingi elfu tatu na yeye alipewa elfu ishirini ina maana alipewa mshahara wa miezi saba. sasa sijui kama mishahara ya miezi saba ilikuwa inatosha kujenge nyumba na kumaliza. ila kama ulimsikia vizuri alisema alinunua kiwanja na kuanza ujenzi wa nyumba yake anayoishi sasa hivi.

Lazima mjue mazingira ya kipindi kile kwa kiongozi tu kuwa na nyumba binafsi ilikuwa ni dhambi. maana maswali yangekuja umepata fedha wapi za kujenga nyumba.

ukija kwenye masuala ya hatimiliki ndiyo ulikuwa usipime kabisa. nyimbo zote ni mali ya redio tanzania hupewi hata sumni. hakuna tapes wala cd wala show binafsi. bendi zote zilikuwa ni za mataasisi. mwanamuziki unalipwa mshahara kama mfanyakazi. wachache kama akina mbaraka mwinshehe ndiyo walikuwa wanafurukuta wanaenda nairobi wanauza master tape kwa mhindi kwa ujira mdogo.

elimu na ari ya ujasiriamali haikuwepo kama zama hizi. enzi hizo utaifa na uzalendo ulikuwa namba moja. wengi wao walikuwana vipaji vya hali ya juu kuliko hawa wa kurekebishiwa vyombo na sauti kwenye mastudio lakini hawakufaidi kazi za mikono yao. haya mazingira ya sasa hivi ya mapromo redio binafsi matamasha na kufunguka kwa soko huria na soko la nje hayakuwepo enzi hizo. mambo yalikuwa yamebana sana.

Mkuu umenena vema sana.
 
Wanajisahau mno
wakati kila kitu kwao ilikuwa easy
mashamba ya kuomba tu serikalini
viwanja hununui,unalipa tu ardhi unapimiwa
mi nikiwawaza hawa madingi zetu nakosa raha sana....
life yao ilikua affordable sana, sasa hivi hawana hata cha kutupa....zaidi ni lawama na kutuona sisi ndo tunakosea sana kuendeleza maisha yetu.

anyway back to your topic we have to learn and act though it will be tough enough to make us crazy.....
 
mi nikiwawaza hawa madingi zetu nakosa raha sana....
life yao ilikua affordable sana, sasa hivi hawana hata cha kutupa....zaidi ni lawama na kutuona sisi ndo tunakosea sana kuendeleza maisha yetu.

anyway back to your topic we have to learn and act though it will be tough enough to make us crazy.....

Halafu huwa naishia kuchekea tumboni wanapotoa ule usemi wao kuwa...'tatizo vijana wa siku hizi mna haraka sana'.....Nani anataka siku ya kustaafu arudi kijijini ambako huenda wala hakuwahi kukuendeleza? Manake hicho ndio kilitokea sana kwao, nyumba bure, mpaka fanicha..siku ya kustaafu anaondoka na masanduku yake tu, hata kibanda hana. Na alternative anayobaki nayo ni kurudi kijijini, kijijini nako hakujenga...and the list goes on and on...
 
Mi nafikiria tofauti kidogo hapo mazingira ya kazi hizi ni tofauti sana na wakati mwingi ndio maana utakuta watu wanaolipwa fedha nyingi bado wanshindwa kufanya mambo makubwa na mtu ambaye analipwa kidogo kutokana na mazingira ya kazi
 
gombaneni nae sasa hivi
atawasumbua mno huyo baadae...
Atawatolea laana msipompa pesa...hapo baadae
mngeanza kugombana nae sasa
wababa wengi wametawaliwa na mfumo dume, kwao kisa hela ni zao basi wanataka matumizi yao wayasimamie wenyewe. Wazzazi kama hawa huwaga wanatafuta mtu wa kumlaani baadae.

Nakumbuka baba mmoja mchaga wanae walipoona baba anaendekeza starehe na ni meneja wa sida kanda fulan walianza kuwa wakaksi wao na mama yao. Dingi kama halipi school fees kids wanabaki home, wala mama hastuuki anasema kabaisaa baba yenu awalipie.

Baba akaanza kuona maisha ya kupanga ndio bomba mama akaanza mkakati kila akirudi job, wanagombana kisaha anasaula pesa zote akiachiwa pesa ya msosi hapiki anabana dingi akirudi anaambiwa msosi hakuna pesa zimekwenda kununua site hadi akili ikamkaa sawa.

Huyu mama alihangaika hadi akaweza kununua site na kujenga tena kwa mbinde, mzee wa watu kwa ulevi sukari ikamuadabisha hajakaa sawa maini yakafeli, sasa ikaanza kuwa msala wa mama na watt lkn bora alikomaa wakapata mjengo na watt wakasoma.

Ninachoweza kusema muda mwingine mwanamke unapaswa kuwa ngangari kwa mumeo yani bora lawama kuliko fedheha. Unakaza uso kama mume haelekei.
 
Vijana kuchezea maisha ni jambo linakuja automaticaly so huwezi kupita ujana bila kujirusha.tatizo linakuja pale mtu anapojisahau kuwa anapoteza muda
 
Wanaudhi watu wa aina hii. Halafu usipowasaidia walalamishi hawakumbuki kabisaa walikotoka kweli watu husema mla kunde husahau lkn mzoa maganda huwa hasahau.Tena hujisifia kwamba bila mimi usingezaliwa , basi mwenzio nashangaaga sana na kusema kwani usingezaa wewe mtoto huyo si angezaliwa kwingine tena ulimpotezea opportunities nyingi tu. Ifike mahala wazee wa kesho wasiige hii tabia ya wazee wetu .
ha haaa, umenichekesha tunapoongea pale nyumbani (mbele ya watoto wetu) kuwa tunajiandalia maisha yetu ya baadae....
Tukiwa tunapanga kitu tunajiambia "unajua tutabaki wawili tu", kwa hiyo tunaandaa kwa ajili ya wawili..... sasa wanatuambia yaani wao tunawatenga?
Babangu (RIP) namkumbuka sana wakati alipokuwa analipa ada za shule na kutuzungumzia kuhusu maisha alikuwa anatuambia tujitahidi ili asije akaendelea kulipa na ada za wajukuu zake. nakumbuka siku mdogo wangu alimkorofisha sana akamwambia unafikiri nakuambia kila siku kuhusu maisha ili uje kunisaidia? sitakuja kutegemea msaada wako baadae maana nina uwezo wa kujitegemea mpaka nakufa, ila sitapenda nikiwa nimezeeka bado nitakiwe kulipa ada za wajukuu ambao wazazi wao hawataki kukazana ili wajikwamue na maisha. Huwa nakumbuka sana hiyo statement yake
 
bora tunakubaliana kwa hili.....
yale mengine ambayo huyakubali basi nimeamua kuyapotezea, lol!


Kwenye hili sina ubishi mkubwa mwenzangu....

Mwenzenu hadi sasa, karibia vitu vingi sifanyi bila ruhusa ya bibi....ila wakati mwingine anakaba sana hadi natamani kukimbia nyumba....

Mwanamke wa hovyo ni zaidi ya kiroba cha misumali.....

Ndiyo maana nawakubali na kuwaheshimu akina na mama wenye busara zao, wakiongozwa na Bibi DC, mama yangu mazazi na wengine kibao....!!

Babu DC!!
 
Very true The Boss
hata ukiangalia kwenye makampuni makubwa,utakuta wale wenye mishahara mikubwa sana hawana hata nyumba,
mtu anaambiwa muda wa kuretire umefika ndo anaanza kuomba kuongezewa miaka kazini(contract) hapo ndo ataanza kutafuta kiwanja etc wakati miaka ya nyuma ndo walikua mapapa wa miji
1.watu tunajisahau sana honestly.
2.wrong or poor investment..na kuna wengine wameinvest kwa wanawake
3.hakuna kitu kibaya,as far as am concerned kama mwanamme mwenye wake na watoto wengi tena kila mkoa wachache wameweza kusimama
4.sababu ingine ipo spiritual zaidi,radhi ya mke au mume,wengi walio na uwezo ujanani husahau wake zao na kuinvest kwa nyumba ndogo,i do believe in karma..hela huwa zinapuputika tu
ila naona tofauti kubwa kwa vijana wa sasa.
 
That's right! Unalala vibarazani, kutwa kwenye vijiwe vya majungu, hata kufuga kuku wawili wa kienyeji wasio nagarama kubwa ya madawa na vyakula unashindwa, hata kuweka bustani ya mchicha uani, kupunguza garama ya fedha ya chakula huwezi!
Unapokuwa na nidhamu na bidii kwa vitu vidogo ndivyo Mungu naye anakupa maarifa ya mambo makubwa!

Hebu shangaa na wewe
Inakuaje Mungu ahusike na mambo aliyotupa sisi?
 
Mwokozi nitoe roho niepuke hili balaa
Maisha nilichezea leo hii nalala na njaa
Chemsha bongo kabla hujapagawa utashangaa
Chemsha bongo kabla hujapagawa utaduwaa
 
Kipaumbele kwa wakati ule ilikuwa ni nyumba , sasa gari anahitaji wakati pesa aliwekeza kwa vimada!!!!!!!!!!!!!.
 
Yaani Eiyer umeeleza vzr haswa! Ni dini Fulani ivi ndiyo inawadumaza watu kutokufanya kazi kwa bidii, wala kutopanga future eti Mungu akipenda ndio utakuwa tajiri!
Dini zingine ni za hovyoo na ni za Shetani mwenyewe manake Mungu si dhalimu wala hana upendeleo.
Kama ulivyosema Mungu ameweka kanuni, na ukizifuata huwezi kubaki maskini!

I agree!!!!!!!!!
 
Kwenye hili sina ubishi mkubwa mwenzangu....

Mwenzenu hadi sasa, karibia vitu vingi sifanyi bila ruhusa ya bibi....ila wakati mwingine anakaba sana hadi natamani kukimbia nyumba....

Mwanamke wa hovyo ni zaidi ya kiroba cha misumali.....

Ndiyo maana nawakubali na kuwaheshimu akina na mama wenye busara zao, wakiongozwa na Bibi DC, mama yangu mazazi na wengine kibao....!!

Babu DC!!
ha haaa, hapo kwenye kutaka kukimbia nyumba ndo balaa, lol!
kuna siku niliambiwa "siku hizi sitakuambia unikumbushe, maana inakuwa kero". yaani mimi nikishaona hapa kuna kitu tunataka kukifanya, then nikaambiwa nikumbushe siku nyingine mbona atajutaaaa, atakumbushwa hata anapokuwa usingizini.....
Ila ninachowapendea huwa mnakuwa na shukrani sana ..... mnajua kabisa kuwa haya yamefanyika sababu ya MKE WANGU
 
Samahani Kibibi Jongo, Eiyer na wengineo naombeni mnidadavulie hapa kwenye suala la umaskini na utajiri. Nimesoma maelezo yenu hapo juu na mmeonyesha kuwa juhudi yako ndio utajiri wako na uvivu wako ndio umaskini wako. Kuna watu hawalali katika maisha yao wao kucha kutwa wanahangaika kusaka maisha tena wakiwa na mipango mizuri ya kipesa lakini mwisho wa siku hawafanikiwi wanabakia hohehahe hili linasababishwa na nini? Pia huwa mwanadamu akipata chochote kizuri mfano wa utajiri huwa anamshukuru Mungu kwakuonyesha jinsi gani Mungu alivyompa, je wale waliokosa hali ya kuwa walikuwa na juhudi na mipango kama wale waliopata,wamekosa kwa sababu gani?
 
Last edited by a moderator:
Mara ya kwanza niliposikia Mzee Gurumo wa Msondo Ngoma
anadai ameimba zaidi ya miaka 50 na maisha yake bado
ya 'kimaskini mno' niliona kuna kitu hakiko sawa..
sikuwa na ushahidi tu lakini nilikuwa na uhakika kwa vyovyote vile
'atakuwa alichezea maisha ujanani'

Sasa jana walioona akifanyiwa interview na Salama kipindi cha MKASI
watakubaliana na mimi huyu Mzee na wengine wengi tunaosikia
wakihojiwa na vyombo vya habari ..wakilaumu serikali kwa kutowajali.
wengi wao walipata 'golden opportunities' za kuwa na maisha bora
lakini 'walichezea pesa' na 'opportunities hizo' so many times...

mfano Mzee Gurumo jana alisema alilipwa 'elfu ishirini'
mwaka 1978 ili kuhamia bendi ya Sikinde...kumbuka
kuwa Mshahara wa Rias mwinyi mwaka 1992 ulikuwa 'elfu ishirini na saba tu'
sasa pata picha huyu mzee alikuwa na pesa kiasi gani?
na mshahara wake ulikuwa 'shilingi elfu tatu' mwaka hu0 1978..
wakati kima cha chini mpaka mwaka 1987 kilikuwa hakijafika 'shilingi elfu saba'

Kuna Mzee mwingine alitunga kitabu riwaya 'Simu ya Kifo' alilipwa
'elfu kumi na mbili ' miaka hiyo nyumba Kariakoo zinauzwa shilingi 'mia nne'
na alikufa bila nyumba wala kibanda..

Orodha ni ndefu...na wapo wengine Baba zetu,Wajomba,babu na kadhalika
ukiwaona uzeeni wanavyolalamika na kuomba wasaidiwe....utasema hawakupata chochote ujanani
kumbe anasa,starehe na kuhonga wanawake ndo sababu....

ukweli ni kwamba watu 'huchezea maisha mno' halafu uzeeni hutafuta wa kumpa lawama
mara watoto,mara serikali na kadhalika....


huyu Mzee Gurumo alikuwa sio mtu wa kupewa gari na Diamond...
angekuwa na magari na majumba tele ya kuwarithisha watoto na wajukuu...

Nimejifunza kitu hapa. Ila kubwa nikuwa watu wengi ujanani huwekeza katika starehe na uzee ukiwapata na mambo yakiwa magumu huwa wanatafuta ninani wa kumuangushia lawama zao.
 
Back
Top Bottom