Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Wanaume na 'kuchezea maisha'.....

Mkwe wewe umeshajipanga? Ama bado upo upo? Mie sijielewi kama nishafikia pa kilujipanga ama bado!
!

yaani mkwe nishaanza tatizo son wako ananirudisha nyuma.mkwe ukitaka ufanikiwe kuwa na roho mbaya.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Ok hizo ni kanuni za kiuchumi nazielewa vizuri sana. Mimi msingi wa maswali yangu ni kwamba hata huyo aliepata ufahamu wakielimu akajua how much to consume kulingana na income yake nae kabarikiwa akili hiyo na Mungu. Kwakuwa wapo wenye ujuzi huohuo lakini hawautumii kujipatia hayo maisha safi. Mzee Ngurumo na watu wamfano wake waliobahatika kupata neema kipindi cha ujana wao wakazichezea wao walikosa neema ya ufahamu wa kuwekeza kwa ajili ya maisha ya baadae. Nikiwa na maana kwamba umaskini na utajiri pia ni sehemu ya mipango ya Mungu. Mungu anajua nani atakuwa mzembe ktk utajiri alionao na mwisho ataja kuwa maskini. Sema ni siri yake Mungu kwani hakuna aliezaliwa anajua kuwa yeye atakuwa tajiri au maskini. Huwezi ukakaa tu chini ukawa na fikra kuwa utapata tu kwakuwa Mungu ndie anaejua wewe utakuwa tajiri bali mtu unapaswa kuhangaika na kujitafutia ila ikitokea umekosa pamoja na juhudi zote ulizoonyesha katika kutafuta unapaswa kuamini kuwa Mungu ndie aliepanga hayo na hapo itakusaidia pia Kumshukuru kwakila jambo la furaha au la shida. Ndio maana as a human being we do our best and God do himself the rest. Unapokuwa unasema Mungu hajui nani atakuwa maskini au tajiri manake wewe unakuwa mpingaji wa kwamba Mungu hajui mambo ya siri. Wakati yeye ndio anaejua yaliokuwa, yanayotokea sasa na yatakayotokea kesho tusioijua wewe na mimi. Cc Kibibi Jongo.

Ahsante kwa kuni cc Mkuu! Nimekusoma! Ila hujatuelewa nadhani! Mungu amekupa maarifa akili na utashi wa kujua mema na mabaya.
Nidhamu ya kukusanya (kufanya kazi, juhudi na maarifa) ndiyo Neema yenyewe. Matunda yake ni USTAWI.
Sasa wewe unataka kuhalalisha kwamba unapotapanya, na starehe na anasa kile ulichokipata kwa Neema ni mpango wa Mungu pia!
 
Last edited by a moderator:
Kwanza, za kuadimika?
Kwa maneno mengine, mwanaume akiharibu au akitengeneza ni sababu ya mwanamke? Akicheat au akiwa mwaminifu ni sababu ya mwanamke? yeye hana will na uwezo wa kufanya maamuzi yake mwenyewe?
ha haaaa, umenipeleka kona mbaya sana rafiki........
naomba kwa sasa tuishie kwenye kujenga/kubomoa future ya familia....
hayo mambo yanayohusu moyo tuje nayo siku nyingine
 
umenikumbusha wakati mzee kastaafu akafanikiwa kujenga kibanda last minute, kwa mara ya kwanza nikapata kusikia sauti ya mvua kwenye nyumba ya bati ambayo haijawekwa ceiling it was hard, ukizingatia nimezaliwa na kukulia kwenye nyumba za sirikali za vigae.

Anyway kwa watoto wa baba yetu, we took it positive kiasi kwamba hakuna mtoto ambaye alifikisha 30yrs bila kuwa na nyumba, so tulijifunza kutokana na makosa ya mzazi; you can do the same.

baadhi ya wazazi wa kiume wana shida sana, mie mzee wangu kaja kujenga ka nyumba juzi juzi tena nadhani hakajaisha, na alizishikaga haswa lakini kwake tunaelewa zilipokuwa zinaishia, starehe/wanawake, alioa kila mji, anaishi kimaskini sana sana sasa hivi yaani basi tu, na ni mtu ambae angejipanga angekuwa mbaliii sanaaa.
 
na ukipata mume wa hovyo je?

Mimi nafikiri ukipata mke wa hovyo na ukakubali kufuata uovyo wake nawe ni wa hovyo au akili zako ni za kushikiwa. Ofcourse kama couple mnahitaji kuwa na malengo mliyokubaliana na strategy mlizokubaliana.
ukipata mume wa hovyo ndio kwisha habari yako ujue.
 
Nimesoma maelezo yenu hapo juu na mmeonyesha kuwa juhudi yako ndio utajiri wako na uvivu wako ndio umaskini wako. Kuna watu hawalali katika maisha yao wao kucha kutwa wanahangaika kusaka maisha tena wakiwa na mipango mizuri ya kipesa lakini mwisho wa siku hawafanikiwi wanabakia hohehahe hili linasababishwa na nini?
kwasababu hawalali wanasaka maisha huku wakiwa hawana afya njema na unajua afya nayo ni muhimu katika kujibidiisha.
 
baadhi ya wazazi wa kiume wana shida sana, mie mzee wangu kaja kujenga ka nyumba juzi juzi tena nadhani hakajaisha, na alizishikaga haswa lakini kwake tunaelewa zilipokuwa zinaishia, starehe/wanawake, alioa kila mji, anaishi kimaskini sana sana sasa hivi yaani basi tu, na ni mtu ambae angejipanga angekuwa mbaliii sanaaa.

My dad alikuwa yeye na his dear bottle, imagine miaka 5 ya ndoa alikuwa akipata mshahara anamkabidhi mama, na mama anampa za matumizi binafsi; lakini later in the years mama alikuwa ni wa kumsachi suruali kila akija mbwi ndipo aongezee kwa mahitaji.
 
Gombaneni nae sasa hivi
atawasumbua mno huyo baadae...
atawatolea laana msipompa pesa...hapo baadae
mngeanza kugombana nae sasa
The Boss , kuna wazee wengine hawashauriki, mimi mwenyewe baba yangu alikuwa hivyo, na ni mtu wa East Africa, alistaafu na mamilioni ya pesa , lakini hakuwa na hata kibanda, sana sana alienda kuoa mke mpya akamdaharau mama yetu,Uzuri mama yetu naye alikuwa anafanya kazi na ana nyumba 5 hapa mjini, yeye aliondoka na pesa zilipoisha akarudi home, so mtu kama huyo mnamfanya kama mbwa wa kizungu anakula bure, analala bure, anafuliwa, lakini hapewi hata senti tano. na nahisi anajua jinsi tunavyomchukia kiasi hamuombi hata mmoja wetu pesa. Jukumu letu ni kumlea mpaka utakapofika mwisho wake full stop.
 
Mkuu tuwasamehe, hawakuwa na motivation ya kujenga aisee...
After all, walikuwa anaogopa magonjwa ya zinaa tu...tena mengi yakitibiwa kirahisi na PPF!!

Ndo maana natamani kusikia wakitupa na upande huo..

Babu DC!!

Babu wala hujakosea aisee... umenikumbusha kisa kimoja nitakisimulia hapa.....

Mimi nilipoanza kazi mwaka 2003 kuna mzee mmoja alikuwa ameajiriwa kwa mkataba (baada ya kustaafu serikalini na huko ameshika nafasi kadha) akawa anatuangalia tunavyofanya mahesabu ya kutafuta viwanja hata kwa mkopo (kumbuka ni mwaka wa kwanza kuajiriwa) yeye bado anapanga na bado anasomesha akaniita na kuniambia, Kijana wangu...... Nikiwaangalia mlivyo aggressive na maisha naguswa sana. Sisi enzi zetu wala hatukujua kuwa kuna kitu kinaitwa kujenga wala kununua kiwanja.... Sana sana nilikuwa nikihamishwa sehemu moja kwenda nyingine unabeba tu shuka zako maana vitanda na magodoro unavikuta humo humo....unapewa nyumba ina kila kitu sasa utawaza kujenga?
Sana sana tulikuwa tukipata hela ni wanawake na pombe basi.... Hata magonjwa yalikuwa hayapo sanasana tuliogopa kisonono tu basi.....

Sasa The Boss anachosimamia ni cha kweli kabisa, wapo wazazi wetu ndugu na jamaa kama hawa kina Gurumo (binafsi nampenda sana kwa ajili ya kazi zake) wapo mstari wa mbele kusimulia jinsi walivyoponda raha enzi zao na walivyopiga madili ya hakika kama hizo pesa za kuhamia Sikinde lakini ukimwuliza ulifanya nini hawana majibu. Sana sana atakuwa amesambaza watoto kila kona ya mji.Pamoja na kuwaonea huruma watu kama hawa ni vyema tukawaeleza ukweli kwa lengo la kuwafanya watu wawajibike wanapokuwa na nguvu na wawe responsible kwa vitendo vyao hapo umri unapowatupa mkono.

Nimekuwa nikijiuliza sana ni kwanini wanamuziki wa Tanzania wanakufa masikini kiasi hiki lkn walau the boss umenifumbua macho. Angalia pamoja na sifa zote alizokuwa nazo Marijani Rajabu, kafa hohehahe hata waliobaki wanashindwa kutunza vizuri kaburi lake pale kisutu walau vizazi vijavyo vikaendeleza historia, sio huyo tu huwa namsikiliza sana Rajabu Zomboko kwenye hizi nazo ya Radio One kila Ijumaa, historia za wanamuziki wengi sana hazitofautiani na huyu Mzee Gurumo wameishia hawana kitu, Masikini wa kutupwa....

Pamoja na ukweli kuwa Serikali inapaswa kuwajibika kulinda haki za wasanii zinazoporwa kila uchao, nafasi ya wasanii hawa kutengeneza maisha yao ya baadaye ni muhimu na ni lazima tuwalaumu kwa kutokufanya hivyo, Hili la Gurumo liwe mfano.
 
Last edited by a moderator:
ha haaa, hapo kwenye kutaka kukimbia nyumba ndo balaa, lol!
kuna siku niliambiwa "siku hizi sitakuambia unikumbushe, maana inakuwa kero". yaani mimi nikishaona hapa kuna kitu tunataka kukifanya, then nikaambiwa nikumbushe siku nyingine mbona atajutaaaa, atakumbushwa hata anapokuwa usingizini.....
Ila ninachowapendea huwa mnakuwa na shukrani sana ..... mnajua kabisa kuwa haya yamefanyika sababu ya MKE WANGU

Mke wangu balaa...swali la kila mara ni kutoka kwenye upangaji mbona nilikoma! Ila kuna familia mama ni starehe tu na mavazi na magari.
 
Ahsante kwa kuni cc Mkuu! Nimekusoma! Ila hujatuelewa nadhani! Mungu amekupa maarifa akili na utashi wa kujua mema na mabaya.
Nidhamu ya kukusanya (kufanya kazi, juhudi na maarifa) ndiyo Neema yenyewe. Matunda yake ni USTAWI.
Sasa wewe unataka kuhalalisha kwamba unapotapanya, na starehe na anasa kile ulichokipata kwa Neema ni mpango wa Mungu pia!

Nimekucc baada ya kuona coment yako moja hapo juu yenye kuashiria kuna dini inawafundisha watu wake vibaya na kuwapelekea kuwa maskini kama mlivyofanya kamjadala ofisini kwenu ndio nikaona nikuulize maswali yangu japo hukunijibu ila naamini tuko pamoja.
 
My dad alikuwa yeye na his dear bottle, imagine miaka 5 ya ndoa alikuwa akipata mshahara anamkabidhi mama, na mama anampa za matumizi binafsi; lakini later in the years mama alikuwa ni wa kumsachi suruali kila akija mbwi ndipo aongezee kwa mahitaji.
ha haa, siku hizi wanajidai mishahara inaingizwa bank, lol!
labda tudai kupewa bank cards, mbona kazi.
Ila inaudhi sana baba asiye responsible.
Mi nakumbuka uncle wangu alikuwa kila akitoka job anarudi home anauliza kama kuna shida atatatua shida zenu then huyooooo kwenye bottles......... akirudi kabla hamjalala basi ujue huko hakujanoga, otherwise atarudi kesho kuchukua funguo za ofisi na kuwahi job
 
The Boss , kuna wazee wengine hawashauriki, mimi mwenyewe baba yangu alikuwa hivyo, na ni mtu wa East Africa, alistaafu na mamilioni ya pesa , lakini hakuwa na hata kibanda, sana sana alienda kuoa mke mpya akamdaharau mama yetu,Uzuri mama yetu naye alikuwa anafanya kazi na ana nyumba 5 hapa mjini, yeye aliondoka na pesa zilipoisha akarudi home, so mtu kama huyo mnamfanya kama mbwa wa kizungu anakula bure, analala bure, anafuliwa, lakini hapewi hata senti tano. na nahisi anajua jinsi tunavyomchukia kiasi hamuombi hata mmoja wetu pesa. Jukumu letu ni kumlea mpaka utakapofika mwisho wake full stop.

kwa kweli umenivunja mbavu, mie sijawahi kuona mama anaeweza kufanya upuuzi na maisha ya watoto wake aisee, huyo mama atakuwa sio mzima, lakini hawa baba zetu hawa, ni hatari.
 
Ndio hivyo, walioziona opportunities leo hiio ni matajiri wa kutupwa. Msasani 'Butiamba' kwa Nyerere kulikuwa pori tu miaka hiyo. Na mpaka miaka ya 1990 kulikuwa bado kuna nyumba za ''mbavu za mbwa'' za Wamakonde.

Halafu leo hii eti timu kongwe kama Simba hawana hata uwanja wa mazoezi......!! Nahisi siasa ya ujamaa ilidumaza uwezo wa kufiri wa Watanzania wengi! Ni wachache tu walioshtuka enzi za Mwinyi milango ya fursa ilipofunguka!
 
ha haa, siku hizi wanajidai mishahara inaingizwa bank, lol!
labda tudai kupewa bank cards, mbona kazi.
Ila inaudhi sana baba asiye responsible.
Mi nakumbuka uncle wangu alikuwa kila akitoka job anarudi home anauliza kama kuna shida atatatua shida zenu then huyooooo kwenye bottles......... akirudi kabla hamjalala basi ujue huko hakujanoga, otherwise atarudi kesho kuchukua funguo za ofisi na kuwahi job


halafu ninavyoona msukuma alivyo kwa wanae, nazidi kumchukia mzee wangu, ameshaombaa weee tumfate/yaishe lakini wapi, mie namwambiaga yameisha habari za kuja kutujua uzeeni haikubaliki aisee.
 
Back
Top Bottom