Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,753
haya yanatokea kwa mtu ambayo yupo very close na mimi.....Bila uchochezi now watakuja 'kumbeba huyo baadae'
sasa ndo wasimuonee haya..
babake alikuwa anajulikana mji mzima kwa hela, watoto wake walikuwa wanatembea kwenye magari tu, enzi hizo ambazo umiliki wa baiskeli ulikuwa shida. alibahatika kuwa na mtoto mmoja (nje ya ndoa), ambaye kwa sababu alikataliwa na baba na mama wa kambo basi alijisomesha ili angalau aweze kujikwamua kimaisha.
wale watoto wa ndani walikuwa na starehe tu kiasi kwamba hakuna aliyekumbuka shule.
huwezi amini kwa sasa huyo mtoto aliyekataliwa ndo anahudumia ukoo mzima, kuanzia baba/mama aliyemkataa, watoto wa watoto wao ambao walikataa kwenda shule, na watoto wa mzee ambao bado wanaenda shule......
na sasa mzee sababu anaona mwanaye alishasamehe na kuamua kuhudumia "familia" yake basi ameanza kudai haki yake kama mzazi, anatamka kabisa kuwa nahitaji kiasi hiki kwa mwezi..... bila aibu