MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,564
- 847
Nafikiri kuhama mtandao wa voda siyo ubaguzi wa aina yeyote ile ila ni kupambana na mafisadi mpaka wasalimu amri! waiache Tanzania istawi kama ilivyobarikiwa kuwa na rasilimali tele! wewe kama kweli unataka kupambana na mafisadi huna budi kuacha kutumia bidha zao zote! mwenye kujua bidha za mafisadi azitaje ili tusinunue. Kwa kweli inauma sana na ni aibu kwa nchi yenye kila rasilimali halafu wananchi wake wamechoka mbaya! huduma za jamii aibu tupu!
Je niki kuambia kampuni zote za simu Tanzania zina dalili za ufisadi utaacha kutumia huduma za simu moja kwa moja? Upo tayari kukaa bila simu mkuu? Ujue kuwa haya mambo ya kususia bidhaa ni kama kuna alternative bora. Kuna vitu nina uhakika kabisa kama haona alternative nyingine hata uonyeshwe ushahidi wa ufisadi wake ni uta tumia tu. Mfano rahisi ni kama upo sehemu ambapo hakuna mtandao mwingine una kamata zaidi ya Vodacom hata katika hali hiyo utaacha kutumia hudumza zao? Telling people to boycott Vodacom na huduma zake siyo solution kwa sababu kuna watu wana faidika na huduma zake directly or indirectly. Kama huduma za Vodacom zina kubalika bado watu wataendelea kui tumia tu kwa sababu watu wengi hawajali nani ana miliki nini bali wana angalia ubora wa huduma. Kuna sehemu hakuna mtandao unashika zaidi ya Vodacom, watu wa huko hawata acha kuitumia hata kama ina milikiwa na Vodacom. Kuna watu gharama zao za simu wana lipiwa na ofisi ndiyo inaamua mtandao gani uta tumika, hawa nao hata uwaambieje hawata acha kutumia Vodacom. Kuna waajiriwa wa Vodacom ambao kuwepo kwa Vodacom ndiyo kuwepo ajira yao hawa nao hawa jali Vodacom ina milikiwa na nani hawata acha kui tumia. Na kuna mifano mingi zaidi kama hii siwezi kuitaja zote. In short kama hauta kuja na sababu za maana na za msingi hamna mtu ataacha kutumia kitu simply because someone said so. Kama wewe umeweza kuacha kutumia Vodacom sawa ila situations zina tofautiana mtu hadi mtu. Kilicho nafuu kwako siyo nafuu kwa wengine. Bado tunam subiria muanzisha mada aje kutoa maelezo zaidi.