Wanaharakati: Ziachieni simu za VodaCom!

Wana JF kama kweli ni mwanaharakati uwe makini na VODA kwani ni ya Fisadi RA sasa kama unapanga kukata mirija yake ya unyonyaji atafuatilia kwani Simu zote anasikiliza.Raia kwa Wabunge wanaharakati muachane na VODA msije mkahusika kwenye ajali za kupanga.Maharamia hawa wa ajali za kupanga walipofanikiwa kwa Wangwe sasa wameona ni njia nzuri ya kuwadhuru maadui wao.Hongera kwa aliyetoa Rai ya kuachana na VODA.Mimi naitupa sasahivi na RA ajue ameula wa chuya kwa kufuatilia mawasiliano ya watu.Serikali itaharibu sekta ya mawasiliano kama itawaachia Mafisadi wawe kama mashushushu kwenye mitandao ya simu za mkononi.
 
Thread ya kuisusa VodaCom ilishaanzishwa humu siku za nyuma. Tukaijadili mpaka basi. Tusipande pia ndege za PrecisionAir, kuna akina Mramba humo. Mafisadi wamejenga hadi misikiti na makanisa, tusisali humo. Kuna mashule yamejengwa na mafisadi, tuwatoe watoto wetu huko. Rais tulienae kachangiwa sana na mafisadi kwenye kampeni zake 2005, tumkatae, tumwondoe, tumng'oe?

Ili tufike huko lazima tuanzie harakati zetu mahali fulani hasa pale palipo dhahiri kama...
 
voda ni ya wenye uwezo kama mimi,
kama huwezi gharama nenda tigo,

usiniharibie hamu ya kiti moto hapa kona bar!!!
mweeee!
 
Endasuphai Wana Jamii,Habari inoo,Za siku nakubaliana kabisa na Ole Mwanakijiji sasa hivi kama wewe ni (mwanaharakati) na unatumia Mtandao wa Voda wataanza ku-trace simu za watu wote wanaowatilia shaka hasa (wanaharakati) hivyo kaeni chonjo saa mbaya.
 
Makampuni ya simu Tanzania na ufisadi wake:

(a). VodaCom- Kuna RA (share holder 35 %), Somaiya (Shivacom -super dealer ), Lowasa - Alphatel (dealer)

(b). Zain (wameifisadi TTCL hadi ikabinafsishwa kwa bei chee na wameingia TZ kwa wizi na utapeli mkubwa)

(c). Tigo (wamekuwa wakibadili majina kila baada ya miaka 5 kukwepa kodi: 2001 from Mobitel to Buzz, 2006 from Buzz to Tigo) na ukifuatilia tangu kuanzishwa kwake mwaka 1993 ikishirikiana na shirika la posta na simu wakati huo mpaka sasa ime-undergo several dubious contracts na serikali. Mpaka sasa kampuni inamilikiwa na Millicom ya Luxemburg kwa asilimia 100 % kinyume na sheria za nchi

(d). TTCL - hii nayo imebinafsishwa kwa Wa-Kanada kifisadi kupita kawaida na bila shaka mafisadi wana share huko. Kwahiyo tunatupa simu zote na kufunga landline zetu zote tuwasiliane kwa internet na barua.
Du! sasa tufanye nini? Tuache kupiga simu?
 
Nilikuwa Tunduma pale nilishangaa watu wanajiproud kwa kutumia Voda huku wakinishangaa mm nae tumia tiGo dah kwakweli watu akili zao hazifanyi kazi kabisaa wametekwa kama si kuzama kabisa.
Mtu anajiona ufahari kutumia pesa nyingi kwenye line ya voda na anasema huu ndo mtandao wa sisi wenye pesa maskini mtaendelea kutumia tigo.
Miafrika jamani bado sana.

Hii imetokana na marketing ya Voda. Sio watu kuwa wajinga bwana. Mbona Ulaya kuna hali hii hii kwa upande wa vitu kama maduka, nk. Au utavitofautisha hapo?
 
voda ni ya wenye uwezo kama mimi,
kama huwezi gharama nenda tigo,

Mkuu Edson tutashukuru sana kama utatuchangia huo uwezo wako na hapa JF......we seriously need your unconditional contributions here to make JF online indefinately!

usiniharibie hamu ya kiti moto hapa kona bar!!!
mweeee

Heee....na huko Norway kuna KONA BAR? au mkuu umeshamaliza ile kozi yako kule?
 
Mwanakijiji amwambie bosi wake Mengi apige marufuku vyombo vyake vya habari kutoa matangazo ya Vodacom kwanza. Ukimalize hilo weka tundiko la kususia Precision air kwa kuwa Mramba ana hisa na ni fisadi.

Bila kusahau wasafiri wote wa ndege watumie Jomo Kenyata airport halafu waje kwa bus kwa kuwa uwanja wetu wa ndege unatumia rada ya mafisadi. Tususie noti za benki kuu kwani huko ndio asili ya ufisadi mkubwa

Pia usisahau kuhamasisha wananchi wasitumie umeme wa IPTL, Dowans, Songas, Kiwira (kama upo ) nk
 
Mwanakijiji amwambie bosi wake Mengi apige marufuku vyombo vyake vya habari kutoa matangazo ya Vodacom kwanza. Ukimalize hilo weka tundiko la kususia Precision air kwa kuwa Mramba ana hisa na ni fisadi.

Bila kusahau wasafiri wote wa ndege watumie Jomo Kenyata airport halafu waje kwa bus kwa kuwa uwanja wetu wa ndege unatumia rada ya mafisadi. Tususie noti za benki kuu kwani huko ndio asili ya ufisadi mkubwa

Pia usisahau kuhamasisha wananchi wasitumie umeme wa IPTL, Dowans, Songas, Kiwira (kama upo ) nk


Mkuu Masatu kumbe kweli unajua huo ufisadi upo kama ulivo uainisha mwenyewe hapo juu, isipo kuwa hupendi tu hao mafisadi watengwe/wakwamishwe?


Mimi nadhani kwa vile wote tunawajua hao mafisadi wapo, jithihada yoyote ile ya kuwakwamisha/kuingilia mirija yao ya kuendelea kutufisadi ni ya kuungwa mkono kwa nguvu zote!
 
thanx to Pundamilia and furthermore we have not been given concrete grounds for having to do away with Vodacom do's....
i'll be back
 
it is too late now but not too late enough.. Kama uko kwenye mapambano dhidi ya ufisadi na hauko tayari kusalimu amri, nakushauri kuachilia namba za simu za vodacom asap. As a matter of fact, hamia "kwingine" within the next 72 hours (beginning monday). Do it or be ready to live with the consequences.

Nilikuwepo.

M.m.


hii ni habari?vitisho?mkwara? Wewe kama mwandishi wa siku nyingi wa kijarida na majarida kwa nini usieleze kitu kikaeleweka hata kwa sentence 1 kuliko kutoa vitisho na kuacha habari ina ning'inia itatufanya tuamini hata habari nyingine ni kwa 'bora siku iende'/kusukuma siku mbele au kuchangamsha genge na habari kama hizi ni sensitive sana.
 
hii ni habari?vitisho?mkwara? Wewe kama mwandishi wa siku nyingi wa kijarida na majarida kwa nini usieleze kitu kikaeleweka hata kwa sentence 1 kuliko kutoa vitisho na kuacha habari ina ning'inia itatufanya tuamini hata habari nyingine ni kwa 'bora siku iende'/kusukuma siku mbele au kuchangamsha genge na habari kama hizi ni sensitive sana.


Kubembelezwa jama, lazima kwanza kupetpet na kumfagilifagilia, kwa mfano kumwambia mzee safi sana.... tuko pamoja mkuu....wewe ni kichwa sana...kila siku unasema haya.....umeshaandika sana kuhusu....unajua sana....ndio mzee...unayosema ni kweli na kweli tupu....hakuna mwanaharakati zaidi yako....., hilo nalo neno.....

Yanafuata mazungumzo baada ya habari hata kwa PM.
 
Mwanakijiji kawatahadharisha wanaharakati wa KWELI, wanaofahamika kwa kauli na matendo yao kuhusu ufisadi. Sio sisi tunaopinga ufisadi kwa majina bandia!
 
Kwa wale msio kwenye system..viongozi kibao sikuizi wanaongea kwa mafumbo kwenye simu...zinasikilizwa! Watanzania hatujui privacy ni nini tcra wanatuambia tukaregister sim card..kuna thread nilianzisha watu wamechunia..ukweli ndo huo..ata ulaya its not a must to register a sim card!! Kuna mambo yanafanyika na haki zetu kuvunjwa sisi tunabaki kubishana juu ya nia za Mwanakijiji...
 
Mwanakijiji kawatahadharisha wanaharakati wa KWELI, wanaofahamika kwa kauli na matendo yao kuhusu ufisadi. Sio sisi tunaopinga ufisadi kwa majina bandia!

Wildcard,

Kwa nini unadhani JF hakuna wanaharakati wa kweli?

Kuna mbinu nyingi za kupigana vita, si lazima wote tushike bunduki na kwenda mstari wa mbele! Wengine kazi yao inaweza kuwa ni kupeleleza uwezo wa adui na mambo anayokusudia kufanya na si kushambulia!
 
Wachangiaji wanashindwa kuelewa "targeted audience" = Wanaharakati
Mwanakijiji ni mwanadamu, ana madhaifu yake, hisia, vionjo na ushabiki. Lakini katika hili ana ujumbe mzito tena wa Kizalendo. Asiye Mwanaharakati ni kinyume chake na hana haja kuwa na wasi kuendelea kutumia Vodacom maana hana lolote la ki-harakati au ki--mkakati analoweza kuanika wala kupoteza bali kuongeza nguvu ya kiuchumi ya wasio Wanaharakati.
Sikuwepo!
 
Wildcard,

Kwa nini unadhani JF hakuna wanaharakati wa kweli?

Kuna mbinu nyingi za kupigana vita, si lazima wote tushike bunduki na kwenda mstari wa mbele! Wengine kazi yao inaweza kuwa ni kupeleleza uwezo wa adui na mambo anayokusudia kufanya na si kushambulia!
SMU,
Najua humu JF pia wamo. Nawashangaa wale wanaomshambulia Mwanakijiji badala kushambulia hoja yake ambayo ina walengwa wake.
 
Masatu nafikiri hapa umekosena kidogo kwa kauli zako zidi ya mwana kijiji, inadhihirisha kuwa wewe ni mtu mmoja wapo moga sana,huyu jamaa ametumia haki yake ya kutowa maoni yake haina mana kwamba kila mtu atakubaliana nae au atapingana nae, mwache ale hoja zake na watu wazipime.Umenifanya niwaze mambo fulani likiwemo hili la hii Blog isije ikawa wazamini wake ni miongoni mwa hao wanaoogopewa ? (I hope I m wrong)hapa kwetu wazee wetu hutwambia (Mficha Uchi Hazai )sasa kama watu wafumbie macho maovu kweli tutafika ?

Wait a minute.... unadai yeye katumia haki yake kutoa maoni na haina kila mtu atakubaliana nae au atapingana nae. Upo sahihi kabisa! and thats exactly wot im doing here... kwani hiyo haki ya "kutoa maoni" ni ya Mwanakijiji tu wengine hatuna?

Kwa taarifa yako na wewe pia umetumia haki yako kutoa maoni na kuna watakaokuunga mkoo na watakao kupinga ndio maana ikaitwa public forum.

Baada ya kusema hayo wewe endelea kutoa maoni kwa uhuru nami niache niji nafasi
 
tukisusia voda tuamie mtandano upi? mzee MM tafadhali nahitaji ushauri wako?
 
Back
Top Bottom