Wana-jf nimefiwa na mke wangu!!

Pole sana Sajenti, Mwenyeenzi MUNGU awape nguvu wafiwa na aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi
 
Pole sana kaka,
Hope vijana utawaendeleza kwa kuwapatia ELIMU bora, itakayo wasaidia maishani mwao.
Sijuhi maisha yako ila chondechonde kama kuna mlicho chuma na mzazi mwenzio jitahidi kuvitunza viwe vya wanenu hao wawili na bila ya kuuza au kufuja kwa aina yeyote ile au sio kwenda kuoa mke mwingine atakaye kuja kuleta fujo( na uzoefu na hili na limenikuta)
 
Sajenti,

Pole sana ndugu yangu. Yote ni ya mwenyezi mungu, tunamuomba muweza wa yote akupe ustahamilivu katika wakati huu mgumu.
 
Pole sana mkuu.naomba ni pm no ya Simu nitoe Rambi rambi zangu

Tupo pamoja.
 
POLE SANA NJENGA...Mungu ailaze roho ya dada mahali pema peponi...nilikutafuta sana kwa simu sikukupata..Nipo Morogoro sikuweza kuja kuhudhuria mazishi...POLE SANA NJENGAAAAAAAA

kweli ngondomwitu simu ilikuwa busy sana kwa hiyo huenda ndio muda uliokuwa unanitafuta!
 
Pole sana Best! Hakika uko ktk wakati mgumu.

Jipe moyo wa ushindi kwn hakika umempoteza kiungo muhimu.
Pole sana Best wetu, Pole sana!

MUNGU MWENYE UWEZA WA YOTE TUNAKUOMBA UMLAZE MAMA WATOTO MAHALA PEMA PEPONI.

Amen!!!!
 
Nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8.

Kiukweli ametutangulia tu sote tutafuata huko maana ndiyo makao yetu ya milele! Pole sana Sajent, kikubwa ambacho nakuomba ni kushikamana sana na hao watoto!
 
Mungu akupe moyo wa uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu na maishani.

Pole kwa kumpoteza Mke na wape pia pole wadogo zangu kumpoteza mama.

Roho yake ipumzike kwa amani.
 
Pole sana mkuu. Mungu akutie nguvu katika kipind hiki kigumu
 
Back
Top Bottom