Hii ni habari ya kusikitisha sana mkuu, lakini maisha ndo yalivyo, leo kwako kesho kwa mwenzio, asnate kwa taarifa na hii itukumbushe kwamba sote tuko njiani. Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya kipenzi chako.
Pole sana mkuu ni kipindi kigumu hasa kwako na watoto! Mungu awajalie amani yake na kama utahitaji mtu wa kuendelea nawe katika maisha muombe mwenyenz MUNGU akupatie atakae penda watoto wako kama wewe!
Ohhhh!
Pole sana kwa msiba wewe na familia yako yote.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, na awajalie ujasiri wa kupambana na kipindi hiki kigumu.
Pole sana Mkuu kwa msiba mkubwa uliokufika wa kufiwa na mkeo. Mwenyezi Mungu awape nguvu na faraja katika kipindi hiki kigumu kwenu na ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi~AMEN.
POLE SANA NJENGA...Mungu ailaze roho ya dada mahali pema peponi...nilikutafuta sana kwa simu sikukupata..Nipo Morogoro sikuweza kuja kuhudhuria mazishi...POLE SANA NJENGAAAAAAAA
Nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8.
Pole sana mkuu SAJENTI, inshallah Mwenyezi akutangulie katika kipindi hiki kigumu kwako na familia yako kwa ujumla. Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa, ...........
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.